Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

Heshima kwetu sote mkuu.
Raia wanaona kuvaa tai ndio heshima na status. Halafu tukipita na magogo yetu toka porini tunakuja kuuza mbao mjini wanatuomba rushwa.
Anakagua vibali vyote vimetimia. Mzigo haujazidi hata nusu kilo, lakini anakuambia umpe hata ya maji........
Hiyo mil 20 ya kukopa unarudisha miaka 5. Sisi huku tunaitengeneza ndani ya miezi kadhaa.
Nakiri si kazi rahisi, businesses are full of chaos.
Nipo kazini kama mtumishi kwa miaka mingi ila ukweli ni kuwa wajasiriamali na wafanyabiashara waliotuliza akili wanapiga hela na ni hao wanaotuweka mjini sisi maana nikikwama wananibeba ila nisitie aibu ndugu yao .

Ila natamani kusema biashara sio ya kila mtu aisee tukianza kuandika yaliyotukuta basi hata hizi ndoto zangu za kuacha pombe zitapotea tu .

Ila hongera sana kaka , Mungu akuzidishe zaidi na zaidi , ipo siku na mimi nitajipata huko nitoke huku tumwani .


Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Accessibility
Muajiriwa anauelipwa hio 700K anaweza kumiliki vibanda km hivyo zaidi ya vitano ila wewe mzee mchoma chips sio rahisi kuwa Muajiriwa wa mshahara wa 700K

Reputation
Muajiriwa wa 700K muda wote msafi rahisi kuji Address kwa watu na kutambulisha always he/she is presentable na anaheshimika ila wewe mchoma chips huna yote haya.

Workdone
Muajiriwa wa 700K anaingia kazini morning na kutoka saa 8 na pia jumamosi na jumapili harndi job, ila wewe mchoma chips unafungua morning hadi saa 4 usiku na huna weekend....Pia Muajiriwa anafanya soft works most of time ana relax job ila mchoma chips uamke 11 uende sokoni kubeba gunia za viazi, mkaa nk ukate gunia la viazi, ukaange siku mzima jikoni "nataka rojorojo" "nataka kavu ikaushe" this is hell.

Risk And Security
Muajiriwa wa 700K hata uumwe mwezi mzima still you receive your pay, wewe ukiumwa siku moja tu kazi unayo, Muajiriwa ana mafao zaidi ya 60 Millioni baada ya kazi wewe huna chako nk

This life is full of uncertainty ukiwa na Ajira ya 700K kwa asilimia kadhaa financial uncertainty zitapungua kwako ila mchoma chips Mungu ajaalie kwakweli.

Financial Credit
Mfanyakazi wa 700K anaweza kopa zaifi ya 20 Million ajafanya most potential move, ila mchoma chips hata 100K mtu kukukopesha mtiti.

Ni vizuri pia kujifariji kwasababu hakuna namna na haya maisha.
We jamaa una akili. Aisee una akili kubwa sana mwamba. Mwamba umeweza kutuonyesha ulimwengu wa pili sio kila siku watu wanatulisha matango pori ya kuajiriwa ni utumwa.... Wabongo wanapenda kukariri sana...
 
I hate hope. Kuna kauli nazichukia sana. Sijui ni mipango ya Mungu. Sijui kwa mapenzi ya Mungu. Sijui jipe moyo tu mambo yataenda sawa, komaa tu utafanikiwa, hazina uhalisia kabisaaaaaaaaaaaa JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala that's why kuna mijitu haiamin hata uwepo wa Mungu mtu anakwambia tu sijui tumwachie Mungu utapata kazi tu ukicheck huna Connection, huna pesa ufukara kuanzia ngazi ya familia, connection ulizonazo hazina maana huthaminiw huna kitu mtu kitu....
Mimi mwenyewe naumia sana Mkuu yan mpka unahisi kuna watu sijui wanamuomba Mungu yupi sababu na ww unasali tena unafunga unaomnba miujiza hyo hyo lakn wanapata wengine wanaojiweza na walio vizuri kiuchumi😔😔
 
Iwapo wauza chipsi na bodaboda wote wataamua leo hii kuacha hizo kazi, trust me tutatamani warejee. Kila mmoja ana umuhimu wake
Sawa na akina mpwayungu wanawaponda walimu, kila cku wanashawishiwa waachane na ualimu. Hebu imagine walimu wote wakiacha ualimu cjui watoto wetu watafundishwa na nani.
 
Alafu mbona Kuna mkanganyiko hapa kwenye hii mada!. Hatuwezi kupima ubora wa elimu kwa kigezo cha ajira. Hapa tutakuwa tunajadili 'Hamna'. Msingi wa elimu unataka Nini?. Tatizo la ajira linasababishwa na nn?.


Hatuwez kupima ubora wa elimu iliyopo kwa kigezo cha ajira.
 
Alafu mbona Kuna mkanganyiko hapa kwenye hii mada!. Hatuwezi kupima ubora wa elimu kwa kigezo cha ajira. Hapa tutakuwa tunajadili 'Hamna'. Msingi wa elimu unataka Nini?. Tatizo la ajira linasababishwa na nn?.


Hatuwez kupima ubora wa elimu iliyopo kwa kigezo cha ajira.
Mzee wa kuchambia CV za wenzako[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Inahuzunisha sana kuona kazi wafanyazo watoto waliosomeshwa kwa gharama wakiwa bodaboda na wachoma chips.

Mzazi kugharamia masomo ya mwanao ili aje kuwa mpambaniaji wa kazi hizo na za namna hiyo au kutokuja kuwa na future yoyote mtaani inaleta huzuni kwa mtoto mwenyewe hata kwa mzazi pia.

Wanasiasa hawafanyi ujinga huu kamwe wao na kizazi chao wanaandaliana future bora watoto wao. Hakuna mwanasiasa hata mmoja ataruhusu mwanae awe boda boda au mchoma chipsi wala kutanga tanga mtaani hovyo bila future yoyote ile.

Mzazi jukumu lako lisiishie kuzaa na kupeleka mtoto shule pekee bali muandalie na future bora mtoto wako.

[IMG alt="lukesam"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/275/275627.jpg?1500562796[/IMG]

lukesam

JF-Expert Member​

  • "Hatuwezi kuwa matajiri wote kama Bakhresa lakini ni vizuri sisi watu weusi tukajifunza kwao na jamii nyingine kama za wahindi.
Inawezekana wazee wetu walishakosea huko nyuma ila sasa ni muda wa kujisahihisha na kuwa bora kuliko wao.

Wazazi wa kiafrika wana tabia za kichoyo na kibinafsi, hata akiwa na duka lake hataki mtoto wake auze au ajue jinsi ya kuendesha biashara, anaogopa kuibiwa hata kijana wake hamuamini.

Watoto wetu wanahangaika sana kutafuta ajira kwasababu walienda shule kusomea taaluma za ndoto zao bila kujua baada ya kumaliza wataenda kufanyia kazi wapi. Tofauti na sisi, hawa wenye asili ya kihindi na matajiri wengine, watoto wao wanaenda shule kusomea taaluma ambazo wanajua wakitoka hapo wataenda kupata ajira kwenye miradi ya familia.

Tuweke nguvu katika kuanzisha miradi ya kifamilia, familia za kitanzania tuache ubinafsi. Ndio maana hata ukimshauri mtu aandike wosia au agawe mali zake akiwa hai anakushangaa, mzee kabisa anataka afe akiwa anamiliki mali zake zote.

Suluhisho la kusomea uhasibu au uchumi na kuishia kuwa muuza chipsi au bodaboda ni kuanzisha miradi ya kifamilia. Binafsi naona hii itapunguza sana tatizo la ajira na hali ya umaskini katika familia zetu.

Inaumiza sana kupoteza miaka mingi shuleni na kuishia kufanya kazi ambazo hata hazihitaji elimu".
Wabongo bwana..sijui mnaona hizo kazi ndogo hazina hela ama vpi...mnadhan kukaa ofisin kuvaa vizuri ndo kuwa na hadhi inayoendana na elimu yako?...na ndo maana wasomi wengi wanaogopa kufanya vikazi hv vidogovidogo wanaogopa kudhalilika

Kuna dogo mmoja nipo nae pale mtaani..ni form 4 tu...kahangaika sana kujitafuta lkn mambo yakawa hayamwendei poa...

Siku moja nipo likizo akaja home kunisalimia..baada ya mazungumzo ya hapa na pale akaniambia changamoto zake za ujasiriamali( alikuwa anauza maji stand pugu b4 haijaamishwa)..sasa katika kupiga stori tu nikamwambia kwa nn asipige biashara ya chips(ilikuwa kama utani tu hata sikuitilia maanani)

Bhana wee..yule dogo wiki iliyofata akanifata akaniambia amepata eneo...kafungua kibanda..utani utani tu...

Wiki iliyopita j2 nilirudi likizo home..nikamfata pale kijiweni kwake(saa 4 huyo usiku)..akaniambia bro..mm hapa nafunga sa 10 asubuhi...nauza mpk nashngaa...kwa siku akitoa kila kitu anakunja si chini ya 90k..yani hiyo ni siku hajauza sana...kuna siku anapiga mpk 140k huko(hasa weekend)

Sasa kwa mwez hyo ni sh ngap?ww unaekaa ofisin unalipwa laki 7 kila siku kugombania daladala na yeye anaetoka kwake anaenda kazini kwa miguu dk 0 kashafika nan anaishi vizur?

Hzi biashara ndogondogo zinalipa..inshu ni location..ukiipatia location..utashangaa mwenyewe mpk unajiuliza siku zote ulikuwa WAPI
 
Yes tunakubaliana hapa, je kutoamini kwamba kuna nguvu ya Mungu katika maisha ya binadamu ni sawa?
Unauliza kama kutoamini kuwa kuna nguvu ya Mungu ni sawa? Au ni kuamini kitu kilicho kweli?

Tushaona imani unaweza kuamini hata uongo, kitu cha muhimu ni ukweli. Kwa nini unajikita kwenye imani bado?

Hayo ni maswali mawili tofauti.

Swali la kwanza, kuamini, au kutoamini kwamba kuna nguvu ya Mungu (hizi ni pande mbili za shilingi moja ile ile) sio tu ni sawa, hii ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania. Pia, hii ni haki ya binadamu iliyopitishwa katika Universal Declaration of Human Rights. Azimio hili limepitishwa na Umoja wa Mataifa December 10 1948.

KIla mtu ana haki ya kibinadamu ya kuamini au kutoamini nguvu za Mungu wake anavyotaka. Na katika kuongelea imani, maadam tunaongelea imani tu, hakuna imani iliyoishinda nyingine, maadam haiingilii uhuru wa wengine.

Kwa hivyo, ukitaka kuamini nguvu za Mungu wako ambaye ni mti wa mbuyu, una haki hiyo, na hilo ni sawa. Ukitaka kuamini Mungu wako ni Yesu Kristo Masiha, una haki hiyo, na hilo ni sawa. Ukitaka kuamini Mungu wako Allah, ni haki yako, na hilo ni sawa, ukitaka kuamini miungu yako isiyo na idadi, una haki hiyo, na hilo ni sawa, ukitaka kutoamini Mungu yeyote, kama mimi, ukasema hizi habari za Mungu zote ni ujinga mtupu, hiyo nayo ni haki yako ya kibinadamu, ni sawa tu.

Na mimi, licha ya kutoamini Mungu yeyote, tukiwa katika habari za imani, natetea haki za watu wote kuamini wanavyotaka, au kutoamini, ilimradi kuwe na mipaka mizuri ya kutoingiliana.

Hilo ni swali la kwanza, kutoamini katika nguvu ya Mungu katika maisha ya binadamu ni sawa?

Kwa kuwa tumekubaliana awali kwamba ukweli ni muhimu kuliko imani, kwa sababu ukweli upo mmoja tu, na imani unaweza kuamini hata uongo, tunapata swali la pili tofauti. Swali la kuangalia ukweli.

Je, ukiamini katika nguvu za Mungu unaamini katika ukweli? Huyo Mungu yupo kweli?.

Jibu ni, kwa kuanzia Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote anayesemwa kuwa ni muumba wa vyote, Mungu huyu hayupo, anaweza kuoneshwa kimantiki kwamba huyu ni muhusika wa hadithi ya kutungwa na watu tu, na hivyo, kuamini katika nguvu zake ni sawa na kuangalia sinema ya James Bond 007 na kujirusha kutoka ghorofani ukiamini kwamba utaruka kwa nguvu za Ki James Bond kutika katika filamu ya Casino Royale.
 
Mkuu Kiranga
Samahani naomba unitag au link ya ule Uzi WA Buddhism.

Nataka nisome upya zile 8 folds of perfections
Mkuu na mimi nimeupoteza uzi kwa maana imekuwa siku nyingi.

Ila kama unataka vitabu vya Buddhism, vya bure, soft copies za pdf, mtandao huu una vitabu vingi sana.

 
Nipo kazini kama mtumishi kwa miaka mingi ila ukweli ni kuwa wajasiriamali na wafanyabiashara waliotuliza akili wanapiga hela na ni hao wanaotuweka mjini sisi maana nikikwama wananibeba ila nisitie aibu ndugu yao .

Ila natamani kusema biashara sio ya kila mtu aisee tukianza kuandika yaliyotukuta basi hata hizi ndoto zangu za kuacha pombe zitapotea tu .

Ila hongera sana kaka , Mungu akuzidishe zaidi na zaidi , ipo siku na mimi nitajipata huko nitoke huku tumwani .


Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Asante mkuu. Jipange tu, na mimi si kwamba najisifu. Maana kazi nilikua nimeajiriwa mpaka mwaka huu huu. Sasa hivi najiona niko huru mno, napata muda hadi wa kuabudu na kureflect maisha kwa upana sana. Sina tena kuwaza kuamka saa 11 asbh niwahi kazini, jioni unatoka unawaza foleni za barabarani hadi unafika home uko hoi.
Nilikua nasimamia sales team, kuna siku unasubiri hadi last person atoke sokoni ndio uondoke, unatoka kazini saa 2 usiku. Kesho imagine saa 1 na nusu upo tena.
Muda wa kuabudu hamna, Jumapili unaamka umechoka unadoji ibada. Jumuiya huonekani. Unaishi kikafiri sana.
Napata muda wa kusocialize mno, misiba mtaani, sherehe, jumuia na kila kitu. Najiona kama niko likizo vile kumbe ndio yameshakuwa maisha yangu.
 
Wabongo bwana..sijui mnaona hizo kazi ndogo hazina hela ama vpi...mnadhan kukaa ofisin kuvaa vizuri ndo kuwa na hadhi inayoendana na elimu yako?...na ndo maana wasomi wengi wanaogopa kufanya vikazi hv vidogovidogo wanaogopa kudhalilika

Kuna dogo mmoja nipo nae pale mtaani..ni form 4 tu...kahangaika sana kujitafuta lkn mambo yakawa hayamwendei poa...

Siku moja nipo likizo akaja home kunisalimia..baada ya mazungumzo ya hapa na pale akaniambia changamoto zake za ujasiriamali( alikuwa anauza maji stand pugu b4 haijaamishwa)..sasa katika kupiga stori tu nikamwambia kwa nn asipige biashara ya chips(ilikuwa kama utani tu hata sikuitilia maanani)

Bhana wee..yule dogo wiki iliyofata akanifata akaniambia amepata eneo...kafungua kibanda..utani utani tu...

Wiki iliyopita j2 nilirudi likizo home..nikamfata pale kijiweni kwake(saa 4 huyo usiku)..akaniambia bro..mm hapa nafunga sa 10 asubuhi...nauza mpk nashngaa...kwa siku akitoa kila kitu anakunja si chini ya 90k..yani hiyo ni siku hajauza sana...kuna siku anapiga mpk 140k huko(hasa weekend)

Sasa kwa mwez hyo ni sh ngap?ww unaekaa ofisin unalipwa laki 7 kila siku kugombania daladala na yeye anaetoka kwake anaenda kazini kwa miguu dk 0 kashafika nan anaishi vizur?

Hzi biashara ndogondogo zinalipa..inshu ni location..ukiipatia location..utashangaa mwenyewe mpk unajiuliza siku zote ulikuwa WAPI
Bora nifanye kazi serikalini nalipwa hio 700K kuliko kuwa muuza chips Kama na kuingiza hio 100K kwasiku kam huyo dogo.

I have dozens of reasons including Workdone muuza chips mpaka anatengeneza 100K kwasiku hio Workdone yake aloyofanya sio kazi bali ni Hell kazi kubwa Sana tena iliyokula muda wake wa siku mzima akitoka Hapo ni kulala, Workdone-Kulala, Kulala-Workdone.

Hio nguvukazi kubwa anayoifanya kwa kupata hio 100K per day Mimi kazi yangu ya kuajiriwa na kutoka saa 8 naiwekeza kwenye Modern Hustling zangu kwenye Technology in few years nameki pesa ndefu nikiwa kwenye viti yeye akiendelea kupokea Oder tu "nataka rojorojo" "nikaushir kavu"

Maisha ya sasa mtu mwenye malengo anahitaji Constant Cashflow kama ajira ya 700K, then anahitaji muda wa kutosha Weekday kunzia Saa 8 hadi usiku, Weekend full day free ana Push ndoto na passion zake za kumtajirisha.
 
I hate hope. Kuna kauli nazichukia sana. Sijui ni mipango ya Mungu. Sijui kwa mapenzi ya Mungu. Sijui jipe moyo tu mambo yataenda sawa, komaa tu utafanikiwa, hazina uhalisia kabisaaaaaaaaaaaa JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala that's why kuna mijitu haiamin hata uwepo wa Mungu mtu anakwambia tu sijui tumwachie Mungu utapata kazi tu ukicheck huna Connection, huna pesa ufukara kuanzia ngazi ya familia, connection ulizonazo hazina maana huthaminiw huna kitu mtu kitu....
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mwanangu unajua kijiwe cha chipsi kina pesa chafu?

Watu tunalaza 80,000 mpaka 100,000 after all expenditures daily we unachukulia poa chipsi.?

Najua kuna chipsi vibanda haviingizi hiyo hela, sawa. Lakini nanyi huko kazini si wote mnaingiza hela nzuri. Wengine wana degree tangu mwaka 2015 waajiriwe kwa mshahara wa 750,000 mpaka leo hii hawajapata nyongeza. Sijui ndio Samia mwaka jana kaongeza kidogo.

Sema wabongo mmekariri kila aliyepita shule lazima aajiriwe hata kama analipwa kiduchu ili tu mzazi afurahi kuona mwanawe yuko kwenye payroll na akisimama kujitambulisha aseme nafanya kazi sehemu fulani ilihali ni kapuku.

Cha msingi maokoto, nunua kigari chako, jenga nyumba huko Kibamba.
Shida mkiona mtu ana gari mnawaza anafanya kazi wapi? Ushawahi kufikiria mtu amejiajiri?
Huhitaji degree na mkopo wa HESLB kuuza CHIPS au kuendesha bodaboda.
 
Back
Top Bottom