Mwelekeo wa Ndoa yangu umefikia pabaya sana

Mwelekeo wa Ndoa yangu umefikia pabaya sana

Achana na mambo ya haramu mtoto wa watu umemzalisha maziwa yashalala kama ndala hutaki kumuoa ndo mgogodro ulipo then unaenda nje kuzalisha wa pili Sasa jifanye nunda kao huko nje kama hautokuja kurogwa
Dah!! Huyu sijui atamwagiwa mafuta ya,moto!?!?
 
Ambacho sijasema ni kuwa nilikutana nae akiwa na mtoto, na kibaya nilijua hilo kwa baadae sana kwa hiyo hajazalia kwangu
Hakukuambia ana mtoto? na je huoni haoni matumaini ya ndoa kwako ndio maana amekuwa na hali hiyo ya sasa maaana mpaka unaamua kuishi naye maanake hapo kabla hakuwa na taabia hizo. Mkuu mpe elimu huyo dada kama hajawahi kukucheat na baba mtoto wake wa kwanza angalia uwezekano wa kumrudisha kwenye hali yake.
Suluhisho sio kumwacha.
 
Nilishasem uwezo wa kupeleka mahali ninao mda wowote ila changamoto aina ya maisha tunayoyaishi ndio hayaridhishi kabisa nakumbuka alishawahi kunipiga na kukimbia na nilivyotaka kumkimbiza kuna wazo likanijia nitaonekana mjinga mbele ya jamii kwa hiyo huwa namwacha, tu ila ni tukio haliwez kufutika kila nikiwaza kumrasimisha kuwa mke wng
Mkuu Kwanza Mimi ni miongoni mwa wapinga mahali, sidhani Kama kutoa mahali kutaifanya ndoa yako iwe imara, nasema no!! ,Pili huyo mke wako sioni sababu ya wewe kuendelea kuwa naye kwa kigezo Cha kuhofia watoto kuteseka, yaani umekumbatia mzinga wa nyuki, nyuki wanakugonga huku unajipa matumaini ya kupata asali, hakika utaumia

Ni kweli Maisha ya ndoa yana changamoto , lakini kwa kiwango mlicho nacho hiyo sio ndoa, yaani mmesubiri kifo kiwatenganishe ili mmoja wenu awe huru na ashangilie, hii siyo ndoa. Ujue kuwa Maisha ya dunia hii ni mafupi sana, hivyo fanya lolote lakini hakikisha unayaishi kwa Raha, Kama Mama watoto wako Ni changamoto mpe likizo akajifunze, lete mke mwingine naye akizingua fukuza lete mwingine, Babu yangu alioa wanawake wanne kwa nyakati tofauti, nadhani hicho ndo kilimsaidia yeye kufa akiwa na umri wa miaka 90.Lakini kwa Maisha yako usipokuwa makini hata 60 huifikishi, hii ni utokana na kero unazozipata kwa familia yako.
 
Pili huyo mke wako sioni sababu ya wewe kuendelea kuwa naye kwa kigezo Cha kuhofia watoto kuteseka, yaani umekumbatia mzinga wa nyuki, nyuki wanakugonga huku unajipa matumaini ya kupata asali, hakika utaumia
Wrong advice!
 
Kama Mama watoto wako Ni changamoto mpe likizo akajifunze, lete mke mwingine naye akizingua fukuza lete mwingine,
Hovyo kabisa. Yani washauri ndo nyinyi!!? Alafu uwe balozi wa nyumba kumi utavunja ndoa zote.
Wacha avune alichopanda. Mke ni lazima aoe na watoto ni lazima alee.
 
Ndio kitu nafkiria ila natafta njia ambayo haitamuathiri pia ila sina tena ham ya kuishi nae nataman nimpangie safar ya kwenda kwao nimpe hata M5 then akifika ndio nimwambie apambane na maisha yake asirud tena
Afu watoto sasa mkuu?

Wana umri gani?

Sema inabidi utulize akili sana, wanawake wengi wanafanana tabia..tena unaweza kusema Bora hata huyo unayemuona kimeo

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Saf ndugu yangu nashukuru maana umepatwa na uchungu kuona mwanaume mwenzio anapata shida shkran mkuu
Huyo anakupoteza hata usimsifie...amini nakwambia[emoji848]

Wewe mtoe out huyo wife wako ongea nae kiupendo muulize shida ni nini atakwambia tu then msolve tatizo

Mwanamke kashakuzalia watoto wawili ni upendo mkubwa sana kwako mkuu, labor isn't a joke mzee baba!

Kaa nae kwanza msikilize, usije kujuta mbele nakwambia[emoji848]

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Nilishasem uwezo wa kupeleka mahali ninao mda wowote ila changamoto aina ya maisha tunayoyaishi ndio hayaridhishi kabisa nakumbuka alishawahi kunipiga na kukimbia na nilivyotaka kumkimbiza kuna wazo likanijia nitaonekana mjinga mbele ya jamii kwa hiyo huwa namwacha, tu ila ni tukio haliwez kufutika kila nikiwaza kumrasimisha kuwa mke wng
Maisha hayakuridhishi ukamzalisha mtoto wa kwanza.

Maisha hayakuridhishi ukamzalisha mtoto wa pili.
 
HABARI wakuu, kwanza kabla ya yote niwatakieni mfungo mwema,

Umri wangu ni Miaka 33, Nipo katika ndoa pia nina Watoto Wawili na huyu mwanamke, naona nisiandike Mengi kuhusu maisha yangu na huyu Mwanamke ila kimsingi tu ni MTU ambae ninapitia changamoto nyingi sana katika mahusiano haya, yaani kiufupi tu hata sielewi mwelekeo wa ndoa hii, Tulikutana nae tukachukuana nae Tukaamua kuishi pamoja hadi Sasa Tuna watoto wawili, lakini sijamtolea mahali, lakini sio kwamba sina uwezo wa kutoa mahali ila kinachonichelewesha ni aina ya maisha ambayo tunaishi nae, Yaani siku za furaha ni za kuhesebakika kuliko siku za kununiana, ana vijisababu visivyokuwa na mashiko anajinunisha, Mara utastuka usiku unamkuta MTU amekaa kitandani analia bila sababu, Mara atoke akae jikoni usiku, Mara ajidai amepandisha presha nianze kumpepea usiku yaani ni mateso bila ya kifo, Kimaisha siko vibaya ninamtimizia kila hitaji pia ninakaa kwangu sijapanga na Mimi ni MTU wa kutoka asububi narudi jioni kutokana na aina ya harakati zangu zinazoniweka mjini, Sasa kulitokea kasumba Kikitokea kimgogoro kidogo ananinyima unyumba, hadi inafkia mda unazuka ugomvi ndo napewa huwa nawaza namna ya kuachana nae, ila nawaonea huruma sana wanangu, pia hata yy namuonea huruma, maana nishamzalisha watoto Wawili wote alafu nimuache huwa kimsingi naishi nae kwa sababu ya huruma, pia kwa sababu ya kuwaonea huruma wanangu nilitamani wanangu walelewe na wazazi wao ila mwelekeo wa Maisha haya sijajua hatima,

Tangu mwezi wa Pili kuna shida ilitokea nikawa nanyimwa unyumba hadi ikafikia hatua nikakosa namna ikabidi nianzishe uhusiano na mtu mwingine ila kibaya nilianzisha kama njia ya kumaliza haja zangu nikirudi nyumbani najilalia zangu maana sikutaka ugomvi wa kutaka mbususu kwa wife ila kibaya naona nimezama mazima yani huyu mtoto anajua kucare, anajali kiufupi ninapata kila kitu ambacho nilikuwa nakosa awali, lakini kibaya zaidi na bahati mbaya kwa sasa huyu Mtoto ana ujauzito wangu, hapa nipo njia panda, Kusema kweli ingekuwa uwezo wngu ningemuoa huyu mtoto maana kimsingi mke ninaekaa nae ameshindwa kutambua thaman yangu, lakini kila likija swala la wanangu huwa naishiwa nguvu maana siwezi kuruhusu wanangu kukaa mbali na Mimi pia sina imani kama mwanamke huyu ataishi na wanangu vizuri mda ambao Mimi sipo, kusema kweli najikuta naishi katika majuto niliingiaje 18 za huyu mwanamke! Na ni namna gani nitaepuka hili!

Pia kuhusu suala ya yeye Pengine ana mahusiano mengine siwezi jua na huwa sina asili ya kifuatilia maisha yake maana nipo bize sana na pia huwa sitaki kabisa kufanya kumfuatilia maana matokeo ya kumfuatilia MTU siku zote hayawi mazuri,

Kibaya zaidi ni kuwa jamii tunayoishi nayo inatuona tuko vzuri maana mchana tunaigiziana ila ikifika usiku hakuna MTU anamsogelea mwenzie.

USHAURI WENU MHIMU.
Mi ka wewe tuu saa hii nahangaika na talaka aliyoiomba yeye lakini akabadili mtizamo et ameghairi anataka ndoa tena baada ya kunikuta mi nimekaza nataka apewe talaka yake.

Hugo mama watoto atakusumbua na ashajua uzaifu wako atakupiga tukio hilo mwenyewe utajuta huruma zako.

Nb: pengine analilia mahari kwann usimuoe kabisa???
 
Back
Top Bottom