Mtoto wako amewahi kukuaibisha mbele za watu?

Mtoto wako amewahi kukuaibisha mbele za watu?

Kuna dada mmoja rafiki yangu,alinitembelea home, siku hiyo nilikua nipo na kabinti kangu , kana miaka mitatu .

Tukawa tupo mezani wote watatu wakati wa chakula cha mchana .

Baada ya kumaliza kula binti wa watu kabakiza chakula , akadai kashiba.

Kabinti kangu kakaropoka" icho chakula unamwachia nan? , unadhani baba yangu anapesa za mchezo" .

Duh niliona aibu sna ,sijui ayo maneno kayatolea wapi.
Ila hii tabia ya mtu anajipakulia chakula mwenyewe halafu eti anakula nusu au robo anaacha huwa ni tabia mbaya sana.
 
Mwanangu amekulia sehemu ambayo hakuna Waislamu hajawahi ona mtu akiwa amevaa yale sijui majuba au hijabu manguo meusi ya kufunika uso na mwili mzima.

Nilienda naye Morogoro kwa wazazi, asubuhi akakutana na mama wa kiislam Jirani yetu amevaa yale manguo. Naona mtoto kaja ndani spidi analia na kumuita Mama yake. Mamaaaaa kuna jini linakuja. Kidogo tunaona yule mama anakuja nyumbani. Dogo yupo chumbani amejifunika blanket. Ikabidi tuombe msamaha kwa yule mama maana alisikia na akawa amekasirika. Tukaanza muelekeza mtoto kwani alikuwa mtoto wa miaka 4 kipindi hiko.
Una malezi ya hovyo.... Halafu kwa nini nguo za wenzio unaita manguo?? Wewe na mwanao wote sawa tuu..
 
Tuliwahi kumtembelea jirani, tukaletewa soda hatujakaa sawa mtoto wake akaja na likikombe likubwa anaomba soda, ukimuwekea anaipiga tarumbeta anaomba tena, sio mtoto wangu ila nilihisi aibu.
Ulitakiwa umiminie nusu huyo mtoto, na akimaliza muongezee tena iishe yote ili kupeleka ujumbe kwa mwenyeji wako kuhusu malezi...
 
Mwanangu amekulia sehemu ambayo hakuna Waislamu hajawahi ona mtu akiwa amevaa yale sijui majuba au hijabu manguo meusi ya kufunika uso na mwili mzima.

Nilienda naye Morogoro kwa wazazi, asubuhi akakutana na mama wa kiislam Jirani yetu amevaa yale manguo. Naona mtoto kaja ndani spidi analia na kumuita Mama yake. Mamaaaaa kuna jini linakuja. Kidogo tunaona yule mama anakuja nyumbani. Dogo yupo chumbani amejifunika blanket. Ikabidi tuombe msamaha kwa yule mama maana alisikia na akawa amekasirika. Tukaanza muelekeza mtoto kwani alikuwa mtoto wa miaka 4 kipindi hiko.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kitoto changu nilikipeleka hospital kuchek malaria sasa baada yakutoka hospital tukakaa bar flan jiran na hospital kumnunulia chips akawa anagonga pale mara siakaamza kulilia bia , eti nataka biaaa ,ninunulie bia nikawa nazuga pale muhudumu naomba malta huyu dogo malta anaitaga bia dogo likaanza sitaki hio nataka pombee kulikuza na wazee pale wakawa wananiona kama mpinga kristo halafu Chakushangaza sijawah kula gambe mbele yake na mama yake hanywi na kilikua na miaka miwili dah
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Niliwahi kukaribishwa chakula kwenye familia fulani ya kishua nikapikiwa ugali na nyama ya mchuzi. Nikaona ili nifaidi vizuri lile chuzi nikawa kila nikimega tonge natumia dole gumba langu kupiga lile shimo katikati ya donge la ugali ili kuchota ule mchuzi. Kumbe kuna dogo wao wa miaka mitatu hajawahi kuona kile kitu. Basi aliponiona kakimbia kwenda jikoni akiita mama mamaa njoo uone mama yake kaja dining anamuulizia nione nini. Dogo karopoka mgeni anatengeneza kwa kutumia ugali kichoteo cha mchuzi. Niliona aibu acha tu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nilijisikia vibaya pale mwanangu aliposema baba hapa tunakula mpaka tunashiba, hivi naweza kubaki hapa mpaka shule ifunguliwe mwakani? Alikuwa anayasema haya kwa jirani yetu tulipokwenda kutoa pole ya msiba.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] aibu hii
 
[QUOTE="

Na hiyo tabia ya kuropokaropoka watoto wwnu wanaiga kwenu wazazi na walezi,wafundisheni watoto kuwa na khaba si kila wanachokiona/kusikia ni lazima waongee,

i,[/QUOTE]

Ni kweli.Mimi nakumbuka siku moja nilienda na mtoto wangu kumsalimia rafiki yangu.Tulipofika tulikaa muda mrefu bila kukaribishwa kitu chochote kama wageni.
Mimi mtoto wangu alishazoea nyumbani wakija wageni lazima tuwanunulie soda.Sasa yeye alivyokaa muda mrefu bila kuletewa soda,alinyanyuka alipokuwa amekaa (maana alikaa mbali na mimi) akanifuata akaniuliza,mbona hatupewi soda? Nilicheka sana.Ninachotaka kusema hapa hakuropoka na tabia hiyo amekua nayo maana sasa ni mtu mzima 22 years lakini kama kuna mgeni akitaka kukwambia kitu lazima akusogelee aongee kwa sauti ndogo.
 
Watoto ni wazuri sana .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Sure..

Comedy zao burudani sana.

Kuna mwamba wangu mmoja yeye anakimbiza vifaranga anavinyonga, yaani kuku akitotoa pale home inabidi wawekwe mbali nae.

Kosa umfunge kuku kamba asweze kukimbia utamkuta yeye anamchezea chezea shingo, nataka nije kumfundisha kuchinja kuku sabab naona ndo anapoelekea
 
Wakuu kwema?

Kama tunavyojua watoto walivyo, hawana aibu, wanafanya kile wanajisikia kwa wakati huo, japokuwa kuna wengine wananya kukukomesha. Wanajua mama/baba huwa hataki kuninunulia kitu fulani mkifika supermarket anapiga kelele duka zima wanasikia analilia mdoli😂😂.

Ama unajua mtoto wako huwa hali kitu fulani, unakaribishwa umpe mtoo unasema mwananguhuwa halagi hivi, picha linaanza mwanai alaililia na kula kitu!

Vipi mdau, ni tukio gani mtoto wako aliwahi kukuambisha mbele za watu?
Miaka kama mitatu hv imepita kabinti kangu kalikua ndo kana miaka mi5 na wa kiume ana miaka 2

Sasa nipo sebulen nmekaa wao wanaangalia tamthilia fln hv na mm nazuga tu naangalia wala akili haipo kwenye TV, ikafika scene waigizaji wanataka kukiss kale ka kike kakamkimbilia mwenzake mdg wa kiume kakamziba macho kwa kiganja. Nilicheka sana hio siku
 
Kuna katoto changu kana miaka miwili kanapenda pombe balaa.kakiipatia kanaigonga kinoma hata kisungura.Sasa hivi huwa nakaficha kasiione.
😂😂😂😂😂😂
Duh we jamaa wewe, so na wewe unagonga kisungura
 
Kuna katoto changu kana miaka miwili kanapenda pombe balaa.kakiipatia kanaigonga kinoma hata kisungura.Sasa hivi huwa nakaficha kasiione.
Mimi wa kwangu alikuwa na miaka kama minne, so nilikuwa nikienda washroom anaipiga pombe yote kwenye grasi then anarudishia so mimi nikirudi sijui kama kaipiga ya kwenye grasi. Hawa watoto hawa
 
Mimi wa kwangu alikuwa na miaka kama minne, so nilikuwa nikienda washroom anaipiga pombe yote kwenye grasi then anarudishia so mimi nikirudi sijui kama kaipiga ya kwenye grasi. Hawa watoto hawa
Mwanao alikua na haki zote kuipiga pombe Yako sababu pombe haikai kwenye grasi
 
Back
Top Bottom