Mwigulu Nchemba ang'aka kuagiza mabasi 60, asema hana biashara hata ya bajaji

Leta ushahidi wa Biashara anazomiliki. Kwani Ile fomu yake ya maadili kwa watumishi wa Umma imejazwa nini?
Hivi unadhani una akili Sana na Wana jf ni wajinga Kwa kiasi unachofikiri? Hii nchi wanasiasa hawajawahi kusema ukweli popote na hiyo tume haina maana ya kuwepo kwani inachangia kuwaficha wanasiasa wabadhirifu wa Mali za umma walizoiba!
Kwa taarifa Yako hiyo tume haina tofauti na mlinzi wa mlangoni ambaye kazi yake ni kumzuia yeyote asiyehusika kuingia humo na ndio maana wanawaweka majaji wao waliokwisha kuzeeka kuhudumu hapo!
Waambie hao jamaa zako kina madelu et Al biashara zao zipo kitaa na huko ndiko tukoishi na wateja wao ni sisi majobless! Tunajua Kila kitu ila pa kuwasemea pamefungwa!
 

Kama Mwigulu anasema Wananchi ndio walipendekeza Tozo, anategemea ni nani atamuamini kwa lolote analosema?
 
Imefika muda apumzike pembeni atuachie nchi yetu tuiendeleze.
 
John the baptist ndo engineer wa hii kitu mabasi ya Easther
 
Haya ni matunda ya mfumo mbovu tulionao. Kwenye nchi zenye demokrasia ni vigumu sana kwa wanasiasa kuficha vyanzo vya vipato vyao au utajiri wao.
 
Ila huyu jamaa ana kiburi cha asili
 
Yani Kuna anguko linakuja hilo, kiburii kikipandaaaa mwisho inakuja kushushwa.

Kuna watu watapandaaa Wataona Sasa tupo ktk maximum level halafu anguko nalo litakuja ghala kama mwizi.

Sio mtu atakaye watoa bali mkono wa Mungu utasimama hapo, hata wakaloge na kuloga havitalogeka,

Kwa Sasa hawaoni cz Mungu kawapiga upofu wasijione kuwa wapo wrong.
Mungu aibarik Tanzania
 
Hapo mwishoni siajaelewa mheshimiwa amesemaje "...utala phiya awafumu...??? Ndio kamaanishaje hapo? 🤔
 

Mwigulu Nchemba ang'aka kuagiza mabasi 60, asema hana biashara hata ya bajaji, sasa atutajie mmiliki wa hayo mabasi ya kampuni ya Ester kama sio yeye.​

alternatively mmiliki wa kampuni hiyo ajitokeza hadhani ili Jf imuombe radha kwa kumkosea,​

 
Nyerere hakucheka na viongozi wenye tabia kama ya Mwigulu.

Sielewi waliopokezana vijiti baada ya Nyerere kustaafu wamekwama wapi
 
Jf inanguvu hadi imemtowa waziri alikojificha.Hongereni na heri sana kwa jf.Tunamsubiri mh waziri wa kilimo aje atowe ufafanuzi wa yanayoendelea ktk kuandikisha wakulima.
Hatukatai lakini ushahidi muhimu ku attach kwa mtu anayetuhumu

Credibility ya Jamii forums itakuwa juu sana kwa allegation kama hizi zikiwa na supporting documents zenye evidence

Lakini ukisoma.thread zote ni mikelele tu isiyo na documentary evidence hata moja

Kwa maoni yangu credibility ya jamiiforums haipandi kwa mikelele kama hii isiyo.na evidence
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…