My week end is super crazy

My week end is super crazy

naona upo blessed nenda nao tu taratibu

utayamiss hayo makelele 🥰🥰
 
Pole sana.

Ila mimi nimefikia stage natamani sana watoto, hususan wadogo kabisa wale ambao mtu anaweza kuwalea vizuri yeye mwenyewe.


Ila tatizo siku hizi hata ukiwalea vizuri utotoni wakifika kwenye u teenager wanakubadilikia 😂😂😂
Asante🙏🏼

Wadogo wanafurahisha sana.
Hasa ile kuona jinsi wanabadilika kidogo kidogo tokea wako wachanga ni burudani na faraja sana na ndio inafanya mtu utamani kuwapa malezi bora sbb hutamani kuona wakiharibikiwa.

Hapo kwenye u teenager panaogopesha😀 ila naamini teenager mwenye malezi bora anaweza kuvuka hiyo hatua salama kuliko asiye na malezi mazuri
 
Ila nahisi naanza kuzoea sarakasi zao😀😀
Nawamiss ule muda wako shule na mimi niko kwa mishe.

Pamoja na yote wakiondoka naamini ndo nitakonda😀😀
Why don't you find your own twins if you sometimes miss them? Have your own twins
 
Zamani ndio mtoto alikua wa jamii, Kwa Sasa ulezi umekua mgumu sana.

Wangu nawapenda sana, na wao wanalijua hilo, lakini pia wanazingatia kwamba wakikosea kipigo chake utafikiri wamevunja chungu chenye mboga ya familia.

Pole sana Kwa heka heka. Lakini huyo wako pia ukipata nafasi, mfanye achanganyike na wengine kidogo, itamsaidia sana.
Sasa hivi akiharibika wanakusaidia kumharibu zaidi.Hawajui wakimuokoa watasaidia asiharibu na wa kwao

Asante mkuu.
Nitajitahidi kijana achangamane zaidi japo huwa anapatana akiwa na wa umri wake
 
Ila maisha haya jamani, mie katv kamoja tu ni kamgogoro. Ila kuna watu wananunulia kila mtoto na tv yake😭😭😭
 
Ila maisha haya jamani, mie katv kamoja tu ni kamgogoro. Ila kuna watu wananunulia kila mtoto na tv yake😭😭😭
Unatakiwa kuwa na TV mpaka ya akiba stoo ikiharibika moja hata hununui nyingine unachukua tu stoo 🤣🤣🤣
 
Unatakiwa kuwa na TV mpaka ya akiba stoo ikiharibika moja hata hununui nyingine unachukua tu stoo 🤣🤣🤣
Mweh mweeeh mweeeh! Ngoja kwanza nijipige pige ninunue hata hako kamoja kwanza.
 
Hahaaaa.

Unawaambia tu "shukuruni nyie si watoto wa baba yangu, mngekuwa watoto wake hilo suala hata msingelifikiria".

Tatizo wakimtafuta babu kumuuliza (kama yupo bado) naye wanamkuta kalainiiiika uzeeni siyo yule wa kipindi kile😂😂😂

Babu Yao alishatuacha kitambo. Ila hua nafurahia sana kuwa nao...
Juzi kakiume kamekuja kananiambia nisome kitabu kimeandikwa how to use your money wisely! Kamekomaa Daddy you must read that book, you real need it. Nikashangaa...nikamuuliza why? Sasa Kuna siku niliinunua machungwa mengi safarini kumbe nimepigwa hayakua mazuri, wakaishia kuyatupa.

Kingine Ile kununua vitu Kwa bulk anaona kama tunanunua vitu tusivyovitumia. Anasema tununue kidogo kidogo kikiisha, tunanunua kingine. Ikabidi Mama yake aingilie kati kwamba hivyo ni vitu vya mwezi mzima, sie tunajua Kila kitu kinahitajika kiasi Gani kwa mwezi.

Siku hizi nikipata muda tunaenda kutembelea watoto yatima, Mara Moja Moja tunaenda kusabahi Bibi, waone maisha mengine yalivyo.

Hapa nilisafiri navyo mkoani vikasema havili chakula Cha hotelini, ikabidi kufungaisha mazagazaga kutoka nyumbani.

Screenshot_2024-09-27-16-25-29-66_99c04817c0de5652397fc8b56c3b3817.jpg
 
Sasa hivi akiharibika wanakusaidia kumharibu zaidi.Hawajui wakimuokoa watasaidia asiharibu na wa kwao

Asante mkuu.
Nitajitahidi kijana achangamane zaidi japo huwa anapatana akiwa na wa umri wake

Afadhali imekupa uzoefu mpya na kujifunza mambo mapya hasa namna bora ya kumlea kijana awe tayari kuishi mazingira tofauti tofauti.
 
naona upo blessed nenda nao tu taratibu

utayamiss hayo makelele 🥰🥰
Naenda nae polepole dear.

Kuna saa natamani nivitupe nje ila siku wakiondoka nitahuzunika
 
Ila maisha haya jamani, mie katv kamoja tu ni kamgogoro. Ila kuna watu wananunulia kila mtoto na tv yake😭😭😭
Wala usijali sana yawezekana nina ma tv mengi ila na wewe una kitu hata nikiuza hizo tv zote siwezi kukipata.

Pia maisha ni furaha.
Kuwa na ma tv mengi haimaanishi mtu ana furaha.
Kama una furaha ushayapatia maisha.
 
Teenager mbali sana kaka, kwanza vina tambua haki zao na ipeo mkubwa sana wa mambo.

Mfano vijamaa vyangu vinapenda sana vipikiwe chips, Sasa tukakubaliana kwamba, wakila chips mchana, usiku wale chakula kingine.

Siku hiyo taarifa inatolewa, vinasema but that is not fair, how can you make a decision for us? You should have called a meeting...wakati huo vitoto hata miaka 10 havijafikisha.
Watoto wa hichi kizazi wana ujasiri na hawaigopi kusema.
Sio kama sisi tumekuzwa na hofu na kuwekewa kutojiamini.

Hayo maneno angeambiwa baba wa enzi za utoto wangu sipati picha😀

Naamini hawa watoto wetu ndo watakaoleta mabadiliko ambayo sisi wazazi wao tunayatamani lakini tunaogopa kuyapambania.
 
Babu Yao alishatuacha kitambo. Ila hua nafurahia sana kuwa nao...
Jusi kakiume kamekuja kananianbia nisome kitabu kimeandikwa how to use your money wisely? Kamekomaa Daddy you must read that book, you real need it. Nikashangaa...nikamuuliza why? Sasa Kuna siku niliinunua machungwa mwrngi safarini kumbe nimepigwa hatakua mazuri, wakaishia kuyatupa.

Kingine Ile kununua vitu Kwa bulk anaona kama tunanunua vitu tusivyovitumia. Anasema tununue kidogo kidogo kikiisha, tunanunua kingine. Ikabidi Mama yake aingilie kati kwamba hivyo ni vitu vya mwezi mzima, sue tunajua Kila kitu kinahitajika kiasi Gani.

Siku hizi nikipata muda tunaoenda kutembelea watoto yatima, Mara Moja Moja tunaenda kusabahi Bibi, waone maisha mengine yalivyo.

Hapa nilisafiri navyo mkoani vikasema havili chakula Cha hotelini, ikabidi kufungaisha mazagazaga kutoka nyumbani.

View attachment 3108343
Ujue unaweza kumchukulia poa huyo dogo alivyoumia kuona matunda mengi yanatupwa hadi kukushauri usome hicho kitabu ila ameonesha kuwa na kitu kikubwa ambacho hata watu wazima wengi hawana.

Sio kawaida kwa mtoto wa umri huo kuonea huruma pesa.Kuna watu wazima wanatupa chakula,wanatumia vitu vibaya hasa vikiwa vingi ndani hata hawajali sbb vikiishwa vinaletwa vingine .
Hao madogo hao nimewapenda.
Hongea kwa baba na mama
 
Back
Top Bottom