Mume amfikisha mahakamani mkewe kwa kupeleka mshahara wake kanisani

Mume amfikisha mahakamani mkewe kwa kupeleka mshahara wake kanisani

Kwa hiyo mkewe akiwa period anavuna damu amuombe mumewe aliyempa ATM akatoe pesa ampe akanunue pedi ?
Au chupi imechakaa akaombe mpenzi naomba Ukatotoe pesa kwenye ATM yangu chupi imechakaa

Huyo mwanaume mjinga
Chupi ikiisha mwanaume ananunua,pedi mwanaume ananunua,ila pesa za mwanamke,zinapelekwa kanisani,is it fair?
 
Wanaume wa JF huwa wanajifaragua kwenye mada za aina hii ili waonekane Gentlemen.😁!

Tena ikitokea kuna kabinti anakafukuzia huko PM ndiyo balaa.

Haya madhehebu ya kilokole yasikie tu,hata kama isingekuwa suala la mshahara nina uhakika wangeachana kwa mengi tu.
 
nieleweke jambo moja hapa cjaunga mkono hoja ya huyo jamaa yakutaka kuchukua ATM ila nafikiri kuna vitu vingi nyuma ya pazia lakn kwa uelewa tu mdog unaweza ona jamaa anapambania kumuokoa huyo mama ambaye tayarii fikla zake za kipato ni kukielekeza kwa huyo mchungaj.
Huyo mwanaume anajuaje kama hizo pesa anapeleka kwa mchungaji

Mwanamke akimchoka mwanaume aweza kuanza kujenga nyumba yake kwa siri akaanzisha biashara kwa siri kuwa siku.mwanaume akimpiga chino anahamia Kwake na kwenye biashara zake

Huyo mwanaume ana ushahidi gani kuwa huyo. Mwanamke pesa zote akitoa ATM anapeleka kwa mchungaji heri angesema hajui anakopeleka kuliko kusema anapeleka kwa mchungaji
.Japo mwanamke hata akisema hivyo.ana hakinya kutumia kipato chake atakavyo sio kupangiwa na kudaiwa

Mwanaume haikutakiwa kwenda mahakamani angekaa na mkewe na kumuomba tu kistaarabu kuwa nisaidie hiki my dear
 
Chupi ikiisha mwanaume ananunua,pedi mwanaume ananunua,ila pesa za mwanamke,zinapelekwa kanisani,is it fair?
Sidhani iko sahihi ulichoandika
Mwanamke hawezi hata siku moja kuomba hela kwa mwanaume akanunue pedi au chupi yuko tayari hata kutafuta mpiga debe amhonge kuliko.kumpigia Magoti mwanaume mumewe ampe pesa ya kununua pedi au chupi!!

Muulize mke wa mtu yeyote anakwambia mbili kama hilo halipo
 
Naona watu wengi hasa wanaume wanamshambulia huyo mwanamme. Binafsi naona sio vyema kabisa mwanamke kushindwa kusupport chochote ikiwamo kujihudumia yeye mwenyewe, na mambo mengine, ilhali anafanya kazi na wakati mwingine unakuta mshahara kamzidi mumewe. Kama hawezi, ni vema aache kazi ili ashinde nyumbani atunze watoto na majukumu mengine ya nyumbani. Tatizo lingine naona ni ubinafsi na kukosekana kwa upendo katika hiyo ndoa, inakuwaje mpo kweny ndoa lkn hamuhaminiani ktk mambo ya fedha?
 
Amuache tu,aoe mama wa nyumbani tu.Wadada wapo wengi sana.
Huenda sio mchepuko lkn pesa ya mwanamke huwa haiguswi mkuu.

Labda uwe na mke anayejitambua sana mara moja moja akupige tafu endapo umeyumba.
Vinginevyo siku zote wanaume ndio mtaji wa familia na jamii
 
Sidhani iko sahihi ulichoandika
Mwanamke hawezi hata siku moja kuomba hela kwa mwanaume akanunue pedi au chupi yuko tayari hata kutafuta mpiga debe amhonge kuliko.kumpigia Magoti mwanaume mumewe ampe pesa ya kununua pedi au chupi!!

Muulize mke wa mtu yeyote anakwambia mbili kama hilo halipo
Nimewahi kuona mke wa mwalimu mkuu anamsubiri mume wake aje anunue bulb imeingua,nilishangaa sana,eti hana hela nayeye ni Mwalimu pia.Walifika mahali wakaachana,mwalimu akaoa mmama wa nyumbani tu.
 
Hayamhusu huyo kidume kiofisa koko cha magereza kilinda wafungwa wakinya wasije kutoroka

Mwanamke akipata pesa yake kwa nini utake kudhibiti pesa yake matumizi? Mkataba wa ndoa unatamka kuwa ukioa utadhibiti matumizi ya pesa za mkeo? Mbona wewe hakuombi ATM yako?

Hii kesi tamu hukumu yake itakuwa landmark kuonyesha kama mke ana haki ya chake akipatacho kwa jasho lake kuwa lazima kidhibitiwe na mwanaume aliyemuoa kuwa mwanamke hana uhuru wa kutumia pesa yake hata kununua pedi bila ruksa ya mume aliyeshikilia ATM kisa alilipa mahari.Kuwa hata akitaka pedi ambembeleze mwanaume kuwa naomba ike ATM niliyokupa Katoe pesa nikanunue pedi navuja siku zangu mume wangu niko chini ya miguu yako katoe
Huyo mwanaume atakuwa na mchepuko sasa matumizi yamekuwa makubwa anataka wasaidiane na mkewe, apambane tu na hali yake.
 
Katika muunganiko wowote hasa NDOA, jambo la kwanza la kuangalia ni upendo, upendo ukizidi yote mambo mengine ni rahisi ku deal nayo. Binafsi mke wangu ni mtumishi, ila kati ya vitu ambavyo hatuna tatizo kabisa ni suala la pesa, tunafanya kwa kushirikiana sana na ikitokea atoe fedha zake basi ananipa mimi ndio nampa. Hakuna mtu kati yetu mwenye uroho wa kutumia pesa zetu. Atm card zetu za mishahara zipo hapo tu na password wote tunazijua( ingawa nina account zingine za DEV). Hivyo, kama mwanamme, pamoja na kumzidi mshahara lazima nifanye kazi ya ziada kupata pesa nyingi zaidi na hii inasaidia sana, maana ni mara chache kutumia fedha zake ingawa tupo huru sana. Shemeji yenu anampenda Mwamposa sana ila nilimpiga beat, amebaki kumtazama kwenye tv tu, nilimwondoa kabisa na wachungaji wa kilokole maana walianza mazoea sana mpk magroup ya whatsap. Kama wanaume tunapaswa kutumza ndoa zetu, wanawake huwa wanakosa imani hasa akigundua fedha mnazotunza ndizo unahonga michepuko, au kugawa hovyo hovyo, tujitahidi kuwa vyanzo vya ziada vya mapato ili kuwa na backups ambazo mwanamke hajui, mwisho kuishi na mtoto wa mtu ni MTEGO.
 
Duuuh, umenikumbusha mjeshi mmoja alimtimbia kakobe chachi ilikuwa kizaazaa, mjeshi yupo misheni dafur sudan huku mke kila kitu kapeleka mwenge
Alikuta frig lake lipo kwa kakobe akalifuata haa haa sio wale wakulia lia[emoji23][emoji23]
 
Bora Huyo Mwanamke aolewe na 'Mchungaji'....! Usikubali Kamanda !

Yaani Wewe Umuoe...Halafu Mchungaji apelekewe Salari...! Huyo Mchungaji si Angeenda Kwao Kumuoa Yeye ijulikane Moja!
 
Pesa ya mwanamke ni yake akitoa shukuru, pesa ya saloon hiyo, ukute hata hajui mke anasuka nywele kwa shiling ngapi ila anataka kujua hiyo laki tatu ya mke inaenda wapi![emoji23]
Kwa point hii ina maana kila mtu abaki na pesa yake,suala la matunzo ya watoto ustawi wa jamii wataamua.Maana kila mtu ana kipato chake
 
Kuna mama mmoja, kwa nia njema tu, mume wake alimwambia "Neno siri" la ATM card take ya Bank, kwamba in case kunatokea dharura, mfano accident, nk, basi Iwe rahisi kushughulikia matatizo!

Laa! siku moja mume kaburudika zake K-Vant, saafi na kausingizi kanono, mama akasachi mifukoni akaondoka na ATM card alfajiri, akakomba hela kibao!
Kimyakimya akairudisha kadi mahali pake!
Jamaa kwenda Bank, kachomeka card yake kwa nguvu zote, kisha: "Tafadhali huna Salio la kutosha kukamilisha muamala huu"
Kilichoendelea baada ya hapo sijui!!!
 
Wengi humu mnamlaumu mume mmesahau kujadili hayo makanisa ya kilokole na wachungaji wake yaan hao ni kama kupe wanakuteka kiakili Kisha unakuwa unawachumia wao tu na huko mbeya ni chimbuko lao.
 
Dadeki yan mshahara wote unapeleka kanisaniiio hata miii nakumwaga bora niwe na mtu ambae najua hana kazi kabisa
Hapo hoja ya mume ni pesa inakwenda kanisani alafu nyumbani mke hajitutumui kutoa support kwa damu yake, nadhani kama ingekuwa haiendi kanisani sidhani kama mume ange-mind yaani hata ingekuwa inapotelea kusikojulikana
 
Kama hujawahi kuwa na mwanamke aliyekimbilia kwenye ulokole ni ngumu sana kumuelewa huyo mwamba, wanawake wanaohama madhehebu wakiwa kwenye ndoa na kwenda kwenye ulokole ni pasua kichwa, wanakjwa wanatiwa viburi sana na wachungaji, hasa hawa wenye mishahara, wachungaji wanakula sana hela zao.
Mke wangu wa zamani aliingia huko wakati tukiwa mm nasali RC na yeye Anglican, akaingia kwa walokole sijui sloam, ndani ya mwaka we had to separate and later divorced. Sasa baada ya divorce, na kujikuta anatakiwa kutumia hela yake kwa maisha yake na kujua kuwa huko aliko anapigwa tu hela zake, amehama tena hilo dhehebu na karudi anglican. Yaani kwa ufupi, wanawake wanaohamia kwenye ulokole baada ya ndoa ni pasua kichwa
 
Back
Top Bottom