Mwaka 1988 Chakachaka alipiga show Makondeko Kibamba kiingilio kilikuwa 100,000

Tupe story za city pub na mbeya pazuri na ueleze bata hua likoje anzia uyole, mbalizi, iyunga pale breakpoint, mafiati pale carnival, sae pub, au tueleze hata viwanja vipya vya mama john, sisi hapa ni story tu hatuna maneno na mtu
Bata uwe na ela mkuu
Sisi wengine bata letu linaishia kwa mchungaji abiudi kishindo nyumbani🤣🤣🤣🤣🤣
 
Yawezekana anamfananisha Mj wa USA na yule wa Ruaha Galaxy enzi zile teh teh
Ruaha Galaxy pale Kimara Korogwe miaka ya 90 mwanzoni ulitamba sana. Shoo za wasanii wa enzi hio zimepigwa sana pale

Kule Kimara mwisho kulikuwa na ukumbi wa washua ulikuwa unaitwa Kimara Motel umejificha mazingira tulivu sana sasa hivi umefanywa shule ya Midlands
 
Basi MJ wa Bongo alikuwa ananing`inia kwenye visigino kumuigiza MJ original, basi ilikuwa hatari tupu.
 
Naelewa kuwa dala ilikuwa ni shilingi tano,
Nilikuwa najaribu kuelezea kwa nini ile sarafu ya sh 5 iliitwa dala!!
One dollar ilikaa muda mrefu sana ilikwa na thamani ya sh 5 , ile sarafu ilipotoka ikaitwa one dollar , waswahili tukaibatiza dala
 
tumsamehe bureeeeee, hajui tupo watoto wa mnazi mmoja humu. Muulize Pat Shange alikuja lini pale Taifa.
Mimi nimesoma mnazi mmoja primary headteacher akiitwa Chalila baadae akaja Mtolela,namkumbzka mwalimu mtenga
Pesa ilikuwepo kipindi hicho. Mzee wangu alisafiri mwaka 1994 dar hadi malawi kwenda tamasha la mnyama lucky dube.
Ahaa mzee wako alitisha,mzee Ruksa hatutamsahau
 
Naelewa kuwa dala ilikuwa ni shilingi tano,
Nilikuwa najaribu kuelezea kwa nini ile sarafu ya sh 5 iliitwa dala!!
One dollar ilikaa muda mrefu sana ilikwa na thamani ya sh 5 , ile sarafu ilipotoka ikaitwa one dollar , waswahili tukaibatiza dala
Na mimi hili nimelisikia sana japo huwa naamini kuna uwezekano sababu ikawa nyingine, au ilipewa tu hilo jina na watoto wa mjini tu kwa sababu kila sarafu au noti ilikuwa na jina lisilo rasmi.
 
Itoshe kusema wewe ni born town uliyetembea hapa nchini .

Arovera bado kirando panatema au kwasasa ni buyubuyu ?
 
Wapi papa Musofe ? Je kizaizai ila sitamsahau wala kumsamehe Mzamiru Katunzi
 
Siku watembelee pale Hyatt Regency level 8 wajionee watu wanaotumia pesa hapa mjini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…