Mwandishi mkongwe Abdallah Majura, ahoji kuhusu redio kujadili michezo asubuhi

Mwandishi mkongwe Abdallah Majura, ahoji kuhusu redio kujadili michezo asubuhi

Asubuhi mtu anaanza kusikiliza michezo ukianza na Wasafi, Crown, Clouds, EA Radio, Bongo FM, EFM vipindi vinaisha saa 6 mchana. Halafu hao EFM wanahamia kwenye TV yao sijui kuna yule Dada anaitwa Maongezi kipindi hadi saa 9 mchana. Then kuanzia saa 8 mchana zinaanza mechi za ligi kuu hadi 3 usiku. Baadae unakutana na ligi za Ulaya, EPL, La Liga, UCL, sijui Europa... aiseeh hili taifa sijui kama tutapata maendeleo maana vijana wengi wameangukia huko afu hapo jumlisha na kubeti sasa, bado hawajaanza kubishana kwenye vijiwe na mitandaoni, bado hawajacomment kwenye page za CAF hahahaaaa 😀 😀 😀, hatutoboi!!
U nailed it👏🏽👏🏽
 
Mwandishi wa habari mkongwe nchini Tanzania, Abdallah Majura amehoji kuhusu radio kuwa na vipindi vya michezo asubuhi na kujadili mambo ya Simba na Yanga.

“Tangu asubuhi watu wanatangaza michezo tu, lakini siamini kwamba Watanzania wote wanapenda michezo tu”

Nafikiri Majura atakuwa anawalenga, Crown FM, Wasafi FM, Clouds Fm na Efm
Si ndo wanachokijua
 
Huezi kuanzisha kituo cha redio halafu habari za simba na yanga usizipe airtime ya kutosha,,,utaifunga hiyo redio,,watu wenye biashara zao wanataka matangazo yawafikie watu wengi na wanapatikana simba na yanga....hata azam inaporusha mechi za yanga na simba matangazo yanakua ni mengi zaidi ya mechi ya mfano KMC na Namungo.
 
Sio redio tu na tv nyingi pia vinapewa airtime kubwa sana kujadili michezo kutwa mzima. Ni sawa na miziki ya Tanzania kuimba mapenzi tu
 
Kuna rafiki yangu mwanza kuna neno moja nakumbuka.Ukiona mwanzo mwisho watu wanajadili michezo ya mpira na wasanii basi ujue na ccm ndio sehemu yao kisiasa kuwatumia wajinga.

Kidumu chama cha NSSF imevunja katiba.
IMG_0612.jpeg
 
Bongo fm wana bao la asubuhi, Clouds fm wana Hili game, hao wapuuzi wengine sijui wana nini maana wanasikika jijini Dar tu. Wengine wana sports round up, sports machine, kambi ya michezo ila muda wao si asubuhi
 
Bongo fm wana bao la asubuhi, Clouds fm wana Hili game, hao wapuuzi wengine sijui wana nini maana wanasikika jijini Dar tu. Wengine wana sports round up, sports machine, kambi ya michezo ila muda wao si asubuhi
Hiyo yote inatokana na ushindani lakini pia Kuna jamaa wanaitwa Ipsosy Hawa wanatoa taarifa zao ndio hupelekea hizo redio kuigana na kuwa na vipindi km hivyo
 
Nina maoni tofauti, Hizo redio zipo kibiashara zaidi kwa hiyo zinaangalia kwenye maslahi na wapi wanapata matangazo
Kama wewe hupendi kusikiliza michezo zipo redio asubuhi tu huzungumzia siasa,dini,kilimo nakadhalika
Kwa hiyo chaguo ni lako
Uko sahihii, Kuna tafiti huwa wanazinunua toka Ipsosy,Geopoll, za kibiashara ,
 
Binafsi sijawahi kusikiliza hivyo vipindi kwa sababu mimi sio shabiki wa mpira wa bongo, ila sijaona tatizo mana ndio kazi yao inayowaweka mjini.
 
Asubuhi mtu anaanza kusikiliza michezo ukianza na Wasafi, Crown, Clouds, EA Radio, Bongo FM, EFM vipindi vinaisha saa 6 mchana. Halafu hao EFM wanahamia kwenye TV yao sijui kuna yule Dada anaitwa Maongezi kipindi hadi saa 9 mchana. Then kuanzia saa 8 mchana zinaanza mechi za ligi kuu hadi 3 usiku. Baadae unakutana na ligi za Ulaya, EPL, La Liga, UCL, sijui Europa... aiseeh hili taifa sijui kama tutapata maendeleo maana vijana wengi wameangukia huko afu hapo jumlisha na kubeti sasa, bado hawajaanza kubishana kwenye vijiwe na mitandaoni, bado hawajacomment kwenye page za CAF hahahaaaa 😀 😀 😀, hatutoboi!!
Ndo vizuri, mapopoma wakiwa wengi wenye akili wachache wanakula nchi, si wanajitakia hawa vijana hawataki shida wanataka kula kilaini kwa kubeti na kusikiliza na kubishana soka eti tulia kalia nenda kwenu na ubaya ubwege!

Fainali uzeeni, kama watafika
 
📌📌📌Thadi wadi country a.k.a SHITHOLE COUNTRY a.k.a Banana republic then what do you expect!!!
 
Huezi kuanzisha kituo cha redio halafu habari za simba na yanga usizipe airtime ya kutosha,,,utaifunga hiyo redio,,watu wenye biashara zao wanataka matangazo yawafikie watu wengi na wanapatikana simba na yanga....hata azam inaporusha mechi za yanga na simba matangazo yanakua ni mengi zaidi ya mechi ya mfano KMC na Namungo.
Pale Azam tv kukiwa na mechi kati ya Yanga vs Simba vs Azam Fc hata gharama za kurusha matangazo ni tofauti na kukiwa na mechi hizo nyingine.
 
Back
Top Bottom