Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Kitabu gani kinachosema kuna watu walikuwepo kabla ya Adam?
Soma Historia za Wazee wako na Babu zako na Jadi utajua Ukweli. Adam na Hawa si Binadamu wa Kwanza

Afrika Kulikuwa na Watu na Ulaya Pia Kulikuwa na Watu.
 
Similarities, tufanyaje ili tuondoe izo brainwashing
Tumieni akili Timamu Waafrika wenzangu. Na Jueni kweli kwa Kuchunguza Mnavyoletewa mtu hawezi kukusimulia mambo Ya Viumbe wengine halafu Yeye mwenyewe hajijui ametokea wapi. Leo hii mtu anakusumulia kuhusu Israeli na makabila yake ila Yeye kabila Lake hajui limetoka wapi

Jijue kwanza wewe kabla ya Kujua Wengine na Vita zao zisizokuhusu
 
Kuna Mambo Yapo Ulimwenguni ukiyatafakari kwa Kina hayaingii Akilini ndugu waafrika wenzangu

Kuna Historia katika Vitabu kwamba Mungu alimtoa Mwanae Ili aje Kuikomboa Dunia katika Dhambi (ambazo zipo mpaka Leo)

Ukiangalia kwa Undani Historia hii ya kuzaliwa kwake inatia Shaka sana kabla ya Kujua Majibu ya kuzaliwa kwake inakuja Historia kwamba hana Baba. Kabla hujapata Majibu ya Baba ni nani Inakuja Kwamba ni Uwezo wa Mungu ndio akazaliwa. Yanakuwa Maswali juu ya Maswali

Kumbuka Yusufu na Mariam si kwamba Walikuwa ni Wachumba la hasha bali walikuwa tayari wapo Ndani (wameoana) wanaishi pamoja. Hakuna wachumba Wanaoishi pamoja kwa Utaratibu wa Kuishi. Ukichumbia wewe utakaa kwako na Huyo mchumba atakaa kwao. Kama Waliishi pamoja maana Yake waliweza Kushiriki Tendo la Ndoa yao na Ukifuatilia kwa Makini Yusuf alikuwa Pamoja na Mariam kila Sehemu hakuna Sehemu inayosema Alikuja Kumuoa mariam Ikiwa na Maana Kwamba Tayari alikuwa keshaoa maana yake ule uchumba ulio andikwa Tayari ukayeyuka

Binadamu huzaliwa Kwa Mwanaume na Mwanamke hili halina ubishi. Ila Kuna Kuja Utata wa Hapa Kwamba Yesu alizaliwa bila Mfumo maalumu wa Uzazi wa Baba na Mama ila Roho Mtakatifu kama Wanavyodai (kumbuka Hata Huko india Wapo Watu wenye Hadithi hizi hizi za Kuzaliwa bila Baba)

Sasa Hapa Unajiuliza Maswali. Mungu huyo aliyeweza Kumuumba Mwanadamu wa Kwanza Bila Kutumia mifumo ya Uzazi Inakuwaje leo aje Aanze Kumuumba Binadamu mwingine anayedaiwa ni Mwanae kwa Mifumo ya Uzazi na Akaenda kwa Mariam ambaye alikuwa teyari ana Mume(kumbuka Hapa Mungu hazai na Wala Hakuzailiwa)

Sasa Anamzaa mwanae kupitia Mariam mara Yusufu atake kumkimbia Mariam maana Kuna Siri May be Yusufu aliiona akaona Hapa Nimepigwa na Baada ya Yesu kuzaliwa Yusuf Anapotea Ghafla kwenye Maandiko na Historia yake inaishia Hapo hapo

Mungu anamtoa Mwanae. Anakuja Mnamkataa, mnampiga, mnamtesa anawahubiria mnagoma Kukubali maneno yake mnamfukuza kwenye masinagogo yake, Anaenda Kusali mlimani peke yake, anakusanya wanafunzi wake. Hao wanafunzi nao mnawakataa mnawafukuza. Hivi Mungu hapo anawaogopa Nyie kisa Nini mpak Awafanyie Haya Yote Nyie Viumbe wake

Yaani Mungu mpaka Anatoa Mtoto wake Wa Pekee ili awabembeleze nyie mmrudie Yeye na Mnakataa. Sasa Hapo Mungu Anakuwa na Ule Uwezo na Kutoshindwa Kitu kweli. Kama Kawatumia Mwanae na Mmemgomea kawatumia Manabii na Mitume mmemgomea Tena na hamtaki kumrudia. Hivi Mungu anawalemba Hivyo Ili Iweje

Si kila Mtu anayezaliwa bila Baba Yake basi Baba Yake ndio Mungu. Wachawi wanazini na Binadamu kila Siku na Wachawi hao hao ndio Binadamu wenzenu. Wanawake wanabeba Mimba zingine wasizozijua zimetoka wapi

Basi Mjue Kwamba Hapo Mwenye Enzi Mungu hayupo na Mnaozeshwa Akili zenu ndugu zangu. Kaeni Chini Mtafakari kwa Akili zenu Timamu. Mungu hawezi kufanya hayo Kwa Viumbe wake. Yeye hayupo Hivyo

[emoji3507]Mungu si Mmoja
[emoji3507]Mungu si Wengi
[emoji3507]Mungu si Baba
[emoji3507]Mungu si Mama
[emoji3507]Mungu si Kiumbe
[emoji3507]Mungu hachukii Viumbe
[emoji3507]Mungu hapendi Viumbe wake ila Ana Enzi na Viumbe wake (usijione wewe Kiumbe Mtu unapendwa na Mungu Kuliko Viumbe wake wengine aliowaumba)
[emoji3507]Mungu hakuzaa wala Kuzaliwa

Yachunguzeni maandiko Yenu mtajua kwamba si Maandiko ya kiucha Mungu ila Maandiko ya Viumbe wenye Tamaa

ASANTENI
Mkuu unaonekana unaamini uchawi. kuamni uchawi na unavyoviandiaka kwenye nyuzi zako, inanifanya nikupotezee.
 
Dini zinasambazwa kwa lazima, kuna mataifa ukiwa mkristo unakatwa kichwa mfano Afghanistan. Hivyo siyo ukristo tuu ulioenezwa kwa lazima.
Kwahiyo kumbe Unajua kwamba ilikuwa ni lazima uupokee Ukristo na hizo dini zingine nazo zipo zinalazima Mzikubali

Wazee wenu na Babu zenu walilazimishwa hivyo hivyo
 
Acha kutumia muda mwingi kuandika visivyoeleweka.maana hadi hapa nimegundua wewe ndiye ambaye hutaki kuelewa kilichomaanishwa kwenye biblia.badala yake inaunga unga nadharia zako ambazo hazina mantiki.

Umesema Yesu ni Mungu. Aliuawa na Akafa siku tatu akafufuka. Nimekuuliza kwahiyo Dunia Ilikuwa haina Mungu Kwa Siku tatu?

Sema Mantiki yangu Haipo wapi
 
Kwa hivyo unataka kusema Biblia Ni uongo kumuita Mungu Yehovah. Kama Biblia Ni uongo endelea kufanya Uzinzi na dhambi zingine.
Nani kakuambia watu walikuwa hawazini na Hawana Dhambi mpaka biblia ilipokuja. Na nani kakuambia Biblia imeandika ukweli kama ingekuwa imeandika ukweli watu wasingetawanyika Kwenda kuutafuta

Maana Humo humo kwenye Biblia kuna Wasabato.. Walutheri.. Wakatoliki. Wazumaridi.. Wa AIC.. Wa Anglicana.. Walokole na Madhehebu mengine 1000 na Kidogo

Mungu gani anataka Muwe makundi makundi hamna Umoja
 
Yaani hakuna sehemu Mungu huwa anadharaulika na kutukanwa Kama jf, Kama una Imani yako imelegalega unaweza Hadi kurudi nyuma kiroho.Mungu aturehemu
Imani yako haiwezi Lega Lega kama Una ukweli ndani yako ndugu yangu. Wale wasio na Ukweli ndio wanalega lega na Kupotea Direction maana wanachokiamini hawakijui kwa Undani wake
 
Japo wakristo wamekataa kunipokea ila niwasaidie tu kujibu swala la kutoa sadaka na hayo mengine mtoa mada haujarleweka zaidi ya kuleta ubishi tu wa vijiweni.
Mungu ahitaji sadake zetu ila sisi tunahitaji kutoa sadaka ili tuwe kama yeye. Yeye na sisi tunaotofauti kama vile nguo safi(yeye) na nguo chafu(sisi).
Sisi tunatenda zambi ila yy hatendi zambi na tunatumia nguvu na jitihada nyingi ili tuwe kama yeye.
 
Ndugu kila mmoja ana hiari ya kutangaza Imani yake ilimradi asivunje sheria. Sisi tunatangaza Imani yetu, Ni hiari yako kuiponda au kuikubali. Ila jehanamu ipo na wengi wataenda huko Kama hawakumpokea Yesu Kristo na kuishi Maisha matakatifu hapa duniani.

Ndio maana watu wanakuuliza Maswali uitetee hiyo imani kama Ni ya kweli Wataufuata. Sasa unapoulizwa maswali unaanza Kumtisha Mtu na Jehanamu kisa hayampokea Yesu unakuwa unawatisha Watu ndugu yangu.

Mtu ambaye ni mtakatifu si Mcha Mungu. Mtu yeyote anaweza kuwa Mtakatifu manaa Utakatifu ni unadhifu tu ukioga na Kuoendeza Na Kuvaa Nguo safi wewe tayari ni mtakatifu.

Takatifu ni Nguo iliyooshwa na Kutolewa uchafu (imetakata) na Kuwekwa mahala pale ukiivaa wewe na Huku umeoga na Kuwa msafi ndio Unakuwa Mtakatifu

Kwahiyo Njiani huko unakutana na Watakatifu kibao tu Ndugu yangu ila si Wacha Mungu
 
Mwana wa Mungu ni Mungu au binadamu?.
Nani alisema ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu ?

Je katika Biblia tamko mwana limetumika kwa Yesu tu peke yake ?

Kwanza nataka tufikie muafaka hapa je ni kweli Yesu ni mwana wa Mungu. Naomba nithibitishie hilo, sababu nachojua mimi Mola wetu hajazaa wala hakuzaliwa na wala hana mfano wa kitu chochote.
 
Unapojadili kuhusu ukweli halafu una quote Kitabu ambacho watu wanautafuta Ukweli hawauoni kuna Leta ukakasi kidogo na Kwamba wewe mdugu yangu hutaki kutumia akili timamu

Unaposema Baba Maana Yake yeye Ni Binadamu kama Wewe maana Neno Baba Ni Mzazi wa Kiume

Shida kubwa ni uelewa wako wala sio kutokueleweka kwa maandiko
Baba maana yake ni muanzilishi/Muumbaji

Muumbaji wa kwanza na pekee ni Mungu na yeye aliwarithisha binadamu kazi ya kuuendeleza uumbaji katika ulimwengu huku mwanaume akiwa muumbaji katika ngazi ya kuongeza uzazi yaani baba

Baba asili yake ni muumba sio wewe uliye mwanaume wa leo
 
Shida ya mtoa mada ni kuwa umeziamini sana Akili zako na kuona ww unauwezo mkubwa wa kuchanganua mambo na kuyaelewa..
labda tu nikwambie kitu ambacho kitafanya ujue kuwa akili uliyonayo ni ndogo sana kwa ufahamu wa mambo ya Mungu(Yesu).
Hiki ndicho kitu kilichowaharibu sana Waafrika mpka mnaambuwa IQ zenu ni ndogo. Ndugu yangu hakuna kitu kikubwa kama Akili yako Timamu uliyonayo na Mungu mwenye Vyote ndie aliyekuwekea. Ukitegemea Mzungu aje ndie akutafsirie Sijui Roho gani ije Ikuingie ndio ujue Maandiko utazidi haribikiwa.



.
hapa duniani sio watu wote wamezaliwa na baba na mama, kuna watu wengi sana wanatembea wakionekana ni watu lakin sio watu, wengine majini, wengine walozi waliovaa miili ya watu, wengne misyuka lkn wanaonekana katika hali ya mwili kabsa. so usiishi kwa kukariri...

Hao ndio viumbe wanaowaharibu akili sana Mpaka leo Hamjijui Mnataka Nini. Kama Wewe mwenyewe umekiri kwamba Kuna Viumbe wanatembea na Miili kumbe si Watu basi kubali Pia Unaweza Hubiriwa Pale Kanisani na Huyo Huyo Jini na Walozi



.
ushauri wangu kwako:- mambo ya Mungu(Yesu) ni mambo ya kiroho kwaiyo ukitaka kuyaelewa vzr nenda kiroho zaid lakini ukienda kimwili kwa akili hizo unazozitegemea hakuna kitu utaelewa

Mimi nina Mwili unatakaje niende kiroho wakati unatakiwa Unieleweshe nikiwa na Akili zangu mwenyewe ndugu yangu. Wewe unataka Upate Akili kutoka kwa Nani ndio uelewe. Yaani Ili Nielewe inabidi hii akili yangu niiweke Pembeni nisubiri akili kutoka Kwingineko ndio nielewe

Hapo ndugu yangu si unaona Kabisa unakuwa Msukule kabisa. Yaani Hao Viumbe wamewaambia Ili Myajue Maandiko inabidi Mtolewe akili zenu za Kawaida mpewe zingine. Daaah
 
Kwanza Hongera kwa kuwa na akili ya udadisi ( curiosity). Nilivokuelewa haimaanishi kwamba ulichokiuliza haujui ukweli No unaujua ila unajaribu kuupindisha ukweli kuwa uongo kupitia elimu na maarifa yako ya kidunia kwenye spiritual zone sehemu ambapo unamuhitaji Sana Sana sana roho mtakatifu mpaka uelewe bila hivo ni vigumu Sana.

Sasa Nini maana Ya Kuja Kunihubiria Kama unayenihuburia siwezi kuyaelewa. Hivu hili jambo Lako linaingia akilini kweli yaani Mimi Nione umesema Kikombe au umeandika Kikombe ila Nisitafsiri ni Kikombe ila nisubiri Akili Nyingine ije iniambie kwamba Kile si kikombe ni Sahani. Kuniambia Mimi kwa Mafumbo maana Yake unakitu unataka nisijue



Pamoja na hayo ila inaonesha Kuna vitu vingine kweli hufaham kwa swala la utatu wa Mungu na namna unavofanya kazi katika maisha yetu ntakueleza kwa ufupi Sana ila zaidi kasome kitabu Cha Mwanzo(Old testament) walau sura ya 1-6 ni vitu ambavyo vipo deep deep Sana then nenda kasome Mathayo ( New testament) chote kina sura 28 kwa utulivu wa Hali ya juu unaweza kuelewa Mungu akisaidie.

Ila Mwisho ya yote Mungu Ni mmoja kweli na Ni roho ambayo ina nafsi 3.....Mungu Baba,Mwana na Roho mtakatifu na ndio maana wakati wa uumbaji ilitumika nafsi ya wingi NA TUMFANYE MTU KWA MFANO WETU.

Hivo basi hiyo nafsi ya pili ya ambayo ilikuja duniani kwa njia ya mwili ili kufikisha ujumbe kwetu Sisi binadam tuache maovu na kutoa dam (sacrifice) ili tuokolewe baada ya kuwa mateka wa shetani kwa muda mrefu kumbuka bila ile damu hakuna chochote ambacho kingeweza kuleta upatanishi kati ya sisi na Mungu Baba na ndo maana hata waganga mpaka Sasa wanatumia damu ili kuingia maagano au upatanishi na nguvu za Giza,Na ndio maana jina lake Yesu likapewa nguvu na mamlaka duniani na hata mbinguni na Mungu Baba kwa kazi kubwa aliyoifanya,jiulize kwa Nini pepo ukilikemea kwa jina la Yesu linapiga kelele na kutoka utaelewa lakini tumia jina lingine lolote uone kama Kuna maajabu yeyote yatayotokea.

Na hiyo nafsi ya tatu hata wewe hapo unayo ambayo pia Ni Mungu ambayo inakuongoza kutenda yaliyo mema na kukuhukumu pale unapofanya mabaya ila huwez ukawa nayo ikiwa Kama utaendelea kuishi maisha ya dhambi na kuamini imani za kishirikina au majini au kitu kingine chochote chenye uungu ndani yake.

Mwisho nipende kukwambia ili uweze kufisha ujumbe kwa jamii au tamaduni Fulani basi Ni lazima na wewe na ile jamii (Be natural) Kama n wamasai basi vaa kimasai alafu kawape elimu watakuelewa sana ndivo ilivokuwa kwa yesu ambaye Ni Mungu nafsi ya pili ilibidi avae uhalisia wa kibanadamu ili ujumbe ufike lakini angekuja kama Mungu watu wangeogopa na wasingeelewa na kwanza hakuna ambaye angeweza kumuona kwasababu Ni Roho yenye nguvu Sana.

In short Ni hayo MUNGU AKUBARIKI.

Mungu hawezi akawa Mmoja Halafu akawa tena Na Wengine wawili. Hivi hili jambo linaingia Akilini kweli. Au ndio Ukiuliza Unaambiwa Ni Fumbo la Imani

Tutumie tu akili Zetu. Ndio maana Utatu hauna Majibu yanaoingia Akilini ndio maana Inafikia Hatua Mnasema Ni Fumbo la Imani. Fumbo maana Yake ni Kufungwa Kutoakujua Kitu chochote kwahiyo usiseme wewe unaujua Utatu wakati Umeshambiwa Ni Fumbo
 
Mtu alipigwa kipigo cha mbwa koko akashindwa kujitetea akaanza kumlilia Mungu wake amsaidie bado watu wanasema mtu huyo ni Mungu.. cha ajabu zaid hadi wasomi wakubwa wapo kwenye mkumbo huo yaan elimu zao za kwenye makaratasi hazijawasaidia kufikiria zaid.

Hivi hizo siku 3 alizokufa dunia ilikuwaje? Nani alikua akiongoza hii dunia? Hayo madhambi mbona yanazidi kama alifia msalaban kwa ajili yenu?

Waafrica njli watumwa sna kujikomboa kiuchum na kifikra tutasubiri sana
 
Andiko litanoga ukitujaalia Reference materials (Books, Journals, Reports, etc).

Bila hivyo hili andiko linafanana na Ramli zinginezo.
Kwahiyo bila Kutumia Vitabu vilivyoandikwa na Binadamu wenzako wewe Akili zako pekee huziamini mpaka Upate reference

Kwahiyo ukiambiwa hata Yesu ndio Mungu Mkuu unakubali tu kisa Imeandikwa sehemu ingawa unajua Sivyo
 
Back
Top Bottom