Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

Mtu ukiwa na pesa, somesha mwanao international schools, achana na hizi exam based schools or education

huo uwezo wataupimaje na kukuamini wakupe hiyo kazi?kama hizi shule za english medium tu wanaaminika walimu wa kutoka kenya na uganda
Utaifa wa mwalimu si kigezo bali uwezo wake. Kumbuka gharama kubwa za ada ndizo hipelekea mishahara minono.
 
Si kweli. Tunaona changamoto sana kwa hawa waliosoma Kayumba na kubahatika kufika level za kimataifa kwenye kazi za kimataifa.
-
Wengine walifanikiwa kufika level hizo kwa Connection tu. Kwa mfano nafanya kazi na Mtanzania mwenzangu kwenye International Organizational nchini Nambia, huyu Mdada amepata kazi kwenye hiyo Organization kwa sababu tu Ndugu yake ni Balozi wa Namibia.
-
Imemlazimu kufanya short course kuanzia Lugha mpaka Communications Skills na nyinginezo kwa sababu yeye mwenyewe anajionea aibu.
-
Hizo International school zinawajenga watoto vizuri sana hata kwa KUFIKIRI na kujiamini na mzazi ukiwa msimamizi mzuri wa mtoto wako atafika mbali sana na atakuwa very presentable kwa fadhila za International Schools.
-
It is very serious issue sisi tulio kwenye International Organization tunaona mengi na tunaona changamoto ya Mfumo wetu wa elimu na Africa kwa Ujumla.
-
Ukiona Kayumba yupo kwenye hizi Organization na anafanya vyema ujue huyo kaji mix sana na anapenda kujifunza vitu mbalimbali au ana exposure ya maisha.
-
Kwanza sisi wabongo hata kuongea hatujui, sijui kwa nini ! Sio English wala Kiswahili, hatujui kuongea na wala hatufikirii tunachongea.
-
Ukitaka kuona hilo angalia wasanii wetu wanavyojibu maswali, angalia wachezaji mpira wakihojiwa akiwemo Samatha, zero kabisa, njoo kwenye ngazi za viongozi, zero kabisa, sio Kiswahili wala English.
-
Msanii anaejua kuongea vyema Kiswahili na English ni Sepetu na Vanesi na Kiongozi ni Mkapa na January tu.
-
Shida ipo sana eneo hili na ndio maana once it comes about International Interviews , yaani WATZD huwa ni wa mwisho na hapo unakuta mtu ana vyeti vizuri na pass Marks zake.
Kama Trump mwenyewe hawezi kujieleza lakini ndo Rais wa taifa kubwa duniani,tafuta pesa mzee mengine yote yatakuja yenyewe..ushawahi kumsikia mzee Bakhresa akiongea? au marehemu Mengi? hawawezi kuongea sentensi tatu ukazielewa direct bila ya kudhania walichomaanisha.
 
Mkuu umewaza kwa mapana sana ni kitu ambacho hata mimi nimekifikiria.
Talent ni nini
Na wewe ndiyo utupe mifano ya hao ma international scholars waliokuzwa vipaji vyao mashuleni kwao tuwaone kitaifa na wawe wakubwa kimataifa sio kusifia tu hizo shule nadhani wengi wao wanaishia ama kusimamia biashara za familia zao au kupewa nyazifa kwenye serikali ambao labda wazazi wao ni viongozi na wengine kuajiriwa nje huko ambayo inawakuta hata waliosoma shule za kata na ku scholarship

Lakini katika mpira, mziki, uigizaji, ngumi,dancerz na vipaji vingine vingi ni akina sisisi tu na Kama ukimkuta huko
Aliyesoma international kwenye familia huwenda wanamuona Kama kapotea vile
 
Kuwa mjumbe wa Bodi wa Shule kumenisaidia kufahamu mengi juu ya hizi shule za serikali.Hizi shule za serikali siku hizi zimejaa siasa na mihemuko. Syllabus haifuatwi,kuna wataalamu wa elimu wanaojiita wakuu wa shule na maafsa elimu wa halmashauri kutwa kubuni vitu vya ajabu ajabu mara;

Wanafunzi wanakatazwa kusoma masomo mengine wasome Civics na Kiswahili eti wapate 'D' mbili za cheti.

Kuna baadhi wanaambiwa waache kabisa kusoma somo la hisabati. Wengine wanakatazwa walimu wasifundishe badala yake wawape wanafunzi mitihani na wasolve! Jumlisha mitihani ya inter- school, pre - mock,Mock,pre NECTA ,Terminal,Mid-term nk. Kunawafanya walimu wasifundishe kabisaa.

Maagizo ya mara kwa mara toka kwa wabunifu wa wilayani na ubunifu wa mkuu wa Shule yasiyofuata na kuzingatia syllabus sio tu yanapunguza maana ya mtaala pia malengo yaliyokusudiwa.
Sylabus enyewe majanga. Hata wangefuata hiyo sylabus nukta kwa nukta bado haiondoi kukaririshwa! Hao maafisa elimu na waalimu ni product ya sylabus ya kukaririsha unategemea nini? Hadi Universities Hali ni hiyo hiyo.
 
Mbona wengine tumesoma hizi hizi shule za sirikali, tena shule ya msingi kijijini kwa babu kuongea kilugha mwanzo mwisho lakini tumefanikiwa kupata scholorship kusoma Masters na PhD kwenye international universities ambazo zipo kwenye world ranking ya 10 bora, what happened?
If it's true then that was a fools errand.
 
Ukitaka kuanza safari, agana na nyonga.. Mtoto ili atoke nursery mpaka amalize chuo kikuu, ana miaka kama 20 ya kusoma.
Je wewe mzazi una uhakika kipato chako kitakuwa mwake kwa miaka hii 20? Kama huna uhakika, mpeleke shule za umma.. Come rain, come sun, mtoto anakuwa na uhakika wa masomo.
Acha uoga.

Kati ya watoto 100 wanaosoma huko uma ni 10 tu wanaotoka na elimu stahiki..na hao ni akili zao binafsi, 90 huudhuria tu kuitika jina na kuhesabu namba.
 
Unajifariji tu. Scholarship unapata lakini haina maana kuwa ubora wako uko kama wa graduate wa IST. Walimu wanafundisha hapo chuo kikuu lakini hawezi kujieleza kwa Kiingereza.
Kuna mkuu mmoja alikuwa anatoa maagizo kwa wachina, Aisee kile kiingereza chake anatakiwa aoongee mtoto wa la nne B.
 
Mtu ukiwa na hela ya kueleweka ama kama unataka kuwekeza kweli kwa watoto wako, wasomeshe international schools au shule zenye mitaala ya kimataifa.

Hizi shule zenye mitaala ya kimataifa zinawajenga watoto kwenye analytical skills, reasoning, logic, creativity, competence na mambo kama hayo.

Ukikutana na mtoto wa darasa la 6 wa hizi shule, reasoning yake ama analytical skills zake ni sawa na kijana wa form six wa necta schools.

Shule hizi hazilengi kuona mtoto anapata nini au maksi gani darasani bali kuibua talents nyingine alizonazo mtoto sio hizi za necta ambazo zimejikita kwenye ufaulu tu wa mwanafunzi.

Ukitaka kuwekeza kwenye elimu ya kweli kwa mwanao na kama uwezo upo peleka mwanao shule zenye mitaala ya kimataifa.
Unazungumziaje shule za seminary ambazo wanatumia necta? Kama lengo ni kuwa international mkataa kwao ni mtumwa. Upo wapi uzalendo?

Hata niwe bilionea mwanangu atasoma seminary - uru seminary, st James, maua seminary these are the best seminary schools in Tanzania.
Mbali na passmark kupata selection tu ni ishu.
 
Kuwa mjumbe wa Bodi wa Shule kumenisaidia kufahamu mengi juu ya hizi shule za serikali.Hizi shule za serikali siku hizi zimejaa siasa na mihemuko. Syllabus haifuatwi,kuna wataalamu wa elimu wanaojiita wakuu wa shule na maafsa elimu wa halmashauri kutwa kubuni vitu vya ajabu ajabu mara;

Wanafunzi wanakatazwa kusoma masomo mengine wasome Civics na Kiswahili eti wapate 'D' mbili za cheti.

Kuna baadhi wanaambiwa waache kabisa kusoma somo la hisabati. Wengine wanakatazwa walimu wasifundishe badala yake wawape wanafunzi mitihani na wasolve! Jumlisha mitihani ya inter- school, pre - mock,Mock,pre NECTA ,Terminal,Mid-term nk. Kunawafanya walimu wasifundishe kabisaa.

Maagizo ya mara kwa mara toka kwa wabunifu wa wilayani na ubunifu wa mkuu wa Shule yasiyofuata na kuzingatia syllabus sio tu yanapunguza maana ya mtaala pia malengo yaliyokusudiwa.
Mfumo mzima wa elimu nchini ni wa ajabu.
Haufai kufuatwa
 
Mkuu kuna world scholars kibao ambao hawajakanyaga hizo international schools na wanaheshimika kwenye field zao. Nafikiri hizo shule zimeanzishwa purposely kwa ajili ya watoto wa mabalozi kwenye nchi husika, hakuna jipya...
Unadhani.....
 
Mbona wengine tumesoma hizi hizi shule za sirikali, tena shule ya msingi kijijini kwa babu kuongea kilugha mwanzo mwisho lakini tumefanikiwa kupata scholorship kusoma Masters na PhD kwenye international universities ambazo zipo kwenye world ranking ya 10 bora, what happened?
Nina mashaka kama umesoma. Ungekuwa umesoma na kuelimika ungegundua mwanzisha mada hakusema kuwa wote wanaosoma huko kajamba nani wanaishia pabaya ila ameongelea zaidi wenye chance kubwa.
 
Mkuu umewaza kwa mapana sana ni kitu ambacho hata mimi nimekifikiria.
Nnachoamini hapo kama wewe ni masikini na ukapata pesa nyingi msomeshe mwanao international school kwa sababu mwanao atakuwa mtu mwenye connection kwa sababu marafiki zake wengi ni kutoka familia zenye pesa kwahiyo suala la ajira litakuwa ni uhakika
 
Hahaa...mtoto akiwa bright huhitaji kumpeleka mashule yenye majina makubwa sijui ada mil. 10. Mwache hapo hapo ila habari yake wataipata tu kwenye matokeo ya kitaifa. Mimi ilinigharimu niliposoma O-level private ambapo kila kipindi mwalimu anaingia, shida ikaja A-level mwalimu humwoni na material unajitafutia. Kwenye mazingira kama hayo ndo utamwona mwanafunzi ambaye ni kichwa.....
Hapa nimehakikisha kabisa wewe ni wale waliosoma shule za kukariri. Focus yako iko kwenye kupass mitihani wakati mwenzako anaongelea kitu kingine kabisa. Shule nyingi za Bongo zimejikita kwenye kukaririsha wanafunzi ili wa pass mtihani kwa gharama yoyote lakini unakuta hawana upeo wa kuchambua mambo.... kama wewe!
 
Hahaa...mtoto akiwa bright huhitaji kumpeleka mashule yenye majina makubwa sijui ada mil. 10. Mwache hapo hapo ila habari yake wataipata tu kwenye matokeo ya kitaifa. Mimi ilinigharimu niliposoma O-level private ambapo kila kipindi mwalimu anaingia, shida ikaja A-level mwalimu humwoni na material unajitafutia. Kwenye mazingira kama hayo ndo utamwona mwanafunzi ambaye ni kichwa.....
Kichwa kwenye kumeza au? Kichwa gani kwa maana huyo kichwa atatoka na one kali halafu atakutana chuo kimoja na yule aliyepata division three na wote watapata mkopo na wote watasoma chuo kwenye carriers zao na wote watamaliza na kupata cheti.
Sasa hapa najiuliza faida ya kuwa kichwa ni nini hasa na je? Kuna faida ganinya kuwa na special schools?
 
Nnachoamini hapo kama wewe ni masikini na ukapata pesa nyingi msomeshe mwanao international school kwa sababu mwanao atakuwa mtu mwenye connection kwa sababu marafiki zake wengi ni kutoka familia zenye pesa kwahiyo suala la ajira litakuwa ni uhakika
Sasa kinachosahaulika hapo pesa zangu ndio zitakuwa zimemsaidia sio hizo shule.
Kwani kuna wale watoto wa kiarabu wanaomiliki biashara ya mabus na magorofa pale kariakoo pia walisoma kwenye shule hizo?
 
Hatujui kuongea wala kuandika Kiswahili na kiingereza kwa ufasaha. Huu nao ni ukweli usiopingika. Au wazee wetu hawakuwekeza katika lishe bora, hence vizazi vyetu vimekuwa below average.

Je, hao waliosoma International schools wamelisaidia vipi taifa? Wametoa mchango gani tofauti na hawa kina sisi St. Kayumba? Maana tusiangalie elimu ya darasani wakati taifa bado lipo nyuma sana na tuna mchanganyiko wa wasomi wa shule mbovu na za kimataifa.
 
Back
Top Bottom