Mwenye historia ya Nabii Mwamposa kabla ya kuanza huduma yake

Huu Unabii wa Watu kunya, kukojoa, kujifungua, kutapika Kobe, Hirizi, Mjusi, Mende, panya, tandu, wadudu, Nyoka, paka kufa nje ya Nyumba ni Unabii na Utume toka Kwa Nani? Anayemtukuza Mbona hakuwahi kuwafanyia Wafuasi wake hivyo? Anyway Kizazi Cha Kulogwa, kuchawiwa, kutaka Mafanikio ya Kimwili kimepata Nabii.
 
Hao mitume hawakuibukia tu kama uyoga.

Yesu aliwachagua mwenyewe. (Vetting).

Akaaa nao kipindi chote kabla ya kupaa. ( walipitia training).

Hivyo ni muhimu sana kupata mafunzo na kukidhi vigezo vya kazi husika kabla ya kuifanya.
Si kweli
 
Ni kwamba hawa jamaa wanahubiri jinsi ya kuitawala dunia(urafiki na dunia) wala hawafundishi kuhusu ufalme wa Mungu. Sasa sote twamjua mtawala wa dunia hii, ndicho kizazi cha manabii wake.
 
Anaishije bila mke?!
 

Kama hana mke lazima anatafuna kuondoo wake. It's just common sense
 
But even devil can do miracles, unakumbuka issue ya Musa na Farao? [emoji137][emoji137]‍[emoji3601]
 
Tujuze sasa mbona Kama umepanic? Lete hoja yako tuone how valid it is!
 
Umeonaje au kuyajua haya Kama wewe siyo mchawi?!
 

Kipawa au Karama haipo hivyo. Wewe inaongelea mafunuo. Mafunuo yanakuwa na ujumbe ndani yake. Tofautisha karama na mafunuo.

1. Kuhusu Yesu kutemea mate udongo ulikuwa ni ufunuo sio Karama ya uponyaji. Ina maana aliondoa laana ya ardhi iliyomtengeneza mwanadamu na ndio maana alipompaka yule kipofu akaona.

Mafunuo yanafanyika Mara moja tu Basi. Ndio maana humuoni Yesu akipaka watu matope. Sasa Mawamposa yeye mafunuo anafanya kila siku, huo ndio uongo wenyewe.

2. Kuhusu Elisha kumwambia Naaman akaoge Jordan ilikuwa sio Karama bali mafunuo. Ndio maana humuoni Elisha tena alimwambia mtu mwingine akaoge Jordan.

Ujumbe ni Kwamba kujiishusha na kutii kunaweza kukupa uponyaji. Naaman alikuwa jemedali wa Vita, hivyo alijua kwamba Elia akimwekea mikono atapona lakini, Elisha akampa sharti la kwenda kuoga Mto Jordan na kweli akapona.

Hivyo ni vizuri kutofautisha karama ya uponyaji na mafunuo. Karama ya uponyaji Inafanya kazi kwa jina la Yesu Kristo aliye hai lakini Mafunuo unaweza kupona bila Karama ya uponyaji, ni maelekezo kutoka kwa Mungu.

Sasa manabii wa uongo hutumia mafunuo na kulazimisha kuwa karama ya uponyaji. Nao hutumia maandiko kujustify wanachokifanya. Huwezi kuwa na Karama ya uponyaji, lakini daily ni kutumia mafuta na maji au udongo, huo unakuwa ni uchawi au uganga. Ita watu waombee kwa jina la Yesu Kristo wapone.
 

Nikusahihishe kuhusu matiya, mitume walipiga kura na kura ikamwangukia matiya. Lakini kazi ya matiya haikuwa na matokeo, ndio maana Mungu mwenyewe akaamua kumleta Mtume Paulo.
 

Padri yeyote anayetetea ushoga sio mtumishi wa Mungu.
 
Lakin anatumia mafuta na maji kwa jina la nani jomba

Kwanini atumie maji na mafuta?. Kwanini asikemee pepo kwa jina la Yesu Kristo. Paulo akasema alitokea mtu anahubiri injili tofauti na hii msimsikilize.
 

Please usimlinganishe Yesu na Mwamposa. Tatizo mnadhani kwa sababu Yesu Kristo alifanya hivi na mimi nifanye hivyo. Yesu alifunga siku 40 bila kula Wala kunywa. Kuna binadamu anaweza hilo?. Msitumie Yesu Kristo kuhalalisha unabii wa uongo.
 
Kwanini atumie maji na mafuta?. Kwanini asikemee pepo kwa jina la Yesu Kristo. Paulo akasema alitokea mtu anahubiri injili tofauti na hii msimsikilize.
Paulo Mwenyewe alitumia leso na nguo kutoa pepo hakukeme tu kasome hapo

Matendo 19:11​

Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida; hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini mwake, magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu wakawatoka.
 

Naomba nijibu kidogo ulichosema.

1. Kwanza kuhusu Luka 9:49-50, Yule mtu walimkuta anatoa pepo kwa jina la Yesu Kristo. Hilo ndilo la muhimu, alitumia Jina la Yesu Kristo kutoa mapepo na sio maji Wala mafuta. Kama wanafunzi wa Yesu wangemdaka huyo jamaa anatumia maji kuponya watu basi jibu la Yesu Kristo lingeweza kuwa tofauti.

Lazima ujue kwamba kuendelea kutumia zana za upako ni dalili za kuonesha kwamba Jina la Yesu Kristo alijitoshelezi hivyo tunalisaidia kwa kutumia chumvi au maji au mafuta.

Kuna maeneo wanatumia Hadi pipi au keki za upako. Shida ipo wapi kutumia jina la Yesu Kristo?. Kwanini usitumie jina la Yesu pekee mpaka uanze kuwambia watu wakanyage mafuta na kunyunyiza mafata kwenye majumba yao?.

Kazi ya shetani ni kulishusha jina la Yesu Kristo na kulifanya halina nguvu.

2. Pili, kuhusu Waefeso 4:11-13. Lazima uelewe zile ni huduma tano.
Mitume
Manabii
Waalimu
Wachungaji
Wainjilisti

Hizo huduma tano unapewa na Mungu sio unajipa mwenyewe. Baada ya kuokoka na ukajazwa Roho Mtakatifu Kuna huduma Mungu anakupa na wewe utaifahamu maana itakuwa ina imba ndani yako. Sasa hizi ni huduma sio vyeo au ngazi za madaraka.

Naomba nitoe mifano;

A. Kwanza mitume, mitume kazi yao kubwa ni kutembea ulimwenguni kote na kufungua kazi ya Mungu. Tena hutakiwa kwenda maeneo yaliyoshindikana au yasiyomjua Kristo Yesu. Ndio maana Paulo Kama mtume alitembea karibia dunia nzima akifungua kazi ya Bwana Hadi uarabuni. Sasa Leo tuna mitume wa vyeo sio huduma, ndio maana utakuta mtu anajiita mtume ila anasimamia kanisa. No mtume kwa huduma Hana kanisa bali anazunguka sehemu mbali mabli kufungua makanisa. Mitume wanatakiwa kwenda Somalia au Sudan au Iraq ambako injili haijafika, lakini leo ili utambulike kama mtume lazima ufanye miujiza au uponyaji basi.

B. Pili, manabii, manabii kihuduma Ni Jicho na mdomo wa Mungu. Kihuduma nabii hawezi kuchunga kanisa , Bali anaweza kuwa mshirika wa kawaida kanisani lakini mwenye uwezo wa kuona mambo ya mbele au mambo ambayo wengine hatuyaoni. Pia nabii husema Yale ambayo Mungu anataka kuonya kanisa au nchi au kundi fulani etc. Hivyo nabii kihuduma sio wa kuchunga kanisa bali kutoa mafunuo ambayo yanatoka kwa Mungu, kunifahamisha taifa yatakayokukuta mbele, kulionya taifa kuhusu dhambi na etc. Hivyo ni muhimu kuwa na huduma ya kinabii kanisani ili kanisa likomae.

Tatizo ni kwamba unabii wa Leo umekuwa ni cheo. Unabii Kama hudumu ni mchache Sana, ndio maana manabii wengi Leo hawaoni ya mbele au kkusema ya kutoka kwa Mungu ili kunenga ufalme wake. Utasikia Nabii anakuuliza unanifahamu au tunafahamian, anaanza ninakuona upo Mwanza, Mara naona jina Grace halafu watu wanachanganyikiwa. Kuna uganguzi na unabii. Uganguzi unabase kwa mwanadamu basi ila unabii ni kutoka mbinguni ili kuujenga ufalme wa Mungu duniani na kuonya kuhusu dhambi.

Niishie hapo kwa leo, ila ni muhimu kutofautisha utume na unabii wa kihuduma na utume na unabii wa kicheo.
 
Kuna shuhuda nyingi ukifatilia vizuri niza uongo tena uongo mkubwa. Na wanao zitoa wako trained kabisa kwa ajili ya hiyo kazi.

Ukiwa na akili kama za bata huwezi elewa ila ukifatilia vizuri mtiririko wa shuhuda na matukio yaliyomo utaelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…