Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Kwanini uwaze kupunguza instead of training.., kama mwalimu ambae tayari anaujuzi ni rahisi kumtrain kuliko useme upunguze uajiri wapya,
 
Muhimu zaidi ni walimu. Kuwa mwalimu IST ni lazima uwe na masters hata mwalimu wa PE (mazoezi ya viungo na michezo)... Hata ukijenga maghorofa ukaacha walimu wale wale haitosaidia.
 
Hao hao walimu unaowadharau na jizo grade zao ndio waliokufikisha hapo ulipo,
Na ndo maana hata thinking capacity yako ni finyu mno
 
Ndio hupelekwa mafunzo Kuna mtu namfahamu mwalimu wakawaida alikuwa international alipelekwa mafunzoni, na wengine hutoka hata udsm alikuwa international kikubwa ni mtaala unasemaje na kazi inafanyika. Kuna mwingine naye katoka udsm Yuko international ya Ada milion arobaini wakawaida tu. So shida sio waalimu ni mtaala unasemaje?
 
Shida kubwa ni walimu hayo mengine mapambo tu. Tanzania ni Anglophone. Tunatumia Kiingereza kufundishia na tunataka wanafunzi wazungumze Kiingereza kwa ufasaha. Utajifunzaje Kiingereza kutoka kwa mwalimu ambaye yeye hawezi. Labda mitaala unayosema iwe ya Kiswahili sasa. Kikubwa ni mwalimu, hata chini ya mwembe kama una mwalimu mzuri, utakuwa mzuru tu.
 
Bado unazungumza mambo ya kusoma kujibu paper, International school watoto wana fundishwa kuelewa Dunia na vitu kama Exposure
Which you can still get at the University level...
 
Hivi inamaana hatuwezi kubadilisha mitaala ya hizi shule zetu ziwe kama za kimataifa. Najiuliza tu. Kwani hatuwezi au ni nini shida
Mifumo yetu ndio shida na kuibadilisha kwa hali hii ya tanganyika yetu kisiwa cha amani itachukua muda sana labda miaka 100+ mbele
 
Mimi naona mitaala ya kufundishia maana walimu waliotoka vyuo vyetu nao hufundisha hzo shule wakutoka nje ni wachache Sana,
 
Walimu Watanzania wanaofundisha international school wanaitwa assistant teachers. Ni wasaidizi wa walimu ambao wengi ni wageni. Kazi yao kubwa siyo kufundisha ni kuwasaidia walimu. Kama watoto bado ni wadogo sana, kuwasaidia kwenda msalani nk. Kama umesoma shule za sekondari za serikali kama mimi utakuwa unajua ninachokisema. Walimu wangu wa sekondari walikuwa hawawezi kuzungumza sentensi 2 za Kiingereza kwa ufasaha bila ya kuweka Kiswahili. Hata chuo kikuu ni hivyo hivyo. Sijui wewe unaongea walimu gani hao? Tofautisha pia international schools na English medium schools. Tusije kuwa tunaongelea vitu viwili tofauti.
Mimi naona mitaala ya kufundishia maana walimu waliotoka vyuo vyetu nao hufundisha hzo shule wakutoka nje ni wachache Sana,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…