TANZIA Mtoto wa mwanamziki Davido Afariki Dunia akiwa anaogelea

TANZIA Mtoto wa mwanamziki Davido Afariki Dunia akiwa anaogelea

Hao ni devil worshipper,,hiyo ni sadaka kwa miungu yao
Alooh hivi hizi mambo mnazitoaga wapi? Mbona case za watu kufa kwenye ma pool na mito na bahari ni nyingi tu.. kwa nini mtu tajiri mumfikirie hivi?
 
Shukra mkuu lakini usimsemee mtu.
Kila mtu ana siri kubwa saana linapokuja suala la mafanikio na ndo maana utakuta ni twins lakini hawafanani mafanikio kamwe.
Tukutane muda wa matumizi tuu ila mara nyingi huwa hatuulizani juu ya namna tumepata hizo pesa.
Wenye pepsi na coca mpaka leo hawasemi na hawatokaa waseme abadani hiyo formula
Ni kweli mkuu ila ninaowasema ni ndugu wa damu ambao niko nao pamoja na hakuna hata fununu ya kusemwa

Binadamu hawana siri mkuu na hakuna kinachofichwa
We work hard bro [emoji123] na ndumba mwiko kwetu
Sioni sababu ya kwenda kutafuta uchawi kwa masikini asiyeweza kutajirisha wanae au jamaa zake hilo tu huwa linanipa ukakasi

Lakini kila mmoja ana maamuzi yake
Lakini sisi tunafanya biashara pamoja wote
 
Mkuu davido tumeanza kumjua/kumskia miaka kadhaa nyuma kutokana na kazi yake ya usanii na tangu davido ametoka kwenye game hajawahi kushuka

Kwa Tanzania tumekuja kumfahamu vizuri kipindi ambacho ameshirikiana na msanii wetu Diamond mwaka 2014, nadhani ili kujaribu kutrace back history ya usemacho tukianzia hapo sio mbaya, tuanze na mwaka huu

1.Mwaka 2022 amefiwa na Mtoto wake
2.Mwaka 2021 alifiwa na rafiki yake karibu
3.Mwaka 2020 alifiwa na nani wa karibu?
4.Mwaka 2019 alifiwa na nani wa karibu?
5.Mwaka 2018 alifiwa na nani wa karibu?
6.Mwaka 2017 alifiwa na nani wa karibu?
7.Mwaka 2016 alifiwa na nani wa karibu?
8.Mwama 2015 alifiwa na nani wa karibu?

Karibu utujuze mkuu
Uzi wa makafara huu[emoji23]
 
Sio vibaya kuwa navyo
ila hivi vitu swimming pool na bembea ni vitu hatari hasa kwa watoto wadogo
Kuna jamaa alipoteza mtoto baada ya bembea kukatika ikamrusha mtoto kwenye jiwe alipiga paji la uso kimbiza hospital cf hospital 2 days akafariki
Kwa watoto ni vitu vinataka awepo mtu mzima hapo karibu lakini ndo hivyo.
Maji nayo hayakopeshi kama huyamudu
 
Sio vibaya kuwa navyo
ila hivi vitu swimming pool na bembea ni vitu hatari hasa kwa watoto wadogo
Kuna jamaa alipoteza mtoto baada ya bembea kukatika ikamrusha mtoto kwenye jiwe alipiga paji la uso kimbiza hospital cf hospital 2 days akafariki
Kwa watoto ni vitu vinataka awepo mtu mzima hapo karibu lakini ndo hivyo.
Maji nayo hayakopeshi kama huyamudu
Na meza za vioo,hasa coffee table.
 
Ni mawazo yangu na fikra zangu , naomba yaheshimiwe , ni Bora ukadhibitisha uongo wangu alaf na mm nikudhibitishie ukweli wangu .... !!

Sio kila mara unachofikria wewe ukafkr ni sahihi
Ni ngumu sana kuheshimu mawazo ya kipuuzi, sema huyo jamaa alipaswa akupuuze
 
Sio swimming pool.tu hata haya majakuzi ni hatari kwa watoto
Sana, kuna family member aliwahi kupoteza mtoto kutumbukia kwenye ndoo tu mtoto kaingia chooni tu anachezea maji yalikuwa yamejazwa kwenye ndoo. Mimi nakuwa mkali sana kwa mtoto kuingia chooni au kuchezea maji yaliojazwa. Nadhani mzazi yoyote ajifunze kwa watoto wadogo sababu hupendi kusikia yanamtokea mzazi yoyote, Davido maarufu leo tunaongea hapa ila yanatokea sana familia nyingi. Tuwe makini sana
 
Kumbe huyo mwamba alikuwa na mtoto na huyo manzi...

R.I.P mtoto mdogo
 
Kuna mzee nilienda kwake he's rich kutoka Burkina Faso ana swimming pool lake akimaliza kuogelea analifunga na juu anaweka Meza na viti watu wanakunywa na kustarehe na huwezi kujua kama ni indoor swimming pool na hana watoto

Sijui wengine wanafeli wapi huku wakijua wana mtoto mdogo ambae hawawezi kumuangalia kila wakati

Ukisoma Habari zao wanasema mtoto alikuwa humo kwa mda mrefu
Hata hilo kuna siku shetani akiamua anatembea nao tu.

India watu walijiachia darajani wakapiga na ma selfie muda ilipofika daraja likaenda chini watu wakanywa maji.

Hakuna ajuaye dk 2 zijazo kitu gani kitatokea.
 
Hata hilo kuna siku shetani akiamua anatembea nao tu.

India watu walijiachia darajani wakapiga na ma selfie muda ilipofika daraja likaenda chini watu wakanywa maji.

Hakuna ajuaye dk 2 zijazo kitu gani kitatokea.
Mkuu daraja la India lilikuwa halijapata hata cheti cha usalama wake, watu wakajazana kupita kiasi
India ni kama sisi tu waafrika
Na kuhusu ajali zinatokea sana ila tahadhari inasaidia kwa asilimia kubwa

Swimming pool zipo za kufunika mkuu na ni gharama zako tu na ni imara ni kama paa la nyumba yako tu kuanguka kwake ni nadra sana
 
Nashkuru Kwa kunielewesha mkuu, kwahiyo hayo majina ni watu tu ambao wamefariki around Davido tu? Kuna ushahidi wowote wa kuniaminisha kuwa hao ni watu wa karibu sana na Davido kama ilivo Kwa rafiki yake aliefariki mwaka Jana na Mtoto wake?

Kibinadamu tu wewe tangu ukiwa mdogo hadi sasa umepata vifo vya watu wangapi ambao wanakuznguka? Maana neno around ni pana ata kama nitafiwa na jirani yangu huku huyo ni basi ni around me, je Kwa upande wako Ukiwahesabu watafika wangapi hadi Leo hii?

Hivi unajua kama ukiwa na pesa au maarufu unakuwa na connection ya watu wengi sana kuliko mtu fukara?

Mfano Steve Nyerere amezika watu wengi sana ambao wapo kwenye mzunguko wake Kwa sababu yeye ni maarufu na anazungukwa na watu wengi

Mtu ambae amefanikiwa au maarufu anakuwa na marafiki katika kila stage anayopitia, na Kwa sababu anafanikiwa au maarufu mara nyingi mzunguko wake waga haufi tofauti na sie wakina kajamba nani

Vitu vingine ni ujinga tu kudhani kwamba kuna kundi la watu Fulani wao hawatakiwi kufa na kama wakifa basi vifo vyao sio vya halali, kwahiyo davido watu wake wa karibu wanatakiwa kuishi milele?

Ni fikra za kimaskini ndio zinatusumbua na wala sio kingine, na wala sio kwao tu ata kwako IPO siku yatakukuta, we tafuta tu hela na Mungu akusaidie uzipate kuna siku utaitwa FREEMASON na siku ukifiwa na mtu wako wa karibu utaambiwa umtoa kafara

Hesabu za probability zinasema kwamba popote pale penye number kubwa ya watu au vitu basi kuna % kubwa za matukio kutokea kuliko pale ambapo kuna number ndogo

Kwahiyo ukizungukwa na kundi kubwa la watu jua kwamba utashiriki sana kwenye Sherehe za harusi na utashiriki sana kwenye misiba, ila kama huna watu basi kuna matukio wewe utakuwa unayaskia tu Kwa watu
Inahitaji akili huru kukuelewa.

Mtu akifungamanishwa na ushabiki hawezi kukubaliana na wewe
 
Davido alivyopewa taarifa alichana nguo yake na kutaka kukimbilia barabarani.
Yaani alichanganyikiwa kabisa.
 
Inahitaji akili huru kukuelewa.

Mtu akifungamanishwa na ushabiki hawezi kukubaliana na wewe
Jamii yetu imejaa wajinga sana, utadhani huku mitaani kwetu watu hawafi, ila Vifo vyetu sie ni vya halali ila Vifo vya watu maarufu na wenye pesa ni Kafara

Sasa sijui ni kwenye maandiko gani tumeambiwa watu wenye hela wanastahili kuishi milele na hawatakiwi kufiwa na watu wanaowazunguka

Huyu aliekazana Leo kusema mtoto ametolewa kafara ndio huyo huyo atakuja kuitwa freemason endapo kupambana kwake kutakutana na bahati na kufanikiwa kuwa mwenye pesa

Huyu huyu anaesema wenzeie wanatoa kafara akipata pesa atakuja kufiwa na ataambiwa katoa kafara na wale wale watu aliokuwa nao katika kundi lao la wajinga

Hii shida inaletwa na umaskini wa maendeleo pamoja na umaskini wa Akili, Leo hii Diamond kutokana na umaarufu wake na anavozungukwa na watu wengi akisema ashiriki kwenye kila msiba basi almost kila mwezi atakuwa anaonekana msibani na hizi story za kutoa watu kafara zitaanza kumuandama

Tofauti ya mastaa wengine na Davido ni moja tu, Davido kakuta pesa chafu kwao tangu anazaliwa kwahiyo hana ulimbukeni wa pesa na hiyo hali inamfanya kuwa na marafiki wale wale miaka yote tofauti na sie ambao mafanikio tunayapatia ukubwani ni kila kukicha kubadili marafiki na kusahau wapi tulitokea

Kama kupata utajiri ni kuuwa watu basi wengi sana wangekuwa matajiri maana Kwa roho zetu za kibongo zilivo kumuuwa mtu uwe tajiri ni dakika sifuri tu, ila kwakuwa sio kweli tunaishia tu kuwasema watu waliotoboa
 
Hakuna kitu sipendi kwenye nyumba kama swimming pool nikienda nyumba yoyote na watoto kuna swimming pool nakosa amani kabisa nimeshuhudia kwa macho mtoto akitaka kuzama wa miaka 5 japo tulimuwahi kumtoa lakini kila nikikumbuka lile tukio nakosa amani kabisa ndio maana najisikia vibaya kwa family yoyote waliyowahi kupoteza mtu kwenye hali hii. Mimi nyumba ya swimming kama kituo cha police, family nyingi zimepitia hii hali ni hatari sana. Nawashauri wazazi msikubali watoto zenu kuingia humo mimi hata kama najuwa mtoto anajuwa kuogelea lakini akiingia katika maji sina amani. RIP
Kuna baharia mmoja namjuwa nyumbani kwake kunduchi kulikuwa na pool
Sasa kuna wakati lile pool juu walilifunika na plastic kubwa kuzuia uchafu nk
Sasa kuna siku mtoto mdogo alidumbukia mule lile fuko likamfungafunga,mtoto alikata moto pale pale
Mpaka leo lile bwawa jamaa kageuza dampo la taka tu

Ova
 
Watu tisa ndani ya nyumba na bado mtoto anazama kwenye swimming pool,haki hichi kifo kina walakini.Ngoja tusubiri hiyo report ya kifo kama itawekwa hadharani na Polisi.Ila hamna watu wanaongoza kwa kutoa makafara kama Wanaijeria nimefika kwao nimeishi nao kwa mda aisee ni balaa zito.Nashangaa hawa wanaobisha kwa ufupi tu jaribuni kugoogle voodoo mjionee hii ni mojawapo ya ndumba maarufu.Tufiakwa
 
Back
Top Bottom