Mwamposa: Mimi siyo Freemasons na sijui kwanini naandamwa na kusingiziwa vingi

Mwamposa: Mimi siyo Freemasons na sijui kwanini naandamwa na kusingiziwa vingi

Wivu kitu kibaya mimi kwa sababu nafanya minyanduo sina uhalali wa kumkosoa mwamposa.. Mwamposa ni nabii na atabaki kuwa nabii na divyo
Kama una site tuu na hujaanza kujenga na plan Kila ukipiga hazikupi mwanya peleka pale ,,,, ndani ya miezi kadhaa unakuja na story nyingine kabisa. Nakumbuka mwaka Jana alikuwa na Kongamano MBEZI mama chanja alienda na udongo wake,,, tunavooongea pagale lipo kwenye kuongea Kiinglishi ....
 
Michongo TU,
Ukienda pale huna pepo mabaunsa watakuangusha, ukifurukuta unapigwa vibao kwa jina la yes, Watu wanashangilia unagalagala unatolewa pepo kumbe vibao vinakuumiza[emoji1787]
Mimi kuna siku nilienda nilipofika nikaambiwa niandike majina yangu, historia yangu na sababu iliyonipeleka, basi nikaamua kuandika majina halafu sababu iliyonipeleka nikaongopa kuna mahali nadai pesa nyingi ila silipwi ndio maana nimekuja niombewe. Ilipofika muda wa maombi nikashangaa kuhania anauliza Skayla ndio yupi, nikasimama, akaniambia unadai pesa mahahali na ninaona kabisa wanataka kukudhulumu kwa sababu kuna roho za wachawi zimeshikilia uchumi wako, nikabaki natoa macho, akasema inabifi unione kabla hujatoka hapa nitakupa mafuta . Na ninaona roho wa Mungu akiniambia wiki hii haitaisha hujapokea pesa yako, na ukipokra unapaswa kuikumbuka mafhabahu hii kwa sadaka

Ibada iliposiha sikukanyaga tena kwenye hilo kanisa maana nilidanganya kwamba nimeenda pale ili niombewe niwlipwe deni, kumbe kuhani huwa anadanganya watu kwamba ana maono wakati anasoma taarifa za watu walizoandika, nilijikuta nashangaa maana sikua namdai mtu sasa hapo aliponiambia kwamba anaona wachawi wameshika uchumi wangu ndio nilibaki hooi
 
Mwamposa tapeli TU,
1. Kwañn viwete anaoponyesha kwny mikutano yake wote wageni eneo la mkutano, hamna hata mwenyeji mmoja[emoji2]
2. Viwete wanaoponyeshwa ulemavu,
wote magongo yao Huwa Ni mapya kabisa brand new. Huwa wanapata wapi muda wa kuyaosha yatakate yawe mapya ndo waende kwny mkutano wake[emoji1787]

3. Sijawahi kuskia mwamposa akamwangusha pepo tajiri yoyote yule,
Kwake waanguka mapepo wote Ni maskini TU[emoji38]
Ila nimecheka jaman[emoji1787][emoji1787]
 
"Juzi nilikuwa Bungeni na tulikuwa Watumishi wengi tu ila nashangaa Picha zangu tu ndizo zinasambazwa kwa Mabaya. Nikibadilisha Viatu hapa Madhabahuni, nikijifuta Jasho na Kitambaa na Nikivaa Cheni naambiwa Mimi ni Freemasons kwanini?" Amehoji Mtume Wenu Mwamposa.

Chanzo: Tv Channel yake muda huu

Kazi ipo.....!!!!!!

=============

Akizungumza na waumini wake, leo Jumapili Februari 12, 2023, Mwamposa amesema: "Yaani mimi nianze kujibizana na watu kwenye mitandao wanavyosema Mwamposa Freemason, nami niingine kwenye mitandao kuanza kuwajibu kuwa mimi si Freemason, sina muda huo hata kidogo.

"Kila kitu nikifanya inakuwa gumzo, juzi nilikuwa Bungeni, nilifanya ibada kwa Wabunge, nilipotoka pale nashangaa picha zinazagaa kuhusu mimi licha ya kuwa watumishi tulikuwa wengi.

"Hata nikiwa hapa (Kanisani) huwa wanashangaa ninavyobadilisha viatu, nabadilisha kwa kuwa mafuta ninayotembea nayo yakimwagikia kwenye kiatu yanakiharibu, hivyo nafaa viatu ambavyo nakuwa comfortable kuzunguka nacho.

"Hata wakiona nimevaa cheni inakuwa gumzo, hata nikivaa kitambaa inakuwa gumzo."

Chanzo: Mwamposa inasemekana freemason wakimfuata mtu kwenda kumshawishi awe mwanachama kwa sababu wameona ana kitu akikataa huwa wanatengeneza propaganda za kila aina.
 
Minakusifu kwa kujua kucheza na huu usemi "life is a game, play it." Unajua kucheza vizuri na akili za watu.
 
Hatari sana. Sasa ni nguvu gani huwa zinawaponya hao waumini wake?
Hapo huwa hakuna aliyepona. Hao wote huwa wazima. Wanafanya mchongo wa kupewa pesa ili wawazuge watu. Hamna cha kuponya wala nini. Hao ni matpeli tu. Ndiyo maana wanaoponywa (supposedly) hawajulikani kwenye sehemu ya kuponyewa na pia wote hawajawahi kuwa na ulemavu wa aina yoyote. Kwa nini asiwaponye walemavu wanaojulikana?
 
Cha muhimu afanye kazi ya utumishi wa Mungu,kama anawahubiria watu neno ili waache dhambi sioni shida,hilo la kuvaa cheni,kuwa na gari za kifahari n.k. ni kaliba ya mtu binafsi,ila kama anawahubiria watu habari za Mungu mwingine,Yesu mwingine au waache kutenda mema watende mabaya hapo atakuwa hana maana katika utumishi wake...
Ila maaskofu wa katoliki kuvaa micheni mikubwa ya msalaba na Pete ya dhahabu ya Ki Askofu ni sawa tu? Shida ni Kwa Mwamposa tu?

Padre wa parokia tu wa kanisa katoliki gari ya thamani ya chini anayotumia ni Prado.
 
Back
Top Bottom