Muungano wetu: Mgao wa Fedha za IMF na Zanzibar kupewa asilimia 18, ni sahihi?

Hebu eleza utaratibu wa kulipa deni la nje ukoje,, je huwa tunaguatwa mmoja mmoja kulipa au ni vipi, wanzanzibar hawalipi kodi?,
Zanzibar walijitoa kuomba mkopo chini ya Tanzania wakiongozwa na Masoud VP wa Zanzibar sasa akiwa mwanasheria mkuu
Z'bar awamu ya kikwete.
Kodi wanalipa kwa Serikali yao ambayo ni bil 400 ukiweka na ruzuku ya bara na wahisani.
Kama walishindwa kulipa deni la 60bil. watewazeje kulipa hili?
Kenya ilijimilikisha mali za EAC baada ya kuvunjika muungano na ndio Zanzibar wanachotaka kufanya.
Wanakuja na nyimbo zao wametatua kero za Muungano na hawaziweki wazi ni kero zipi
na zimetatuliwa vipi, akili kumkichwa.
 
Maswali ya kijinga, madeni mengine huwa analipa nani?
 
Narudia tena sio sahihi ikiwa Ali Hassan Mwinyi, Aboud Jumbe Mwinyi na sasa hivi Hussein Mwinyi wameweza kuwa Rais Zanzibar hoja hiyo haina mashiko mimi nawajuwa watanganyika (Wazanzibara) wengi wameajiriwa Serikalini bila ya taabu na wengine kuwa mawaziri. Suala la Katiba Mpya undeni tuu hiyo ni hiyari yenu suala langu ni uongo kufanywa ndio jambo sahihi kwangu sikubaliani nayo.
 
Hesabu zibadilike sasa kwakuwa tunafanya sensa mwakahuu mgao uchakatwe kwaidadi ya watu yaani uwe hivi ;

Bara
=(wabara ÷ watz) × mkopo/msaada

Zenji
=(wazenji ÷ watz) × mkopo/msaada

Mkopo unalipwa nawatu kwahivyo kilamtizii ahusike kwenye calculation!!
'Wabunye' yetu hayawezi kulisemea hili 'bunyeni' maana kiladakika wanawaza wamfurahishaje 'bibiye' ili waukwae uwaziri au unaibu uwaziri wanaouota kilaiitwapo Leo!!!
Kaziyao nikumsifu 'bibiye' kuliko hata yanavyomsifu Muumba wao...damnittt!!
 
Upo sahihi sana na je..?
Una evidence yoyote kuwa masoko yanajengwa kwa wawekezaji binafsi na si wakati ule ila kwa sasa ndipo serikali inawekeza kwa nguvu zote?.

Hapa i wrote issue ya masoko not bandari ( about bandari we'll discuss in next article)

Either wewe ndiye hujui, hata wakati wa madaraja na ununuzi wa mandege huko bara wengi mlipiga mayowe kuhusu serikali kutumia pesa nyingi za ndani ila, baadaye mkaanza ooh mikopo nk.
 
Weka hapa huo mkataba wa Muungano.Pili unaelewa maana ya kero za Muungano? Na je mkataba ni biblia au msahafu?

Mwisho Zanzibar sio Mkoa ni Nchi na pia ni sehemu ya JMT kwa hiyo ina haki zote na tena haki zaidi ya Mkoa.
Suala ni kwamba Zanzibar inapewa mgao mkubwa kuliko makubaliano rasm ya asilimia 4.5%. Si suala la kinchi wala kimkoa!! Wahusika wanaona malalamiko haya kila siku lakini wameziba masikio!! Kama kuna maelezo kuhusu ukiukwaji huu tuambiwe!! kama kuna utetezi wowote tuambiwe!! Au ndo utaratibu wa mbuzi kula kwa kulingana na urefu wa kamba yake?? Inakera!!
 


Watanzania tuna kazi zana kwa uelewa mdogo. Yaani unafikiri mikopo inatolewa kwa mgao! Mikopo ni tofauti na kodi!

Mikopo inatolewa kwa mahitaji na project sio mgao. Hivyo kama haipo kuwe na sheria nyingine ya mikopo. Unaongelea vitu viwili tofauti mikopo na kodi
 
Tuwekee hayo makubaliano maana naona umekazania uzushi wenu wa 4.5%
 
Kwa ujumla sasa hivi tuna wabunge wa majina. Wamekosa weledi, wamekosa ujasiri, wamekosa maono. Kwa ujumla ni wabunge wa hovyo kabisa ambao hatujawahi kuwa nao katika historia ya nchi yetu.

Bunge la chama kimoja la akina Arcado Ntagazwa, Njelu Kasaka, na wengine nimewasahau, lilikuwa bunge hasa, siyo huu utopolo wa sasa hivi. Haieleweki hata huko Dodoma wanaenda kufanya nini. Ni aheri wangebakia majumbani kwao.

Kwa ujumla wabunge wa safari hii hawana msaada wowote kwa mtu yeyote zaidi ya familia zao.
 
Topic yako ina mislead the public, 4.5 inazungumzia misaada sio mikopo. Chanzo cha mkataba kikowapi ?
On top of that wazanzibari hawana haja na muungano kama unavyofikiria kuwa wanafaidika.
Ndugu yangu, sijampotosha yeyote. Kanuni hiyo ipo wazi, na inasema:

Misaada ya nje na mikopo ya nje, Zanzibar itapata 4.5%.
 
Kama ulivyovitaja, vyote vikawa hivyo, ina maana Muungano utakuwa umekoma.

Tushirikiane katika yale tu tuliyokubaliana:

Ulinzi
Mambo ya nje
Mambo ya ndani
Sayansi na teknolojia
Elimu ya juu
Sarafu
Usafiri wa anga na majini
 
Umetoa mfano mbaya. UNDP huwa haitoi mikopo wala misaada ya ujenzi wa barabara.

Mashirika ya musaada kama USAID wao wanapotoa msaada, wanautoa na kuupeleka ambako wao wanataka, na mlioukosa hamwezi kudai kwa sababu hawapangiwi na Serikali ya Tanzania.
 
Mama anaupiga mwingi
Labda Rais Samia, siyo muumini wa muundo wa Muungano wa sasa, hivyo anafanya mambo yatakayowaudhi Watanganyika ili ifikie mahali, pande zote waone umuhimu wa Serikali 3 au kuuvunja Muungano.
 
Hebu eleza utaratibu wa kulipa deni la nje ukoje,, je huwa tunaguatwa mmoja mmoja kulipa au ni vipi, wanzanzibar hawalipi kodi?,
Kodi ya Mzanzibari inalipwa kwa SMZ. Deni lilikopwa na JMT, SMZ haidaiwi na mkopeshaji bali JMT inatakiwa iidai SMZ.

Ni sawa na wewe uende bank ukope sh milioni 50, uwekee dhamana nyumba yako, halafu uchukue milioni 20 umpe binamu yako. Binamu yako hafamiki kwa benki na wala hadaiwi na benki, unadaiwa wewe uliyekopa. Huyu binamu yako asipokulipa, wewe ndiye utawajibika kwa benki.
 
Hicho ndicho ninachokiona. Zanzibar, nadhani ina mpango wa muda mrefu wa kuvunja Muungano. Wanataka utakapovunjika, wawe wamefaidika kiasi cha kutosha.

Tanganyika ni kubwa jinga ambalo wakati wote linakula hasara. Wakati wa EAC lilipoteza ndege. Zote isipokuwa moja, zilibakia Kenya. Sasa tena kilichotokea EAC kinataka kutokea.
 
Bibi tozo anawafungisha ndoa ya mkeka wazanzibari..
Siamini kama ya Kenya kuhodhi mali za EAC yatajirudia tena kwa Zanzibar.
 
Ngoja tuone mwisho wa hizi ngonjera zao.
"ndani ya miezi sita bibi tozo katatua kero zote za muungano".
 
Nakuonea huruma kwa sababu unachangia jambo usilo na uelewa nalo.

Huo mgawanyo wa Zanzibar kupata 4.5% imetamkwa wazi kuwa ni kwa misaada ya nje na mikopo toka nje.
 
Nakubaliana nawe kabisa. Wabunge wa zamani hawakutanguliza eti kungojea kuteuliwa kwenye uwaziri nk. Wao walikuwa na jukumu la kuwakilisha majimbo yao ya uchaguzi na zaidi ya majimbo yao hayo walihoji sana wakati kulikuwa na tatizo. Hata serikali waliiweka pn toes. Sasa hivi ni kuimba sifa tu. Inasikitisha. Hii elimu mbona haiwasaidii hawa wabunge wetu?
 
Mgao wa zanzibar unatakiwa kuwa proportionate na mikoa mingine ya Tanzania, kimsingi ukubwa na idadi ya watu ya zanzibar ni sawa na mikoa mingine iliyopo Tanganyika...
Hey stop!

Hakuna mkoa wa Tanganyika unaolingana na Zanzibar!

Zanzibar ni ndogo kuliko SIKONGE

ZANZIBAR, eneo la kilomita za mraba 2,462, inaingia Halmashauri ya Wilaya ya SIKONGE, eneo la kilomita za mraba 27,842, mara kumi na nne!

Kwa idadi ya watu, Zanzibar, Unguja na Pemba that is, watu mil 1.4 wanaingia Halmashauri ya Wilaya wa Kinondoni, watu 2.8 mil mara mbili!

Watu wa Zanzibar - kama watu wote wa Kinondoni wangehama wakapaacha wazi for 15 minute in a demographic experiment - Wazanzibar wasingeweza kujaza viwanja, majumba, mashamba, mashule, biashara na ajira za Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni!

Julius Nyerere's most catastrophic decision was indisputably the fat-headed blunder of subsuming out country in a union with the pea-sized Zanzibar archipelago.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…