Mwanangu wa darasa la pili hili swali kakosaje? Au mwalimu ndiye hajielewi?

Refarii ndiyo jibu sahihi kwa mujibu wa kingozi cha mwalimu (marking scheme).

Mwamzi ni jina jumuishi sana mfano mwamzi mahakamani anaitwa Hakimu/Jaji.
Kiongozi cha mwalimu (teachers guide)
 
Aisee darasa la kwanza mpaka la nne nilikuwa nacheza namba 1-3,nilipofika la tano nikaanza kuona mapichapicha mara wa 10 mara wa 50. Secondary ndio usiseme bora nikae kimya
Nalog off
 
Referee ni kiingereza , kiswahili n mwamuzi, mwalimu kakosea
Mwalimu hupima kile alichofundisha.
Je, unafahamu mwalimu alikuwa kafundishaje kabla ya kuandaa mtihani?
 
Mwalimu alishindwa kutunga swali. Alipaswa kuuliza hivi msimamizi wa mchezo uwanjani huitwa...... Ili jibu liwe mwamuzi.

Alichouliza ni mwamuzi kwa lugha nyingine huitwa......
 
Mwalimu alishindwa kutunga swali. Alipaswa kuuliza hivi msimamizi wa mchezo uwanjani huitwa...... Ili jibu liwe mwamuzi.

Alichouliza ni mwamuzi kwa lugha nyingine huitwa......
Upo sawa kabisa
 
Mwanao anaonekana anatumia akili sana katika kutatua matatizo. Yeye amejikita katika kutafsiri neno badala ya kujibu swali. Amekosa kwa kuwa mwamuzi wa mchezo katika mazingira yetu ni refarii na ndio jibu la swali aliloulizwa.
 
Huyo mtoto anaakili sana ndo maana ameshidwa kujibu hilo swali sio kwamba halijui analijua vzr
 
Mwanao ana mwandiko mzuri (kwa darasa la pili, ni jambo kubwa). Hongera zake.
 
Yaani nawe umekaa na mtoto ukamwambia ni kweli mwalimu kakukosesha? we bogus kweli
 
Na pia hizo kategory hufundishwa kwa level mtoto wa darasa la pili atafundishwa in general kwamba mwamuzi wa mpira ni refa akienda level za juu ndo anaweza kuta mgawanyiko wa hao waamuzi
 
Ye amerejea kamusi ya wapi
 
Emu we baba mtoto ulitakaje
 
Sio mbaya akishafundishwa kuhusu kutohoa mambo kama hata hayatamshinda
 

Mfumo wa ufundishaji usio rafiki kwa fikra-tunduizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…