Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

Kaka ubora wa elimu utaupima kwa namna ambavyo huyo mhitimu anaweza kuitumia elimu yake kutatua changamoto za jamii yake ikiwa ni pamoja na kutengeneza ajira,
 
Kwa hio unataka kusemaje? Wasomi wote wawe wachoma Chips?
Hapana,

Nina maana ya kusema kuwa, nia ya usomi ni kupanua uwezo wa mtu kufikiri, kuongeza vitu vipya vyenye ufanisi.

Inawezekana kabisa msomi akaanzisha biashara ya chipsi kisomi, ikaongeza kitu kwenye soko la chipsi, chipsi zikawa na ladha bora zaidi, zikatumia viungo bora, zikapikwa katika mazingira mazuri, akatumia nishati rafiki kwa mazingira kupika, akafanya marketing ya kisasa na kisomi, watu wakapenda sana, akafanya biashara nzuri kabisa.

Biashara nyingi zinaweza kuboreshwa kwa usomi, tatizo la watu wengi ni kufikiri kwamba usomi maana yake ni kufanya kazi ofisini, au za aina fulani tu, na msomi hatakiwi kuuza chipsi.
 
Watu kama ww JF wamebaki wachache

Watu wanapenda sana kunyuka suti,moka na mjusi shingoni lkn akaunti hazisomi milions.

Inshort kama ww ni kijana na akaunt haisomi milions of sh ww ni kijana mpumbavuu.
 
Wewe na wewe akili zako hazina akili, ulisoma Chuo uwe mchoma Chips si ungeacha kitambo uchome chips ukishindwa nini?
Sawa,akili zangu hazina akili. Ina maana kuchoma chipsi huko ndio wamependa? We mwenye akili zenye akili nieleze. Wamependa?? Wakati wanasoma wote si walijua watapata ajira? Haya, hizo ajira hawajapata. Wakae tu nyumbani?

Hawapo ambao hawajaendeleza elimu wakafanya mambo mengine na leo wapo vizuri? Unadhani wangejua hawatapata ajira wasingechukua maamuzi mengine!
Kama umejaliwa kujiajiri au kuajiriwa,usidhani wenzako ambao hawajapata bahati hiyo ni wajinga mkuu.
-Wapo wanaoajiliwa,mwisho wa siku wanarudi walikokuwa kabla ya ajira.
-Wapo ambao hawajaajiliwa,wanakaanga chipsi mwishowe ajira zikitokea wanapata.
Ila nimeuliza hujajibu. Maisha ni ajira tu? Wanaojiajiri hawaendelei?
Au ni kwamba kuna kazi mnaziona za aibu? Unajuaje kama hatoajiliwa labda kupitia mteja atakaekula chips kwake au atakaebebwa kwenye pikipiki yake?
Haya, kila mwaka vyuo vinaachia wangapi?
Una uhakika idadi hiyo yote nafasi zao zinakuwepo halafu wananyimwa?
 
Tupunguze kuzaa ovyo ovyo umetaka watoto wengi kuliko uwezo wako kulea. Kwa ulicho andika hapa ulitakiwa uwe na watoto maximum wawili. Ukiwa na watoto wachache na ukawa nao karibu, ni asilimia ndogo sana watafeli maisha hapo baadae.
Hapa uko sahihi asilimia zote. Lakini pia kumbuka,idadi ya ajira zilizopo na idadi ya wahitimu.
Siku hizi,kuna watu ukiangalia matokeo ya kazi zao,ni balaa tupu. Lakini kwa sababu ni fulani wa fulani,huna namna. Yule aliyestahili kuwa pale hajaweza. Afanyeje labda?
 
Kwanza kabisa unapata kuielewa thamani ya utu wako. Ambayo kwengine popote nje ya madrassa hufundishwi hilo.
Thamani gani hiyo iliyopo madrasa ila mifumo mingine ya elimu haifundishi?

Unamaanishi kuzama jua kwenye tope?
Au ninyi watu watu weusi ni kizazi kilicholaaniwa?

Au kulisujudia Al Kaaba?
Au uaminishwe ustaharabu ulianzia Uarabuni?

Ufundishwe kuidharau, kutweza na kuacha Mila zenu huku mkitukuza Mungu wa Kigeni aitwae Allah?

Au uwepo wa farasi mwenye mabawa?

Thamani ya mtu ipo kwenye Kujitambua na ili ajitambue anatakiwa apate elimu sahihi itakayo weza kumsaidia maisha yake na sio blah blah za zama za ujinga na enzi za ushairi
 
Mkuu kuna kitu hamjamuelewa mtoa mada. Kwa kifupi anamuongelea yule mhitimu alietoka chuo akiwa hana chcohote mfukoni. Hizi mambo za kuuza chipsi, bodaboda n.k zinahitaji pesa mtaji wa chipsi kwa makadirio ya chini kabisa inaweza kuwa almost milioni 1, pikipiki mpya inagonga sio chini ya milion 2.5. Mhitimu atatoa wapi iyo pesa? Nadharia nyingi za watu hapa wanamuelezea mtu ambae tayari ana ajira sasa anataka kupanua kuongeza vyanzo vya mapato hapo muhusika atajibana mshahara wake atafungua biashara halafu ataapply usomi wake lakini anaemuongelea mtoa mada ni mhitimu ambae hana chochote zaidi ya certificates tu. Uko juu nimeona Sean Paul anaponda wasomi kwa kuchagua kazi yeye ana biashara ya chipsi ambayo anapiga hela zaidi ya msomi alieajiriwa at the same time anasema alishaajiriwa kama mtu wa sales akaacha akaingia kwenye kujiajiri unaona huyu alipata ajira kwanza akajichanga ndio akajiajiri hayupo katika kundi analoliongelea mleta mada.
 
Mkuu,

Nakubaliana nawe kuanzisha biashara ya mamilioni wakati mtu labda hata nauli tu ya kwenda mjini tatizo ni njozi

Lakini, kwa huyo unayemuita msomi aliyegraduate karibuni halafu hana ajira ni bora kabisa hata akaajiriwa kwenye kibanda cha kuuza chipsi kuliko kukaa bila kazi. Ilimradi anapiga mahesabu ya kujiongeza.

Yani kama mtu ana talent, ile kuwa na sehemu ya kwenda kufanya shughuli kila asubuhi tu inaweza kumletea connection nyingine kubwa huko huko akaunganisha mambo juu kwa juu. Kuliko kungojea kazi za ofisini ambazo hazipo.

Yani kama mimi nawafanyia interview watu wawili, wote wame graduate mwaka mmoja uliopita, wote wana kila kitu sawa, nitawauliza huu mwaka mmoja tangu u graduate umefanya nini?

Mmoja akiniambia kwamba nilikuwa najishikiza katika kibanda cha chipsi cha mtu nikajifunza mambo mawili matatu kuhusu business na customer care, halafu mwingine akaniambia nilikuwa natafuta kazi inayoendana na usomi wangu sikupata, mimi nitamuona huyo aliyejishikiza kwenye kibanda cha chipsi ana initiative, naweza kumuajiri huyo kirahisi kuliko aliyekuwa anasubiri kazi ya kufunga tai.

Aliyekuwa mfanyabiashara maarufu Tanzania, Ali Mufuruki, aliwahi kuliongelea hili jambo, kwa kusema kuwa uki graduate maana yake si kwamba hutakiwi kufanya kazi fulani, alitolea mfano watu wanaoosha magari mjini wanatengeneza pesa nzuri tu. Sifikiri kwamba kazi ya kuosha magari inahitaji mtaji mkubwa sana. Ila watu hao ma graduate wanaona aibu, wakionwa na wenzao waliosoma nao itakuwaje? Si wataonekana wameshindwa maisha sasa? Hili ni tatizo kubwa, watu hawaishi maisha yao wanavyotaka, wanaishi kwa kuangalia macho ya watu wengine yatawaonaje.

Sasa, usomi wako unatakiwa kukufanya uweze kupiga mahesabu ya kusema kwamba, mimi sitaki kuosha magari au kukaanga chipsi, (yani hata nikikaanga chipsi au kuosha magari, iwe kisomi, kampuni kubwa). Lakini biashara ninayotaka kuifanya inahitaji mtaji wa shilingi milioni mbili na nusu, ambayo sina. Na ajira za ofisini hakuna. Ninachoweza kufanya hapa ni kukubali hii kazi ya kuosha magari, nikichange mpaka nipate huo mtaji wangu, halafu nikishapata mtaji nitajiongeza na kufanya biashara ninayoitaka.

Kimsingi, Ali Mufuruki alionya dhidi ya tabia ya hao wanaoitwa wasomi kudharau kazi za mikono na zile zinazoonekana hazihitaji kisomo, hata kama zinaweza kumpa mtu kipato cha kujikimu na hata kupata mtaji wa kuanzisha mambo mengine makubwa.

Na hii mentality ya "kazi ni kazi, vibaya wizi" watu wengi waliosoma Ulaya/Marekani/Asia wanaielewa, kwa sababu huko wenzetu wengi washafuta ujinga siku nyingi, mtu kupata degree si msomi, ni kitu cha kawaida tu, na unaweza kukuta mtu ana degree yake ya gardening anapiga kazi ya landscaping, huko kwetu tunashangaa mtu ana degree anashughulika na uchafu wa udongo tena? Ulaya/Marekani Watu wanafanya kazi na kujilipia chuo, kwa hiyo si ajabu mwanafunzi wa chuo kuwa anafanya kazi car wash.

Tena mtu anaona fahari kabisa kwenye kazi yake. Marehemu Le Mutuz alikuwa anaona fahari sana kuwa yeye aliweza kufanya kazi ya "Waste Management" ikampa kipato kizuri. Tena mtu anaweza hata kujivunia kazi kifalsafa kwamba kazi yake ina mchango mkubwa sana katika kuboresha mazingira, pengine kazi hiyo ikawa na umuhimu mkubwa zaidi ya banker anayefunga tai na kutoza watu riba inayosaidia natajiri kuzidi kutajirika, na masikini kuzidi juwa masikini.

Yani mtu anaweza kujenga hoja ya kisomi kabisa kwamba kazi ya kuzoa takataka na kuzifanyia recycling ina umuhimu jatika jamii kuliko kuwa afisa wa benki anayefunga tai na kukaa ofisini kwenye kiyoyozi.

"Wasomi" wetu wangapi wanachangamkia kazi za kuzoa taka? Zinadharaulika nankuonekana ni za watu duni kabisa. Wakati ukideal na electronic waste recycling tu kuna hela nyingi sana hapo.

Yani ukienda hata Nairobi tu utaona tofauti kubwa sana ya mentality kwenye mambo haya, huhitaji hata kwenda Ulaya au US.

Sisi kwetu bado tunalimbuka, mtu anayehitimu ki degree chake cha kwanza naye automatically anajiona msomi, wakati Jenerali Ulimwengu anatuambia kamaliza Form Ten tu. Sasa huyu naye analimbuka kuwa yeye ni msomi, hawezi jufanya kazi ya kuuza chipsi na kuosha magari.

Hata kama kazi hiyo anaweza kuifanya kwa mwaka tu na ikampa mtaji wa kufanya mambo yake mengine anayotaka.
 
Narudi kusema kuwa kulea ni kazi kubwa sana. Na mtoto anahitaji ukaribu mkubwa sana na wazazi. Ukiwa karibu naye kuna mambo unamfundisha asirudie makosa yako na kuna mawaidha atajifunza kutoka kwako. Ishu si kuajiriwa bali ni kujenga mtu anayejua kupambania Maisha yake. Mtu ambaye hata ukishaondoka duniani anaweza akasimamia majukumu yako.
 
Watu kama ww JF wamebaki wachache

Watu wanapenda sana kunyuka suti,moka na mjusi shingoni lkn akaunti hazisomi milions.

Inshort kama ww ni kijana na akaunt haisomi milions of sh ww ni kijana mpumbavuu.
Wanataka kuendesha Brevis, huku wanafanya kazi bank, tai na kiatu kinang'aa wakipita pita bank hall sisi tupo kwenye foleni tukisubiri huduma yao wanatuona mafala.
Eti assurance ya kipato......huu ni upuuzi.
Eti anawaza pension gratuity ya mil 100 miaka 30 ijayo.
Sasa hivi unaishije?
 
Hahh ujinga tu

Watu tunakula bata ukituona tulivyo huwezi jua kama tuna kula bata and goodlife.
 
" Elimu siyo njia ya kuukwepa umaskini, bali ni Silaha ya kupambana nao."
 
Umeongea point kubwa sana ila umesahau kuwa kuna waliosoma course zenye kipaumbele na bado wakakosa connection............sidhan kama kuna kumuandalia mtoto future zaid ya elimu
 


No one knows tomorrow, even Magufuli didnt know, tunachofanya wanaume ni:

1. Kuamini.
2. Kuomba Mungu.
3. Kuwekeza kwa watoto.

Matokeo ni ya Mungu.

Kamwe huwezi acha pambana na watoto sababu ya fikra za hovyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…