Mwanangu wa darasa la pili hili swali kakosaje? Au mwalimu ndiye hajielewi?

Such a good hand writing!! Ananikumbusha enzi zangu. So neat!!
 
Lakini mbona swali la tisa kama vile mwalimu kachemsha pia kwa hio ngoma droo
 
Ndo hivo nakomaa nao wapo KAYUMBA! Sina mpango wa private schools hata kidogo! Kila siku tunasoma
 
Huu muandiko mbona kama wa mtu wa sekondari?!!
Hapana: ni mtoto yupo kayumba, sema namzingatia kufuatilia madaftali kila siku, tunafundishana jioni! NAIMANI TUTATOBOA TU KIBISHI maana private sina huo mpango!
 

Hili jibu la "aren't I?" kwenye question tags liliwahi kunipa shilingi 100 ya noti enzi hizo, mwalimu alijua wote tutakosea kumbe nimeshalipata mahali. Tulikuwa darasa la 7.
 
Unajua mfundishaji wa watoto shuleni ni mfundishaji ndio lakini jina specific analoitwa ni mwalimu. Sasa ukijibu mfundishaji haujakosea Sana ila sio sahihi kwa 100%.

Ni sawa na ukamuita mtu mlimaji badala ya mkulima, au muendeshaji badala ya dereva.
Case closed.
 
Refarii ndiyo jibu sahihi kwa mujibu wa kingozi cha mwalimu (marking scheme).

Mwamzi ni jina jumuishi sana mfano mwamzi mahakamani anaitwa Hakimu/Jaji.

Refarii ni (referee) ni neno la kiingereza, je kwenye kiswahili linatumika hivyo hivyo?
Kiplefti -Keep left
 

Yunifomu? Duh
 
Unajua mfundishaji wa watoto shuleni ni mfundishaji ndio lakini jina specific analoitwa ni mwalimu. Sasa ukijibu mfundishaji haujakosea Sana ila sio sahihi kwa 100%.

Ni sawa na ukamuita mtu mlimaji badala ya mkulima, au muendeshaji badala ya dereva.
Referee ni kiingereza , kiswahili n mwamuzi, mwalimu kakosea
 
Refarii ni (referee) ni neno la kiingereza, je kwenye kiswahili linatumika hivyo hivyo?
Kiplefti -Keep left
Hadi hapa sijapata jibu sahihi inamaana huu mtihani na humu wote tungefeli au?
 
Jibu ni REFA

Neno mwamuzi limetumika kuuliza swali, kwahiyo huwez kulitumia kujibu swali. Mfundishe mwanao hii kitu isije kumuathiri huko mbele.

Mkuu hilo neno Referee sio ni kiingereza sema tumeozoea kulitumia tuu kwenye kiswahili kama vile Golikipa, Beki, Kamisaa na Fowadi?
 
Tanzania ina shida hii

Huon hapo unazunguka kwenye kizungu na kiswahili tu ?

Ndio wasomi lakn , mwalimu pamoja na wewe mmefeli
 
Imeishaje ? Hujui Referee n kiingereza na kiswahili ni Mwamuzi? Au wew ndio mwalimu nini?

Wengi tunatumia lugha kwa mazoea,Mkuu mimi ningesema mwalimu kamkosesha dogo, yaani ka set swali bila ufahamu wa kutosha neno referee halijatoholewa kuwepo kwenye kiswahili

Tuangalie huko huko kwenye mpira,hilo neno Referee (Refa) ni kiingereza ila tumeozoea kulitumia tuu kwenye kiswahili kama vile Golikipa, Beki, Kamisaa na Fowadi?

Siku huyo ticha akija na swali akisema

mshambuliaji wa mbele anaitwa nani-- atataka mwanafunzi aseme fowadi.
 
Tanzania ina shida hii

Huon hapo unazunguka kwenye kizungu na kiswahili tu ?

Ndio wasomi lakn , mwalimu pamoja na wewe mmefeli
Umeona nimeandika kizungu hapo?
 
Mtoto yuko sahihi. Sidhani kama tuna neno la Kiswahili zaidi ya kumuita refa.
Nimependa mwandiko wa mtoto!
 
Traffic ni kimasai??

Referee ni neno la kiingereza, kiswahili ni mwamuzi
Kwahiyo katika kiswahili hakuna maneno yaliyoazimwa katika lugha zingine ikiwemo kingereza na yakawa rasmi?

Hospitali ni kiswahili au kizungu? Huwa hulitumii wewe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…