Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Status
Not open for further replies.
Kwa kuongezea,
Kama mungu hayupo, ninategemea kusiwe na ushahidi wa yeye kutokuwepo.
Kwa sababu hayupo.
Hatuna ushahidi wa vitu ambavyo havipo kwamba havipo.
Kwa sababu havipo.
Hatuna ushahidi kwamba juu ya mlima Kilimanjaro hakuna babu mwenye macho matatu anaye control dunia.
Kwa sababu hayupo.
On the other hand. Vitu vilivyopo vinaweza kutafutwa na kupatiwa ushahidi.
Kwa sababu vipo.
Kwa hiyo, kujibu suala hili conclusively, wanaosema mungu yupo ni wajibu wao kuleta ushahidi kwamba yupo.
Wanaobishia kwamba yupo, hata wakikosa ushahidi, wanaweza kusema wamekosa ushahidi kwamba hayupo kwa sababu hayupo.
Huwezi kuwa na ushahidi kwamba kitu hakipo, kwa sababu hakipo.

Sisi tumeshasema Mungu yupo na sababu tumetoa
Ni jukumu lako wewe kuthibitisha kuwa ushahidi wetu sio wa kweli

Badala ya kufanya hilo wewe unasema hujui
Sasa unakataa nini?
 
Thibitisho ni kwamba umeomba uthibitisho.

Ni sawa na kusema kuwa umethibitisha kuwa huna hela kwasababu umeomba hela
Hujui kuwa kuomba hela sio ishara ya kutokuwa na hela!
 
Hata ulicho quote hukielewi?
Kazi ipo!

Kimeparaganyishwa kwa bad formatting kiasi haijulikani nani kam quote nani na ipi ni subquote ya ipi.

Kabla hata ya kuanza kusoma, ile formatting tu ni headache!

I had to insert two more end quotes just to put it up in a way that is visually logical, lakini hata sina hakika nani kam quote nani hapo.

It's a mess simply.

Jifunze ku format quotes kwanza, otherwise hata kama una arguments tutaziruka tu kwa sababu ya bad formatting.
 
kaka Kiranga kuwa chonjo sana na huyu mkuu Stefano Mtangoo.nina wasiwasi atakuwa ni askofu kilaini au ni mseminary wa level ya juu sana.hawa jamaa kabla hawajapata upadre huwa wanasoma philophy kwanzwa.u can tell frm the way he argues/present his point.kwa kweli mleta mada upo juu.nakushauri kiranga round hii rudi library ukajipange upya kaka.
 
Last edited by a moderator:
Kimeparaganyishwa kwa bad formatting kiasi haijulikani nani kam quote nani na ipi ni subquote ya ipi.
Kabla hata ya kuanza kusoma, ile formatting tu ni headache!
I had to insert two more end quotes just to put it up in a way that is visually logical, lakini hata sina hakika nani kam quote nani hapo.
It's a mess simply.
Jifunze ku format quotes kwanza, otherwise hata kama una arguments tutaziruka tu kwa sababu ya bad formatting.

Nimekuuliza maziwa ni nini unajibu mahindi ni chakula cha nguruwe huko Marekani
Yaani hujui hata nimekuuliza nini

Pia hujui ulichouliza

Umeuliza sio kweli nini
Maana yake unataka kujua ni kwanini nimesema sio kweli
Nikakuambia hata ulichokiquote hujakielewa nikirejea ulipotoa kauli yangu ya kanushi

Hapa unakuja na maelezo yanayozungumzia post nyingine ambayo hata hivyo nimeshayajibu tayari
Hii pia inaonesha vile ambavyo huwezi kujenga hoja kutokana na maandishi husika
Unachanganya mambo tu

Hujui ni wapi nimesema sio kweli na wapi nilijiquote kimakosa
Wewe unaona hayo ni jambo moja

Utaelewekaje wewe?
Utaweza kujieleza hata kile unachokihitaji kweli wewe?

Jifunze kujibu na kuuliza kwa utaratibu mzuri laa sivyo utaonekana hamnazo zaidi ya ulivyokwisha kuonekana hapa!
 
kaka Kiranga kuwa chonjo sana na huyu mkuu Stefano Mtangoo.nina wasiwasi atakuwa ni askofu kilaini au ni mseminary wa level ya juu sana.hawa jamaa kabla hawajapata upadre huwa wanasoma philophy kwanzwa.u can tell frm the way he argues/present his point.kwa kweli mleta mada upo juu.nakushauri kiranga round hii rudi library ukajipange upya kaka.

Hahahaa,

Waseminari waliosoma philosophy ya juu hawawezi kuingiza mguu hapa, wakiingiza mguu watachomoa mara moja kama alivyofanya mwalimu Augustine Mushi , mzee wa kilatini ambaye nilikuwa nakwenda naye pound for pound kuanzia ontological argument, cosmological argument, tunazama kwenye ma Anselm na Augustine philosophy huko, tunarushana kwenye Bertrand Russell na wengine wengi.

Hawa wengine hata "immanent criticism" hawajawahi kuisikia.

Huyo champion wako nimemchallenge kwa swali moja tu la "the problem of evil" mpaka sasa hajanijibu.

Wengine wananijibu wananiambia mungu anapunish watu kwa dhambi zao, sasa mtoto anayezaliwa kilema kafanya dhambi gani? Kama wazazi wake wamefanya dhambi, ni haki kumhukumu yeye?

Wengine wananiambia ooh, mungu anataka tuwe na uchaguzi kwa sababu anapenda sana uhuru wa uchaguzi.

Kama anapenda sana uhuru wa uchaguzi mbona hakuniuliza kama nataka kuzaliwa dunia hii kabla sijazaliwa?

Watu jiiii.

Majibu yao yanaza maswali zaidi ya majibu.

Na hawayajibu hayo maswali.

Hapana, usiwapandishe chati bure.

Hawajajibu maswali yangu bado.

Wamefanya kubabaisha tu, halafu wanasema "si jibu umepewa, kwani lazima liwe jibu sahihi, jibu si jibu tu?"

Wababishaji kama hawa hawawezi kuwa watu waliosoma falsafa ya juu na theolojia, kama wapo watu hao wanaoweza kunipa majibu hapa JF sijawaona bado.
 
Nimekuuliza maziwa ni nini unajibu mahindi ni chakula cha nguruwe huko Marekani
Yaani hujui hata nimekuuliza nini

Pia hujui ulichouliza

Umeuliza sio kweli nini
Maana yake unataka kujua ni kwanini nimesema sio kweli
Nikakuambia hata ulichokiquote hujakielewa nikirejea ulipotoa kauli yangu ya kanushi

Hapa unakuja na maelezo yanayozungumzia post nyingine ambayo hata hivyo nimeshayajibu tayari
Hii pia inaonesha vile ambavyo huwezi kujenga hoja kutokana na maandishi husika
Unachanganya mambo tu

Hujui ni wapi nimesema sio kweli na wapi nilijiquote kimakosa
Wewe unaona hayo ni jambo moja

Utaelewekaje wewe?
Utaweza kujieleza hata kile unachokihitaji kweli wewe?

Jifunze kujibu na kuuliza kwa utaratibu mzuri laa sivyo utaonekana hamnazo zaidi ya ulivyokwisha kuonekana hapa!

Wewe unayeleta haya bila ushahidi ndiye unayechanganya mambo zaidi yangu.

Weka link hapa, wapi umeuliza maziwa.
 
Huwa siwaelewi mnapomkana Mungu na kuleta "problem of evil". hili swali nimelijibu katika uzi huu na kama hujaelewa nitarudia. Kiranga , unaposema "problem of evil" huoni unafanya "assumption" zinazodai/zinazolazimu uwepo wa Mungu? Unatofautishaje mema na mabaya katika ulimwengu ambao hakuna Mungu? Maana kusema tu "evil" una "imply" aina fulani ya sheria ya maadili (Moral Law) na hivyo Mtoa/Mtunga sheria hiyo (Mungu). Sasa kama wewe huamini kuwa Kuna Mungu, unatofautishaje kati ya zuri na baya? utuambie hili kwanza kabla hata hujauliza kuhusu "problem of evil". maana kama huwezi kutuambia tofauti ya jema na baya, then kwanini tuendelee zaidi ya hapo?


Wewe ulitaka afanyeje? atengeneze watu ambao hawana uhuru wa kuchagua? Kama angefanya unavyotaka unafikiri angekuwa ameumba watu kwa mfano wake? Unafikiri kuna upendo bila kuchagua?

Imagine mke wako ukitaka akubusu anakubusu hata kama yeye hataki. Utakwenda mtaani kifua mbele kuwa kuna upendo kati yenu?

Mungu yuko sahihi kabisa kuumba ulimwengu wa namna hii na ndio maana Yesu ni mwanakondoo aliyechinjwa kabla ya misingi ya ulimwengu kuwekwa. Hii ni kwa sababu Mungu aliamua (in his Sovereign choice) kuumba ulimwengu ambao si tu kwamba alijua maovu yanawezekana bali alijua pia Mwaadamu huyu ataasi. Na akaamua kuonyesha ni wa Upendo zaidi kwa kufanya njia ya kumwokoa toka katika uovu wake: Mpango ambao wewe Kiranga unaukana leo hii.

Kwa kuumba ulimwengu wa namna hii Mungu amedhihirisha upendo mkuu sana (Yohana 3)



Simple! Kuna Magonjwa kwa sababu kuna dhambi. Kuna dhambi kwa sababu Mwanadamu aliamua kumwasi Mungu. Mwanadamu alimwasi Mungu kwa sababu ya kutumia vibaya utashi wake. Mwanadamu alikuwa na utashi kwa sababu Mungu alimuumba na uwezo wa kuchagua. Mungu alimuumba na uwezo wa kuchagua kwa sababu Mungu nu pendo. Kwa hiyo "ultimately" kuna magonjwa kwa sababu kuna Mungu!



Unadhani kuna mahali popote ambapo ni sahihi kwa mtu kumbaka mtoto mchanga na kumkatakata vipande kisha kula nyama yake? Jibu lako lina maana gani (what does your answer imply)?




Hili tatizo lingine la wasioamini Mungu! Kama unaamini katika naturalism (kama ambavyo nimekusoma katika nyuzi kadhaa) kwa nini utumie "compassion, logic, ethics," vitu ambavyo havionekaniki wala kushikika? Na pia hapa unajaribu kusema kuwa "God is morally wrong" na mimi nauliza "Under which Moral Law is God wrong?". Unapimaje ethics za Mungu na kuzithibitisha kuwa ziko chini? What are the scales?




Katika ulimwengu/Dini unayoiamini ya "random and chance" kuna tatizo gani mtoto kuzaliwa kipofu? Katika dini yako ya "Hakuna Mungu" na hivyo hakuna "Ultimate Law" kuna tofauti gani kati ya mema na mabaya? Hitler aliona ni jambo Jema kuua wayahudi Mil 6+ na Stallin akaona ni jambo zuri tu kuua mamilioni ya Warusi. Kuna watu wanaona ni vyema wakibaka au kuua. Katika dini yenu ya hakuna Mungu, unawahukumu wana kosa? Kwa sheria ipi?



Baba A akiona ni vyema kuwapa watoto chakula na Baba B akaona ni vyema watoto wake wakafa na njaa, na wote hawa ni binadamu, nani atakuwa amekosea? Kwa sheria ipi hiyo ya ubinadamu maana hawa wote ni wanadamu!

Hujatuambia pa sheria hiyo mtunzi wake ni nani na kwa mamlaka gani aliitunga sheria hii!


You are right na ndivyo alivyo!


Una maana hata pale viumbe hawa wanapochagua mauti badala ya uzima Mungu awalazimishe? Mfano, wewe Kiranga leo umemkataa Mungu mbele yetu sote, halafu unatarajia kwa sababu ya upendo wake akuachie tu uende, are you kidding? Hakimu anapotoa hukumu huitoa kwa upendo kwa kuwa ni haki stahili. Haya Magonjwa ni haki stahili ya Mwanadamu kwa sababu ya kuukaribisha uasi (dhambi). Huwezi kukaribisha adui halafu ukalalamikia madhara yake. Each choice have its consequence!

Bill hajawahi kumsaidia Mungu kazi hata siku moja. kupeleka chanjo Afrika haijawahi kuwa kazi ya Mungu. Umelipata wapi hili?


Jibu la swali hili nimeshalijibu hapo juu...madhara ya kukaribisha adui si kazi ya Mungu kuyabeba. Ukweli hata kama unauma ndio ukweli wenyewe!




Check the answer above! Huna haki ya kudai habari ya mabaya wakati unasema hakuna Mungu!



Swali hili unabadili tu namna ya kuliuliza na nimeshalijibu hapo juu!


Anyway hujaweka ushahidi wowote kuwa hakuna Mungu zaidi ya kuhoji kwa nini Mungu kama yupo alifanya A B C. Hakuna mahali umefuta point zangu na kwa ukweli umehakikisha nilichokisema kuwa ni dini yako tu inayokataa uwepo wa Mungu inakulazimisha kufika uliko. Si kwa sababu hakuna Mungu bali kwa sababu hutaki kukubali uwepo wake ambao pia wajua ni halisi

Umeruka na kukimbia point zangu badala ya kuzijibu moja baada ya nyingine.
Mungu yupo, alikuweko na ataendelea kuwepo!
Huu ndio ukweli mchungu!

Mmmh; Kiranga, mwaka huu kazi unayo!
 
Last edited by a moderator:
What is uniform? Which things are uniform? How big is the universe? How much of it have you observed? How much of it is observable?

Mimi sijajibiwa swali langu pia.

Kama mungu ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa nini kaumba ulimwengu uliojaa maovu?

Kwa nini karuhusu viumbe wake wateseke? Watoto wazaliwe na vilema?
Kwani mfinyanzi akiamua kuvunja vitu vyota alivyovifinyanga, ni kipi kati ya hivyo kitamwuliza kwa nini amevivunja?
 
Mmmh; Kiranga, mwaka huu kazi unayo!

Kazi wanayo wao ambao hawajajibu "the problem of evil".

Huyo mseminari uchwara anakwambia huwezi kuwa na ethical system bila mungu.

Wakati watu wanakwiba mpaka Vatican huko na makanisani kwingine, huku huko Asia kuna jamii ambazo zinakataa kuwepo kwa mungu na zina ethics nzuri tu.

Tatizo ni kuwa mtu wa kitabu kimoja, hujui hata watu wengine wanaishije duniani, lazima utakuwa kama yule kipofu aliyepata kushika mkia wa tembo.

Akiulizwa "Tembo yukoje?" ni lazima aitaje reference yake moja tu anayoijua.

Atakwambia "Tembo yupo kama kamba hivi".

Kwa sababu ndiyo experience yake pekee ya tembo.

Mkia.
 
Hahahaa,

Waseminari waliosoma philosophy ya juu hawawezi kuingiza mguu hapa, wakiingiza mguu watachomoa mara moja kama alivyofanya mwalimu Augustine Mushi , mzee wa kilatini ambaye nilikuwa nakwenda naye pound for pound kuanzia ontological argument, cosmological argument, tunazama kwenye ma Anselm na Augustine philosophy huko, tunarushana kwenye Bertrand Russell na wengine wengi.

Hawa wengine hata "immanent criticism" hawajawahi kuisikia.

Huyo champion wako nimemchallenge kwa swali moja tu la "the problem of evil" mpaka sasa hajanijibu.

Wengine wananijibu wananiambia mungu anapunish watu kwa dhambi zao, sasa mtoto anayezaliwa kilema kafanya dhambi gani? Kama wazazi wake wamefanya dhambi, ni haki kumhukumu yeye?

Wengine wananiambia ooh, mungu anataka tuwe na uchaguzi kwa sababu anapenda sana uhuru wa uchaguzi.

Kama anapenda sana uhuru wa uchaguzi mbona hakuniuliza kama nataka kuzaliwa dunia hii kabla sijazaliwa?

Watu jiiii.

Majibu yao yanaza maswali zaidi ya majibu.

Na hawayajibu hayo maswali.

Hapana, usiwapandishe chati bure.

Hawajajibu maswali yangu bado.

Wamefanya kubabaisha tu, halafu wanasema "si jibu umepewa, kwani lazima liwe jibu sahihi, jibu si jibu tu?"

Wababishaji kama hawa hawawezi kuwa watu waliosoma falsafa ya juu na theolojia, kama wapo watu hao wanaoweza kunipa majibu hapa JF sijawaona bado.

Csemi kitu...haya mkuu.
 
Kwani mfinyanzi akiamua kuvunja vitu vyota alivyovifinyanga, ni kipi kati ya hivyo kitamwuliza kwa nini amevivunja?

You are getting ahead of yourself in a circular way.

Ni lazima uoneshe kwamba kuna mfinyanzi kwanza.

Halafu, mfinyanzi akijinadi kwamba yeye anapenda sana kazi yake, na ana uwezo na ujuzi wote, na alivyovifinyanga vina uhai, na vinaogopa kufa, na kavikataza kuuana, akija yeye kuvivunjilia mbali na kuviua wakati ana uwezo wa kuviepusha na maumivu na kifo, atakuwa haeleweki.

Upande mmoja anasema anavipenda viumbe vyake, upande mwingine ana uwezo wa kuzuia visipate maumivu, vilema etc, lakini hazuii.

Ni contradiction.

Mungu angesema "mimi ni badass, nimewaumba binadamu lakini siwajali, kivyenu" nisingeshangaa.

Lakini tunaambiwa mungu ana uwezo mkuu na ujuzi mkuu na upendo mkuu.

Sasa mbona huu upendo mkuu kama unapitwa na upendo wa kibinadamu tu?

Mungu anawaumba binadamu bila chanjo. Wamekufa kwa kupuputika kwa mamilioni ya miaka, wameumwa magonjwa yanayozuilika kirahisi kwake, na mpaka leo wanatatizwa.

Yeye kaangalia tu.

Mpaka binadamu wahangaike saaana wagundue dawa/ chanjo wenyewe.

Kwa nini anakuwa anatubania hivi wakati yeye mwenyewe ndiye aliyetuumba na ana uwezo wote na upendo wote?

Au hizi ni stories tu?

Mana hali halisi imekaa inconsistent na mungu mwenye uwezo wote na upendo wote anavyoweza kufanya.

Hata wanadamu tu ambao hawana uwezo wote na upendo wote na ujuzi wote wana moyo wa huruma zaidi ya huyu mungu.

Sasa inakuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote awe mkatili kuliko wanadamu amabao hawana ujuzi wote, uwezo wote wala upendo wote?

cc Anheuser
 
Csemi kitu...haya mkuu.

Hata kusema husemi kitu ndo ushasema hivyo.

Old schoolers wanaweza kukumbuka hadithi ya darasa la pili "Heri mimi Sijasema".

Kuna mtu alipigwa mkuki vitani (mafichoni) kwa kusema "heri mimi sijasema" akikebehi wenzake waliopigwa mikuki kwa kulia badala ya kuvunga kufa.

Kama unavunga kufa vunga kufa tu.

Ukisema "heri mimi sijasema" ndiyo unakuwa ushasema hivyo, mkuki unakufuata.
 
Wewe unayeleta haya bila ushahidi ndiye unayechanganya mambo zaidi yangu.
Weka link hapa, wapi umeuliza maziwa.

Hii akili ndio iweze kumjua Mungu kweli?

Mtu haelewi anachoandikiwa ataelewa kikubwa kuliko hicho?
 
Kazi wanayo wao ambao hawajajibu "the problem of evil".

Huyo mseminari uchwara anakwambia huwezi kuwa na ethical system bila mungu.

Wakati watu wanakwiba mpaka Vatican huko na makanisani kwingine, huku huko Asia kuna jamii ambazo zinakataa kuwepo kwa mungu na zina ethics nzuri tu.

Tatizo ni kuwa mtu wa kitabu kimoja, hujui hata watu wengine wanaishije duniani, lazima utakuwa kama yule kipofu aliyepata kushika mkia wa tembo.

Akiulizwa "Tembo yukoje?" ni lazima aitaje reference yake moja tu anayoijua.

Atakwambia "Tembo yupo kama kamba hivi".

Kwa sababu ndiyo experience yake pekee ya tembo.

Mkia.

Naomba majibu ya maswali yangu
Yapo page no 5

Hebu jibu acha kupiga blabla tu hapa!
 
Hata kusema husemi kitu ndo ushasema hivyo.

Old schoolers wanaweza kukumbuka hadithi ya darasa la pili "Heri mimi Sijasema".

Kuna mtu alipigwa mkuki vitani (mafichoni) kwa kusema "heri mimi sijasema" akikebehi wenzake waliopigwa mikuki kwa kulia badala ya kuvunga kufa.

Kama unavunga kufa vunga kufa tu.

Ukisema "heri mimi sijasema" ndiyo unakuwa ushasema hivyo, mkuki unakufuata.

hahaha
 
Hii akili ndio iweze kumjua Mungu kweli?

Mtu haelewi anachoandikiwa ataelewa kikubwa kuliko hicho?

Haiwezi kumjua mungu, kwa sababu hayupo.

Kama yupo toa uthibitisho.
 
Hata wanadamu tu ambao hawana uwezo wote na upendo wote na ujuzi wote wana moyo wa huruma zaidi ya huyu mungu.

Sasa inakuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote awe mkatili kuliko wanadamu amabao hawana ujuzi wote, uwezo wote wala upendo wote?

Hahaa yaani binadamu yuko compassionate zaidi ya mungu!

Ndo maana nishasema ukiamua kuamini hizi habari za mungu ni lazima ujitoe fahamu walau kidogo la sivyo utaishia kuona dhani nzima ni a bunch of BS tu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom