Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Tunaishi chini ya paa la serikali inayotuongoza...Je ni haki serikali kutulazimisa wananchi wote kuwa waislam?

Tunaishi kwenye dunia ya Mungu, Je Mungu anatulazimisha kumhauamini na kwenda kanisani?

Serikali haina Dini.
Ndio maana hiyo degree yako inatia Shaka Sana.
Unashindwa kufanya uhusisho wa hoja zako.

Secular state haiwezi kukupangia mambo ya Dini kwani yenyewe haina Dini.
Lakini Non-secular state kama Iran au Saudia Arabia au Qatar wao watakuambia na kukulazimisha ufuate sheria za Dini yao
 
Tunaishi chini ya paa la serikali inayotuongoza...Je ni haki serikali kutulazimisa wananchi wote kuwa waislam?

Tunaishi kwenye dunia ya Mungu, Je Mungu anatulazimisha kumuamini na kwenda kanisani?
Unaishi chini ya paa la mzazi wako, kama hutaki si unahama tu mkuu. Ukiwa chini ya mzazi utafuata kanuni zake ukiona waweza jitegemea basi hama.
Mimi nlikuwa naenda kansani nikiwa kwa wazazi now nina miaka sijui mingapi sijakanyaga
 
Mkuu asante kwa ushauri. Nimesoma vitabu vingi sana vya dini ambavyo najua hata wengi wanaoniattack hapa hawajawahi hata kuvisikia.

Wewe unaamini nikivisoma hivyo vitabu lazima nitaamini Mungu, je una uhakika? Okay tuseme unao uhakika.
Je ni sahihi kumlazimisha mtu kusoma hivyo vitabu hata kama hapendi?
Acha kubishana na akili fupi , huwezi bishana na wapumbavu waliokuwa brainwashed ,ni ngumu .Utamaliza nguvu zako bure . Let them believe the garbage that they want to .
 
Kadigrii kako ndio kanakufanya ujione exceptional,special,much know.
Sasa mama yako unamuona yuko brainwashed.
Enyi watoto watiini wazazi wenu, mpate kuishi siku nyingi.
Fuata mafundisho mema ya wazazi wako na yatakusaidia kwa vizazi vyako.
Au labda wewe watoto wako utawafundisha nini?!
 
Serikali haina Dini.
Ndio maana hiyo degree yako inatia Shaka Sana.
Unashindwa kufanya uhusisho wa hoja zako.

Secular state haiwezi kukupangia mambo ya Dini kwani yenyewe haina Dini.
Lakini Non-secular state kama Iran au Saudia Arabia au Qatar wao watakuambia na kukulazimisha ufuate sheria za Dini yao
Kwani umekariri ndoa ni kanisa ni na msikitini tu ? , Au hujawai sikia ndoa za kiserikali ? .
Na kwani ni lazima wafunge ndoa ? ,By the way hakuna hata ndoa sikuhizi viini macho tu .Sikuhizi kuna ndoa au disco vumbi tu .na vituko tu .
Ni napenda watu wenye free mind ,watu wenye uwezo wa kukaa chini na kutafakari mambo na kuquestion paradigms ,sio majitu yanaishi kama misukule ,tabia ya kukariri mambo .
By the way mimi mwenyewe ni nonconformist ,I'm against so many pre established society norms which to me seems to be garbage ,non logical and tyrannical .I'm a pro free mind a hardcore nonconformist
Unategemea kufunga ndoa ya aina gani? usije ukaanza kumsumbua mama akakuombee kwa viongozi wa kanisa
 
Kadigrii kako ndio kanakufanya ujione exceptional,special,much know.
Sasa mama yako unamuona yuko brainwashed.
Enyi watoto watiini wazazi wenu, mpate kuishi siku nyingi.
Fuata mafundisho mema ya wazazi wako na yatakusaidia kwa vizazi vyako.
Au labda wewe watoto wako utawafundisha nini?!
Huyo brainwashed ndiye kamzaa na kumpa hiyo degree , sasa huyu malezi ya mwanaye yatakuwaje, kama hayatakuwa ma'mpotompoto.
 
Kwani umekariri ndoa ni kanisa ni na msikitini tu ? , Au hujawai sikia ndoa za kiserikali ? .
Na kwani ni lazima wafunge ndoa ? ,By the way hakuna hata ndoa sikuhizi viini macho tu .Sikuhizi kuna ndoa au disco vumbi tu .na vituko tu .
Ni napenda watu wenye free mind ,watu wenye uwezo wa kukaa chini na kutafakari mambo na kuquestion paradigms ,sio majitu yanaishi kama misukule ,tabia ya kukariri mambo .
By the way mimi mwenyewe ni nonconformist ,I'm against so many pre established society norms which to me seems to be garbage ,non logical and tyrannical .I'm a pro free mind a hardcore nonconformist
Mbona umeni- quote Mimi?
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Wazazi zaeni watoto mpunguze chango tumboni. Hizi ni fibroids kabisa. Hutaki kapange kwako eboooo
 
Hiyo ni 'imani' yako.
Yani ulivyosema hivyo ni kama vile wanaoenda kanisani hawatendi dhambi vile.

Let me tell you, mimi siendi kanisani lakini kwa maisha ninayoishi naweza kuwa wa kwanza kwenda mbinguni...(Kama ipo)
Wewe binti ni Msagaji na hiyo dhambi inakusumbua na imekuathiri Samahani kusema hivyo ila wewe ni Msagaji
 
Mkuu asante kwa ushauri. Nimesoma vitabu vingi sana vya dini ambavyo najua hata wengi wanaoniattack hapa hawajawahi hata kuvisikia.

Wewe unaamini nikivisoma hivyo vitabu lazima nitaamini Mungu, je una uhakika? Okay tuseme unao uhakika.
Je ni sahihi kumlazimisha mtu kusoma hivyo vitabu hata kama hapendi?
Hongera sana mdogo wangu kama umesoma vitabu vya dini tofauti japo, nilikushauri tu
Labda nikuulize;
1. una amini kuwa Mungu yupo?
2. una amini kuwa ipo siku ya mwisho/siku ya hukumu?

Kama una amini, ni hatua nzuri na kama huamini, ni kwa nini?
Mimi nilikaa miaka saba bila kusali huku nikimtafuta Mungu kwenye vitabu (Biblia, Quran nk) na pia nikihudhuria Makongamano mbali mbali ya dini zote hivyo I can feel your concern.
Mwishowe nilijiridhisha niikae upande gani (kwa matakwa yangu mwenyewe)

Kwangu ilikuwa rahisi kwa kuwa nilikuwa najitegemea
 
Umesoma vitabu gani? Vitaje nataka nisome.

Unaishi na mama pekee au huko nyumbani yupo na baba? Naomba nifaham ili nitoe ushauri.
Niko na mzee, ila mzee hana time na haya mambo,...mama ndio anashupalia.

Vitabu ni vingi sana, kwasababu nilipokuwa form 2 nilikuwa na passion sana na dini. Yani ile tunaenda prepo wenzangu wanasoma physics mimi nilikuwa nasoma dini kila siku, so asilimia 80+ ya prepo zangu from form 2 to form 5 nilikuwa nasoma dini tu.
Vichache ni kama
Old & New testament
Heaven is for real-Todd turpo
The case for christ-Lee strobel
The attributes of God-Arthur Pink
Systematic theology-Wayne Grudem
The desire of Ages, The great controversy-Elen G. white
Catechism of the catholic church-
Roman catholic Encyclopedia karibia zote nilizisoma maana zilikuwa library shuleni
Here I stand-Maisha ya Martin Luther
Faragha ya kiroho, ukuaji wa kiroho-somebody Meinard Mtitu
Za wachungaji wa kibongo ndio usiseme
Vya kina mwakasege, Deo Njeni, na wengine wengi ambao hata sasa sivikumbuki majina

Vile vya ushuhuda kama nililala nikaamka usiku Yesu akanichukua akanipeleka kuzimu na mbinguni, nilishasoma vingi mno.
 
Post za jamii forums za wale Wasioamini uwepo wa Mungu zinakupotosha.
Nyie ndio mapaster na masheikh ushuzi mnaopotosha watu kwenda kuwaibia sadaka tu na kuwafanya misukule yenu kuendelea kuneemesha matumbo yenu huko kwenye makanisa na misukule , unafiki tu .Dini ni unafiki na takataka .
We angalia mtu mweusi alivyodumazwa na dini uchwara , na akili imekuwa kama makamasi ,dini ni minyororo ya kiakili ,na ni bora minyororo ya mkoloni iliyokuwa inafunga miguu na mikono kuliko hii minyororo ya kuabudu mapicha ya machoko kama Cesar Borgia ,masanamu ,mavitabu ya uongo , matakataka ,Total rubbish .
Dini ni certified superstition ,Hamna tofauti ya mtu anayependa kwa waganga wa kienyeji au mkishirikina na mtu anayeamini ma upuuz ya dini hayo, dini hizi ni michongo ya watu kuendelea kuwatawala watu wengine na kujinufaisha kiuchumi
 
Husianisha mada yako ni hiki ulichoeleza hapa kwenye maoni haya.
Ndio maana nikakuambia itakuwa maajabu Kama kweli Una Degree.

Nitajie Kanisa au dini yoyote inayotaka FGM,
Unajua unapotoa hoja unatakiwa utumie AKILI ili kuepuka kudharauliwa!

Unaeleza hiki unarukia hiki, unashindwa kufanya Reflection Kama msomi?

Kukaa nyumbani Kwa mtu lazima ufuate sheria zake,
Elewa sheria za watu na kwenye familia zinagaidiwa/zinaongozwa na sheria za nchi pamoja na Dini wanazoziamini.
Kwa hiyo hawawezi kukuagiza mambo yaliyonje ya sheria za Dini au za Nchi.

Kumbuka mpaka iitwe Dini ndani ya nchi yetu lazima iwe imesajiliwa kisheria.
Sasa nafikiri umeelewa ni Kwa nini hawatakuambia mambo ya uhalifu.

Ninachokiona kwako ni unajifunza kujenga hoja. Na upo hatua za awali kabisa.
Hivyo jitahidi utumie akili na Logic katika kujenga hoja zako
Hahaha let me laugh. Im sorry lakini nilishindwa kujizuia.

Tulikuwa tunaongelea sheria (in general) za kufuata ukiwa chini ya wazazi.Ukasema ni lazima ufate sheria zote za wazazi ukiwa chini yao hata wakikuambia ukasali kwa mashetani, na ndio nikatoa mfano hapo wa sheria, wazazi wakilazimisha mtoto ukafanyiwe FGM na wao wanaamini kabisa kiutamaduni wao inapaswa ufanyiwe.
je ni haki?? Hauna haki ya kukataa??ni haki kusema huamini katika FGM kama wao??
Again hapa swala ni imani.
Iwe imani ya kidini au kiutamaduni, usichengeshe magoli.
 
Kula chakula cha mama yako huoni kama unalazimishwa, au kuingilia uhuru wako...

Kupelekwa shule na kulipiwa ada hukuona kama unalazimishwa na kuingiliwa uhuru wako...

Kununuliwa nguo za kusitiri uchi wako hukuona kama unalazimishwa kuvaa nguo na kuingiliwa uhuru wako...

Kulala kwenye kitanda na godoro usilochangia chochote huoni kama unalazimishwa na kuingiliwa uhuru wako...

Lakini suala la kiroho pekee yake ndio limekuwa nongwa kwako...
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Huna imani ila imani ya kula chakula Cha bure unayo 😁 Lana sumaka
 
Back
Top Bottom