Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Naomba nikuulize kwa nia njema kabisa!! JE UNAAMINI KUWA MUNGU YUPO???
 
Siku ukiishi kwako ndio tutajadili kisomi.
Kwa sasa humu watu wote mpaka wajinga wanashangaa mtu mwenye Degree kuwa na upeo mdogo kiasi hiki.

Huo usomi unaojifanya nao utumie kujitegemea uondoke hapo nyumbani. Au ukishindwa utumie kuelewa kuwa hapo kwenu ni mamlaka kamili inayojiendesha Kwa taratibu na sheria za familia kulingana na utashi wa mama au Baba WA hiyo nyumba
Kwahyo mama/Baba akiamua sasa nikafanyiwe tohara ni sawa kwakuwa ni mamlaka na sina uhuru wa kuchagua???

Wala sishangai wengi unaowaita 'wasomi' na wasio wasomi wakinishangaa....sijaandika kwaajili yao. sijaandika hii kwaajili ya average minds Nimeandika kwaajili ya wale wachache watakaonielewa. (Above average)
Screen Shot 2016-05-23 at 9.50.12 AM.jpg

Zingatia hii graph
 
Kua na Age 18+ au 18- Sio kigezo cha kua na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo.. Kuna wengine wana30+ lakini bado ni wa hovyo tu... Kua uyaone!!

NB: Kua makini sana na Unayosikia, Unayotizama na Unayosoma..
Kwahyo kigezo cha kumpa mtu uhuru wa maamuzi kwakuwa amekua ni kipi? (Kama sio umri)
 
Mkuu asante kwa ushauri. Nimesoma vitabu vingi sana vya dini ambavyo najua hata wengi wanaoniattack hapa hawajawahi hata kuvisikia.

Wewe unaamini nikivisoma hivyo vitabu lazima nitaamini Mungu, je una uhakika? Okay tuseme unao uhakika.
Je ni sahihi kumlazimisha mtu kusoma hivyo vitabu hata kama hapendi?
Umesoma vitabu gani? Vitaje nataka nisome.

Unaishi na mama pekee au huko nyumbani yupo na baba? Naomba nifaham ili nitoe ushauri.
 
Kabisa na ukitaka kujua upumbavu na udumavu wa akili wa mtu mweusi ,we soma hizi comments humu .
Kuna quote nimesahau nani alisema "Religion can make even a proffesor act foolish"
Yani kabisa bado karne hii unakuta professor anaamini akifumba macho akasali kuna invisible force in heaven itamsikia na kumletea majibu. Na isipomjibu ni "mapenzi yake yatimizwe"
 
Ukitaka uhuru basi jitegemer uwe na kwako, mimi hapa nina miaka karibia 10 silijui kanisa na hakuna mtu ananiuliza.

Ukikaa kwa watu fuata masharti.

Sent using Jamii Forums mobile app
Masharti mengine yote sawa. ila hili naona linahusiana na imani. Sasa mtu umlazimishe kuamini kitu fulani ni haki?
Yesu alishikisha watu mapanga akawalazimisha kuamini dini yake?
 
Kwahyo mama/Baba akiamua sasa nikafanyiwe tohara ni sawa kwakuwa ni mamlaka na sina uhuru wa kuchagua???

Wala sishangai wengi unaowaita 'wasomi' na wasio wasomi wakinishangaa....sijaandika kwaajili yao. sijaandika hii kwaajili ya average minds Nimeandika kwaajili ya wale wachache watakaonielewa. (Above average)View attachment 2439026
Zingatia hii graph

Husianisha mada yako ni hiki ulichoeleza hapa kwenye maoni haya.
Ndio maana nikakuambia itakuwa maajabu Kama kweli Una Degree.

Nitajie Kanisa au dini yoyote inayotaka FGM,
Unajua unapotoa hoja unatakiwa utumie AKILI ili kuepuka kudharauliwa!

Unaeleza hiki unarukia hiki, unashindwa kufanya Reflection Kama msomi?

Kukaa nyumbani Kwa mtu lazima ufuate sheria zake,
Elewa sheria za watu na kwenye familia zinagaidiwa/zinaongozwa na sheria za nchi pamoja na Dini wanazoziamini.
Kwa hiyo hawawezi kukuagiza mambo yaliyonje ya sheria za Dini au za Nchi.

Kumbuka mpaka iitwe Dini ndani ya nchi yetu lazima iwe imesajiliwa kisheria.
Sasa nafikiri umeelewa ni Kwa nini hawatakuambia mambo ya uhalifu.

Ninachokiona kwako ni unajifunza kujenga hoja. Na upo hatua za awali kabisa.
Hivyo jitahidi utumie akili na Logic katika kujenga hoja zako
 
Swala sio shurti ila kwa kuwa upo kwenye mamlaka yake lazima utii ila ukiwa nje ya kwakwe uko free kufanya unavyojisikiw yeye anaweza kukushauri tu.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Unasema sio shurti halafu unasema tema Lazima nitii...hiyo si ndo maana ya shurti?

Wewe kwa imani yako unaamini katika kulazimishana dini?
 
Masharti mengine yote sawa. ila hili naona linahusiana na imani. Sasa mtu umlazimishe kuamini kitu fulani ni haki?
Yesu alishikisha watu mapanga akawalazimisha kuamini dini yake?

Yesu alikuwa na nyumba?
Au je Yesu alikuwa ana familia au watoto kama wewe hapo kwenu?
Tumia Logic unapotoa hoja zako.

Sheria inasema; Waheshimu Baba na Mama yako.
Hiyo ni SHERIA na amri.
Ukishakuwa upo nyumbani lazima amri hiyo uitekeleze iwe Kwa hiyari yako au Kwa nguvu.
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?

Kwa ushauri, take it slow. Wengi wa wazazi wetu wamekua wakiamini dini kwa asilimia mia. Kumtoa mia (kuamini dini bila kuhoji) mpaka sifuri (atheism) ni kumuonea. Ni ngumu mno. So we cheza naye tu 50/50 hapo afu mpe muda wa kuadjust. Itafika kipindi atakuewa tu.
Mimi nimeamua play low maana bibi yangu akijua siendi church kwa sababu nimeona hizo fiction zimenichosha, nahisi atafariki kwa kihoro ndani ya mwaka tu na nisingependa kumpoteza kizembe hivyo so I play around tu. Fortunately nipo kwangu, yupo kwake.
Cheers!
 
Unaishi chini ya paa lake, ama fuata mwongozo wake au kajitegemee hatokusumbua.
Yeye ukiishi chini yake anaona ni wajibu wake kukuongoza
Tunaishi chini ya paa la serikali inayotuongoza...Je ni haki serikali kutulazimisa wananchi wote kuwa waislam?

Tunaishi kwenye dunia ya Mungu, Je Mungu anatulazimisha kumuamini na kwenda kanisani?
 
Unasema sio shurti halafu unasema tema Lazima nitii...hiyo si ndo maana ya shurti?

Wewe kwa imani yako unaamini katika kulazimishana dini?

Tofautisha mamlaka au tawala na Imani.

Mzazi anachokifanya ni kutumia utawala na mamlaka yake kuhakikisha sheria alizoziweka hapo nyumbani ikiwa ni pamoja na members wote wa familia kwenda kanisani wanafuata amri hiyo.
Suala la kuwa unaamini au hauamini hiyo sio juu yake. Hiyo ni juu yako.
Yeye anachotaka ni kutii matakwa yake. Wala mambo ya Imani yako hayamhusu.
 
Kuna kuzaa na kutoa maradhi mwilini (alisikika mlevi mmoja akisema)
Yani mpaka umefikia hatua ya kusema kuwa mwanao akiacha dini sio mwanao bali ni maradhi.

Hii inadhihirisha jinsi dini yako ilivyokula nafasi kubwa kwenye ubongo wako.

Tena hiyo ilikuwa nafasi ya muhimu kabisa ambayo ungeitumia kufikiria mambo ya maana, ila wewe umeijaza dini.
 
Back
Top Bottom