#COVID19 Mtazamo, Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Serikali na Wananchi kuhusu Ugonjwa wa Corona - COVID-19
Hii kauli ya MAKONDA ina maana tofauti na tulivyoipokea,ukiunganisha dots unataona kabisa nchi inaenda Kwenye lockdown ndiyo maana wenye nyumba wanaombwa kupunguza Kodi Kwa kipindi ambacho wananchi watakuwa ndani...
Idadi ya walio victims ni kubwa ukiunganisha na Ile ya serikali tusishangae tukaona na Sisi tunapewa siku 21 za kujifungia ndani

Shida iko sehemu moja mkuu, Wenye nyumba wakipunguza Kodi je na wao Serikali imewapunguzia Kodi? Maana unaweza kupunguza Kodi harafu ukakosa pesa ya kulipa Kodi ya Serikali
 
Nimewaza tu jinsi tulivyoelekezana kitaani kutengeneza sanitaiza, kwa uchumi wetu huu wa hand to mouth inafikirisha sana ,kikubwa tumwombe Mungu tu,

Sent from my Infinix X559C using Tapatalk
 
Ni muda sasa Dunia ikiwa ina pambana na Janga la Corona.

Modelling ya Wanasayansi nchini Kenya inaonesha kufikia mwishoni mwa mwezi April 2020 kuna uwezekano wa Kenya kuwa na Wagonjwa 10,000. US inaonesha by August 2020 marehemu wanaweza kuwa zaidi ya 82,000. Italy kwa sasa vifo ni zaidi ya 12,000.

Nchi zetu za Africa hasa Tanzania zimewekeza sana katika Siasa na kubakia madarakani na siyo Tafiti za kuliendeleza Taifa. Nchi yetu imeshindwa hata kufanya tafiti za kuzuia magonjwa ya Mhogo!

Siyo kwamba wataalam hawapo nchini, laa asha! Wataalum wapo wengi sana.
Tatizo kuu la Tanzania ni vipaumbele. Mbunge wa Tanzania sifa kuu ajue kusoma na kuandika tu, mshahara mnono, Gari zuri, Allowances kibao, mikopo, Ruzuku on spot akistaafu. Na huyu ndie apange sera za Taifa karne ya 21 dhidi ya US, Germany, Russia na China. Kweli au ni mzaha?

Bunge letu ni muda sasa haliidhinishi pesa za Tafiti karibu 90% hata ya Pesa ndogo ilioombwa. Hakuna nchi itaendelea duniani bila Research & Development. Hizi ndizo huzaa Innovation (patent rights) kwa wagunduzi.

Utashangaa Mjinga mmoja ana ropoka ni muda sasa wa Maprofessor, madaktari , Watafiti na Wahadhiri kuja na Tiba ya Corona! Yaani Professa umlipe Tshs 3m. Researchers Tshs 1.5m na Wahadhiri Tshs 1.5M (bila gari, nyumba kapanga, no allowances, nk). Afu Kibaji na Mlinga uwalipe Tshs 15m kwa Mwezi! Tena bila pesa za Tafiti!

Ni muda sasa:

1. Serikali itenge at least 1% ya GDP kwa ajili ya R&D.
2. Serikali ijenge Vyuo/Centers za Utafiti. Ziwepo za Virus, Bacteria, nk. Ziwepo za Mazao, wanyama, nk. Ziwepo Centers za Gunduzi za bidhaa, huduma, maarifa, nk. Siyo kila kukicha CBE New Branch, UDSM New Branch, Chato University, nk.
3. Serikali itume vijana wa Sayansi Takribani 2000 nchi zote duniani kuiba maarifa kila nyanja. Na kuwarudisha baada ya miaka 10. Hatujachelewa tuanze sasa!

Hivi ni nchi gani hii hadi Toothpick tunaagiza China? Hand Sanitizers MSD wanaagiza China? Mask hadi msaada?

Ni muda muafaka sasa kuheshimu wasomi na Sayansi. Ni muda wa wasomi kuongea. Siyo kila Mjinga anaongea kuhusu CORONA.

Tuendelee kujikinga na Corona kwa kufuata ushauri wa Wataalam wa Afya. Corona inaua vibaya!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ninakushauri usimini sana taarifa za Covid19 kutoka Kenya. Viongozi wao wengi ni wapiga dili, wanaweza kuandaa taharuki ili waibie wananchi. Vilevile usiamini DR Congo, Sudan, South Sudan, Ethiopia na nchi nyingi ambako rushwa ni kama jadi yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio maana tunaendelea kuwa masikini hutujiongezi kutafuta tusiyoyajua kwenye uchumi/sayansi....
tunasubiri kukopi tu.
 
Bashite aoneshe mfano kwa kupunguza bei za dawa kwenye Phamacy zake badala ya kutaka wenye nyumba wasitoze. Kodi!!

Bashite inaelekea hajui kuwa wenye nyumba wanalipa kodi za viwanja kwa serikali kila mwaka zinazotokana na kodi za pango; sasa kama anaona ni busara wenye nyumba kusitisha kutoza kodi basi angeshauri na serikali isitishe kodi za viwanja!!!
 
Ili kupata projection ya uhalisia wa athari za Corona nchini kwetu kwa siku za usoni, ninaishauri serekali iwe ina monitor hii kitu inaitwa "Fatality Rate" ambayo inapatikana kwa ku calculate idadi ya vifo gawanya kwa jumla ya maambukizi.

Kwa kigezo hiki, takwimu hadi leo asubuhi zinaonyesha kuwa Tanzania ina "COVID-19 Fatality Rate" kubwa kuliko nchi zote katika EAC block, kama hesabu hizi hapa chini zinavyothibitisha:

Tanzania 1/20 = 5.0%
Kenya 3/110 = 2.7%
Rwanda 0/84 = 0%
Uganda 0/45 = 0%
Burundi 0/3 = 0%

Ili tuweze ku improve kwenye score hii, inabidi tuongeze uwezo (in terms of testing centres & equipment) wa upimaji ili tuwe na sample size kubwa.
 
Tahadhari hii ni ya muhimu sana.

Katika mambo ya kisayansi,data hutoa picha na kutumika kama dira.

Tunakushukuru umekuja na hoja ya msingi sana.
tatizo chini ya awamu hii kila kitu ni siasa siasa siasa.

hakuna kiongozi yoyote chamani na kwenye kabineti (hata maprofesa) anayeushughulisha ubongo wake.
wote naona wamegeuzwa kuwa ni roboti tu huku mwenye rimoti akiwa kule Chato!
 
Ili kupata projection ya uhalisia wa athari za Corona nchini kwetu kwa siku za usoni, ninaishauri serekali iwe ina monitor hii kitu inaitwa "Fatality Rate" ambayo inapatika kwa ku calculate idadi ya vifo gawanya kwa jumla ya maambukizi.

Kwa kigezo hiki, takwimu hadi leo asubuhi zinaonyesha kuwa Tanzania ina "COVID-19 Fatality Rate" kubwa kuliko nchi zote katika EAC block, kama hesabu hizi hapa chini zinavyothibitisha:

Tanzania 1/20 = 5.0%
Kenya 3/110 = 2.7%
Rwanda 0/84 = 0%
Uganda 0/45 = 0%
Burundi 0/3 = 0%

Ili tuweze ku improve kwenye score hii, inabidi tuongeze uwezo (in terms of testing centres & equipment) wa upimaji ili tuwe na sample size kubwa.
Ili iweje?

Anza kujikinga mwenyewe kwanza, kwa kufanya hivyo utakuwa umeikinga na jamii.
 
Kwa kigezo hiki, takwimu hadi leo asubuhi zinaonyesha kuwa Tanzania ina "COVID-19 Fatality Rate" kubwa kuliko nchi zote katika EAC block,
Duh.. !. Mkuu Mbabe, tusutishane.
Imeelezwa vifo vya Corona vinatokana na udhaifu mwingine uliokuwepo mwanzo, Corona ikaja kukusindikiza tuu.
Please please please, tusitishane!.
P
 
Kile kimama ummy kije hapa kijifunze kitu kinachoweza isaidia nchi kupambana na huu ugonjwa sio kinakuja na idadi ya ndoo na cock za maji utadhani kibibi maji
Ummy ndiyo alikuletea Corona?

Anza Kwa kujikinga mwenyewe usitegemee Ummy au mwengine yeyote kuwa anaweza kujikinga na maambukizi kama wewe mwenyewe huchukuwi tahadhari.

Kumbuka tu, kujikinga na tahadhari zako zote hakumaanishi kuwa ikiwa wa kufa kwa Corona basi kuna cha kuzuwia.

Moja ya tahadhari ni kujitayarisha kisaokolojia kuwa corona yupo na unaweza kumzuwia asikupate na akikupata basi hatokuwa na madhara makubwa kwako na kwa jamii inayokuzunguka Kwa kuwa umejiandaa na kujitahadhari nae vya kutosha.
 
Back
Top Bottom