Pre GE2025 Mtangazaji wa ITV na Tundu Lissu hakika mmetutendea haki sisi watanzania kwenye kipindi cha dakika 45

Pre GE2025 Mtangazaji wa ITV na Tundu Lissu hakika mmetutendea haki sisi watanzania kwenye kipindi cha dakika 45

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mama SSH amepoa sana, yaani inakuaje huyu chiba anaipata nafasi ya kwenda kituo Cha tv kumtukana yeye na familia yake?!!!!! Dah, angekuwepo yule mwamba huyo mtangazaji hata kutokea asingetokea........angesingizia anaumwa malaria na kwamba amelazwa hospitali.

Nje ya mada;
Hivi Kuna ITV na vipindi flani flani hivi vya urahisi?!!!! Awamu ya 3 (Mkapa), walikuwa karibu kweli na serikali......ilikuwa inatukuzwa na hata hakukuwa na uhamasishaji wa uhuru wa kuongea kwa wapinzani kama Lipumba na wanaharakati wengine.
Awamu ya 4 (Kikwete), ilikuwa mwiba sana kwa serikali.....maadui wa Kikwete walialikwa hapo kama wote Hadi kufikia muda kuongezwa na kina Masako!!!!
Awamu ya 5 (Magufuli), ilikuwa pamoja mno na serikali na hakuna mwanaharakati yeyote uchwara aliyepewa airtime.
Awamu ya 6 (Samia) mambo tayari........ishaanza kujitenga na serikali. Kina Tundu wanaulizwa mpaka maswali yanayotweza utu kabisa wa Raisi. Tutawashuhudia wengi zaidi, bila shaka!!!

Ni coincidence hii au?!!!!!!!!!!
Acha uchonganishi wewe..hakuna kituo Cha TV kinashirikiana na serikali ya awamu ya sita Kama ITV ukiondoa TBC..ni mtazamo wangu lakini..hata hiyo Jana tu Naibu Waziri mkuu alikuwa hapo ITV kudhihirisha dhana ya mashirikiano mazuri Kati ya serikali na IPP media..na jumatatu ijayo nadhani anaweza kuwa kwenye Dakika 45 na Farhia
 

View: https://www.youtube.com/live/ZL2V3hUw5Hg?si=ucxs0XUFwPi8526W





Ushauri kwa Tundu Lissu, Kama yupo serious anataka urais, asisubirie kuzunguka kwenye majukwaa na vyombo vya habari. Na yeye awe updated kwenye mitandao ya kijamii awe anatoa clip fupi za dakika 1 mpaka 2 anapost mitandao yote ili kuwafikia vijana. Hasa Instagram (Instagram reels, instalive), Whatsapp channel, Telegram Channel, Youtube Channel, YouTube shorts, Facebook, TikTok, TikTok video, TikTok live. Awalenge zaidi vijana hasa hali ngumu ya kiuchumi na ukosefu wa ajira. Awe anapost kila siku consistently bila kuchoka.



Erythrocyte

Hili ni wazo zuri sana, kazi hiyo Lissu mwenyewe haiwezi ila anaweza kuisimamia hata kwa muda mchache aupatapo. Cha kufanya ni kwa Chadema kwa vile ina vijana mahiri sana na wenye akili, iundeTEAM ya watu kama 20 hivi watakao fanya kazi hiyo kwa uratibu maalumu wa kumuuza Lissu na kazi zake katika mitandao ya jamii na uratibu wa vyombo vya habari.
Kazi hiyo iwe maalum na walipwe vizuri vijana hao waaminifu na wenye uelewa mkubwa na mapenzi mema kwa nchi, Chadema na hususani kwa Lissu mwenyewe. ITALIPA!
 
Tundu Lisu anatakiwa kwasasa akiwa na media tour waandishi waulize maswali mengi yanayohusu maswala ya sheria sheria kuliko ya chama chake

Huyu ni mtu muhimu sana anayeweza kufikisha ujumbe kwa wananchi wa kawaida na kuweza kuwafungua wajitambue na kutambua haki zao

Nimsaada mkubwa sana kwenye elimu ya uraia na sheria, maswali yakilenga "engo" hiyo yatawasaidia wengi halafu hayo ya chama chake atayaeleza kwenye majukwaa ya kisiasa
Wewe ndugu Kiranja wa jamii ni strategist mzuri sana kwa haya maoni yako.
Nami naamini kabisa hivi ndivyo inapaswa kufanywa.

Kongole sana.
 
Tuache ushabiki pembeni, mtangazaji wa ITV alijipanga vyema sana katika kufyatua maswali ya msingi yenye kumuweka kwenye kona Lissu, na Lissu aliweza vizuri sana kukabiliana nayo moja kwa moja bila kukwepa, kuzunguka mbuyu au kulipua lipua.

Hakika ulikuwa mjadala mzuri wenye kusisimua na kuvutia kuufuatilia. Kwa uchache, hoja hizi ziligusiwa.

1. Rushwa ndani ya Chadema

2. Fununu za Lissu kutaka kuondoka CHADEMA ili kuanzisha chama kipya.

3. Lissu kuletewa hongo na mtoto wa rais

4. Misuguano ya viongozi ndani ya Chadema

5. Ruzuku kwa vyama vya siasa

6. Utata wa kisheria katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

7. Dhana ya Chadema kuleta uchochezi.

8. Demokrasia ndani ya vyama vya siasa.

9. Mpango wa Lissu kutaka kugombea urais.

10. Taswira nzima ya uendeshaji wa chaguzi za serikali za mitaa.

View: https://youtu.be/ZL2V3hUw5Hg
 

View: https://www.youtube.com/live/ZL2V3hUw5Hg?si=ucxs0XUFwPi8526W





Ushauri kwa Tundu Lissu, Kama yupo serious anataka urais, asisubirie kuzunguka kwenye majukwaa na vyombo vya habari. Na yeye awe updated kwenye mitandao ya kijamii awe anatoa clip fupi za dakika 1 mpaka 2 anapost mitandao yote ili kuwafikia vijana. Hasa Instagram (Instagram reels, instalive), hhWhatsapp channel, Telegram Channel, Youtube Channel, YouTube shorts, Facebook, TikTok, TikTok video, TikTok live. Awalenge zaidi vijana hasa hali ngumu ya kiuchumi na ukosefu wa ajira. Awe anapost kila siku consistently bila kuchoka.



Erythrocyte

Hii strategy kaitumia Trump, ameingia TikTok hivi karibuni ili kuwafikia vijana wengi. TL anahitaji timu maalumu kufanya haya.
 
Lissu aje na hoja mpya sio Kila siku hizo hizo
Fafanua hoja mpya zikoje, jadili ili nasi tupate kujifunza ili tusije tukawachosha na hoja za kizamani, akili ya binadamu inahifadhi kila kitu tunacho kiona na kusikia ama kujifunza na uwezo wa kutafsiri tulivyo hifadhi kwenye ubongo ndiyo akili zenyewe, nafahamu kwamba binadamu ana akili sana na binadamu huyo huyo ni mvivu wa kufikiri, lakini pia wale ambao tunadhani wana akili kuahirisha kufikiri kwa nafsi a.k.a kujizima data
 
Hamna hoja hapo
Kuelewa hoja ni lazima uwe na uwezo, yaani uwe na akili iliyopevuka. Ukikosa, watu wanaweza kuwa wanaongea mambo ya msingi, lakini kitokana na wewe kukosa uelewa, unaona kama wanapoteza muda.
 
Back
Top Bottom