Mufindi: Afungwa Jela miaka 20 kwa kukutwa na kilo 32 za nyama ya Tandala

Mufindi: Afungwa Jela miaka 20 kwa kukutwa na kilo 32 za nyama ya Tandala

Kilo 32 eti thamani yake milioni 7,3..........
Yaani kila kilo sh laki mbili na zaidi.
Uongo uliokubuhu huu.
Pole yake, tulimwambia hizi nyama za porini ni kwaajili ya wazungu na waarabu yeye hakusikia.
Daah.... Ndo basi tena
 
Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, imemhukumu Mbogo Tinda (45), Mkazi wa Kijiji cha Ihoanza Tarafa ya Malangali, wilayani hapa, kutumia kifungo cha miaka 20 gerezani, baada ya kumtia hatiani kwa makosa mawili.

Makosa hayo ni lile la kukutwa na nyara za Serikali (nyama ya Tandala – Kudu, yenye uzito wa kilo 32), lakini pia kujihusisha nyara za Serikali bila kuwa na kibali.

Hukumu hiyo imetolewa jana September 4, 2023; na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Benedict Nkomola, ambapo imedaiwa mshtakiwa huyo alipatikana na nyama ya Tandala yenye thamani ya Sh7, 859, 136 milioni.

Akisoma shtaka hilo, hakimu huyo amesema mnamo August 26, 2023 katika Kijiji cha Idope, Kata ya Ihoanza, wilayani hapa, mshtakiwa huyo alikutwa na nyama ya Tandala ambayo alikuwa anaiuza bila kuwa na uhalali wa kufanya shughuli hiyo.

Inadaiwa kuwa mshtakiwa alinunua na kuuza nyama ya Tandala kilo 32, yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha ambayo ni mali Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwa na vibali au leseni ya kuuza nyama hiyo.

Pia hakimu huyo amesema kosa hilo ni kinyume na kifungu namba 86(1) (2) (a) na kifungu (3) cha sheria ya uhifadhi wa wanyapori sura 283 rejeo la Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 14 Jedwari la kwanza la vifungu vya 57(1), na 60 (1) (2) vya sheria ya makosa ya uhujumu uchumi na makosa ya kupangwa, sura 200 rejeo la Mwaka 2022.

Aidha katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 11, 2023; mshtakiwa alikiri kutenda makosa hayo, ndipo mahakama ikamtia hatiani na kumhukumu kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kwanza na pili ambapo adhabu hizo zitaenda sambamba.

Awali akizungumza kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ahmad Magenda, aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa.

"Niombe mahakama yako itoe adhabu kali kwa washtakiwa wote ambao wanafanya makosa kama haya ya kuhujumu wanyapori ambao ni vivutio kwa watalii, sanjari na kukuza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla," amesema Magenda.

MWANANCHI
Gharama ya hizo kilo 30 inalingana na gharama za kumtunza huyo mfungwa kwa miaka 30?
 
Kilo 32 eti thamani yake milioni 7,3..........
Yaani kila kilo sh laki mbili na zaidi.
Uongo uliokubuhu huu.
Pole yake, tulimwambia hizi nyama za porini ni kwaajili ya wazungu na waarabu yeye hakusikia.
Daah.... Ndo basi tena
Kama hamjui
Kesi hizi husimamiwa na wale jamaa wenye kinga ya kesi za mauaji.....

Najua mnanifuatilia. Siogopi kusema


Acheni kutumia risasi kuua nzi huku mafisi mkiwazawadia mabucha
 
Hii serikali ina sheria za kipuuzi sana. Wageni kutoka nje mfano Waarabu, na watawala ndiyo wanajiona wana haki ya kula wanyama wa porini.

Ila sisi wanyonge tukijaribu tu kuua hao wanyama kwa ajili ya kitoweo, tunaishia kufungwa vifungo virefu magerezani. Huu ni upumbavu.
Kwani mkikutwa na watu wa misitu au game hata na njiwa unajua ukatili ambao Huwa wanawafanyia watu?
 
Soma habari vizuri,huyu hakuwa na kibali,hao wengine unaowataja itakuwa wana vibali,huyu angekuwa amekata kibali yasingemfika haya.Mnatakiwa muwafahamishe wananchi,kuwa ukifanya biashara ya wanyama pori uwe na kibali,na ukakate kibali na leseni, mahali fulani,ni sawa na dereva aendeshe gari bila leseni,au mfanyabiashara asiwe na leseni,au ufanyekazi ya udaktari bila leseni,uwe na duka la dawa bila leseni,wategemea nini,kama sio kuvunja sheria.
Na sheria za kulinda wanyamapori ni Kali
 
Huyo aliyeuza nyama ya porini,bila kibali,ndio umtetee,ukisikia kibali,ni pamoja na nyama kupimwa na daktari wa wanyama,kua alikufa kibudu,na alikufa na maradhi gani,na pia kama kachinjwa,je hakuwa na maradhi ya kuambukiza binadamu?
Wewe unamtetea muuaji,je kama nyama ina maradhi,na yakaambukiza binadamu,wewe na wenzako wengine,utalaumu serekali,kwa kutoweka sheria ya vibali,baada ya kukaguliwa nyama kabla ya kuuuzwa na kufanywa kitoeo.
Kweli wewe ni Mpemba, nyama pori tunauwa kwa risasi na haipimwi popote, usiongee kitu usichokijuwa.

Nimefanya professional hunting na kampuni na nimefanya local hunting tunajiorganise wenyewe.

Hapa naandika kitu ambacho nakijuwa fika na nimekiishi tangu nikiwa Mdogo.

Wanyama wanaopimwa ni nyama za machinjioni kwenye mifugo ya kufugwa, mambo ya wildlife tuachie wenyewe hujui lolote.
 
Tumia akili.Nyama zikiuzwa holela,na kusmbukiza maradhi binadamu,wewe na wenzako,ndio mtakuwa wa kwanza kulaumu serekali.Nyama lazima ipimwe,mnyama kafa ana maradhi ya kuambukiza,au siyo.
Nyama pori haipimwi wala wanyamapori hawapigwi sindano za chanjo, usidanganywe.
 
Mdogo wake rostam mnakumbuka ile kesi yake ya nyara za taifa mwaka 2019?
Mimi Niko hapa kunyoosha ukweli, nothing but the truth.

Rostam Ana kampuni ya uwindaji inaitwa miombo Safari ipo Masaki, kwa kampuni za uwindaji store zao huwezi kukosa nyala na bunduki nyingi tu na vyote ni halali.

Zile zilikuwa ni siasa chafu za Magufuli kupora pesa wafanyabiashara hakuna kingine.

Siwapendi kabisa hawa kina Rostam lakini ukweli halisi ndio huu lazima tuuweke wazi.
 
Kilo 32 eti thamani yake milioni 7,3..........
Yaani kila kilo sh laki mbili na zaidi.
Uongo uliokubuhu huu.
Pole yake, tulimwambia hizi nyama za porini ni kwaajili ya wazungu na waarabu yeye hakusikia.
Daah.... Ndo basi tena
- Sheria ya Trophy valuation, inasema hivi kwenye kuthaminisha thamani ya mnyama pori, tunaangalia thamani ile ya jumla ya mnyama, kwa mfano ukikutwa na nyama hata kilo1 ya nyama ya mnyamapori mwenye thamani ya shilingi Milioni 10, hatuangalii thamani ya kilo Moja ya huyo mnyamapori tunaangalia thamani ya mnyama wote.
 
Ni kosa kubwa kula nyama anayokula sultan (dubei🤣)

Ndugu yetu yamemkuta. Loh
Kina mzee mmnoja aliwahi niambia kua tz mwisho wa kula vyakuka vizur ilikua ni enzi za Nyerere, sahii vitu org vinapelekwa hukoooo
 
Huu ni uonezi kabisa,hukumu hizi mbona zinatolewa Kwa wazawa tu,kila siku wageni wanakamatwa na hizo nyara ila wanalipa faini,yaani Mwananchi mwenye mali yake anahukumiwa kiasi hiki..... Mahakimu na Mahakama huu Muhimili lazima ujitafakari sana katika kutekeleza haki
Kweli mkuu kama yule Mchina juzikati hapo alipigwa Fine ya Laki mbili tu. Huu ni uonevu.
 
Back
Top Bottom