Mwarabu mlokole
JF-Expert Member
- Jul 8, 2023
- 231
- 386
Kweli aisee hizi ni nyama za wenye hela tu kapuku ukikutwa unakula ni jeraKilo 32 eti thamani yake milioni 7,3..........
Yaani kila kilo sh laki mbili na zaidi.
Uongo uliokubuhu huu.
Pole yake, tulimwambia hizi nyama za porini ni kwaajili ya wazungu na waarabu yeye hakusikia.
Daah.... Ndo basi tena
Gharama ya hizo kilo 30 inalingana na gharama za kumtunza huyo mfungwa kwa miaka 30?Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, imemhukumu Mbogo Tinda (45), Mkazi wa Kijiji cha Ihoanza Tarafa ya Malangali, wilayani hapa, kutumia kifungo cha miaka 20 gerezani, baada ya kumtia hatiani kwa makosa mawili.
Makosa hayo ni lile la kukutwa na nyara za Serikali (nyama ya Tandala ā Kudu, yenye uzito wa kilo 32), lakini pia kujihusisha nyara za Serikali bila kuwa na kibali.
Hukumu hiyo imetolewa jana September 4, 2023; na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Benedict Nkomola, ambapo imedaiwa mshtakiwa huyo alipatikana na nyama ya Tandala yenye thamani ya Sh7, 859, 136 milioni.
Akisoma shtaka hilo, hakimu huyo amesema mnamo August 26, 2023 katika Kijiji cha Idope, Kata ya Ihoanza, wilayani hapa, mshtakiwa huyo alikutwa na nyama ya Tandala ambayo alikuwa anaiuza bila kuwa na uhalali wa kufanya shughuli hiyo.
Inadaiwa kuwa mshtakiwa alinunua na kuuza nyama ya Tandala kilo 32, yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha ambayo ni mali Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwa na vibali au leseni ya kuuza nyama hiyo.
Pia hakimu huyo amesema kosa hilo ni kinyume na kifungu namba 86(1) (2) (a) na kifungu (3) cha sheria ya uhifadhi wa wanyapori sura 283 rejeo la Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 14 Jedwari la kwanza la vifungu vya 57(1), na 60 (1) (2) vya sheria ya makosa ya uhujumu uchumi na makosa ya kupangwa, sura 200 rejeo la Mwaka 2022.
Aidha katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 11, 2023; mshtakiwa alikiri kutenda makosa hayo, ndipo mahakama ikamtia hatiani na kumhukumu kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kwanza na pili ambapo adhabu hizo zitaenda sambamba.
Awali akizungumza kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ahmad Magenda, aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa.
"Niombe mahakama yako itoe adhabu kali kwa washtakiwa wote ambao wanafanya makosa kama haya ya kuhujumu wanyapori ambao ni vivutio kwa watalii, sanjari na kukuza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla," amesema Magenda.
MWANANCHI
Kama hamjuiKilo 32 eti thamani yake milioni 7,3..........
Yaani kila kilo sh laki mbili na zaidi.
Uongo uliokubuhu huu.
Pole yake, tulimwambia hizi nyama za porini ni kwaajili ya wazungu na waarabu yeye hakusikia.
Daah.... Ndo basi tena
Zamani Babu zetu waliwala mno Hawa,.Kwa msaada wa Wikipedia View attachment 2739669
Kwani mkikutwa na watu wa misitu au game hata na njiwa unajua ukatili ambao Huwa wanawafanyia watu?Hii serikali ina sheria za kipuuzi sana. Wageni kutoka nje mfano Waarabu, na watawala ndiyo wanajiona wana haki ya kula wanyama wa porini.
Ila sisi wanyonge tukijaribu tu kuua hao wanyama kwa ajili ya kitoweo, tunaishia kufungwa vifungo virefu magerezani. Huu ni upumbavu.
Kumbuka unahesabiwa ni jangiliMaisha magumu ila tupambane mishe zinginešŖšŖ
jamaa mtaani alipigwa miaka 20 hv hv kisa nyama pori, familia inahangaika shemeji analiwa ovyo
Na sheria za kulinda wanyamapori ni KaliSoma habari vizuri,huyu hakuwa na kibali,hao wengine unaowataja itakuwa wana vibali,huyu angekuwa amekata kibali yasingemfika haya.Mnatakiwa muwafahamishe wananchi,kuwa ukifanya biashara ya wanyama pori uwe na kibali,na ukakate kibali na leseni, mahali fulani,ni sawa na dereva aendeshe gari bila leseni,au mfanyabiashara asiwe na leseni,au ufanyekazi ya udaktari bila leseni,uwe na duka la dawa bila leseni,wategemea nini,kama sio kuvunja sheria.
Ni uonevu tu.
Jina jingine ni kudu, ni jamii ya swala wakubwa anamzidi kidogo nyamela.Picha ya tandala tafadhali, aliyemfungisha mtu miaka 20.
Kweli wewe ni Mpemba, nyama pori tunauwa kwa risasi na haipimwi popote, usiongee kitu usichokijuwa.Huyo aliyeuza nyama ya porini,bila kibali,ndio umtetee,ukisikia kibali,ni pamoja na nyama kupimwa na daktari wa wanyama,kua alikufa kibudu,na alikufa na maradhi gani,na pia kama kachinjwa,je hakuwa na maradhi ya kuambukiza binadamu?
Wewe unamtetea muuaji,je kama nyama ina maradhi,na yakaambukiza binadamu,wewe na wenzako wengine,utalaumu serekali,kwa kutoweka sheria ya vibali,baada ya kukaguliwa nyama kabla ya kuuuzwa na kufanywa kitoeo.
Nyama pori haipimwi wala wanyamapori hawapigwi sindano za chanjo, usidanganywe.Tumia akili.Nyama zikiuzwa holela,na kusmbukiza maradhi binadamu,wewe na wenzako,ndio mtakuwa wa kwanza kulaumu serekali.Nyama lazima ipimwe,mnyama kafa ana maradhi ya kuambukiza,au siyo.
Ni kosa kubwa kula nyama anayokula sultan (dubeiš¤£)Zamani Babu zetu waliwala mno Hawa,.
Dunia ya Leo imebadikika sana.
Mimi Niko hapa kunyoosha ukweli, nothing but the truth.Mdogo wake rostam mnakumbuka ile kesi yake ya nyara za taifa mwaka 2019?
- Sheria ya Trophy valuation, inasema hivi kwenye kuthaminisha thamani ya mnyama pori, tunaangalia thamani ile ya jumla ya mnyama, kwa mfano ukikutwa na nyama hata kilo1 ya nyama ya mnyamapori mwenye thamani ya shilingi Milioni 10, hatuangalii thamani ya kilo Moja ya huyo mnyamapori tunaangalia thamani ya mnyama wote.Kilo 32 eti thamani yake milioni 7,3..........
Yaani kila kilo sh laki mbili na zaidi.
Uongo uliokubuhu huu.
Pole yake, tulimwambia hizi nyama za porini ni kwaajili ya wazungu na waarabu yeye hakusikia.
Daah.... Ndo basi tena
Kina mzee mmnoja aliwahi niambia kua tz mwisho wa kula vyakuka vizur ilikua ni enzi za Nyerere, sahii vitu org vinapelekwa hukooooNi kosa kubwa kula nyama anayokula sultan (dubeiš¤£)
Ndugu yetu yamemkuta. Loh
Rule no one of the game, "Never get caught"Si ya haki. Nafikiri magereza kwa nchi hii ni kwa ajili ya masikini. Ni double standards!. Ni ushamba.
Kweli mkuu kama yule Mchina juzikati hapo alipigwa Fine ya Laki mbili tu. Huu ni uonevu.Huu ni uonezi kabisa,hukumu hizi mbona zinatolewa Kwa wazawa tu,kila siku wageni wanakamatwa na hizo nyara ila wanalipa faini,yaani Mwananchi mwenye mali yake anahukumiwa kiasi hiki..... Mahakimu na Mahakama huu Muhimili lazima ujitafakari sana katika kutekeleza haki
Isije kua kuna njamaa za kumuondoa Jamaa mtaani ili waliobaki wajimilikishe vya kwake! Dunia ina mengi sana hii!!Ila kama Kuna namna kwenye hii kesi