Mwanza inapokea 10% tu ya mizigo kutoka Dar huku Kigoma ikipokea 41% ya mizigo. SGR ya Mwanza ni White Elephant project

Mwanza inapokea 10% tu ya mizigo kutoka Dar huku Kigoma ikipokea 41% ya mizigo. SGR ya Mwanza ni White Elephant project

Mbona husemi bwana Ladogosa amejibuje hilo, unakuja na maoni ya upande mmoja?
Ndiyo maana ya mjadala...

Kama na wewe ulifuatilia mjadala huo, ungeweza kusema tu kuwa, hata hivyo DG wa TRC ktk kulitolea ufafanuzi hilo, amejibu hivi na vile...

Anyway vyovyote iwavyo...

Wote tunajua kuwa mpango ni kujenga reli ya SGR kwenda hadi huko Kigoma...

Kinachogomba hapa ni vipaumbele (priorities). Kwamba, tunajua kama kweli tutasambaza SGR nchi nzima, basi itatuchukua miaka hata 30 ijayo kukamilisha project hii...

Jambo muhimu ilikuwa tuanze kujenga kuelekea wapi ili tuanze kuvuna faida haraka...

Ni ujinga kuanza kuelekeza reli ya SGR utakayoijenga kwa awamu kadhaa na kuchukua miaka 30 kuikamilisha awamu zote, kwenye eneo ambalo mahitaji yake ya usafirishaji mizigo ni 10% badala ya kuanza na eneo ambalo linasafirisha mizigo 41% kuelekea huko...!!
 
Natoa ushauri mmoja kwa serekali yetu tukufu, hatujachelewa sana!! Contract ya Isaka to mwanza ibadilishwe iwe Makutopora to Isaka!! Gharama zote za Isaka to Mwanza kujenga reli ya kuwa white elephant, hayo mabehewa yatapitia wapi hadi isaka kama huna sgr maktopora Isaka!!!???
Mkuu, kuna sababu zake za kujenga hii reli katika vipande vipande namna hiyo.

Ujenzi wa Mwanza - Isaka hauwezi kuishia hapo na kubaki bila kutumika. Maana yake ni kwamba Makutopora hadi Isaka ni lazima ijengwe kwa kuhimizwa na hiyo iliyojengwa tayari toka Mwanza hadi Isaka.

Hakuna kichaa yeyote atakayeingilia ujenzi wa vipande hivyo viwili; hakuna atakayekubali hasara hiyo.

Unaona ya sasa hivi, toka Pugu hadi Morogoro inakamilika, hata kabla ya kipande cha Dar Stesheni hadi Pugu. Haitawezekana hicho kipande kisijengwe hadi Pugu.
 
Hujui kitu unabaki unacheka cheka
GIA angani tayari baada ya kuona ni mradi hewa.

Kwa akili zako za kindezi nyie wasukuma shida yenu kuu ni sgr? Sgr ndio itapunguza au kuondoa umaskini?

Reli zimekuwepo toka enzi za wakoloni na walizijenga kwa tija za kiuchumi zilizokuwepo sasa hii ya Sasa ambayo inaongezewa kasi inajengwa kwa tija gani huko kwenu?
 
Mleta mada,

Target kubwa mbili za SGR ni kiuchumi na huduma kwa wasafiri (wananchi)

Katika target ya kiuchumi SGR itapita pale Isaka ambapo ndio lango kuu la bandari kavu ktk kuhudumia maeneo hasa ya Kigoma, Kahama, Geita nk nchi jirani kama Rwanda, Burundi nazo zitanufaika pia

Katika kuboresha utoaji huduma ktk usafiri, endapo SGR itafika Mwanza basi wasafiri wa mikoa jirani na Mwanza kama Shinyanga, Mara, Geita, Kagera watakuwa wanufaika wakubwa ktk huduma ya treni hii.

Hvyo kwa namna hiyo utaona ufikaji wa treni mpaka Mwanza utahudumia wasafiri wa mikoa takribani MINNE inayozunguka/jirani na Mwanza

Pia, tusisahau hii SGR ni mpango mkakati wa nchi kuendelea kuwin soko lake la kuzilisha nchi jirani kwasababu mwenzetu Mkenya nae anakimbizana na SGR yake ili apore soko letu hasa nchi ya Rwanda na Burundi,, hvyo natoa raí kwa viongozi wetu waongeze kasi ktk ujenzi wa SGR yetu
Mkuu, umeeleza vizuri sana, lakini kutokana na mada ilivyowasilishwa sidhani kwamba mleta mada ataelewa ulichoeleza hapa.

Isaka itakuwa ni Bandari.

Wote wanaokwenda kuchukuwa mizigo Dar hawana sababu tena ya kwenda huko. Hata hiyo 41% anayodai mleta hoja, sehemu kubwa itakuja hapo. Rwanda, Burundi, eneo kubwa la DRC , mashariki hadi kaskazini, na Uganda, hiyo itakuwa ni bandari yao ya kuchukulia mizigo.

Mizigo inayosafirishwa toka Mombasa, kupitia Uganda na kupelekwa DRC; ya nini usumbufu wote huo kama mtu anakwenda Isaka na kubeba mizigo yake?

Tushindwe tu sisi wenyewe kuendesha Bandari zetu, za Dar na hiyo Isaka kwa ufanisi, vinginevyo Mombasa watalizwa.

Lakini bado atakuwa haelewi!
 
Kwa mujibu wa BBC ikimhoji mtaalam wa Uchumi imebainika kwamba mzigo unaoingia bandari ya Dar es Salaam kuelekea Nchi za jirani via Central corridor ni asilimia 10% tu ya mzigo huo unaelekea bandari ya Mwanza wakati asilimia 41% huelekea bandari ya Kigoma.

Mtaalamu wa uchumi Bw. Walter Nguma azungumzia faida je SGR Reli ianze Kigoma au Mwanza ?

Moja ya maswali makubwa ambayo wengi walijiuliza baada ya kifo cha Rais John Magufuli nchini Tanzania lilikuwa ni: ipi hatma ya miradi ya maendeleo aliyoianzisha? Mrithi wake, Rais Samia Suluhu Hassan ameahidi kuendeleza miradi yote ya kielelezo ya mtangulizi wake, na ujenzi wa reli ya SGR ni kielelezo muhimu.
 
Wewe akili yako ni matope tu. Upeleke sgr kigoma uache kanda ya ziwa ? Rudi tena darasani.
GIA angani tayari baada ya kuona ni mradi hewa.

Kwa akili zako za kindezi nyie wasukuma shida yenu kuu ni sgr? Sgr ndio itapunguza au kuondoa umaskini?

Reli zimekuwepo toka enzi za wakoloni na walizijenga kwa tija za kiuchumi zilizokuwepo sasa hii ya Sasa ambayo inaongezewa kasi inajengwa kwa tija gani huko kwenu?
 
Miradi ya kipuuzi na isiyo na tija kama hii hata kwa wanaoishabikia sio ya kuipelekea pesa.

Hivi huko serikalini kuna watu kweli wanaofikiria? Yaani baada ya kukamilika waanze tena kutuongezea kodi eti kulipia kujiendesha? Huu ni wehu
BBC ndio mtaa gani kwanza tuanzie hapo. Nchi HII hatuongozwi na uzandiki wa BBC.
 
Mabandiko yako yote huwa ya kipumbavu tu. Huna lolote endelea kuota ndoto huku miradi ya daraja la Busisi, sgr ikikamilishwa. Ama sivyo kajinyonge.
Kuna wakati niliweka bandiko humu kuhusu upendeleo uliofanywa na serikali ya awamu ya 5 kupeleka SGR Mwanza badala ya Kigoma ambapo ndiko economic viable kwa huo mradi. Kikundi fulani kikiongozwa na Mgambilwa ni muntu wakapinga hoja hiyo na kushadadia kuwa kupeleka SGR Mwanza ni bora zaidi.

Kwa takwimu hizi nathubutu kukitambua kukundi cha kina Mgambilwa kuwa ndio wale Sukumagang.

Vv
 
Back
Top Bottom