Mungu mwenye Upendo hawezi kuchoma watu kwa moto. Huo ni Ushetani

Mungu mwenye Upendo hawezi kuchoma watu kwa moto. Huo ni Ushetani

Kwahyo dhambi haijaanzishwa na shetani.....hio idea ya dhambi aliweka mungu mwenyewe....au ndo utakuja kwenye story za tunda la mtini ...ya nini yote hayo Hadi kuweka Hilo tunda kama kweli alitaka tuishi tu bila huo ufaham ...hakuona kwenye CCTv camera zake kwamba huyu Eva ata muingiza mkenge Adam.... Ujue mungu asitutanie ..Yan ajue kinachofata na bado ahukum

hapana siji na story za tunda usibeti.

huoni kama hilo tunda lilikuwa ni la muhimu sana mpaka wewe sasa hivi unajiamulia tu utoe ndogo au uichunge!!!

maana kabla njia ilikuwa ni moja tu,hakuna hata anayejua hata kama inaliwa.
 
MPAKA SASA UPO NEUTRAL

kaka robert kadri unavyozidi kusoma naona unafunguka kuwa tu mkweli kama sisi mungu mwenye upendo wote, ujuzi wote na nguvu zote hayupo.
Wanazunguka zunguka sana kukiri kwamba Mungu hayupo.

Yani wana jaribu kutafuta tafuta sababu za kuonesha Mungu Yupo lakini wanakwama.

Hawawezi kukubali kwamba Mungu hayupo.
 
Huwezi ukasema ni hiyari wakati usipofanya anavyotaka yeye anakuchoma moto. Anatulazimisha
Ni hiyari, QUR'AN inasema 'na tumemjaalia/mpa binaadam njia mbili,imma afuate njia ya kukufuru au ya kushukuru'..ni kama kwenye misosi tu uchague pilau nyama choma au bia,gongo nk..
 
Kama moto hakuna basi hakukuwa na sababu ya Yesu kufa msalabani, haya ni maandiko yanayothibitisha uwepo wa moto hivyo ni vyema ujue hivyo kuwa baada ya maisha ya duniani kuna kwenda motoni au mbinguni

Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.

Matayo 3:12

bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.

Waebrania 10:27

Na jicho lako likikukosesha, ling'oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;

Marko 9:47

Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,

Matayo 13:49

na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Matayo 13:50

Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.

Ufunuo 21:8
 
Muombe Mungu akusamehe kwa Uzi Huu, Kisha waombe Mods waufute Uzi Huu!!.


Ni Mungu huyuhuyu muumbaji na Upendo, aliwachoma moto sodoma na gomora sijataja zama za Nuhu, huyu Mungu alompa Samson nguvu awauwe wafilisti na maadui wa Israel, ni Mungu huyohuyo alokua anawaagiza Wana isarel wawaue maadaui zao kuanzia Watu mpaka Kuku !!.


Ni Mungu yule yule alombariki Eliya, Ayubu, Daudi,

Ni Mungu yuleyule alomponya Jenerali Naamani na wengine.

Ni Mungu alomfufua Lazaro ,na wengineo !!.


Ni Mungu yuleyule anayeturuhusu tupumue Hata Sasa tunapoandika hapaa !!!.


Kwa sisi tuonafanya kazi Ma Hosp, tunaelewa Kifo ni nini !! Na kwamba, Huchukua Sekunde Moja tu kubadili Historia ya mtu kutoka mtu kuongea, mpaka mtu kushindwa hata kufungua jicho !!.


Ni Mungu huyuhuyu aloruhusu uwe hapo ulipo.

Ni huyohuyo Mungu, aloiweka ahadi ya kutoigharikisha Dunia Kwa maji badala yake akasema, NITAICHOMA DUNIA NA WADHAMBI WOTE KATIKA ZIWA LIWAKALO MOTO.


Njia pekee ya kuukumbia Huu moto ni Kutokufanya dhambi, na tutaliweza Hilo Kwa kumuomba Mungu ili atupe Uwezo na neema zake, huku wenyewe tukichukua Jitahada binafsi.




HAKIKA, KICHWA CHA MWANADAMU KINAWAZA UPUMBAVU,,,, ILA MWANADAM ANAPOFIKIA HATUA YA KUFANYA KUFURU KWA MUNGU, NI ZAIDI YA UPUMBAVU !!.


UWEZO NA UKUU WA MWANADAMU, KAMWE HAUCHUNGUZIKI !!! NI MUNGU ATABAKI KUA MUNGU !!.
Mzee wa kazi kumbe ukitulia unaandika madini sana..
 
😀😀

Waliumbwa hivyo.
Hawatakuja Kupata uthibitisho Kwa sababu hakuna aliyewahi kumuona huyo Mungu Mkuu, Kwanza Hana mfano, alafu hafanani na chochote, yaani Kwa Lugha nyepesi ukisema hayupo haujakosea na ukisema yupo haujakosea.

Na kusema Mungu Mkuu hayupo haibadilishi chochote kuwa yupo au hayupo, haimuumi Kwa sababu hata Hilo wazo la kusema hayupo au yupo linatoka kwake.
anafanana na binadamu mkuu
 
Source ya mawazo hayo ni ipi ? kama hakuna source wala ushahidi bali ni mawazo yako basi yatakosa nguvu kwa maana mtu yeyote anaweza kuja na mawazo tofauti na yako akiwa amebuni baada ya kushiba kande.
 
Anaandika Robert Heriel,
Mtibeli.

Kuna Mungu Muumba wa mbingu na nchi halafu kuna miungu. Mungu Mkuu ambaye hajawahi kuonekana na kamwe hatokuja kuonekana Daima milele, hawezi kufanya wala kuwaza huo upuuzi wa kuchoma watu, hilo haliwezekaniki!

Miungu hii inayoabudiwa ndio inaweza kufanya hivyo, lakini yule Mungu wa miungu huo muda hana, na hawezi kufanya hivyo.

Mungu Mkuu ni Upendo, na kamwe upendo haulazimishwi. Yaani, ati Mungu aliyekuumba akulazimishe umpende (umuabudu) wakati alikuwa na uwezo wa kukuumba automatic ukawa unampenda!

Kwanza umpende (umuabudu) ili yeye apate nini? Halafu usipompende ati akuchome, wewe kosa lako lipo hapo? Yaani moyo wako haumpendi Mungu aliyekuumba, unapenda jambo jingine nini kosa lako, iko wapi haki hapo?

Mungu mwenye Upendo na muweza wa yote, anataka mtu apende anachokipenda! Kwanza yeye ndio aliyekufanya uwe hivyo ulivyo, upende unayoyapenda, achana na yale unayoyatamani na kuyachukia.

Huwezi lazimisha kupendwa bhana, na kamwe Mungu hawezi kukulazimisha umpende. Kukulazimisha haibadilishi ukweli kuwa haumpendi. Kumbuka Mungu ni Haki na Kweli.

Mchongo ukoje? Ipo hivi;

Jinsi uonavyo Ulimwengu wa nje (huu unaoonekana) ndivyo katika Ulimwengu wa ndani usioonekana, Ulimwengu wa Nafsi.

Itazame Dunia, Dunia ni moja lakini inamazingira tofauti tofauti, kuna sehemu zenye baridi kali mpaka barafu, kuna sehemu za jangwa, kuna sehemu za hali ya hewa ya kati, kuna sehemu zenye mvua nyingi, na zipo zenye mvua za Waarabu.

Kuna milimani na mabondeni, sehemu zenye maziwa, mito na bahati, sehemu yenye misitu mine, nyasi na vichaka, sehemu yenye wanyama wa aina hii sehemu nyingine hakuna.

Sasa ni uchaguzi wa mtu kutumia kile akipendacho, ukitaka kuishi kwenye baridi ni wewe, Mungu hawezi kukulazimisha uishi sehemu isiyo ya baridi wakati wewe unapenda. Haipo hiyo. Ukitaka kula chakula au wanyama fulani ni wewe mwenyewe.

Ila elewa kuwa vipo vitu ni sumu na cool vitu sio sumu. Ni wewe mwenyewe unachagua ule sumu au usile. Nasema ni wewe mwenyewe, ni kutokana na upendo wako.

Kama unavyoishi hapa Duniani kulingana na umri wako, jinsia yako, kipato na hadhi yako, mtazamo wako ndivyo nafsi yako itakavyoishi baada ya mwili wako kuondoka.

Mfano huwezi ishi Masaki, Mikocheni, Upanga wakati kipato chako na daraja lako ni kuishi kwa walalahoi huko.

Kunguru na njiwa hawawezi kaa pamoja, wanasema ndege wafananao huruka pamoja. Nenda hata wodini huko mahospitalini utaona kabisa kuwa mgonjwa wa akili hawezi lazwa wodi ya wazazi au mgonjwa aliyemahututi hawezi lazwa wodi ya wagonjwa wa meno.

Maisha ni uchaguzi wa mtu mwenyewe. Mungu kamwe hana huo muda wa kukuamulia nini chakupenda. Kuku hawezi zaa bata, kila mmoja atakaa sehemu yake. Vivyohivyo hata ukifa roho yako itaenda mahali inapopapenda, na wala hautachomwa moto.

Kama unapenda uzinzi na kuchukua wake za watu na kuua watu basi nafsi yako itaishi katika Ulimwengu wa watu wa aina yako ili mchukuliane wake na waume zenu kwa jinsi mpendavyo, ili muone utamu wa kile mnachokipenda.

Sheria siku zote sio upendo, Sheria hizi za nchi zipo kwaajili ya kudhibiti matendo ha mwili na sio nafsi. Upendo upo kwenye nafsi ya mtu wakati sheria ipo katika mwili wa mtu. Mtu anapoua akahukumiwa jela kinachoadhibiwa ni mwili wake lakini nafsi yake haiadhibiwi.

Utalipwa sawasawa na matendo ya nafsi yako, Dhamiri na utapelekwa kwenye Ulimwengu unaofanana na nafsi yako. Hiyo ndio tafsiri ya moto wa Jehanum na sio kuchomwa kama wengi walivyotafsiri au wanavyojua.

Mungu Mkuu hukupa na anatoa kitu kulingana na mtu au kiumbe husika, Ulimwengu wa wapenda haki, wapenda dhulma, wenye upendo, wenye chuki, wasema uongo na wauaji, ulimwengu wa wasema kweli na watoa uzima.

Ni wewe tuu unachagua wapi unapenda na hayo ndio yatakuwa maisha yako mpaka Mungu Mkuu atakapoona imetosha. Ukitaka kubadili vitu upendavyo ni wewe, lakini mpaka Mungu atakapoona inatosha, uende katika Ulimwengu mwingine.

Ni kama hapa Duniani, vile unavyoishi ndivyo ulivyoamua kuishi au wazazi wako walivyotaka uishi (kumbuka ulikuwa katika mwili wa wazazi wako). Hakuna kulaumiana wala hakuna wakumlaumu. Hayo ndio maisha!

Acha nipumzike sasa,
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Haloo, nimeishia njiani siwezi kumalizia kusoma huo ni upotoshaji namim sitaki kupotea kama wewe, maana yako nishaijua yaan huna tofauti na serikali kuhusu suala la bandari wako katkat kurudi nyuma hawawezi kwenda mbele nako imekuwa ngumu, ko ata wewe na wenzio najua hauko peke yako... yaani mnajifariji kwakuwa mmejikinai kwa kutenda maovu ndipo sa huoni pa kukimbilia ko mmeamua kujitaftia namna ya kujifurahisha katika dhambi, lakini ukweli ni kwamba nafsi lazima inakushtaki tu, ushauri wangu....mungu anasamehe kabisaaa na unaanza maisha mapya...
 
Hivi wewe naomba nikuulize, iv unajua kwanini upo hai/umeletwa duniani ili iweje! ukinijibu hilo naungana nawewe kwenye imani yako
 
Anaandika Robert Heriel,
Mtibeli.

Kuna Mungu Muumba wa mbingu na nchi halafu kuna miungu. Mungu Mkuu ambaye hajawahi kuonekana na kamwe hatokuja kuonekana Daima milele, hawezi kufanya wala kuwaza huo upuuzi wa kuchoma watu, hilo haliwezekaniki!

Miungu hii inayoabudiwa ndio inaweza kufanya hivyo, lakini yule Mungu wa miungu huo muda hana, na hawezi kufanya hivyo.

Mungu Mkuu ni Upendo, na kamwe upendo haulazimishwi. Yaani, ati Mungu aliyekuumba akulazimishe umpende (umuabudu) wakati alikuwa na uwezo wa kukuumba automatic ukawa unampenda!

Kwanza umpende (umuabudu) ili yeye apate nini? Halafu usipompende ati akuchome, wewe kosa lako lipo hapo? Yaani moyo wako haumpendi Mungu aliyekuumba, unapenda jambo jingine nini kosa lako, iko wapi haki hapo?

Mungu mwenye Upendo na muweza wa yote, anataka mtu apende anachokipenda! Kwanza yeye ndio aliyekufanya uwe hivyo ulivyo, upende unayoyapenda, achana na yale unayoyatamani na kuyachukia.

Huwezi lazimisha kupendwa bhana, na kamwe Mungu hawezi kukulazimisha umpende. Kukulazimisha haibadilishi ukweli kuwa haumpendi. Kumbuka Mungu ni Haki na Kweli.

Mchongo ukoje? Ipo hivi;

Jinsi uonavyo Ulimwengu wa nje (huu unaoonekana) ndivyo katika Ulimwengu wa ndani usioonekana, Ulimwengu wa Nafsi.

Itazame Dunia, Dunia ni moja lakini inamazingira tofauti tofauti, kuna sehemu zenye baridi kali mpaka barafu, kuna sehemu za jangwa, kuna sehemu za hali ya hewa ya kati, kuna sehemu zenye mvua nyingi, na zipo zenye mvua za Waarabu.

Kuna milimani na mabondeni, sehemu zenye maziwa, mito na bahati, sehemu yenye misitu mine, nyasi na vichaka, sehemu yenye wanyama wa aina hii sehemu nyingine hakuna.

Sasa ni uchaguzi wa mtu kutumia kile akipendacho, ukitaka kuishi kwenye baridi ni wewe, Mungu hawezi kukulazimisha uishi sehemu isiyo ya baridi wakati wewe unapenda. Haipo hiyo. Ukitaka kula chakula au wanyama fulani ni wewe mwenyewe.

Ila elewa kuwa vipo vitu ni sumu na cool vitu sio sumu. Ni wewe mwenyewe unachagua ule sumu au usile. Nasema ni wewe mwenyewe, ni kutokana na upendo wako.

Kama unavyoishi hapa Duniani kulingana na umri wako, jinsia yako, kipato na hadhi yako, mtazamo wako ndivyo nafsi yako itakavyoishi baada ya mwili wako kuondoka.

Mfano huwezi ishi Masaki, Mikocheni, Upanga wakati kipato chako na daraja lako ni kuishi kwa walalahoi huko.

Kunguru na njiwa hawawezi kaa pamoja, wanasema ndege wafananao huruka pamoja. Nenda hata wodini huko mahospitalini utaona kabisa kuwa mgonjwa wa akili hawezi lazwa wodi ya wazazi au mgonjwa aliyemahututi hawezi lazwa wodi ya wagonjwa wa meno.

Maisha ni uchaguzi wa mtu mwenyewe. Mungu kamwe hana huo muda wa kukuamulia nini chakupenda. Kuku hawezi zaa bata, kila mmoja atakaa sehemu yake. Vivyohivyo hata ukifa roho yako itaenda mahali inapopapenda, na wala hautachomwa moto.

Kama unapenda uzinzi na kuchukua wake za watu na kuua watu basi nafsi yako itaishi katika Ulimwengu wa watu wa aina yako ili mchukuliane wake na waume zenu kwa jinsi mpendavyo, ili muone utamu wa kile mnachokipenda.

Sheria siku zote sio upendo, Sheria hizi za nchi zipo kwaajili ya kudhibiti matendo ha mwili na sio nafsi. Upendo upo kwenye nafsi ya mtu wakati sheria ipo katika mwili wa mtu. Mtu anapoua akahukumiwa jela kinachoadhibiwa ni mwili wake lakini nafsi yake haiadhibiwi.

Utalipwa sawasawa na matendo ya nafsi yako, Dhamiri na utapelekwa kwenye Ulimwengu unaofanana na nafsi yako. Hiyo ndio tafsiri ya moto wa Jehanum na sio kuchomwa kama wengi walivyotafsiri au wanavyojua.

Mungu Mkuu hukupa na anatoa kitu kulingana na mtu au kiumbe husika, Ulimwengu wa wapenda haki, wapenda dhulma, wenye upendo, wenye chuki, wasema uongo na wauaji, ulimwengu wa wasema kweli na watoa uzima.

Ni wewe tuu unachagua wapi unapenda na hayo ndio yatakuwa maisha yako mpaka Mungu Mkuu atakapoona imetosha. Ukitaka kubadili vitu upendavyo ni wewe, lakini mpaka Mungu atakapoona inatosha, uende katika Ulimwengu mwingine.

Ni kama hapa Duniani, vile unavyoishi ndivyo ulivyoamua kuishi au wazazi wako walivyotaka uishi (kumbuka ulikuwa katika mwili wa wazazi wako). Hakuna kulaumiana wala hakuna wakumlaumu. Hayo ndio maisha!

Acha nipumzike sasa,
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Umesema kwasasa ni wapiii?
 
Why people wanalazimisha uwepo wa Mungu while ukifikiria kwa undani kuna vitu unaona kabisa havipo sawa ... wat daz it mean? Ina maana mimi pekee ndie mwenye ubongo mbovu au mim nafikiria tofaut na wengine au shida ni ipi hasa mpaka nakuwa tofauti na wengine kwenye kufikiria haya mambo?
 
Kwanini umeamua kusema hayo? Mbona ni Mungu mwenyewe anayekuambia kuwa moto ameandaliwa shetani na wafuasi wake? Kwani wewe umeamua kuwa mfuasi wa shetani? Kwanini hutaki kufanya toba na kumrudia Mola wako?

Hakika anasema tumwelekee kwa toba, ibada, sadaka na zaka. Mungu wetu ni mwema sana. Tukimfuata hakika tutaufikia ufalme wake wa furaha na amani.
 
Why people wanalazimisha uwepo wa Mungu while ukifikiria kwa undani kuna vitu unaona kabisa havipo sawa ... wat daz it mean? Ina maana mimi pekee ndie mwenye ubongo mbovu au mim nafikiria tofaut na wengine au shida ni ipi hasa mpaka nakuwa tofauti na wengine kwenye kufikiria haya mambo?
Bado hujaionja furaha ya kuwa ndani ya Yesu.
 
Back
Top Bottom