Mtanzania kufia Ukraine Tanzania iidai Urusi fidia

Yasemekana alikuwa mfungwa. Kama mfungwa alikuwa na uhuru gani wa maamuzi?
Ukiwa mfungwa una pewa options na wewe ndio una takiwa kupima...

Nina miaka saba jela je nitumikie?

Nina ofa ya kwenda vitani, sio jeshini ni vitani kwa miezi sita then nabaki huru na pesa napewa...

Akili ya kawaida hapa una tumika na utakufa tu hautotoka hai/salama, kama sio wao basi vita vita kuondoa

Madili haramu sio ya kuamini, ukikubari kuingia hautotoka na ukitaka kutoka utakwenda na maji tu

Huwezi toka ukaweke siri adharani ni ngumu, utakuja kuwa kama dkt shika (RIP)

Ni bora ukae jela miaka 7 ni salama zaidi, short cut ni long cut... vya bure ni gharama

Amebet ila haikwrnda upande wake, kufaulu kulikuwa ni kudogo sana...
 
Wala hukusikia fidia kwa mauaji ya Kombe? Wala wale wa ajali ya precision air? Au wewe ndiye yule mkuu aliyekuwa akiendelea kuwasiliana na marubani?
Pale kuna bima ambayo inafanya kazi... kama hao wanajeshi bima ipo hivyo basi watanufaika

Umesha wahi kukata bima za hizi nchi za wenzetu ulaya ulaya huko nk?

Kuna manufaa una yapata mengi tu, sio hizi za kutibiwa tu...
 
Duuh aisee na nchi kama zile kutorokaa huwezii yanii...!! Hatari sana apumzike kwa amani sema angekubali kukaa Gerezanii tuu hapo nahisi pia hii haikuwa Option ukute walilazimishwaaa.
 
Huu mchanganuo wako unaupata wapi ndugu? Kwani wewe leseni ya hao Wagner group na Russia unaijua ina masharti gani?

Kwanini unadhani Russia haihusiki kwa lolote sasa ila Wagner, kwani huyu bwana alikuwa kwenye magereza ya nani au waziri Tax unadhani anawasiliana na nani?

Tuacheni ujuaji hapa Russia hawezi kuacha kubeba lawama. Wakuanzia alikuwa huyu balozi wake. Ila sasa Kwa serikali yetu ipi?
 
Pale kuna bima ambayo inafanya kazi... kama hao wanajeshi bima ipo hivyo basi watanufaika

Umesha wahi kukata bima za hizi nchi za wenzetu ulaya ulaya huko nk?

Kuna manufaa una yapata mengi tu, sio hizi za kutibiwa tu...

Tofautisha bima na biashara ya wafungwa au matumizi ya wafungwa vitani Russia.

Mawili hayo hayakubaliki. Russia kama nchi inastahili kuwajibishwa.
 
Mikataba ya ujanja ujanja kama hii unayojaribu kuiangazia inafahamika na imeridhiwa uwepo wake na nchi zetu?

Nikidhani wajibu wa serikali ni pamoja na kuhakikisha ustawi wa watu wake kokote waliko? Kama sivyo watu hawa serikali wenye balozi hadi huko Moscow watakuwa na kazi gani kumbe?

Tuseme unachosema ni sahihi kama wao hawajui na sasa raia wao wanaingizwa mkenge kijanja janja watakuwa ni wa kazi gani kumbe?
 
Kama ume soma vizuri post yangu nimezungumzia street dealer (wauza vipipi mtaani), kwa gram alizoshikwa nazo (4.5 grams) huyo sio big fish.

Nakubaliana na wewe biashara ya madawa yeyote anaweza fanya. Hata ivyo in most cases popote pale duniani including Tanzania wageni wengi wanauza in kilo’s kwa suppliers wa mtaani ambao na wenyewe wana watoto zao ambao wana nunua in grams kusambaza (average age ya wauza vipipi ni 15-25) na wengi elimu yao ndogo.

Sasa it doesn’t make sense mtu anaesomea engineering masters anunue vi grams halafu auze vipipi, maana kuwa supplier (au punda wa kupeleka mzigo Russia kutoka Tanzania) namkatalia.

Kwanini namktalia hiyo nchi ina border na Afghanistan sehemu yenye mashamba makubwa ya madawa na kuingiza Russia wala sio deal. Ninewahi kuangalia documentary bei ya heroin Russia ni amongst the cheapest in the world kama ilivyo Pakistani (wote hao wanatoa Afghan) na huko ata wachanganyi sana maana hizo dawa alizoshikwa nazo ni mixer tu kwenye heroin.

It doesn’t add up kwa mgeni ambae hana ata miaka mitatu kwenye nchi, hana hiyo historia kuuza mtaani, umri umeenda na anasoma masters kuuza dawa za kulevya mtaani Russia.

Huko ulaya waafrika wengi over 30, Pakistan na wengine wanaopata/ingiza in Kilo’s awauzi kitaa vipipi hizo kazi ni za vijana wadogo rarely kufanywa na 30+ ukiwakuta hiyo age group wanauza pipi labda clubs popular za wazungu (tena cocaïne and ecstasy pills only but not heroin) lakini sio kitaa.

Huyo jamaa doesn’t fit the profile ya muuza vipipi ni kesi ya kupikwa.
 
Kwani mustakabali wako unaamuriwa na nchi au wewe binafsi.
Ukienda front utakutana na mawili live or die ni unconditional choice.
Vitani uchagui kufa au kuishi.
Kama mfungwa una uwanja kiasi gani wa kuchagua mustakabala wako? Unajua makwetu hata muda wa kulala, kuamka, kula au hata kumwona daktari si ya kwako? Sembuse shuruti ya kwenda kuponda mawe au kwenda kumlimia afisa magereza?
 
Utopolo kwa lipi wakati mwenyewe alikuwa mfungwa na njaa yake na ujinga wake ndivyo vimemponza. Acheni kutaka vya dezo

Sio vya dezo. Kumtumia mfungwa kwenye Vita hairuhusiwi. Seema to alikuwa mwanachama wa CHADEMA ndio maana inaonekana sio la maana.
 

Samiah ana lipi la maana, zaidi ya kutukuzwa na machawa wake?
 

Hajajiunga kwa hiari. Kuna programme ya kutumia wafungwa kwenye Vita Urusi.
 
Sheria zina kataza kujiunga na jeshi la nchi yoyote... tofauti na majeshi yetu

Kwa namna hiyo, marehemu kwanza ana kosa la kujibu kwa jamhuri

Au tuishitaki familia kwa niaba yake?

Punguza ujuaji. Wafungwa wanatumika na Urusi kwenye Vita na Ukraiane angekataaje?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…