Tunapoharibu ni kutaka kumgeuza mwanamke kama mtumwa wako, dunia ilishatoka huko muda mrefu, jadili na mke wako, jengeni uchumi imara, wekezeni ili mkizeeka muweze kwenda vacationa, wewe kitanda hicho hicho toka unamuoa mtoto wa watu, unataka avae vitenge na mishono ya tukuyu miaka yote what the hell, tubadilike tutauana sana kwa ujinga, ukute text baby nambie unalipuka kama mtungi wa gesi haujui wanawake wanaitana baby, mamie, mazoezi haufanyi unafuga kitambi kila saa kujamba huyo mwanamke hisia atazitoa wapi, kila lawama kwenye ndoa mwanamke hivi mara vile unashindwa kujiangalia wewe unakosea wapi, tubadilike vinginevo mauaji yatakua mengi wazee zamani waliheshimika kwanza walijitambua wao wenyewe na sio lazima mke awe mtumwa mfanye awe rafiki mshikaji uone kama hutofurahia maisha hata ukiishiwa atabaki tu.