Mume amemtuma mtoto wetu wa miaka mitano dukani usiku ni sahihi?

Alikaa baada ya mtoto kurudi na kumwambia baba ake naogopa .....inshort hakukua na emergency ya kaisi hicho ya kufanya mtoto atumwe muda huo.
Still alijali asingekaa hata baada ya mtoto kusema anaogopa hilo lingekuwa tatizo lingine lakini kama alitoka nje kumsubiri mwanae bado ni Baba bora hiyo alikupa wewe kama lesson.

Sasa ni usiku muamshe hapo m'boreshe ndoa yenu kesho weekend mkishinda wote hapo home muelekezane taratibu za kuishi lengo ni mfike pamoja,next time usiwe mwepesi wa ku-panic kuwe na emergency kusiwe na emergency always ili jambo liharibike au liimarishwe lazima kuwe na sababu na sababu zenyewe ndiyo kama hizi.
 
Sawa Ahsante
 
Kwani duka hatua ngapi toka kwenu? Huyo Mama Mkwe anarudi lini kwake? Umezunguka sana ila ishu hapo ni mama mkwe.
 
Hiki ni kitu cha kuleta mtandaoni kweli? Wa kwangu ana miaka 6 namtuma kwa mangi anaenda na mdogo wake wa miaka miwili. Freah tu bila tatzo....

Wasiwasi wako ulikua ni nini?
 
Nmejaribu kumzuia nikashindwa akaishia kuniambia nikae kimya
Na kingempata kitu mwanao ungesema alikuzuia? Mtoto wa miaka mitano bila kujali jinsia hatakiwa kuwa nje peke yake giza linapoingia. Na ni wajibu wako kuhakikisha usalama wake bila kujali baba yake ana maoni gani. Inaelekea baba na mama yake wana matatizo yao, ungeenda tu mwenyewe.

Amandla...

Amandla...
 
Kumtuma mtoto usiku inaweza isiwe sawa kutegemeana na mazingira mnayoishi na umbali kati ya duka lilipo na nyumbani.

Ninachoona ni huenda ulipotoa wazo la kwamba ataenda dada au wewe mwenyewe maneno hayo yalitamkwa mtoto akiwepo pamoja na bibi yake huenda na mumeo akisikia. Sasa tafsiri ya moja kwa moja kwa mtoto ni kuwa unampenda na wengine hawampendi na atakuona wewe ndio kila kitu. Na huenda mumeo alihisi unataka kumtenga mtoto na bibi yake kwa kuwa mtoto atamuona bibi hamjali mwishowe bond inakufa.

Kuwa na tahadhari na mumeo maana inaonekana bond iliyopo na mama yake ni kubwa kama ambavyo bond ya mtoto wako wa kiume inakuwa kubwa kadri siku zinavyosonga. Hili swala usipolipa jicho la pili ndoa yako inaweza kufa hata kwa kitu kidogo.

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Watoto wengi hubakwa sababu ya kutumwa dukani usi ruhusu tena mwanao aka tumwa mpaka pale angalau ana miaka 13.
 


Kuna issue 2:

1. Mama Mkwe yupo, hayo mazingira kum challenge mme, kuwa nayo makini especially kwenye issue ambayo Mama mkwe is involved.

2. Kwa nini wewe usinge voluntary amua kwenda instead ya mtoto au kumsindikiza mtoto, halafu bada ya hiyo issue ukateta na Mume wako?

3. Kwa nini Dada wa kazi aende dukan saa 3 mwenyewe? Ninaye Dada wa kazi ana miaka 19, ikifika saa 1 lazima asindikizwe dukani.

Maoni yangu:

- Kwa sababu mume kaona ume mu attack mbele ya Mama ya kum challenge mbele ya Mama yake, akaona akaze, ila amefanya jambo la kipumbavu sana.

- Kwa nini mtoto amwambie Baba yake amuangalie, asikuambie wewe au kwa nini wewe usingeenda na Mama? Inaonekana wewe ni mvivu ana sio kimbilio la mtoto.

Ushauri:

  • Usimtume Dada mtoto wa watu usiku.
  • Usi challenge mme wako akiwa na Mama yake.
  • Jitoe kwa hiyari kusaidia jambo kama unaona mtoto si salama.

Bado nawaza:

Inawezekanaje Baba na Mama wapo ndani, mtoto wa miaka 5 aende dukani, Mume ni mshenzy na wewe ni mtu wa hovyo maana ungeweza inuka ukaenda.

Acha mdomo, the fact kwamba umeleta hii issue humu, ina maana bado unq ligi nayo, acha ligi na Mume, hili ni jambo dogo sana na kueleweshana.

Kuwa makini na huyo Mama Mkwe, hilo jibu lake la sawa sio zuri na ndo limeleta reaction yote hiyo, sasa na mume alivyo wa hovyo akataka mwonyesha Mama yeye ana msimamo
 
Wewe na mkwe wako mnampa changamoto huyo baba mwenzetu.

Ligi zenu anaepata changamoto ni mwanaume aanze kuchagua upande sio jambo sahihi kabisa.

Tumieni busara,

Ila jamaa ikabidi afunike kombe mwanaharam apite kwa kichagua upande wa mama.

Wakulaumiwa hapa ni wewe na mama mkwe wako.

Kama duka lipo karibu ungeacha aende na ukaenda muangalizia badala ya kumzuia, ungeepusha shari na pande zote zingepata ushindi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…