Mungu ndiye aliyempa Urais Mama Samia. Hawezi kushushwa na Mwanadamu mwenye chuki binafsi

Mungu ndiye aliyempa Urais Mama Samia. Hawezi kushushwa na Mwanadamu mwenye chuki binafsi

Basi walaumuni mawakala wenu mliowaamini maana sisi CCM mawakala wetu walisimama imara kusimamia Kura zetu, kwa hiyo kumbe mnaogopa polisi🤣🤣🤣, Basi tutawaletea Tena polisi mkileta makelele yenu😆😆

Kwani mawakala wa CCM huwa wanasumbuliwa na vyombo vya dola mpaka useme walisimama imara? Hatuogopi vyombo vya dola, ila sisi hatushindani kwa silaha bali siasa.
 
Ukiseek followers jua wewe sio leader babu, do ya things wenyewe watajisalimisha ukiwapendeza.
 
Rais Samia Ni kiongozi shupavu na madhubuti Sana, ndio maana unaona nchi ikiwa Tulivu na Amani, Ndio sababu unaona kila kero Inayojitokeza mbele yetu ikikabiliwa kishupavu na serikali yetu, ndio sababu unaona namna tulivyo fanikiwa katika secta nyingi ndani ya muda mfupi wa uongozi wake mama Samia
Utulivu na Amani uliopo ni feki kwa sababu tunaaminishwa kwamba nchi hii ni tulivu na Amani.ila ukweli ni kwamba MTU utapataje Amani hakuna maji,umeme,vyakula bei juu,bando hazinunuliki NK na uchumi bado ni mmbovu Sana huku unaona viongozi wakiiba hela.
 
Rais Samia Suluhu ni kiongozi ambae watanzania wengi tulitamani kua nae hatumii nguvu yeye anatumia akili nyingi sana kuendesha nchi
Kama anatumia akili nyingi lakini Hali IPO hivi siku akianza kutumia akili kidogo si hali itakuwa mbaya zaidi?
 
Haya mwambie mama ako alete maji na umeme uskatike katike
 
KKaika kktu wadhungu walifanikiwa kuhakikisha wanamtawala mwafrica ni kumletea dini. Imetufanya tushindwe kufirki na kuishi kusema "mipango ya mungu"
Hata Hitler na holocust yake yawezekana walisema hivo. Tunakwepa kuwa responsible kwa kumsingizia Mungu na shetani.
 
Kwani mawakala wa CCM huwa wanasumbuliwa na vyombo vya dola mpaka useme walisimama imara? Hatuogopi vyombo vya dola, ila sisi hatushindani kwa silaha bali siasa.
Hata sisi tunashindana kupitia majukwaa na kuendesha siasa na kampeni kisayansi
 
NI sawaa lkn

Huyo huyo lkn huyohuyo MUNGU atamtoaa
Mchana kweupee ,Mungu hapendi Kuona watu wake wanatesekaaa

Hivyo Majibu ni mapema subiri Mungu ashulike
Ndugu zangu Uongozi unatoka Kwa Mwenyezi Mungu anayetufahamu sisi Tungali katika Matumbo ya Mama zetu, Yeye Ndiye Anayejuwa hatima yetu, yeye ndiye mtoa Riziki, Neema na Baraka, yeye ndiye kiongozi mkuu wa viongozi wote hapa chini ya jua. Ndiye mtoa Maarifa na Njia kwa wale wamchao na kufuata njia zake.

Rais Samia yupo hapo ,Amefika hapo kwa kuwa Mwenyezi Mungu Alimuandikia kufika hapo. Mama Samia Hajafika hapo kwa uweza wa Mwanadamu, hajafika hapo kwa ujanja wake, kwa Akili zake, kwa Dini yake,kwa kabila lake, kwa jinsia yake, kwa nguvu zake, kwa mipango ya kiuanadamu, kwa Fedha zake, kwa ukarimu wake, upole wake, ucheshi wake, sura yake, Mwendo wake, Sauti yake, Umbo lake, kimo chake, Maono yake, mikakati na mbinu zake, familia yake na Elimu yake.

Mama Samia Amefika Hapo kwa uweza wa Mwenyezi Mungu, Amefika Hapo kwa mipango ya Mwenyezi Mungu, Amefika Hapo kwa kuwa ndivyo ambavyo Mwenyezi Mungu alimwandikia hivyo, Kwa kuwa ndivyo Mwenyezi Mungu alipanga iwe Hivyo, Ndivyo Ambavyo alitaka agano litimie katika ulimwengu wa kiroho wa uumbaji wa Mama Samia Tangia Akiwa Tumboni mwa mama yake

Mbele za Mwenyezi Mungu kila Jambo na wakati wake na majira yake, huu ulikuwa Ni wakati wa Mama Samia, Haya Ni majira ambayo MWENYEZI MUNGU alipanga iwe Hivyo kwa Rais Samia kuinuliwa kiuongozi kuongoza nchi yetu, siyo sisi wanadamu, siyo sisi tuliyo waamuzi. Ni Mungu Ndiye Aliyempaka Rais Samia Mafuta ya Uongozi, Ni Mungu Ndiye aliyempa kibali Cha kufika Hapo. Ni Mungu Ndiye aliyemcholea Ramani yake na njia yake kufika hapo, Ni Mungu Ndiye aliyemshika mkono kumfikisha hapo, Ni Mungu Ndiye Aliyemvusha katika mabonde na milima, katika majaribu na mitihani, ni Mungu Ndiye aliye mpitisha njia ambayo wengine hawakupitishwa, Ni Mungu Ndiye aliyemlinda na kumpigania kufika hapo.

kwote alikopita na kufanya na watu kazi ilikuwa ni mipango ya Mungu katika Kumwandaa na kumfundisha namna ya kuishi na watu wa aina zote, hao watu na hayo maeneo ya kikazi ilikuwa Ni madaraja tu ya kumvusha, lakini Mipango ya Mungu ilikuwa ni kumuinua Hadi hapa Alipo kwa Sasa nafasi ya mwisho kiuongozi na kicheo. Hivyo Hakuna wakumshushaa Mama Huyu Mzalendo wa kweli.

Sasa wewe Mwanadamu Ni Nani mbele za Mwenyezi Mungu? Ni Nani aliyewahi kuongoza kwa akili zake akafanikiwa? Ni Nani awezaye kushindana na Mwenyezi Mungu? Ni Nani kwa Fedha zake Amewahi kununua Urais wa nchi hii? Ni Nani kwa kusuka makundi ya kumshambulia na kumhujumu Rais wake amewahi kufanikiwa kupata Urais wa nchi hii? Ni Nani huyo? Yupo wapi? Wangapi walikuwa na mapesa na marafiki wenye mapesa waliojaribu kununua Urais lakini hawajawahi kufanikiwa? Wangapi wamewahi kuutamani Urais lakini bado wanausikia kwenye Redio? Nani alitegemea Odinga atafika Hadi Leo hii bila kuapishwa kuwa Rais ? Vipi Hillary Clinton? Nani alitegemea mfungwa Nelson Mandela atakuja kupata heshima ya ulimwengu?

Ndugu zangu Amini Amini Nawaambieni kuwa Kama Haikupangwa Na Mwenyezi Mungu Wewe uwe kiongozi Au Rais Basi Tambua kuwa Hata Ufanyeje utaishia kusononeka tu Moyoni Mwako pale utakapoona miaka inayoyoma huku hakuna Dalili za wewe kutimiza Ndoto Zako.

Rais Samia huwezi Ukamchafua na kumpaka matope kwa watanzania na ukafanikiwa,kwa sababu watanzania tunamkubali Sana Rais Samia kwa kuwa ameonyesha dhamira ya dhati katika kulitumikia Taifa hili, Amekuwa mkweli na muwazi Sana katika kuongoza Taifa letu, kwa kila changamoto tuipitiayo amekuwa mkweli kueleza mikakati ya kukabiliana nayo

Rai Yangu kwa Wana CCM wenzangu na Wazalendo Wa Taifa Hili Tusikubali kuchonganishwa na wenye maslahi Binafsi,Tusikubali watugawe Wala kutupandikiza mbegu za chuki, Marais wote Watano waliopita na kumtangulia Rais wetu mpendwa na kipenzi cha watanzania mama shupavu.

Rais Samia walikuwaa Ni wanaccm na waliotekeleza ilani ya ccm, Hivyo asitokee mtu wakutuletea mbegu za wale na sisi. CCM Ni moja ,Wana CCM Ni wamoja Na Chama Ni kimoja chini ya mama yetu jasiri, Hodari, shupavu, mchapa kazi, mcha Mungu, Mzalendo Na mwenye Dhamira ya Dhati na Taifa hili Mama Samia Suluhu Hassan Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama na Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake
 
NI sawaa lkn

Huyo huyo lkn huyohuyo MUNGU atamtoaa
Mchana kweupee ,Mungu hapendi Kuona watu wake wanatesekaaa

Hivyo Majibu ni mapema subiri Mungu ashulike
Mwenyezi Mungu Ndiye aliyemuinua Rais Samia kufika hapo Alipo fika na ndio anayeendelea kumpa maarifa ya kiuongozi
 
Wewe unazisikiliza clips za kwenye mitandao za watu waliokwama? Usizisikilize
 
Nataka uthibitisho mamlaka aliyo nayo Rais yametoka kwa Mungu.

Nataka pia ufafanuzi jinsi gani unafahamu mamlaka ya Rais au kiongozi fulani yanatoka au hayatoki kwa Mungu. Vigezo gani unatumia?
Unataka uthibitisho katika lipi maana nimetoa hoja 5 hapo?

Katika zote tano hujapata kuelewa hata moja..?

Mathalani. Je, unakataa kuwa mamlaka ya u - Rais aliyo Samia Suluhu (Rais kwa sasa) yanatoka kwa Mungu..?

Kwenye hili unataka nithibitishe kwa namna gani kwa mfano maana kama huamini hili, basi tatizo ni lako kwa kutoamini kwako...!

However, nitafurahi iwapo utakuwa specific unataka uthibitisho katika hoja gani kati ya hizo zote 5...

Thanx
 
Mimi nipo mtaani nako kutana na watanzania wenzangu wa ainaa zote, ambapo kiukweli Ni kuwa Rais Samia anakubalika Sana huku mitaani , hata hili suala la umeme ameeleweka vizuri maana hata wananchi nao wanaona ukame uliopo ambapo hata maeneo yanayokuwag na maji mpaka muda huu kila mmoja anaona namna yalivyokauka,hivyo watanzania bado Wana Subira na kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa na serikali yetu ambayo imekuwa ikifanya mambo kwa uwazi na kuwaeleza watanzania kila kinachokuwa kinaendelea na hatua zinazokuwa zimechukuliwa katika kila kero
Mkuu unanikbusha Malaria Sugu alivyokuwa anamtetea Dkt Kikwete hahahahaha pole sana. Nime dislike comments zako kwa sababu wewe ni mtu mbaya sana mnafiki mkubwa ambaye hauitakii CCM mema na Rais Wetu Samia.
 
Back
Top Bottom