Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Kwanza Hongera kwa kuwa na akili ya udadisi ( curiosity). Nilivokuelewa haimaanishi kwamba ulichokiuliza haujui ukweli No unaujua ila unajaribu kuupindisha ukweli kuwa uongo kupitia elimu na maarifa yako ya kidunia kwenye spiritual zone sehemu ambapo unamuhitaji Sana Sana sana roho mtakatifu mpaka uelewe bila hivo ni vigumu Sana.

Pamoja na hayo ila inaonesha Kuna vitu vingine kweli hufaham kwa swala la utatu wa Mungu na namna unavofanya kazi katika maisha yetu ntakueleza kwa ufupi Sana ila zaidi kasome kitabu Cha Mwanzo(Old testament) walau sura ya 1-6 ni vitu ambavyo vipo deep deep Sana then nenda kasome Mathayo ( New testament) chote kina sura 28 kwa utulivu wa Hali ya juu unaweza kuelewa Mungu akisaidie.

Ila Mwisho ya yote Mungu Ni mmoja kweli na Ni roho ambayo ina nafsi 3.....Mungu Baba,Mwana na Roho mtakatifu na ndio maana wakati wa uumbaji ilitumika nafsi ya wingi NA TUMFANYE MTU KWA MFANO WETU.

Hivo basi hiyo nafsi ya pili ya ambayo ilikuja duniani kwa njia ya mwili ili kufikisha ujumbe kwetu Sisi binadam tuache maovu na kutoa dam (sacrifice) ili tuokolewe baada ya kuwa mateka wa shetani kwa muda mrefu kumbuka bila ile damu hakuna chochote ambacho kingeweza kuleta upatanishi kati ya sisi na Mungu Baba na ndo maana hata waganga mpaka Sasa wanatumia damu ili kuingia maagano au upatanishi na nguvu za Giza,Na ndio maana jina lake Yesu likapewa nguvu na mamlaka duniani na hata mbinguni na Mungu Baba kwa kazi kubwa aliyoifanya,jiulize kwa Nini pepo ukilikemea kwa jina la Yesu linapiga kelele na kutoka utaelewa lakini tumia jina lingine lolote uone kama Kuna maajabu yeyote yatayotokea.

Na hiyo nafsi ya tatu hata wewe hapo unayo ambayo pia Ni Mungu ambayo inakuongoza kutenda yaliyo mema na kukuhukumu pale unapofanya mabaya ila huwez ukawa nayo ikiwa Kama utaendelea kuishi maisha ya dhambi na kuamini imani za kishirikina au majini au kitu kingine chochote chenye uungu ndani yake.

Mwisho nipende kukwambia ili uweze kufisha ujumbe kwa jamii au tamaduni Fulani basi Ni lazima na wewe na ile jamii (Be natural) Kama n wamasai basi vaa kimasai alafu kawape elimu watakuelewa sana ndivo ilivokuwa kwa yesu ambaye Ni Mungu nafsi ya pili ilibidi avae uhalisia wa kibanadamu ili ujumbe ufike lakini angekuja kama Mungu watu wangeogopa na wasingeelewa na kwanza hakuna ambaye angeweza kumuona kwasababu Ni Roho yenye nguvu Sana.

In short Ni hayo MUNGU AKUBARIKI.

Mkuu

Endelea kuelimisha na kuinjilisha. Inatufaa 🙏🏽
 
Wewe unakaribia kuchanganyikiwa. Andaa mkutano uanze kufundisha watu Imani yako na sio kuvamia Imani za watu wengine ili Cha kwako kiwe Bora. Kwa kukufahamisha tofautisha Mungu na miungu yako. Mungu Ni mmoja na miungu Ni mingi zaidi ya elfu kumi.
Kama Mungu ni Mmoja Inakuwaje Yesu ni Mungu!?
 
Imani we Amini tu...., Ukiweka Logic sio Imani tena its a Science....

Kwahio kama wewe upo huko yabebe kama yalivyo... kuepuka kuombewa au kutolewa mapepo...
Logic in faith it's Science.

I can't agree more. Thank you
 
Kasome amri kumi za Mungu. Unafanya dhambi kwa sababu humpendi Mungu na unatumikia mapenzi ya shetani.
Yesu si Alifia dhambi zako msalabani. Inakuwaje wewe bado unadhambi!?
Tena Bado una dhambi ya Asili ambayo hakuifia Hiyo

Katika Amri kumi za Mungu Imeandikwa Usiue Ila Mbona Mwanamke mzinzi aliuawa ila Huoni mwanaume Mzinzi akiuawa huoni Bado Inaenda Nje ya Amri zake
 
Ni kama ile wewe mwanaume unavmiaka karibia 50 unambaka mtoto wa miaka sita halafu kwa aibu eti unapotezea kwa kumuoa akiwa na miaka 9 na bado unaona sawa tu na mabilion ya waja wanakutuza hadi wanachinjana na kujitoa mhanga. Halafuu unajiona mjanjaaaa eti Mungu kakutuma. Kweli huyo ni Mungu gani wa ajabu anaweza kukutuma.
Jikite kwenye hoja ya mleta mada,
Usihamishe magoli.


Sent from my M2101K7BG using JamiiForums mobile app
 
Jibu swali, lete Aya inayosema Yesu si Mungu acha kuleta maelezo.
Tumia Akili ndugu yangu Kadhi Mkuu 1 . Kwani Wewe ubongo wako umeweka Pembeni mpaka Usaidiwe na Aya.

Yesu anatakuwaje Mungu halafu hapo hapo Anaomba Mungu? Hili si swala la Kutumia tu akili.

Basi Wewe niletee sehemu aliposema Yeye ni Mungu
 
Umesoma Biblia au unauliza ili uelewe.
Kasome mistari hii ifuatayo.

Yohana 1:18
Yohana 10:30
Wafilipi 2:5-6

Yeye Mwenyewe hakujinasibu kuwa ni Mungu ila Yohana.. Na Wafilipi ndio walimwita Mungu. Hivi mkuu unajua Kutumia tu akili timamu ni Jambo Jema sana

Hivyo vitabu vya Yohana na Wafilipi waandishi wake hawakuwepo hata Kipindi cha Yesu na VITABU vingi hivyo ni Masimulizi ya Watu ambao wengi wao si Mitume ila viliandikwa kwamba Ni Vitabu vya Mitume wakati Mitume hawakuandika Vitabu hivyo
 
Unaniletea picha ndio nifanyeje?. Unaleta Vita vya zamani uingereza na ottoman unadai ukristo unaenezwa kwa Vita. Wewe ndio ukasome Ni jinsi gani uislamu uliingia misri na majirani zake wakati ilikuwa nchi ya kikristo.

Halafu Acha uongo shule nyingi za dini mpaka leo zipo nyingi, mf mazengo ya zamani, Musoma Tech, Ngaza girls, Nsumba Tabora TTC.
Tafuta Neno Crusade. Sijakuletea Picha Tu Jua hizo vita Zilipiganwa kwa Kupitia Dini Gani
 
Dini zinasambazwa kwa lazima, kuna mataifa ukiwa mkristo unakatwa kichwa mfano Afghanistan. Hivyo siyo ukristo tuu ulioenezwa kwa lazima.
Wewe ni muongo na mzandiki.

Tuonyeshe sehemu iliposema ukiwa mkristo Afghanistan unakatwa kichwa. Hivi ndivyo mnavyodanganyana huko Makanisani kwenu.

Screenshot_20220303-120851_Google.jpg
 
Mama D hivi unaona jinsi Gani akili zetu zimevurugika. Kwahiyo Yesu na Kristo ni Watu wawili tofauti tena. Hapa unakana Kabisa kwamba Yesu hakuzaliwa ila Alizaliwa Kristo ambaye Hata Hatujui ametajwa wapi.



Nabii anaye takwa kama Isaya Alitabiri Kuwa Ataitwa Emanueli Ila Malaika akaja akasema ataitwa Yesu wewe umemnasibu hapo ataitwa Kristo. Sasa Libebwe lipi liachwe lipi ndugu yangu



Mungu akifanya Kazi ndani yako wewe Maana yake Hakuwa na Haja Ya Kukupa Akili hiyo uliyonayo. Na Kama Akifanya Kazi ndani yako hawezi kukutuma Ukazini. Ukaibe. Ukaseme uongo.. Uue n. K n. K mana Ukifanya Hayo maana Yake Yeye ndio kakutuma




Mungu akiwa Baba Inabidi awe na Mama pia. Akiwa Baba Atakuwa na Watoto pia. Neno baba Maana Yake ni Jina La Viumbe wa Kiume wenye Watoto



Mwana maana Yake ni Mtoto wa.. Unaposema Mwana maana Yake ni Ubin wa Mtu. Ukimwita Mungu mwana. Maana yake Kazaliwa Huyo Mungu.




Na je Alipokuwa anaomba Pale mlimani alikuwa anamwomba Nani!?

Hakuna kisichoeleweka hapo ni wewe tuu hutaki kuelewa

Unavyojivuruga mwenyewe kwa kushindwa kusoma maandiko na kuyaelewa badala ya kubeba mistari michache na kukimbia nayo ndivyo unavyozidi kuvurugika

Aliyezaliwa na Mariam ni Kristo ambaye malaika alitumwa amwambie akishazaliwa amwite jina lake Yesu, Sio Yusufu wala Mariam walimpa hilo jina

Mathayo 2: 3-4
"Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye. Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, KRISTO azaliwa wapi?"
Luka 1: 26-27; 30-33
Malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti,
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu.
Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

Ijue maana ya jina Imanueli. Baada ya jina hilo kutajwa kwenye Isaya 7:14 nenda kasome Isaya 9:6. Usisome biblia vipandevipande ukatoa hitimisho, jitahidi kusoma uelewe. Ila kama imani yako sio kwa biblia basi nyamaza tuu sababu utaongea hata yasiyokuwako
Isaya 7:14
"Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli."
Isaya 9: 6
"Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani."
 
Ndugu yangu huoni Unazidi kujipotosha. Mungu haongei na Wala haandiki chochote kile. Ukiona Umeambiwa Usichunguze maana Yake Yana Uongo humo Ndani yake.
Sasa hapo unasemaje juu ya Jiwe kuliweka shirika la ndege chini ya ofisi ya Rais ili lisichunguzwe?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna watu wengi Kama wewe wanaopotosha. Biblia ndio inasema tena Yesu Kristo mwenyewe anasema ya kwamba utafuteni ufalme wa Mungu na mengine yote mtazidishiwa. Hiyo ndio Imani ya Kikristo.
Mungu Kaumba Viumbe wengi. Majini.. Malaika.. Binadamu n.k kwahiyo akakupenda Wewe sana Akakuambia Umtafute

Yaani Amekuumba halafu akakuweka Duniani Halafu akakuambua Umtafute tena yeye Alipo?

Mungu keshakuumba Ukiamua Kumtii ni juu yako ukiamua Kutomtii wala Hakukasirikii maana Teyari keshakupa Akili
 
Kuna Utata mkubwa Sana Katika kuzaliwa kwa Yesu kutokana Na Maandiko ya Biblia. Ila Kwa Akili Timamu Binadamu yeyote lazima Azaliwe kwa Mifumo maalumu ya Mbegu ya Kiume kuungana Na Mbegu ya Kike Tofauti na Hapo Binadamu hawezi Kutokea
Mkuu kwani Yesu ni binadamu au Mungu?
 
Wewe unamatatizo makubwa. Binadamu ndio anamuokoa binadamu mwenzake?. Acha kujitoa akili, nyie ndio mkiuguua tumbo mnaanza kulia Mungu nisaidie nakufa. Wakati wa Nuhu walikuwepo wabishi zaidi yako lakini mwisho ulipofika waliliia Kama watoto. Juzi hapa kulikuwa na Corona Tanzania tukafany maombi ya kufunga, je Kuna binadamu gani alikuwa ana uwezo wa kuondoa corona?.
Kwani Corona Imeisha!? Mbona Raisi wako anasisitiza Ipo na Anavaa Barakoa
 
Shida ya mtoa mada ni kuwa umeziamini sana Akili zako na kuona ww unauwezo mkubwa wa kuchanganua mambo na kuyaelewa..
labda tu nikwambie kitu ambacho kitafanya ujue kuwa akili uliyonayo ni ndogo sana kwa ufahamu wa mambo ya Mungu(Yesu).
.
hapa duniani sio watu wote wamezaliwa na baba na mama, kuna watu wengi sana wanatembea wakionekana ni watu lakin sio watu, wengine majini, wengine walozi waliovaa miili ya watu, wengne misyuka lkn wanaonekana katika hali ya mwili kabsa. so usiishi kwa kukariri...
.
ushauri wangu kwako:- mambo ya Mungu(Yesu) ni mambo ya kiroho kwaiyo ukitaka kuyaelewa vzr nenda kiroho zaid lakini ukienda kimwili kwa akili hizo unazozitegemea hakuna kitu utaelewa
Kama Mshana Jr ??
 
Wewe unakaribia kuchanganyikiwa. Andaa mkutano uanze kufundisha watu Imani yako na sio kuvamia Imani za watu wengine ili Cha kwako kiwe Bora. Kwa kukufahamisha tofautisha Mungu na miungu yako. Mungu Ni mmoja na miungu Ni mingi zaidi ya elfu kumi.
Mungu wa Kweli haubiriwi kama Ulivyokaririshwa Wewe ndugu yangu. Watu wengi sana Hapa Duniani waliitwa Miungu. (Yehovah. Yire.. Zambe..Allah n.k) hao si Mungu mana Hawana Sifa za Mungu
 
Back
Top Bottom