Mimi sitaongelea poll,nitaeleza kidogo kwenye kodi,mfano ukiweka kodi sh1000 kwenye cement,ina maana makusanyo yataongezeka lakini gharama ya maisha kwa mtu wa kipato cha chini itaongezeka (tax incidence),ukiweka tozo kwenye miamala ya simu kodi itaongezeka lakini mtu wa kipato cha chini ataumia,kumbuka mtu wa kipato cha chini ongezeko la shilingi 100 kwake ni kubwa sana na ataumia zaidi ya mwenye kipato kikubwa,kwa hiyo utakuwa umefanikiwa kuongeza kodi lakini kwa kuumiza watu wa kipato kidogo...sasa swala linakuja kwenye matumizi ya hayo makusanyo,wananchi hawa waliokamuliwa wanaona pesa zinaenda kununua ma-V8 na bima ya mtoto ya NHIF inafutwa,huyu mwananchi hawezi kukupigia kura,pesa inatengwa bilioni 300 kufanya ukarabati uwanja wa taifa lakini hakuna mabadiliko tangible yanayoonekana,kitu alichofanikiwa sana Samia ni kuongea bila kutaka kuwaudhi wakubwa,nikisema wakubwa namaanisha dynasty