Mtendaji Mkuu wa TANROADS: Tanzania inashika nafasi ya 9 kwa miundombinu ya barabara na madaraja kati ya nchi 54 za Afrika

Yo’ damn right. Tanania imeipiku hata USA kwenye ukuaji wa uchumi. Mwaka jana tulifikia kama 5.2% wakati US waliishia 2.4% hivi.

Sijui nani apigiwe makofi.
 
Wewe unaongea ukiwa hapo kijijini kwenu Nzovwe au umeshafika SA.
Hiyo barabara hapo Mbeya mjini kuanzia Mwanjelwa mpaka Songwe unailinganisha na barabara ipi SA.
Kikwete alisemaga
"Akili ya kuambiwa changanya na yako"
 
Nimecheka kweri kweri
Hawa labda watawapata wajng wa kuwadanganya ila siyo sisi wengine

Ova
 
Hii nchi Kila mtu akipewa mic tu anasema lolote alilokoswa mahala pa kulisemea. Tumewahi ambiwa jeshi letu ni la6 Duniani na watu wakakubali. Sioni ajabu
 
Natumai miaka miwili mitatu ijayo tutapanda sana chati, baada ya barabara zinazoendelea kujengwa sasa kukamilika na tunategemea mpya za PPP ya mabarabara ya Mkumbo.
 
Yaani Rwanda nchi ndogo Haina hata resources nyingi wapo namba 3 sisi 9 lool
 
Barabara zenyewe za maana zinajengwa Dar es salam tu, mikoani ni choka mbaya vibaya mno, high way zote nchini zina hali mbaya vibaya mno
1.Mwanza,,,,, Dsm barabara imejaa viraka balaa
2.Mwanza,,,,,, Mara barabara kama haipo
3.Dsm,,,, mbeya via mikumi hakuna barabara hapo
4.Dsm,,, mtwara hakuna barabara
5.Dsm,, Lindi road ni choka mbaya
6.Mbeya,,,,,,,,,, Songea choka mbaya
7.Songea,,,,,,,, Dar via Lindi barabara imeoza
Achana na highway ingia kwenye majiji ya hii nchi ukitoa Dsm na kidogo Dodoma, majiji yanayobaki hayana barabara na zilizopo zimechokaa mithiri ya ulimi wa mbwa
Ingia mikoa, wilaya na kata zake ni choka mbaya,
My take,
Kwa sasa barabara zote zinazounganisha mikoa hadi mikoa zinahitajika kuwa njia nne(4lanes) huu mtindo wa 2lanes kama umepitwa na wakati pia ajari nyingi zinasababishwa na wembamba wa barabara, Mfano wenzetu wameshaanza kupiga njia nne, mfano Ndola kwenda zambia wanapiga dual carriage, Nairobi kwenda Mombasa 4lanes,
 
Ukute ni kina Jamaa wa Redent wamekuja kivingine ?! πŸ€£πŸ€£πŸ€”
 
Kwani wanakurupuka?
Wanaweza wasiwe wekurupuka,lakin ujue kubusu lwa adui nikwingi saana, sio kila adui lazima atumie style ya akina sanbalati.Tutumie tuu common sense maana sis ndo wenye nchi yao je!?tuna haja ya kuamin sumuliz wakati tunaijua hali halisi!?nkweli tunajilanganisha na SA!?
 
Hii nchi Kila mtu akipewa mic tu anasema lolote alilokoswa mahala pa kulisemea. Tumewahi ambiwa jeshi letu ni la6 Duniani na watu wakakubali. Sioni ajabu
Kuna chawa alipewa mic kwenye harusi akaropoka 'bibi harusi Ni bikra" wakati mule ndani tu watu wawili walishampitia bibi harusi.
Siku hizi chawa wanasifia Hadi wenye mamlaka wanashangaa.
Hapo Mbeya mjini Kuna barabara mbovu inayosababisha ajali baada ya malori kufeli break na kuua watu wengi kila m wezi. Chawa hiyo barabara hawaoni Kama Ni tatizo na ChoiceVariable Yuko hapo hapo mbeya, Ila anaona barabara za SA.
Chawa kiufupi Ni mtu anayewiwa vigumu kuongea kitu halisi. Yeye anataka kuchekesha watu hata msibani ili mradi wenye mamlaka waonekane wamefanya Jambo.
 
Ujinga sana barabara zenyewe hazina ubora wowote.
 
Labda mmeishinda Burundi, Nimefika South Africa huu ni uwongo wa kifala sana, mleta mada itabidi uende south, ungekuwa umefika south usinge post hii aibu
 
Ubora wa barabara kuipita SA kwa Tan road hii hii iliyofilisiwa mpaka mishahara ni tabu, au mimi ndiyo sielewi. Inawezekana kwa hisia ila sio uhalisia. Barabara ya Ramadi Shinyanga kabla haijakabidhiwa ilikuwa mashimo na madimbwi mpaka ikarudiwa karibu nusu ya mradi. Mifano ni mingi nitajaza tu. Tungekuwa wakali kama China kusimamia miradi hakika tungekuwa mbali. Kusifu au kuweka takwimu feki kujipandishia daraja kimataifa ni kukubali kudumaa. Ukizingatia sasa makampuni hawaogopi tena kuharibu miradi maana mwamba alishatoweka. Mbona tunaziona hizi barabara za mashimo au tunaishi hewani.
 

View: https://x.com/JafferMahmud/status/1852660950479823130?t=pQFCkTHQXVEZHa9r5UssVA&s=19
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…