Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mkuu napokuandikia ujumbe huu,ujue wewe ulibarikiwa kupata bahati ya kushirikiana na wale watu wa haki ambao ni washirika wa walokole wanaomwakilisha mwana wa mmliki ambae wanajimu wanamwita""NYOTA YA MASHARIKI NA MSHINDI WA MLIKI ZA ANGA.!!!
Ukichukua hatua ya kumuamini na kuanza kuhubiri INJILI, lazima utashirikiana nao.
 
MI KINACHONISIKITISHA

Ni kama KILA kitu kilipangwa kabla hata misingi ya ulimwengu haijakuwepo!!

Yaani hata hao wa jehanam na hao wa peponi walipangiwa kuwa fate yao itakua hivyo!!

Unafikiri huyo shetani alipoumbwa na kuwa shetani ilikua by surprise!!?

Yaani chanzo kikuu cha vyote hivi ni muumba mwenyewe hakuna Bahati mbaya wakuu!!

Uwepo wa shetani,moto,pepo vyote ni mpango KAZI hata hao watakaoingia ni mpangokazi rasmi hakuna Bahati mbaya KWA lolote itategemea yeye muumba alikuandikia nini coz hakuna anaewez and kujifanya mtakatifu wala muovu isipokua KWA Mapenzi yake yeye aliemuumba yeye na pande ZOTE mbili yaani shetani na upande wa pili!!!

Ni hayo tu!!
 
Umesoma andiko lote?amesema walokole wamo kwenye makanisa yote na hata nje ya makanisa ikiwemo mashambani,kazini,barabarani n.k,tena kwenye makanisa mengine yanoyojiita ya kilokole/pentecostal walokole hawamo kabisa kwa hiyo akasema ulokole ni mahusiano ya mtu na Mungu sio mahali anaposali.
Upo sahii mkuu
 
MI KINACHONISIKITISHA

Ni kama KILA kitu kilipangwa kabla hata misingi ya ulimwengu haijakuwepo!!

Yaani hata hao wa jehanam na hao wa peponi walipangiwa kuwa fate yao itakua hivyo!!

Unafikiri huyo shetani alipoumbwa na kuwa shetani ilikua by surprise!!?

Yaani chanzo kikuu cha vyote hivi ni muumba mwenyewe hakuna Bahati mbaya wakuu!!

Uwepo wa shetani,moto,pepo vyote ni mpango KAZI hata hao watakaoingia ni mpangokazi rasmi hakuna Bahati mbaya KWA lolote itategemea yeye muumba alikuandikia nini coz hakuna anaewez and kujifanya mtakatifu wala muovu isipokua KWA Mapenzi yake yeye aliemuumba yeye na pande ZOTE mbili yaani shetani na upande wa pili!!!

Ni hayo tu!!
Mapepo, wafu,majini,shetani na Ulimwengu wa Giza Kwa ujumla hawana nafasi ya pili kutubu na kumrudia Mungu,

Lakini wote wenye PUMZI, WANADAMU ni uamuzi wako kuingia Mbinguni au Jehanum.

Amua sasa pa kwenda. Whether ujiunge na Mungu wa walokole au Shetani.

Amen.
 
Mkuu kwa utafiti wako Mimi najiunga na kua Mlokole kuanzia sasa
Mungu wa walokole anawazingira na moto pande zote.Wakiwa wanalima au maofisini au sokoni au barabarani na ukisikia wanakiita kitabu cha kua ni kitakatifu(Biblia)...!!!Basi ujue ni kitakatifu kweli mkuu sababu wakikiombea kinakua kinatoa herufi za moto..!!!!Upo sahii kwa uamuzi huo mkuu
 
Umesoma andiko lote?amesema walokole wamo kwenye makanisa yote na hata nje ya makanisa ikiwemo mashambani,kazini,barabarani n.k,tena kwenye makanisa mengine yanoyojiita ya kilokole/pentecostal walokole hawamo kabisa kwa hiyo akasema ulokole ni mahusiano ya mtu na Mungu sio mahali anaposali.
Makanisa ya Kilokole ndio yamefanya walokole wakawa wengi zaidi...

Kwanini...
Yamewafundisha watu kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wao kwa kufundisha neno kwa wingi...

Uhusiano na Mungu hauwezi kuja kirahisi bila kuwa na neno la Mungu au chakula Cha kiroho hivyo ni lazima litafitwe kwa bidii...na hayo makanisa ya Kilokole na Manabik wengi ndio wameokoa watu wengi...

Na yamefanya watu kuwa karibu na Mungu sana...ndio maana Sasa watu wanamuona Mungu
 
Mkuu wale watu wa mwanga hawana mzaha wanapomlinda mlokole wao.
Hujaeleza tofauti kati ya watu warefu wenye kuakisi mwanga wenye mabawa na warefu wenye kuakisi mwanga wasio na mabawa.

Maana kulingana na BIBLIA,

Luka 20:29-38, Kuna mafarisayo walimuuliza Yesu mtu akifa na mkewe akaolewa na mwingine, siku ya ufufuo mke atakuwa wa nani?

Luke 20:36 alijibu kuwa:

Mbinguni hakuna Kutoa wala kuolewa,

36;"Wala hawawezi kufa tena, Kwa Sababu Huwa sawasawa na MALAIKA, nao ni Wana wa Mungu, Kwa vile walivyo Wana wa ufufuo ".

watu walioigia Mbinguni ,tofauti Yao na Malaika ni kutokuwa na mabawa.

Hata YESU aliyefufuka, amewahi kuwatokea wengi, Hana mabawa.

WATAKATIFU wote waliowahi kuwa na miili ya WANADAMU before hawana mabawa.

Fafanua ulivyoona kuhusu Hilo.
 
NINAENDELEA.......!!!!
WANAJIMU NA WAGANGA :Wanajimu na waganga hawana usharika na walokole katika lolote lile.Wao ni washirika wa wale watu warefu wa baharini.Unajimu haufundishwi kwenye mikusanyiko ya kilokole sababu una makufuru na hatua zake nyingi zina ushirikiano na uganga.Wanajimu wanachukua nyota za wangu na kuzitumia kwa manufaa yao.Wanajimu wanafanya tafukuri ambayo ni laana kiroho.Wanajimu hawana utii kwa mkuu wa mamlaka aliye mkuu wa wote,bali wao wanatii uganga wako na miungu ya kwenye sayari za ndani ya mfumo ww jua wa ulimwengu.Wanajimu wanashirikiana na wale viumbe wa baharini kumuhujumu mwanadamu aliepo duniani.Wanajimu wanatafuta elimu ya anga kwa njia za uchawi wa kale wa kiarabu na kiajemi.Wanajimu hawana maombi ya kubariki bali wana maombi ya kulaani,kwani kwao laana ni sehemu ya matambiko yao.Hivyo wanajimu ndani ya ulimwengu wa kiroho sio watu wema.
WALE VIUMBE WAREFU :Kama nilivyosema pale mwanzo kua,kuna aina mbili za wale viumbe warefu
MOJA :Watu warefu wa angani wanaoakisi mwanga
MBILI :Watu warefu wa baharini wasioakisi mwanga.
WATU WAREFU WA ANGANI WANAOAKISI MWANGA :Wale watu warefu wazuri kwa muonekano,wanaoshika panga na kulinda walokole ni watu wa ajabu sababu ya tabasamu zao na upendo wao.Akikusogelea kwa karibu utatamani ulie kwa furaha maana unapata amani ya moyo iliyopitiliza.Wana upendo mkuu sababu ukiona jinsi wanavyowahudumia walokole lazima upendezwe nao.Walokole ni kama vitoto vidogo mbele ya hawa walinzi wao ""Watu warefu""..Upenda na ulinzi ndio sifa yao kuu.Wao ni moto ndani ya moto wa shaba,wana nguvu kama umeme wa radi.Kimuonekano wengine wana mabawa na wengine hawana mabawa ila wote warefu kwa vimo.
WATU WAREFU WA BAHARINI WASIOAKISI MWANGA :Hawa ni washirika wa waganga na wanajimu na wachawi.Kimuonekano ni watu wa kubadilika badilika.Hawana muonekano mzuri wa kudumu bali wanachukua sura halisi za binadamu,hasa binadamu wa bara hindi na uajemi.Hawana usharika na walokole sababu walokole wanaharibu kazi zao wanazofanya na wanajimu na wachawi.Hawana upendo wala amani ya moyo wakikusogelea,zaidi zaidi utasisimka na kuogopa.Ni washirika wa mkuu wa ulimwengu mwenye vita vya kudumu na walokole.Tusiwazungumzie sana hapa maana lengo sio kuwazungumzia wao bali Mungu wa walokole.
Kwa binadamu wa kawaida unakua na amani ukikutana na hawa watu warefu wa angani ambao ni walinzi wa walokole,maana wanalinda watoto,wanalinda wagonjwa,wanalinda walokole na wasiokua walokole na wanazuia majanga ya kutengenezwa na wale watu warefu wa baharini na washirika wao ambao ni wachawi na wanajimu na waganga na washirikina wa kibinadamu.Popote pale duniani kwenye ulimwengu wa kiroho utawaona wanaruka huko na huko.
Afu mungu wa walokole ambae ni mkuu wa mfumo wa anga kuu nje ya mfumo wa sayari za ulimwengu kaficha siri ya mfumo wa ulimwengu nje ya mfumo wa anga na sayari zote,,maana angani ni kama mfumo wa anga na sayari unaelea ila huwezi jua umejishikiza wapi.
Hesabu za kinajimu zina kikomo ila hesabu za unajimu wa nje ya mfumo wa ulimwengu hazina kikomo na zinaongozwa na mwana wa mmliki.Na ndio maaana huyo mwana wa mmliki na wale watu warefu weupe wanaishi milele toka dahari ya kwanza mpaka dahari isiyo na ukomo kwa kingereza wanaita""Eternity's""".
Walokole wanaposali ndio mda mzuri wa kua nao sababu mungu wao anashuka kwa njia kuu tatu(3)
MOJA :Kama njiwa mweupe wa dhahabu
MBILI :Kama moto wa mataji ya viduara na kukaa vichwani mwa walokole
TATU :Kama wingu za moto unafunika eneo zima.
Sasa kama walokole wakiwa wanasali na wewe upo karibu basi baraka zao kiroho zinakufikia mpaka wewe.Mungu wa walokole hana ubaguzi katika kutoa baraka kwa binadamu,ni kama anatusubiri tumjue atubariki.Lakini pamoja na upole wake,huyu mungu wa walokole ana mzaha pale unapotaka kudhuru walokole wake na haoni hasara kukuua kwa pumzi yake ya moto.Anawapenda walokole wake kuliko kitu kingine chochote.
NITAENDELEA..... ....!!!!
 
Hujaeleza tofauti kati ya watu warefu wenye kuakisi mwanga wenye mabawa na warefu wenye kuakisi mwanga wasio na mabawa.

Maana kulingana na BIBLIA, watu walioigia Mbinguni ,tofauti Yao na Malaika ni kutokuwa na mabawa.

Hata YESU aliyefufuka, amewahi kuwatokea wengi, Hana mabawa.

WATAKATIFU wote waliowahi kuwa na miili ya WANADAMU before hawana mabawa.

Fafanua ulivyoona kuhusu Hilo.
Fuatilia utaona mkuu.
 
Mlokole anaweza kubadilika katika maombi akawa kama Malaika na kwenda kumsaidia mtu au kumfungua aliyefungwa au kuibiwa nyota.

Wana wa ufalme, waliookoka, Tumepewa mamlaka na uwezo mkubwa mno, tatizo ni kutokutumia mamlaka yetu vizuri.
 
MI KINACHONISIKITISHA

Ni kama KILA kitu kilipangwa kabla hata misingi ya ulimwengu haijakuwepo!!

Yaani hata hao wa jehanam na hao wa peponi walipangiwa kuwa fate yao itakua hivyo!!

Unafikiri huyo shetani alipoumbwa na kuwa shetani ilikua by surprise!!?

Yaani chanzo kikuu cha vyote hivi ni muumba mwenyewe hakuna Bahati mbaya wakuu!!

Uwepo wa shetani,moto,pepo vyote ni mpango KAZI hata hao watakaoingia ni mpangokazi rasmi hakuna Bahati mbaya KWA lolote itategemea yeye muumba alikuandikia nini coz hakuna anaewez and kujifanya mtakatifu wala muovu isipokua KWA Mapenzi yake yeye aliemuumba yeye na pande ZOTE mbili yaani shetani na upande wa pili!!!

Ni hayo tu!!
Sasa kama Muumba alipanga hivi, kwanini alimtuma Yesu Kristo duniani?
Kumbuka Yesu Kristo ametumwa Kwa watu wote na imeandikwa kuwa "sauti zao zimeenea duniani kote" na tena " Mungu enzi zile aliwaacha wafanye njia zao ila hakuwaacha bila kuwa na ushuhuda ila kwasasa anataka yeyote atakayesikia ujumbe wake atubu na kuacha njia zake ovu"
 
1.Ni njia gani rahisi ya kujua nyota yako?
2.wachawi wanaibaje nyoto ya mtu?
3.Na kama unahisi umeibiwa nyoto ufanyeje ili uweze kurudihsa kirahisi?
Kwa sisi wakristo, walokole tunayemuamini Mungubwa walokole, hakuna kitu kama hiko kinachoitwa nyota. Achana na hawa manabii wa kisasa wanaowadanganya. Yesu hawajawahi fundisha kuhusu nyota na hakuna sehemu kwenye Biblia inaandika au mitume wanafundisha kuhusu nyota. Sisi watoto wa Mungu wa walokole, tunafanya na kutenda kile Mwana wa mmiliki au mtu yule wa haki amefanya.

Sisi watoto wa mwana wa mmiliki, "yeye ndiyo Nyota yetu" tena ndiye "nyota ya asubuhi yenye kung'ara". Ukimuamini yeye, "nyota ya asubuhi yenye kung'ara inakukuzukia moyoni mwako nawe utanainuka na kung'ara". Fundisho la nyota eti unasafishwa nyota ni la kipagani na la kitapeli. Ukimuamini yeye, hakuna laana kwani yeye alifanya kuwa laana kwa ajili yetu, hakuna umaskini kwani yeye mwenye na tajiri akifanyiwa masikini ili sisi tuwe matajiri, hakuna magonjwa kwani kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Hakuna mizimu, hakuna mapepo, hakuna majini hakuna lolote ka kukutisha kwani yeye ndiye mmiliki wa vyote. Muamini sasa mkuu. Hatuhubiri wala sema habari za Mungu mfu, bali tunahubiri habari za Mungunwa walokole tunayemjua na kuona kazi zake.
 
Mlokole anaweza kubadilika katika maombi akawa kama Malaika na kwenda kumsaidia mtu au kumfungua aliyefungwa au kuibiwa nyota.

Wana wa ufalme, waliookoka, Tumepewa mamlaka na uwezo mkubwa mno, tatizo ni kutokutumia mamlaka yetu vizuri.
Ni sahihi kabisa mtumishi japo Hilo la nyota ni fundisho la uongo. Binafsi nikishaona mtumishi anaongelea kuhusu nyota huwa simsikilizi wala mfuatilia kwani namuona ni tapeli.
 
Back
Top Bottom