Mungu mwenye Upendo hawezi kuchoma watu kwa moto. Huo ni Ushetani

Mungu mwenye Upendo hawezi kuchoma watu kwa moto. Huo ni Ushetani

Kwanza kabisa Mungu hayupo katika uhalisia,
Ispokuwa Mungu ni wazo la mwanadamu.

Yaani wanadamu walitangulia kuwepo ulimwengu ndo akafuata huyo Mungu.

Wanadamu ndio walimuumba Mungu kwa mfano wao ili kuficha ujinga wao..
Mungu aliumbwa akapewa sifa za kibinadamu hadi akakosa logic.

Kwasababu kama kweli huyo Mungu angekuwepo kama alivyoelezwa kwenye vitabu alipaswa kukamatwa na kuwajibishwa kwenye mahakama za kimataifa kwa makosa ya jinai kama mauaji ya halaiki aliyowahi kuyafanya.
Kufuja mali za watu maskini n. K


Usidanganywe na mtu, mwanadamu ndiyo msaada wa pekee.
Mungu hawezi kukusaidia kwasababu hayupo.

Kuna kitu unasahau hapo
Nani anawajibika kwenye suala zima la shida kuwepo ulimwenguni!?

Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo shida isingewezekana kuwepo.

Kwamaana alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao shida haiwezekani kutokea.

Unaelewa hilo?
yofauti yako na yangu ni ndoooogo sana.. mimi naamini Mungu kupitia Mwanadamu yaani nguvu na sifa zote alizonazo utazipata kwa mwanadamu..
hata maelezo yako yananisapoti japo mimi sikatai uwepo wa nguvu za kiMungu kwetu wanadam.. ndio mana tunasameheana. tunasaidiana. tunahukumiana. yunaoneana hutuma. tunazalishana. tunaabudiana. tunaumba na viumbe vingine mfano chawa... nk
 
Kwamba yesu alipokufa ndo ikawa nini.

Kwamba Mungu ndo anamamlaka ya kufuta na kusamehe dhambi.
Halafu amtume yesu aje kufa kwa ajili ya hzo dhambi...

Akifa mwanae ndo dhambi zifutike

This is insane
yesu hakuuliwa na Mungu.. inasemwa hivyo ili kutuliza wafuasi wake.. yesu aliingilia maslah ya watu... hivi kwa mfano. atokee mtu anatibu kila ugonjwa.. anagawa vyakula. hivi watu wa tiba na wakulima au wafanyabiashara watamuacha Hai??
 
Baada ya UASI mbinguni
Mungu alituumba kwa mfano wake, lengo kuu ni tumuabudu.
Kwa kutamka vyote vikawa

Shetani akaileta dhambi duniani

Mungu akamtuma Yesu atukomboe kwa kufa.

Tukapokea Neema na Rehema

Mungu ataangamiza dhambi na dunia ya dhambi, kama binadamu naye ni mdhambi itampasa naye aangamizwe.
 
Kuna vitu hatuvioni kwa macho, je ndiyo tuseme havipo? mfano upepo,mawimbi ya sauti,electronic signals etc . Wewe kutokumuona Mungu haimaanishi hayupo
katika ukweli na kiukweli, kisichoonekana kusikika wala kunusika ujue hiko hakipo.. ila kiimani yaweza kua konyume chake.

na kwanini mnaamini Mungu haonekano huku mkiamini alituumba kwa mfano wake.? Jipende mpende na mwenzako basi utakua umempenda Mungu. MUNGU NI UPENDO FULL STOP
 
yesu hakuuliwa na Mungu.. inasemwa hivyo ili kutuliza wafuasi wake.. yesu aliingilia maslah ya watu... hivi kwa mfano. atokee mtu anatibu kila ugonjwa.. anagawa vyakula. hivi watu wa tiba na wakulima au wafanyabiashara watamuacha Hai??
Si tunaambiwa eti Yesu alitumwa na babaye aje kufa Ili watu wakombolewe kwenye dhambi!?

Au nnakosa ufahamu wa jambo hili?
 
Baada ya UASI mbinguni
Mungu alituumba kwa mfano wake, lengo kuu ni tumuabudu.
Kwa kutamka vyote vikawa

Shetani akaileta dhambi duniani

Mungu akamtuma Yesu atukomboe kwa kufa.

Tukapokea Neema na Rehema

Mungu ataangamiza dhambi na dunia ya dhambi, kama binadamu naye ni mdhambi itampasa naye aangamizwe.
Mbingu haipo, ni hadithi tu

Hata huyo Mungu na shetani ni hadithi tu, hawapo in real dimension.

Kwanini Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote alimshusha shetani kwenye sayari hii ya dunia?

Kwanini asimshushe hata Alpha centauri B huko nje ya solar system?
 
MUNGU MUUMBA MBINGU NA NCHI NI PENDO, HAKIMU WA HAKI... HUHUKUMU SAWA NA AGIZO LAKE... HAPANGIWI.... MWANADAMU AKING'ANG'ANIA JEHENAMU MUNGU AFANYEJE!!! UTAJIHUKUMU KWA MATENDO YAKO... MUNGU ALAUMIWE KWA LIPI WAKATI UCHAGUZI NI WAKO ??
 
Anaandika Robert Heriel,
Mtibeli.

Kuna Mungu Muumba wa mbingu na nchi halafu kuna miungu. Mungu Mkuu ambaye hajawahi kuonekana na kamwe hatokuja kuonekana Daima milele, hawezi kufanya wala kuwaza huo upuuzi wa kuchoma watu, hilo haliwezekaniki!

Miungu hii inayoabudiwa ndio inaweza kufanya hivyo, lakini yule Mungu wa miungu huo muda hana, na hawezi kufanya hivyo.

Mungu Mkuu ni Upendo, na kamwe upendo haulazimishwi. Yaani, ati Mungu aliyekuumba akulazimishe umpende (umuabudu) wakati alikuwa na uwezo wa kukuumba automatic ukawa unampenda!

Kwanza umpende (umuabudu) ili yeye apate nini? Halafu usipompende ati akuchome, wewe kosa lako lipo hapo? Yaani moyo wako haumpendi Mungu aliyekuumba, unapenda jambo jingine nini kosa lako, iko wapi haki hapo?

Mungu mwenye Upendo na muweza wa yote, anataka mtu apende anachokipenda! Kwanza yeye ndio aliyekufanya uwe hivyo ulivyo, upende unayoyapenda, achana na yale unayoyatamani na kuyachukia.

Huwezi lazimisha kupendwa bhana, na kamwe Mungu hawezi kukulazimisha umpende. Kukulazimisha haibadilishi ukweli kuwa haumpendi. Kumbuka Mungu ni Haki na Kweli.

Mchongo ukoje? Ipo hivi;

Jinsi uonavyo Ulimwengu wa nje (huu unaoonekana) ndivyo katika Ulimwengu wa ndani usioonekana, Ulimwengu wa Nafsi.

Itazame Dunia, Dunia ni moja lakini inamazingira tofauti tofauti, kuna sehemu zenye baridi kali mpaka barafu, kuna sehemu za jangwa, kuna sehemu za hali ya hewa ya kati, kuna sehemu zenye mvua nyingi, na zipo zenye mvua za Waarabu.

Kuna milimani na mabondeni, sehemu zenye maziwa, mito na bahati, sehemu yenye misitu mine, nyasi na vichaka, sehemu yenye wanyama wa aina hii sehemu nyingine hakuna.

Sasa ni uchaguzi wa mtu kutumia kile akipendacho, ukitaka kuishi kwenye baridi ni wewe, Mungu hawezi kukulazimisha uishi sehemu isiyo ya baridi wakati wewe unapenda. Haipo hiyo. Ukitaka kula chakula au wanyama fulani ni wewe mwenyewe.

Ila elewa kuwa vipo vitu ni sumu na cool vitu sio sumu. Ni wewe mwenyewe unachagua ule sumu au usile. Nasema ni wewe mwenyewe, ni kutokana na upendo wako.

Kama unavyoishi hapa Duniani kulingana na umri wako, jinsia yako, kipato na hadhi yako, mtazamo wako ndivyo nafsi yako itakavyoishi baada ya mwili wako kuondoka.

Mfano huwezi ishi Masaki, Mikocheni, Upanga wakati kipato chako na daraja lako ni kuishi kwa walalahoi huko.

Kunguru na njiwa hawawezi kaa pamoja, wanasema ndege wafananao huruka pamoja. Nenda hata wodini huko mahospitalini utaona kabisa kuwa mgonjwa wa akili hawezi lazwa wodi ya wazazi au mgonjwa aliyemahututi hawezi lazwa wodi ya wagonjwa wa meno.

Maisha ni uchaguzi wa mtu mwenyewe. Mungu kamwe hana huo muda wa kukuamulia nini chakupenda. Kuku hawezi zaa bata, kila mmoja atakaa sehemu yake. Vivyohivyo hata ukifa roho yako itaenda mahali inapopapenda, na wala hautachomwa moto.

Kama unapenda uzinzi na kuchukua wake za watu na kuua watu basi nafsi yako itaishi katika Ulimwengu wa watu wa aina yako ili mchukuliane wake na waume zenu kwa jinsi mpendavyo, ili muone utamu wa kile mnachokipenda.

Sheria siku zote sio upendo, Sheria hizi za nchi zipo kwaajili ya kudhibiti matendo ha mwili na sio nafsi. Upendo upo kwenye nafsi ya mtu wakati sheria ipo katika mwili wa mtu. Mtu anapoua akahukumiwa jela kinachoadhibiwa ni mwili wake lakini nafsi yake haiadhibiwi.

Utalipwa sawasawa na matendo ya nafsi yako, Dhamiri na utapelekwa kwenye Ulimwengu unaofanana na nafsi yako. Hiyo ndio tafsiri ya moto wa Jehanum na sio kuchomwa kama wengi walivyotafsiri au wanavyojua.

Mungu Mkuu hukupa na anatoa kitu kulingana na mtu au kiumbe husika, Ulimwengu wa wapenda haki, wapenda dhulma, wenye upendo, wenye chuki, wasema uongo na wauaji, ulimwengu wa wasema kweli na watoa uzima.

Ni wewe tuu unachagua wapi unapenda na hayo ndio yatakuwa maisha yako mpaka Mungu Mkuu atakapoona imetosha. Ukitaka kubadili vitu upendavyo ni wewe, lakini mpaka Mungu atakapoona inatosha, uende katika Ulimwengu mwingine.

Ni kama hapa Duniani, vile unavyoishi ndivyo ulivyoamua kuishi au wazazi wako walivyotaka uishi (kumbuka ulikuwa katika mwili wa wazazi wako). Hakuna kulaumiana wala hakuna wakumlaumu. Hayo ndio maisha!

Acha nipumzike sasa,
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
kuna sehemu Mungu amekusikia Fimbo umfuate
Kuna sehemu amekusikia fimbo umfuate achana naye kwanin uteseke
If you think education is expensive try ignorant

Kuna watu kibao hawana dini na wanaishi kawaida kama huamin mapokeo yake achane naye sababu huwezi mbadilisha
 
Baada ya UASI mbinguni
Mungu alituumba kwa mfano wake, lengo kuu ni tumuabudu.
Kwa kutamka vyote vikawa

Shetani akaileta dhambi duniani

Mungu akamtuma Yesu atukomboe kwa kufa.

Tukapokea Neema na Rehema

Mungu ataangamiza dhambi na dunia ya dhambi, kama binadamu naye ni mdhambi itampasa naye aangamizwe.
Mungu mwenye kujua yote, Je Hakujua kwamba shetani atakuja kuwepo amdhibiti?

Mungu mwenye kujua yote tangu mwanzo na hata milele, Alishindwaje kuumba Binadamu na dunia isiyo na dhambi?

Mungu muweza wa yote, Alishindwaje kumdhibiti shetani tangu mwanzo wa uasi?
 
Wanao sema hakuna Mungu naomba mniambie
Ni nini chanzo cha ulimwengu,maji,hewa ardhi na viumbe hai.

Kifo ni nini.
Mimi sifahamu fika chanzo cha huo ulimwengu.

Na naamini hakuna ajuaye zaidi ya nadharia tu,

Wewe unaweza kuwa unajua chanzo cha hayo uliyoyasema ili unieleze nami nisiwe mjinga tena!?
 
Mbingu haipo, ni hadithi tu

Hata huyo Mungu na shetani ni hadithi tu, hawapo in real dimension.

Kwanini Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote alimshusha shetani kwenye sayari hii ya dunia?

Kwanini asimshushe hata Alpha centauri B huko nje ya solar system?
Kama wewe huamin hakuna ni uhuru wako kuamini hivyo sababu hujashikia fimbo umwamini

Lakin sis wengine tunaamini mbingu ipo tutaendelea kuamini
 
Mungu mwenye kujua yote, Je Hakujua kwamba shetani atakuja kuwepo amdhibiti?

Mungu mwenye kujua yote tangu mwanzo na hata milele, Alishindwaje kuumba Binadamu na dunia isiyo na dhambi?

Mungu muweza wa yote, Alishindwaje kumdhibiti shetani tangu mwanzo wa uasi?
Mungu ameshindwa kila kitu basi kuwa mpagani sio lazima umwamin najiulizaga kwanini unateseka kwa kitu au jambo umesha-rule ni uongo we achana naye
 
Anaandika Robert Heriel,
Mtibeli.

Kuna Mungu Muumba wa mbingu na nchi halafu kuna miungu. Mungu Mkuu ambaye hajawahi kuonekana na kamwe hatokuja kuonekana Daima milele, hawezi kufanya wala kuwaza huo upuuzi wa kuchoma watu, hilo haliwezekaniki!

Miungu hii inayoabudiwa ndio inaweza kufanya hivyo, lakini yule Mungu wa miungu huo muda hana, na hawezi kufanya hivyo.

Mungu Mkuu ni Upendo, na kamwe upendo haulazimishwi. Yaani, ati Mungu aliyekuumba akulazimishe umpende (umuabudu) wakati alikuwa na uwezo wa kukuumba automatic ukawa unampenda!

Kwanza umpende (umuabudu) ili yeye apate nini? Halafu usipompende ati akuchome, wewe kosa lako lipo hapo? Yaani moyo wako haumpendi Mungu aliyekuumba, unapenda jambo jingine nini kosa lako, iko wapi haki hapo?

Mungu mwenye Upendo na muweza wa yote, anataka mtu apende anachokipenda! Kwanza yeye ndio aliyekufanya uwe hivyo ulivyo, upende unayoyapenda, achana na yale unayoyatamani na kuyachukia.

Huwezi lazimisha kupendwa bhana, na kamwe Mungu hawezi kukulazimisha umpende. Kukulazimisha haibadilishi ukweli kuwa haumpendi. Kumbuka Mungu ni Haki na Kweli.

Mchongo ukoje? Ipo hivi;

Jinsi uonavyo Ulimwengu wa nje (huu unaoonekana) ndivyo katika Ulimwengu wa ndani usioonekana, Ulimwengu wa Nafsi.

Itazame Dunia, Dunia ni moja lakini inamazingira tofauti tofauti, kuna sehemu zenye baridi kali mpaka barafu, kuna sehemu za jangwa, kuna sehemu za hali ya hewa ya kati, kuna sehemu zenye mvua nyingi, na zipo zenye mvua za Waarabu.

Kuna milimani na mabondeni, sehemu zenye maziwa, mito na bahati, sehemu yenye misitu mine, nyasi na vichaka, sehemu yenye wanyama wa aina hii sehemu nyingine hakuna.

Sasa ni uchaguzi wa mtu kutumia kile akipendacho, ukitaka kuishi kwenye baridi ni wewe, Mungu hawezi kukulazimisha uishi sehemu isiyo ya baridi wakati wewe unapenda. Haipo hiyo. Ukitaka kula chakula au wanyama fulani ni wewe mwenyewe.

Ila elewa kuwa vipo vitu ni sumu na cool vitu sio sumu. Ni wewe mwenyewe unachagua ule sumu au usile. Nasema ni wewe mwenyewe, ni kutokana na upendo wako.

Kama unavyoishi hapa Duniani kulingana na umri wako, jinsia yako, kipato na hadhi yako, mtazamo wako ndivyo nafsi yako itakavyoishi baada ya mwili wako kuondoka.

Mfano huwezi ishi Masaki, Mikocheni, Upanga wakati kipato chako na daraja lako ni kuishi kwa walalahoi huko.

Kunguru na njiwa hawawezi kaa pamoja, wanasema ndege wafananao huruka pamoja. Nenda hata wodini huko mahospitalini utaona kabisa kuwa mgonjwa wa akili hawezi lazwa wodi ya wazazi au mgonjwa aliyemahututi hawezi lazwa wodi ya wagonjwa wa meno.

Maisha ni uchaguzi wa mtu mwenyewe. Mungu kamwe hana huo muda wa kukuamulia nini chakupenda. Kuku hawezi zaa bata, kila mmoja atakaa sehemu yake. Vivyohivyo hata ukifa roho yako itaenda mahali inapopapenda, na wala hautachomwa moto.

Kama unapenda uzinzi na kuchukua wake za watu na kuua watu basi nafsi yako itaishi katika Ulimwengu wa watu wa aina yako ili mchukuliane wake na waume zenu kwa jinsi mpendavyo, ili muone utamu wa kile mnachokipenda.

Sheria siku zote sio upendo, Sheria hizi za nchi zipo kwaajili ya kudhibiti matendo ha mwili na sio nafsi. Upendo upo kwenye nafsi ya mtu wakati sheria ipo katika mwili wa mtu. Mtu anapoua akahukumiwa jela kinachoadhibiwa ni mwili wake lakini nafsi yake haiadhibiwi.

Utalipwa sawasawa na matendo ya nafsi yako, Dhamiri na utapelekwa kwenye Ulimwengu unaofanana na nafsi yako. Hiyo ndio tafsiri ya moto wa Jehanum na sio kuchomwa kama wengi walivyotafsiri au wanavyojua.

Mungu Mkuu hukupa na anatoa kitu kulingana na mtu au kiumbe husika, Ulimwengu wa wapenda haki, wapenda dhulma, wenye upendo, wenye chuki, wasema uongo na wauaji, ulimwengu wa wasema kweli na watoa uzima.

Ni wewe tuu unachagua wapi unapenda na hayo ndio yatakuwa maisha yako mpaka Mungu Mkuu atakapoona imetosha. Ukitaka kubadili vitu upendavyo ni wewe, lakini mpaka Mungu atakapoona inatosha, uende katika Ulimwengu mwingine.

Ni kama hapa Duniani, vile unavyoishi ndivyo ulivyoamua kuishi au wazazi wako walivyotaka uishi (kumbuka ulikuwa katika mwili wa wazazi wako). Hakuna kulaumiana wala hakuna wakumlaumu. Hayo ndio maisha!

Acha nipumzike sasa,
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Hujielewi kijana.

Ukisikia Mungu ndiye hakimu wa haki unaelewa nini?

Kuna watu dunia hii wanaringia vyeo vyao pesa zao kuwanyanyasa wengine ,kuwadhulumu nafsi zao nk ,hao watu wanaringia kwa sababu hakuna lolote wanaweza kufanya, sasa haki ya huyu mnyonge aliyedhulumiwa iwe kuishi au kunyanyaswa vyovyote vile Mungu ndiye husimama kama hakimu kujikimu kesi hii.

Bila Mungu kutoa adhabu unafikiri hao watu waliodhulumiwa haki zao watazipata wapi?

Tuanzie hapa kwanza.
 
Kuna vitu hatuvioni kwa macho, je ndiyo tuseme havipo? mfano upepo,mawimbi ya sauti,electronic signals etc . Wewe kutokumuona Mungu haimaanishi hayupo
Hakuna aliyesema anataka kumuona Mungu

Ulivyovitaja vyote vinathibitishika kuwa vipo,
Vinaweza kupimwa kabisa na ikiwezekana hata kufanyiwa maneuvers.

Huyo Mungu unawezaje kumthibitisha kuwa yupo?
 
MUNGU MUUMBA MBINGU NA NCHI NI PENDO, HAKIMU WA HAKI... HUHUKUMU SAWA NA AGIZO LAKE... HAPANGIWI.... MWANADAMU AKING'ANG'ANIA JEHENAMU MUNGU AFANYEJE!!! UTAJIHUKUMU KWA MATENDO YAKO... MUNGU ALAUMIWE KWA LIPI WAKATI UCHAGUZI NI WAKO ??
Mungu muumba mbingu na nchi anawezaje kuwa Pendo, Kwenye Dunia yenye Uovu, Mabaya, Magonjwa na Majanga ya asili kama radi, mafuriko, matetemeko ya ardhi, vimbunga?

Huyo Mungu mwenye upendo yupo kweli?
 
Mungu aliyeumba mbingu na nchi na vilivyomo.
Asiyejulikana hata jina lake Kwa sababu hajawahi kuonekana popote pale na Wakati wowote ule.
Kwakulazimisha uamuamin mbona unalazamisha mambo hayana mantiki
We kuwa mpagani hata kufanya chochote sababu wewe hutakua wakwanza

Kuna namna nakuonaga una upeo mdogo sana wa maisha kila siku unaanzisha uzi wa kumponda Mungu inshort huna content sababu mada zako ni zile zile kila siku

Unachofanya hata sio unique wala acts of genius kama lengo lako unalotaka lionekane watu kibao walishamkataa Mungu na wakaanzisha dini yao inaitwa atheist
 
Hujielewi kijana.

Ukisikia Mungu ndiye hakimu wa haki unaelewa nini?

Kuna watu dunia hii wanaringia vyeo vyao pesa zao kuwanyanyasa wengine ,kuwadhulumu nafsi zao nk ,hao watu wanaringia kwa sababu hakuna lolote wanaweza kufanya, sasa haki ya huyu mnyonge aliyedhulumiwa iwe kuishi au kunyanyaswa vyovyote vile Mungu ndiye husimama kama hakimu kujikimu kesi hii.

Bila Mungu kutoa adhabu unafikiri hao watu waliodhulumiwa haki zao watazipata wapi?

Tuanzie hapa kwanza.
That is your wishful thinking tu,

Hakuna wa kuwawajibisha hao.

Unataka kusema Simba bob junior nae atalipiwa aliyofanyiwa!?
 
Back
Top Bottom