Mwenye historia ya Nabii Mwamposa kabla ya kuanza huduma yake

Mwenye historia ya Nabii Mwamposa kabla ya kuanza huduma yake

Agano la kale limefungwa kwenye damu za mafahali nikimaanisha wanyama, na vitu vingine kama mafuta ya upako, chumvi na maji ya upako, huku agano jipya limefungwa kwenye damu ya YESU ambao kwa jina lingine ni damu ya mwanakondoo
Ila kudai mafungu ya kumi hapo mnaona agano la kale halijafungwa

Kitabu cha Agano la kale cha Malaki kiko hai ikifika kudai mafungu ya kumi kwa waumini kusema wezi wanamwibia Mungu!!!

Hapo agano la kale linakuwa hai.Fungu la kumi lazima litolewe
 
Umewahi kumshuhudia akishuka ama kupata gari lake? Kama bado tuulize sisi tuliyowahi kuwa waambata wake tukujuze. Unaibiwa wewe.
Bìnafsi sijawahi kumuona akiwa anashuka kwenye gari, watu wa media wanaonyesha msafara tu akiwa anashuka wanachepusha kamera.

Kwa hyo naomba ufunguke kwa manufaa ya umma kama zitto junior alivyotoa mawazo yake kwa uwazi.
 
Unafahamu kuwa hata shetani anaponya? Kwahiyo kufunguliwa kwa watu siyo hoja.

Je, wajua kwamba jina Yesu linatumikq hata ktk nguvu za giza? Kwahiyo kutajwa kwa jina la Yesu kisikuzubaishe.

Mwamposa mhuni Kama wahuni wengine. Umewahi kumshuhudia akishuka ama kupata gari lake? Kama bado tuulize sisi tuliyowahi kuwa waambata wake tukujuze. Unaibiwa wewe.
Jamaa hapandi gari?
 
Yes mke hana,ila kuna mdada kazaa nae kamjengea kighorofa huku Goba Kulangwa,alafu ni wale wadada wa mjini kishenzi.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Anaitwa kate milaya, malaya mstaafu wa china, thailand...hio mimba aliambiwa atoe akagoma.
Kuna dada mwingine mikocheni ana ki Spa cha uongo na ukweli ndo anatoka nae..
Honestly, huyo Mwamposa ni mhuni tu kama wengineo wengi waliopita....hii biashara ya wanyakyusa cc( mwingira, lusekelo...) sio ya kuumiza kichwa kabisa , soon atazuka nabii mwingine lol.
 
Please usimlinganishe Yesu na Mwamposa. Tatizo mnadhani kwa sababu Yesu Kristo alifanya hivi na mimi nifanye hivyo. Yesu alifunga siku 40 bila kula Wala kunywa. Kuna binadamu anaweza hilo?. Msitumie Yesu Kristo kuhalalisha unabii wa uongo.
Hio sio point yangu, point yangu ni kwamba sio kila watu wanaemsema ni muongo ni muongo kweli.

Kama Yesu aliitwa muuongo na watu wa dini vp huyu mfuasi wa Yesu.

Shida ya wabongo sio kuwa Kuna Manabii wa uongo shida n wabongo na waafrika wengi hatuna imani kwa Mungu.

Ndio maana mtu alifanikiwa, waafrika huwa tunascribe responsibility kwa shetan kupitia either uganga au illuminati.

Akili za waafrika ziko hiv
""Mungu yupo ila hafanyi, anebariki na kuponya n Shetani""". Hatukiri haya directly ila mitazamo yetu inakiri hiv.

Kwa waafrika Mungu n kama pambo tu, ila mtenda miujiza n shetani

Ndo maana ukiwa n shida akili zako zinakutuma kwenda kwa waganga, na yeyote akifanikiwa jambo la kwanza kumdhania n either n mshirikina au freemason, sababu hii ndio akili ya waafrika.
 
Ila kudai mafungu ya kumi hapo mnaona agano la kale halijafungwa

Kitabu cha Agano la kale cha Malaki kiko hai ikifika kudai mafungu ya kumi kwa waumini kusema wezi wanamwibia Mungu!!!

Hapo agano la kale linakuwa hai.Fungu ls kumi lazima litolewe
Tofauti ya agano jipya na la kale ni kwenye matumizi ya Damu, la kale ilifanye upatanisho na ulimwengu wa Roho lazima utumie Damu ya mafahali lakin agano jipya upatanasho na ulimwengu wa Roho unatumia Damu ya YESU ambayo ni Damu ya Mungu hio ndo tofauti ya agano jipya na la kale na sio sadaka kama unavyodai sadaka ziko pale pale
 
Jomba mi nadhani yote anafanya.. anabatiza, anaungamisha, anawafundisha maneno ya kwenda Mbinguni...lakini nimesema soma maneno kutoka Luka 9:49-50
Lini amefanya hayo mkuu? Unaweza weka hata clip akibatiza au akiombea watu wajazwe Roho Mtakatifu? Au alifundisha watu waache dhambi sababu Kuna hukumu siku ya mwisho?

Yes nimesoma huo mstari ila Biblia haisomwi hivyo mkuu. Bible inasema magugu yanakua pamoja na ngano ila mwishoni yatachomwa na vile vile inasema sio wote waitao jina la Bwana Bwana wataiona Mbingu!! Means hata huo mstari unahusika ila Yesu hakutaka tu wanafunzi wahukumu maana hiyo kazi ni yake Mungu sio binadamu yoyote.
 
Acha roho mbaya yani kwa maisha haya ya usasa afanyie bure..unadhani hiyo ministry ingesimama..mngemlipa hela ya kukodi hapo tanganyika pekaz...ungemlipia bili za umeme..unhemlipia vyombo vya miziki..usafi..usafirishaji..na mahubiri kwa njia za redio na tv.??

Ebu tumia akili kidogo..Yesu mwenyewe alihitaji fedha hadi akawepo mtunza fedha mzee yuda.

#MaendeleoHayanaChama
Yuda alikuwa anatunza pesa za Yesu?
Interesting....naomba kufahamu zaidi
 
Hio sio point yangu, point yangu ni kwamba sio kila watu wanaemsema ni muongo ni muongo kweli.

Kama Yesu aliitwa muuongo na watu wa dini vp huyu mfuasi wa Yesu.

Shida ya wabongo sio kuwa Kuna Manabii wa uongo shida n wabongo na waafrika wengi hatuna imani kwa Mungu.

Ndio maana mtu alifanikiwa, waafrika huwa tunascribe responsibility kwa shetan kupitia either uganga au illuminati.

Akili za waafrika ziko hiv
""Mungu yupo ila hafanyi, anebariki na kuponya n Shetani""". Hatukiri haya directly ila mitazamo yetu inakiri hiv.

Kwa waafrika Mungu n kama pambo tu, ila mtenda miujiza n shetani

Ndo maana ukiwa n shida akili zako zinakutuma kwenda kwa waganga, na yeyote akifanikiwa jambo la kwanza kumdhania n either n mshirikina au freemason, sababu hii ndio akili ya waafrika.
Umewahi ona mtu anamkosoa Mwakasege, Kimaro, au Kulola kwa level za huyo Mwamposa?

Ukiona tofauti ya mafundisho Yao ndio utaelewa shida inaanzia wapi
 
Kipawa? Ule ni uganga tu kama uganga mwingine. Kwa wakristo Kipawa kipo ndani ya mtu sio mafuta/keki Wala kutoa fedha Ili uombewe/appointment na Mtume!!
Injili yoyote isiyohubiri Toba na Msamaha ni Injili nyingine. Sio injili ya Kutoka kwa Yesu.

Fatilia from A to Z ktk mafundisho yake anza Januarh hadi Dec hutaoba hata siku moja anahubiri Injili ya Toba.
 
Umewahi ona mtu anamkosoa Mwakasege, Kimaro, au Kulola kwa level za huyo Mwamposa?

Ukiona tofauti ya mafundisho Yao ndio utaelewa shida inaanzia wapi
Kwa muda mfupi niliomfatuilia huyu Mwamba yeye Miujiza yake huhusisha Mijusi, nyoka, vyura, hirizi, paka, Mbwa, mende, jongoo.

Enyi watu wa Mungu fatilieni wanaotoa shuhuda zao zote kama zitakuwa nje ya hao wanyama na viumbe.


Kila mwenye kupona au kubarikiwa utamuona anahusisha na hao viumbe au kaviona au vimemtoka.

Hii ni Injili nyingine. Haitoki kwa Yesu Kristo Mnazalethi
 
Mkuu, maandiko hayajawahi kupinga miujiza mikubwa mikubwa kutokea kwa watu, bali imeonya kuwa hata wasio wa Mungu wanatenda hayo. Maandiko yametuonya tuyapime yote na kama yametokana na Mungu. Ni kosa kubwa sana kujenga msingi wa imani yako kupitia miujiza, ziko sababu nzito tu za kimaandiko.

1. Miujiza ni lazima imbadili mtu imani yake. Hili ni kubwa zaidi, tunaona kwa hiki kizazi cha manabii Waislamu na wapagani wengine wakipokea miujiza na kurejea kwenye imani zao. Wengine wengi wamejenga imani zao kwa mwamposa na maji na mafuta anayotoa. Hii ni hila ya shetani kabisa.

2. Miujiza ya mbinguni imelenga kumpa Mungu utukufu kwa sababu Mungu wa mbinguni hashiriki utukufu wake na kiumbe. Licha ya kauli ya kisanii "nani mtenda miujiza? ", lakini ni ukweli usio shaka wafuasi wa Mwamposa humpa utukufu yeye.

3. Msikilize vema Mwamposa, ni mhubiri mzuri sana wa miujiza na mafanikio. HAHUBIRI INJILI YA UFALME WA MBINGUNI. Wafuasi wake WOTE ni genge la wasaka mafanikio na afya pekee, kwani huhubiri habari za uzima ujao na maisha baada ya kifo. Huyu ni mtu hatari mno kwa ufalme wa mbinguni kwani anawafungia watu mlango wa mbinguni kwakuwaahidi raha ya hapa duniani.

4. Baada ya kushuhudia miujiza wafuasi wake hutoka bila uwezo wala upeo wa kumhubiri Kristo badala yake wana nguvu na mamlaka ya kuhubiri uweza wa Mwamposa kuponya. Hii inasababishwa na kutofundishwa neno la uzima bali majigambo na majivuno ya mhubiri kuponya. Wafuasi wake bila kujua hujifanya mabalozi wakubwa wa Mwamposa kwa watu wengi huku wakimnadi ni jinsi gani anaweza kuponya na kukupatia mali nk. Hii ni hila ya shetani.

Yako mengi ambayo ningeweza kuyaandika hapa lakini naishia hapo nisikie unajibu vipi hoja hizi za kimaandiko.
Umemaliza Kila kitu mkuu, wasipoelewa Hili basi shetani amewapofusha kabisa.
 
Umewahi ona mtu anamkosoa Mwakasege, Kimaro, au Kulola kwa level za huyo Mwamposa?

Ukiona tofauti ya mafundisho Yao ndio utaelewa shida inaanzia wapi
Kulola Marehemu huwezi ongelea marehemu

Kimaro na Mwakasege kaz yao kufundisha Bible study tu sio kutoa mapepo na majini yakiyoparamia watu.

Wale wahubiri tu wa Biblia

Kipengele hiki

Mathsyo 10:8​

Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo

Kwao hawakigusi

Siwalaumu bali nawapongeza wanafanya sehemu yao hata kama ndogo Mungu huheshimu chochote hata kidogo unafanya kwenye kazi ya ufalme wake hata iwe kufagia kanisa

Eneo la kufungua watu wakiofungwa vifungo vya Shetani na Mapepo Kimaro na Mwakasege eneo hilo kwao ni bahari wasiyoweza ogelea Hayo ni maeneo ya akina Mwamposya. Wao mwisho wa huduma zao ni tu kuongea Biblia inasema kwenye sura hii na mistari hii Kwenye deliverance ministry sio area yao ni watoto wadogo sana huko

Mwamposya waislamu na dini zote wenye majini na mapepo hufurika kwake kufunguliwa kimaro na Mwakasege asilimia kubwa wanajaza wengi waumini wa kilutheri tu wanaohitaji kujifunza Biblia
 
Shuhuda nyingine za Mwamposa kweli zinatatiza. Nyingi ni physical na si spiritual.

Utasikia mtu katapika/kanya kufuli lililofungwa kumaanisha kuwa alifungwa na wachawi sasa kafunguliwa, mara katapika wembe, uzi, sindano.... Yaani kama mazingaombwe tu.
Kwa hiyo bwana Yesu hawezi kutenda miujiza kama hiyo au..??
 
Kwa wakristo dhambi isiyosameheka ni kumkufuru roho mtakatifu..na manabii (manabii wa kweli)wanaongozwa na roho mtakatifu..hivo kamA huna macho ya kiroho ya kuona kama ni fake au real..ni heri ukae kimya usijekuingia dhambi isiyosameheka kizembe.......
 
Sio kufafanua anatafuta justification kupitia mistari ya biblia najua atakimbilia ule mstari unaosema waweke mafuta juu ya wagonjwa n.k

Lakini issue ni kwamba injili ya kweli ni Ile inyaoongelea mtu kwenda mbinguni. Haiwezekani mtu anaita mpagani anampa mafuta tu anamuacha aende bila kumfanyia Sala ya Toba, bila kumbatiza, Sasa kama sio faida yake kiuchumi unadhani ufalme wa Mungu una gain Nini kupitia huduma yake? Anaweza kweli kusema anasaidia Roho zifike mbinguni au anaacha watu waendelee kupotea gizani yeye anawapa mafuta tu imetosha.
Kwa hiyo mafundisho ya injili hayahusu maisha yetu tunayoishi hapa duniani kabisaa....daaaa...injili inazungumzia safari tu ya kwenda Mbinguni..Ni kweli ..???? Jitafakari na mafunzo uliyonayo
 
Kwa wakristo dhambi isiyosameheka ni kumkufuru roho mtakatifu..na manabii (manabii wa kweli)wanaongozwa na roho mtakatifu..hivo kamA huna macho ya kiroho ya kuona kama ni fake au real..ni heri ukae kimya usijekuingia dhambi isiyosameheka kizembe.......
Ukaeje kimya jomba...unampa shetani nafasi ya kukuingia...hatari sana..usipotoshe..sema endelea kuomba binafsi always ukimwomba Mungu neema na rehema akujalie kutambua yote yatendekayo
 
Back
Top Bottom