Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Nimesema mamako kwa vile nina uhakika mamako unamfahamu. Mimi haunifahamu. Kwa hiyo kusema mimi ni ngwini ni usanii tu.
Mama yangu kaingiaje hapa, huwezi ukawa umesoma PCM kwa design hii ya uandishi..
 
Which you can still get at the University level...
Never.
University zetu hawana tofauti na sekondari, mentality yao ni ile ile, ufaulu. Ndio maana wanafunzi wanasoma wawe na GPA kubwa basi.

Yaani usome elimu ya msingi, sekondari jumla miaka 13 halafu uje kupata exposure university kwa miaka 3? Kua serious mkuu.

Lakini kuna mahala nimeona umeseam ulisoma shule za "sirikali", nimekuelewa.
 
Mtu ukiwa na hela ya kueleweka ama kama unataka kuwekeza kweli kwa watoto wako, wasomeshe international schools au shule zenye mitaala ya kimataifa.

Hizi shule zenye mitaala ya kimataifa zinawajenga watoto kwenye analytical skills, reasoning, logic, creativity, competence na mambo kama hayo.

Ukikutana na mtoto wa darasa la 6 wa hizi shule, reasoning yake ama analytical skills zake ni sawa na kijana wa form six wa necta schools.

Shule hizi hazilengi kuona mtoto anapata nini au maksi gani darasani bali kuibua talents nyingine alizonazo mtoto sio hizi za necta ambazo zimejikita kwenye ufaulu tu wa mwanafunzi.

Ukitaka kuwekeza kwenye elimu ya kweli kwa mwanao na kama uwezo upo peleka mwanao shule zenye mitaala ya kimataifa.
Hapo ume-exaggerate sana, sijajua kama ulikua unanogesha ngano yako au lah. Ni kweli hizo shule ni nzuri hasa hasa kumpa mtoto exposure na kujifunza lugha zingine kwa ufasaha kama kiingereza au kifaransa.

Ila ukija ktk uwezo wa utendaji na ufanisi sio kweli hao wanatuzidi ila wao kwa asilimia kubwa wanaonekana wako smart ni kwa sababu wanakuwa wanajifunza kwa lugha za kigeni tangu awali. Kama ukichanganya mtoto aliyesoma shule msingi Bunge na shule ya kimataifa ya Tanganyika uwapime uwezo wao kwa lugha ya kiswahili utahamaki ukweli wa mambo, ni ngumu sana mtoto anayesoma lugha ya kigeni kwa kugusa gusa awe sawa kwa kujiamini na mtu aliyesoma shule ya kimataifa kwa lugha ya kigeni.

Binafsi nimesoma shule za umma kuanzia darasa la kwanza mpaka chuo kikuu, nimebahatika kufanya kazi na watu waliosoma shule za kimataifa kama Tanganyika na Moshi pia vyuo vikuu wamesoma Ivy league (Harvard, Princeton, Brown) ila sijawahi kuona utofauti mkubwa baina yao na sisi. Jaribu kwenda ofisi kama World bank country office (Mirambo 50) au auditing firms (Kpmg, delloitte, EY, PwC) au oil & gas companies huwezi kuona utofauti baina yao na sisi.

Changamoto kubwa sana niliyoigundua asilimia kubwa ya watu ambao waliosoma shule za umma kuanzia chini mpaka vyuo vikuu ni kupata shida kuimudu lugha ya kigeni kwa ufasaha hii hupunguza hali ya kujiamini kwa kiasi kikubwa sana. Labda serikali wajaribu kuboresha mitaala ya elimu lugha ya kiingereza ianze kutumia kuanzia chini yaani shule ya msingi na sio kuanzia sekondari. Watumie mfumo unaotumika kwa shule za msingi kama Bunge, Mlimani na Olimpio.
 
Kwa sababu wao ni international level.

Huwezi waona au wasikia bongo
International ni wapi mzee
Ninavyojua unavyoongelea international ni kama wasafi wale ni international na wengine maarufu Sana yani ndani na nje hata Kama mtu yuko nje tutamjua kwa umaarufu wake kupitia huko alipo
 
Talent zipi nazani unazungumzia za Ku rap, Hahaaa tupe talent tofauti na za kuimba.

International watoto wanapata Exposure kubwa sana
Talent ni nini
Na wewe ndiyo utupe mifano ya hao ma international scholars waliokuzwa vipaji vyao mashuleni kwao tuwaone kitaifa na wawe wakubwa kimataifa sio kusifia tu hizo shule nadhani wengi wao wanaishia ama kusimamia biashara za familia zao au kupewa nyazifa kwenye serikali ambao labda wazazi wao ni viongozi na wengine kuajiriwa nje huko ambayo inawakuta hata waliosoma shule za kata na ku scholarship

Lakini katika mpira, mziki, uigizaji, ngumi,dancerz na vipaji vingine vingi ni akina sisisi tu na Kama ukimkuta huko
Aliyesoma international kwenye familia huwenda wanamuona Kama kapotea vile
 
Umetoka nje ya Mada.

Talent ni natural born thing wala hufundishwi na hakihitaji shule. Ukianza kufundishwa hiyo sio Talent bali unaweza kugundua Talent yako kupitia elimu na shule.

it is something you have never been taught. It comes out of the blue na ukiulizwa how did you know that , the honesty answer would be I don’t Know.
Ni sawa lakini inasemwa katika huu uzi kwamba international school inakuza vipaji tofauti na shule zetu hizi
hatuzumguzii kufundisha vipaji vipaji havifundishwi wote tunajua hilo ndiyo tukaomba mfano wa watu ambao kusoma international kumewasaidia kukuza talent zao na wao wakaenda kimataifa
 
Usinikumbushe mapito niliyo pitia.
Ile naanza na form five tu mwalimu wa kemia mzungu,mmarekani na Mjapani,hesabu ni mchina wa kimarekani na Mhindi,nageukia Fizikia nakutana na mzee Ngui sijui kabila gani masikini muda wote ni kufoka tu. Halelujaaa DS hii hapa na mzee Mwangoka anafundisha kwa kinyakyusa na stori zake za Tukuyu na kufukuzwa chuo kikuu kwa migomo...
Ikawa mwanzo mwisho ni kumeza tu....
Teh teh teh we jamaa umenichekesha sana
 
Mtu ukiwa na hela ya kueleweka ama kama unataka kuwekeza kweli kwa watoto wako, wasomeshe international schools au shule zenye mitaala ya kimataifa.

Hizi shule zenye mitaala ya kimataifa zinawajenga watoto kwenye analytical skills, reasoning, logic, creativity, competence na mambo kama hayo.

Ukikutana na mtoto wa darasa la 6 wa hizi shule, reasoning yake ama analytical skills zake ni sawa na kijana wa form six wa necta schools.

Shule hizi hazilengi kuona mtoto anapata nini au maksi gani darasani bali kuibua talents nyingine alizonazo mtoto sio hizi za necta ambazo zimejikita kwenye ufaulu tu wa mwanafunzi.

Ukitaka kuwekeza kwenye elimu ya kweli kwa mwanao na kama uwezo upo peleka mwanao shule zenye mitaala ya kimataifa.
Umeongea ukweli,ila ni wachache sana wataelewa unachomaanisha...
 
Hivi inamaana hatuwezi kubadilisha mitaala ya hizi shule zetu ziwe kama za kimataifa. Najiuliza tu. Kwani hatuwezi au ni nini shida
Inawezekana ingawa litachukua miaka mingi sana,elimu hiyo ilikuwepo tena kwenye shule za kawaida sana,ikafa miaka ya 80 mwishoni,ikabakia ile ya mwenye uwezo mkubwa wa kukariri au kuweza kupitia mitihani mingi ya miaka ya nyuma ndio mwenye akili...
 
Wazazi tusake hela jamani watoto wetu wakasome kwenye shule bora, mwezi wa 7 nilikutana na binti mmoja hapa Johannesburg akiwa anajiandaa kurudi Tanzania kwa sababu ya restrictions za covid-19. Huyu bunti amesoma primary na secondary Aga Khan international school ambapo wanatumia mtaala wa Cambridge. Baada ya hapo akaja kujiunga Stellenbosch University iko cape town (1 ya top 3 universities hapa SA).

Anakotoka hela ipo sio kidogo na hapo chuo ada kwa mwaka ni around 20m za kitanzania plus accommodation na extras nyingine. Binti anajiamini huku akijua anachokifanya,anachukua degree ya Mambo kilimo na economics na akimaliza mwakani ana job offer Canada.

Naendelea kuzisaka hela mwanangu at least apite njia kama ile, makapuku tunanyongwa kielimu ndiyo maana wanasiasa hawapeleki watoto zao shule za kawaida za serikali. Pesa tu ya kugharamia elimu bora ndiyo ticket ya kumfanya mwanao aje akae kwenye high table ya maisha.
 
Mtu ukiwa na hela ya kueleweka ama kama unataka kuwekeza kweli kwa watoto wako, wasomeshe international schools au shule zenye mitaala ya kimataifa.

Hizi shule zenye mitaala ya kimataifa zinawajenga watoto kwenye analytical skills, reasoning, logic, creativity, competence na mambo kama hayo.

Ukikutana na mtoto wa darasa la 6 wa hizi shule, reasoning yake ama analytical skills zake ni sawa na kijana wa form six wa necta schools.

Shule hizi hazilengi kuona mtoto anapata nini au maksi gani darasani bali kuibua talents nyingine alizonazo mtoto sio hizi za necta ambazo zimejikita kwenye ufaulu tu wa mwanafunzi.

Ukitaka kuwekeza kwenye elimu ya kweli kwa mwanao na kama uwezo upo peleka mwanao shule zenye mitaala ya kimataifa.
Ungeanza walau kuzilist Shule chache kwa manufaa ya wadau ili wajipange
 
Hawa watoto hawasomi kwa kutoboa, kukariri maswali ya physics sijui hesabu za mody physics.

Hawa wanajifunza elimu ya kuwasaidia kukabiliana na mazingira yanayowazunguka ambalo ndio dhumuni kuu la elimu.

Hizi za necta eti unakuta hadi wanazuia wazazi kwenda kumuona mtoto eti utamharibia concentration, sasa hiyo elimu ama ujinga, kwamba mzazi ukitembelea mtoto utamvuruga asifanye vizuri? Ujinga ujinga mtupu kwenye elimu ya necta.
Shida ingine ni ada ya hizi Shule
 
Hivi inamaana hatuwezi kubadilisha mitaala ya hizi shule zetu ziwe kama za kimataifa. Najiuliza tu. Kwani hatuwezi au ni nini shida
Mtaala kuubadilisha inawezekana ila changamoto ni:
1.Wanaopaswa kuubadilisha wanajua wabadilishe nini? Wako na hiyo elimu?
2. Gharama za kuuendesha huo mtaala kama: vifaa vya kufundishia, ziara za ndani na nje ya nchi za kimasomo wazazi watazimudu?
3. Serikali inaouwezo wa kuweka miundo mbinu n.k?
4. Wazazi wana uwezo wa kugharamia ada na michango mingine? Iwapo sasa hakuna ada ila uniforms zinawashinda wazazi mfano viatu n.k?
 
Nadhani serikali ijaribu kubuni mfumo mzuri utakaojengea wanafunzi ufahamu na uelewa wa kusoma na kuweza kutatua changamoto za mazingira yetu. Sio kusoma ma theory tu yaliyo solve nchi za ulaya na kusahau mazingira yetu na changamoto zake.
Pia sikuhizi primary hesabu ni mutliple choice, huko si ndo kufanya watoto wawe wavivu.
Hili linahitaji mchakato mzito haswaaaa
 
Hivi inamaana hatuwezi kubadilisha mitaala ya hizi shule zetu ziwe kama za kimataifa. Najiuliza tu. Kwani hatuwezi au ni nini shida
Mitaala ya kimataifa iendane na miundombinu ya kitaifa
 
Sisi tabaka la kati tukijivuta saaana basi angalau watoto wetu wanasoma hizi saint saint nani sijui, tunaona angalau kuliko ile elimu bure.... hizo za kimataifa ni chache na gharama sana.

Mchawi pesa.
 
Mkuu kuna world scholars kibao ambao hawajakanyaga hizo international schools na wanaheshimika kwenye field zao. Nafikiri hizo shule zimeanzishwa purposely kwa ajili ya watoto wa mabalozi kwenye nchi husika, hakuna jipya...
Hao ni outliers tu na huwezi kutoa conclusion based on them. Asilimia kubwa humu tumesoma shule hizi duni ila ukweli ni watoto wa huko shule zenye mitaala ya mabeberu wapo vizuri. Huku kwetu ni karama ya Mungu tu unakuta mtu yupo very articulated
 
Back
Top Bottom