Mwenye neno lolote aniambie japo kupoza akili yangu

Mwenye neno lolote aniambie japo kupoza akili yangu

Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima. Niende kwenye mada moja kwa Moja.

Mimi ni Kijana wa kitanzania na hivi sasa nipo chuo kikuu kimoja hapa Tanzania jijini Dar es Salaam, nachukua shahada ya kwanza ya ualimu sayansi.

Natoka katika familia ya kawaida sana yenye jumla ya watoto tisa huku mimi ni wa kwanza yaani first born.

Hali ya uchumi ya wazazi ni duni sana hadi kufika hapa kwa Kweli ni kwa neema tu, kiufupi familia na wadogo zangu nane wananitazama mimi kama mkombozi. Hali unanifanya niishi kwa msongo mkali sana wa mawazo.

Nawaza sana mwakani nitakapomaliza chuo maisha yangu yatakuwaje? Familia na wadogo zangu tawashikaje mkono? Moyo wangu una madonda mabichi sana.

Nilibahatika kupata mkopo wa elimu ya juu lakini kwa hali ya nyumbani pesa yangu ya meals and Accomodation yaan boom huwa naikata mara mbili nusu nabaki nayo nusu natuma nyumbani.

Wanabodi nahisi maneno haya hayawezi eleza nachotaka kufikisha kwenu.

Na umri mdogo lakini sonona nahisi inanitafuna. Nataman nikimbilie South Africa kujaribu bahati yangu.

Muwe na asubuhi njema, hapa nipo njiani naelekea shule maana tupo Field lakini akili haipo Sawa.
'Mkabidhi BWANA kazi zako na mawazo yako yatathibitika'
 
Akili huwa inafikia mwisho wakati mwingine maana ina ukomo, ni logic, ndivyo ulivyoumbwa, kwa uliyoyasema nakuelewa sana.

Ila akili zinapofikia mwisho kuna matuamini, kuna Neema, ambayo inatoka na ahadi za Mungu na hizo ndo kimbilia.

Maisha utakayoishi kutoka sasa mpaka umalize chuo yataamua uendelee na sonona au uso utakate na ufanikiwe.

Mimi kama Mkristo, nikiwa na hali kama yako, tumaini langu huwa katika ukiri wa neno la Mungu tu na hivyo huona matokeo.

Imani ni jambo la Muhimu sana kwa mwanadamu, maana uwezo wake una mwisho, ila ana roho na access ya kuunganishwa na ulimwengo usio na mipaka.
Well said👏
 
South Africa Kama unaenda fata maisha utapata lakini Kama unaenda fata mengine utarudi maiti.
Kazi okozi kwa magraduate wengi waliokimbia south baada ya kuchoka kutembeza bahasha bongo.
Ni Kazi za ulinzi kwenye haya makampuni makubwa ili uweze isoma ramani kwanza,ukishakuwa mzoefu unabadili kazi.
Sawa na ulaya kazi ya kwanza kwa mgeni ni kubeba box ukishakuwa mwenyeji huwezi beba box kazi zipo nyingi tu.
Nenda kihalali fully documents, ogopa wabongo kaa nao mbali hata ukisikia wanaongea kiswahili.
Bora ukajichanganye na wa Kenya
 
Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima. Niende kwenye mada moja kwa Moja.

Mimi ni Kijana wa kitanzania na hivi sasa nipo chuo kikuu kimoja hapa Tanzania jijini Dar es Salaam, nachukua shahada ya kwanza ya ualimu sayansi.

Natoka katika familia ya kawaida sana yenye jumla ya watoto tisa huku mimi ni wa kwanza yaani first born.

Hali ya uchumi ya wazazi ni duni sana hadi kufika hapa kwa Kweli ni kwa neema tu, kiufupi familia na wadogo zangu nane wananitazama mimi kama mkombozi. Hali unanifanya niishi kwa msongo mkali sana wa mawazo.

Nawaza sana mwakani nitakapomaliza chuo maisha yangu yatakuwaje? Familia na wadogo zangu tawashikaje mkono? Moyo wangu una madonda mabichi sana.

Nilibahatika kupata mkopo wa elimu ya juu lakini kwa hali ya nyumbani pesa yangu ya meals and Accomodation yaan boom huwa naikata mara mbili nusu nabaki nayo nusu natuma nyumbani.

Wanabodi nahisi maneno haya hayawezi eleza nachotaka kufikisha kwenu.

Na umri mdogo lakini sonona nahisi inanitafuna. Nataman nikimbilie South Africa kujaribu bahati yangu.

Muwe na asubuhi njema, hapa nipo njiani naelekea shule maana tupo Field lakini akili haipo Sawa.
Tatizo umebeba matamanio makubwa sana.tuliza kichwa focus kwenye masomo fata moja mbili tatu usiruke namba.
 
Kwann usiitumie hio nguvu kazi ya hao ndugu zako shambani,lima mazao yenye Uhakika wa kuvuna hata kwa mvua ndogo mfano kunde, karanga,haya mazao demand yake kwa mjini ni kuwa kilo moja ya karanga lishe ufika hadi elf 4.
Kunde si chini ya elf 2 kilo.
Heka moja unavuna gunia 8-10.
Lima Heka 20.
 
Mwache mwenzako asome kwanza[emoji23][emoji23]
Asome!!!? Shule itamsaidia nini?? Hiyo elementary education aliyoipata inamtosha, shule imeua vipaji vya wengi, shule imekula mitaji ya wengi, atafute cha kufanya kupitia hiyo ada anayoenda kutupa shuleni[emoji23]unaweza ukasema havina mashiko ila ukisoma between the lines utaona vinafikirisha.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Kwann usiitumie hio nguvu kazi ya hao ndugu zako shambani,lima mazao yenye Uhakika wa kuvuna hata kwa mvua ndogo mfano kunde, karanga,haya mazao demand yake kwa mjini ni kuwa kilo moja ya karanga lishe ufika hadi elf 4.
Kunde si chini ya elf 2 kilo.
Heka moja unavuna gunia 8-10.
Lima Heka 20.
Unaijua output ya kilimo cha mkono???


Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza ukapanda zao la nyonyo mbarika Castro oil hata eka 30 uhitaji kulima ni kuchoma tu majani au kama ardhi ni kame au jangwa unapanda tu yanakuwa kwa umande hata kiangazi yanastawi baada ya miezi 3 unavuna mbegu zake unaanika unakamua mafuta.
Unaweza ukaexport au yatumia Kama malighafi ya kuzalisha sabuni za miche unauza unapata pesa ya kuondoa umasikini wa familia.
Huku kila mmoja ukimpatia ujuzi wa maarifa ya uzalishaji.
 
Asome!!!? Shule itamsaidia nini?? Hiyo elementary education aliyoipata inamtosha, shule imeua vipaji vya wengi, shule imekula mitaji ya wengi, atafute cha kufanya kupitia hiyo ada anayoenda kutupa shuleni[emoji23]unaweza ukasema havina mashiko ila ukisoma between the lines utaona vinafikirisha.

Sent from my vivo 2015 using JamiiForums mobile app
Wewe jamaa hapana kwakweli 😂😂😂🙌
 
Back
Top Bottom