Mume amfikisha mahakamani mkewe kwa kupeleka mshahara wake kanisani

Hii ni kwa Wanawake wa kiafrika au siyo,ndio maana wanazeeka bila kuolewa.
Mkisha kuwa pamoja kila kitu ni ku-share equally.
Wanawake wakizungu Wana akili nyingi Sana yani haita tokea Mwanamke wakizungu apokee mshaara awe ana peleke wote kanisani bila kumshirikisha mumewe h

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Principe ni ileile..asikuzidi elimu kipato na umri..
Unazingatiaje vitu hivyo ili uoe,? ukishakua mwanaume hakuna la kukushinda kuli handle shida mwanzo mnaanza vibaya kwenye mahusiano na mwanaume inakuletea shida maisha yako yote
 
Mfano huyo mwanaume angekuwa hahudumii familia anapeleka pesa zake kwa vimada na starehe halafu huyo mwanamke analalamika , je ungeongea haya uliyosema juu ya huyu mwanaume?!

Swala hapa ni kutokuwajibika na kuwa serious na familia. Mwanamke anaonekana yupo very responsible na familia yake. Ukitazama hata kiumri mwanamke ndie mkubwa alitakiwa kuwa na upeo mkubwa zaidi kushinda mwanaume ila ndio kwanza ameamua kuwa mwehu.
 
Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake. Ila mwanamke mpumbavu, huibomoa.
Maisha ya ndoa siku zote ni ya kutegemeana. Na ili muishi maisha mazuri ya furaha, upendo, amani na mshikamano; ni lazima muwe na serikali moja tu.

Mwanaume anatakiwa kuwa Rais, lakini pia Waziri wa Ulinzi wa familia, na mama anatakiwa kuwa Waziri Mkuu, na pia Waziri wa Fedha na Mhasibu Mkuu katika familia.
Kama wote mnafanya kazi, mnatakiwa kila baada ya mshahara kutoka, mnatakiwa kuuweka mezani, na kuupangia bajeti ya mwezi mzima.

Hizi mambo za kuficha ATM card, kupeleka fungu la 10 kwa Mitume na Manabii feki! Hazikubaliki hata kidogo. Hivyo naomba niegemee tu upande wa Afande. Hata ningekuwa mimi, huyo mwanamke ningemuacha.
 
Unazingatiaje vitu hivyo ili uoe,? ukishakua mwanaume hakuna la kukushinda kuli handle shida mwanzo mnaanza vibaya kwenye mahusiano na mwanaume inakuletea shida maisha yako yote

Ku handle mambo kwa wkt huu sio manguvu na ma ukali kama zamani..uchumi,elimu na uwe matured kuliko mke mengine ya ziada
 
Nyie. Mnamlaumu bure jamaa..hamjajua walokole wanawake walivoshikiwa vichwa vyao na wachungaj
Aaah hawa viumbe wanakera aisee wakiingia kwenye haya makanisa hata kama ni mwaminifu unaweza hisi kuna mtu anamkunja huko church.
 
Unaongea vitu gani sijui.... Unakosea sana.
 
Kwahiyo ni haki kwa mwanamke kutumia pesa yake hovyo hovyo nje ya familia na hana msaada wowote kwa mume wake na familia hiyo kazi ni ya muhimu gani sasa si aweke matako yake nyumbani atakuwa na faida kwa familia kulikoni kupoteza muda hapo na kujaza nafasi kwenye nyumba kumbe empty set kabisa.
 
Naona wanawake mnakomaa,lakini undani wa maisha yao hamuufahamu. Kama mwanamke hataki fedha zake zihudumie familia aache kazi. Lakini kutoka asubuhi kwenda kupoteza muda huna unachochangia ni upimbi. Aache kazi ili pesa yake isitumike.
Eti bana. Si aache tu hiyo kazi sasa ni ya muhimu gani sasa.
 
Huo ukristo kama ndivyo unavofundisha hauna maana yoyote sasa, Mke ni msaidizi nasio danga kwamba anakula tu pesa zangu zake haziguswi.

Pia kama upendo ni kuwa mtumwa kwa mwanamke ambae kipato chake hakisaidii familia yake yeye mwenyewe huo upendo hauna Maana.
 
Huyo bwana hazimtoshi
Yakikupata wewe
Sheria inasemaje, wanawake kwan huwa mnadai haki ipi??? Haki ya mwanamke anayo mwanamme? je haki ya mwanamme anayo nani??

Kinachompeleka mwanamme mahakamani ni kuona pesa ya familia (sio ya mwanamke) inapelekwa kanisani kiholela.

Nasema mwanaume yule sio mjinga, anatetea ustawi wa familia yake, kama mwanamke anaona ATM ndio mme basi aende imuowe hiyo ATM.
 
Nikisoma comments za Wanaume wenzangu nimegundua kwa nini wengi wanakufa mapema,kwa sababu ya kujikweza-mwisho anafeli na presha juu.

Kama Mkeo anafanya kazi-lazima msaidiane katika kulea familia,lazima kusaidiana majukumu.
Mwanaume huweza kutegemea hela ya mwanamke kuendesha familia.

Mwanaume wewe ndie baba na kichwa cha familia, ukishategemea hela ya mwanamke ikusapoti kuendesha familia unapoteza haki yako ya kua kichwa cha familia.

Mwanaume siku zote lazima ujue kua hela ya mwanamke ni yake sio ya kwako. Akitoa kusaidia sawa na asipotoa usiumie, hilo ni jukumu lako.

Mwanaume unategemeaje mshahara wa mke wako?
 
Itakua hapeleki kanisa atakua anapeleka sehemu ingine, mume kushtaki sio jambo dogo
Inashangaza mkuu , mume kutaka ATM ni kwa namna ya kumsaidia huyo mwanamke na matumizi ya hovyo.

Fikiria mnaishi na mtu ndani kwa maisha ya sasa yeye hela yake ni kupeleka huko kwenye makanisa ya kiroho harafu huku ndani hafanyi chochote...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…