Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Hii iliwahi kunikuta mie, wakati nipo Advance, wazazi walikua wananipigia kelele sana kisa kutoenda kanisani, na kuacha kabisa kufuata misingi ya dini,

Mwanzoni nilikua nawasikiliza ila kanisani siendi, ikafika hatua wazazi wakawaita watu wazima wanikalishe chini huenda nna tatizo, wale watu walio tumwa niliwapa vipande vyao hadi wakasandaa, wakaenda kutoa majibu kwa wazazi, nashangaa wazazi wakaanza kuninunia na kunisusa fulaan hivi, sikuwa najari hata.

Baadae wakanipeleka kwa katekista azungumze na mie, yulee katekistaa alianzaa kunisema na kuhubiri anayoyajua, nkawa namsikiliza tyuuh, mara akaanza oooh sijui motoni mara jehanamu. Nlichoka kusikiliza uongo wake, nkampa swali

"hayo mambo ya motoni na jehanamu sijui akhera na mbinguni wee uthibitisho unao? Uliwahi kwenda kushuhudia? Ni marehemu gani aliyekufa na kuzikwa akarudi tena duniani kusema kuwa huko kuna mbingu na jehanamu? Sasa km yupo nikutanishe nizungumze nae, km hayupoo naomba uniache sina mda wa kusikiliza hizo ngonjera zako hapa, na ukawaambie wale waliokutuma kuwa kanisani siendi kamweee na sitaki nikiwepo wazungumzie masuala ya dini iwe mwanzo na mwisho"

Yule katekistaaa akapekeka ujumbe kwa wazazi, siku ya pili baba ananambia kuna kikao cha familia, nkasema sawa. Jion yake tukakaa sebulen, mara mama anaanza kulia "mwanangu umekumbwa na nn shetan gan kakushika hvyo, pepo chafu hilo likutoke" nkaona huyu ananiletea uchuro, nkawachana ukweli na nlisema msimamo wangu ni huu na haubadiliki.

"Kuanzia leo nitakapokaa au kuwepo mie naomba masuala ya dini yasiwepo na yakiwepo nisihusishwee, sikuzaliwa ili nije kuridhisha watu, nilizaliwa ili kufurahia na kuishi maisha ya hap duniani. Huko kanisani siendi na sitakwenda kwa matakwa ya mtu yeyote ila maamuzi yangu binafsi, sina pepo chafu, shetani wala ndugu zake, ila mie mwenyewe sitaki na sipendi kwenda kanisani. Siwezi kuishi kwa kuwaridhisha nyie, kingine ambacho hamkijui wazazi mie mwanenu niko real sana, huwa sina sababu ya kufake kitu, siwezi kuinyima haki nafsi yangu kisa nyie hapanaa siweziiii.ntafanya yale ambayo natakiwa kufanya kwenu km wazazi ila masuala yangu binafsi uzazi na utoto nauweka pembeni nasimama mie km mie. Nimemalizaaaaa.


Tangu siku ile had leo sisikii habari zao za dini wala nn, na tunaishi vizuri tyuuh, nakusihi hebu simamia msimamo wako acha kupelekeshwa, mzazi hawezi kukuingilia ktk masuala yako ya imani. Be you!!!

.............
 
Upo right kujiamulia kwenda au kutokwenda kanisani ila wazazi wako wapo zaidi kwenye kuhakikisha hupotei, Unavyosema kuhusu huwaamini manabii wa uwongo upo right ila ungeweza tu kwenda maana nafahamu panapokufanya usiwaamini ni kwenye shuhuda na sadaka lakini ukumbuke pia hao manabii kuna muda wanafundisha kweli kutenda matendo mema sidhani kama ukifika huko wao ni kuongelea pesa tu hapana, bali kuna vitu huviongea pia vya kukujenga ungeenda kuviokota pia ingekuwa pow.


Kingine ukiwa kwenye himaya ya wazazi fuata maelekezo wanayokupatia kwani hakuna mzazi anaemshauri mwanae njia mbaya, Waheshimu wazazi wako upate kuishi umri mrefu na wenye heri.

Kwenda kwako shule au kukaa kwako na watoto wa mjini usione kwamba wewe ndo mjanja kuliko wazazi wako, Kumbuka kuna maarifa ya Duniani na Ya kiroho, Tumia akili unapoishi na wazazi wako hatakama wanachokuambia ufanye hutaki kukifanya basi waaminishe kwamba umefanya hata kama hujafanya then ubaki wewe na Mungu wako.


Sikulaumu wala kukupinga kwa kuwa mimi pia huwa siendagi kanisani ila siishi kwa wazazi na huwa tukiwasiliana wakiniouliza kama naendaga nawajibu ndiyo, Mimi ni mkatoliki ukiniambia nijitetee kwanini siendagi kanisani basi nitatumia huohuo utetezi wako ila ukweli unabaki kwamba Kanisani natakiwa niende tu na nitaenda ni kwamba tu kwa akili zangu hizi za kijinga nataka nipate girlfriend wa kunihimiza tuwe tunaenda wote.
 
Acha upuuzi , jua tofauti ya wajibu na maamuzi ya mtu binafsi ,ndio nyie mnazaa watoto na kuwapeleka shule halafu mwisho wa siku mnaanza kuwaambia nimekulea ,nimekusomesha wtf ,Una akili wewe ? .kwa hiyo ulitaka alelewe na kusomeshwa na makalio ya nguruwe au ?
 
Kama utaki kwenda Kanisani njoo kila jumapili tushinde wote magetoni mpaka mida ya kutoka unarudi kwa mamayako unaonaje Mkuu? Njoo uwe unatulia zako magetoni, unajipikilisha, njoo uchukue kozi ya kuwa Mama na wewe hapo baada ya miezi kadhaa, kama ni movies fresh, kama ni chizi game kama mimi fresh, kama ni mtu wa kupenda mchakato, mchakato unachakatwa mwanzo mwisho ukirudi kwenu mwepesiii, mi mwenyewe sina dini naamini katika Nature. Nikusaidie. Tafuta kitabu kinaitwa children of Matrix. Kipo kwa mjuaji Google bure kabisa. Uongeze Maarifa.

Acha kumzingua bi mkubwa siku akikuzingua yeye sisi hatutakuwepo, za kuambiwa changanya na zako mdogo wangu.
 
Serikali haina Dini.
Ndio maana hiyo degree yako inatia Shaka Sana.
Unashindwa kufanya uhusisho wa hoja zako.

Secular state haiwezi kukupangia mambo ya Dini kwani yenyewe haina Dini.
Lakini Non-secular state kama Iran au Saudia Arabia au Qatar wao watakuambia na kukulazimisha ufuate sheria za Dini yao
Okay tufanye hivi mimi sina degree, ni wewe tu ndio una degree na una akili nyingi sana mkuu.
Maana kila hoja yako ni kama unaniattack kisa nimesema nina degree.
Haufikirii kabisa kwa kina statement zangu, bali unafikiria utafute mapungufu gani katika statement zangu ili ujidhijirishe kuwa wewe ndiye msomi.
Okay nakubali mimi sio msomi. ila tafadhali usifikirie pafupi ukisoma sentesi zangu.
Iran before ilikuwa secular state ila ikabadili gia angani na kuwa nchi ya dini.
Sasa fikiria serikali ya Tz ibadili gia kama Iran ianze kulazimisha watu kuingia msikitini na wote muwe waislam itakuwa haki?

Pamoja na hayo, hakuna nchi nayoijua inayolazimisha watu kuswali au kuamini katika dini yao.
Kama unaijua itaje.
Iran, Saudi arabia kuna wakristo na hawalazimishwi kusilimu au kuswali swala tano.
ila Sheria za dini kama usifuge nguruwe zipo na zinafuatwa, na hata mimi hapa nyumbani sivunji sheria za dini, sizini wala kuiba wala kudanganya.
ila sidhani kama ukristo unalazimisha watu kwenda kanisani.
Kwanini wazazi wanilazimishe?

This time usikurupuke kunimisquote.
 
Unaishi chini ya paa la mzazi wako, kama hutaki si unahama tu mkuu. Ukiwa chini ya mzazi utafuata kanuni zake ukiona waweza jitegemea basi hama.
Mimi nlikuwa naenda kansani nikiwa kwa wazazi now nina miaka sijui mingapi sijakanyaga
Sawa mkuu. So hata wazazi wakiamua nikafanyiwe FGM ni sawa tu kwakuwa ninaishi kwao.
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Ribbon alliance
 
Kama ulicho andika unamaanisha nakwambia iko siku utayakumbuka maneno ya Mama yako nakutamani ungeanza mapema kwenda ibadani
Hiyo ni imani yako. Sikulazimishi uamini nachokiamini mimi...Lakini mbona wewe unataka kunilazimisha niamini unachoamini wewe kuhusu kwenda ibadani?
 
Skia bint umuhim w din n mzur maan siku y kufa kwako tutakuzik kma masai s haun din
 
Back
Top Bottom