Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

Kipato 150,000 kwa mwezi

Idadi ya watoto ni 5

Kuna tofauti kubwa sana kwa huduma atakazopata mtoto mmoja kwa 150,000 kuliko watoto 5 kwa pesa hiyo hiyo.

Nani hajui hili?

Tunajua sana,

Tunajua vyema kabisa maisha ni magumu, kila mtu ameshatamka hili, lakini atabebeshana mimba na kuzaliana kwa wingi.

Elimu inatakiwa iwafikie watu kwa wingi, uzazi usio wa mpango ni janga na kichocheo kikubwa cha umaskini.
Hivi wewe sindo uncle fujo au nimekosea??
 
Mimi sina tatizo na mtoto kuwa boda boda au muuza chipsi. Kuna baadhi ya wauza chipsi wanatengeneza pesa nzuri kuliko wavaa tai wengi kwenye viyoyozi. Huenda hiyo elimu aliyosoma (hata kama ni unrelated) ndio imempa huo mwanga na hayo maono ya kuifanya hiyo biashara yake ya chipsi kwa namna anavyoifanya na kupelekea kupata faida anayoipata.


 
Naomba utume screenshot inafananaje
Screenshot_20231128-132156_1701166996999.jpg
 
Hawa watu wa benki ndiko wanakotajirikia.

Unakuna mtu ana akaunti yake ya siri ambayo familia haijui.

Anapata majanga huko hakuna anayejua kama kuna mahali kaweka fedha zake na kiasi gani .

Basi wahusika baada ya kuona muda mrefu umepita hakuna anayejitokeza wanapita nazo.

Ubinafsi kupitiliza ni mbaya.
 
Hivi baba ako akikusomesha kwa gharama kubwa mpaka chuo kikuu then ukaishia kuwa bodaboda. Hivi baba ako akikukuta pale kijiweni mnakopaki pikipiki hivi cjui mnaangalianaje? Unajisikiaje akikuangalia usoni? Ukiwa unasubiria abiria HV baba ako unaweza kumwangalia usoni kweli?....

I can't imagine kichwa kinaniuma.
 
Poleni sana!
thisi timu nisingependa kuchangia sana ila ifikapo Februari kuna kitu nataka nijaribu kikifanikiwa nitakuja hapa kwa majibu mengine ambayo kwa imani yangu yaweza kuwa msaada!
binafsi nimechoka kulalamika natamani tufike sehemu tuamue nini cha kufanya hata kama itachukua muda mrefu au tutapata hasra lakini ifike wakati wa kutenda kwa kadri ya uwezo wetu.
miaka ya nyuma nilialikwa na kituo kimoja cha compassion nikawatie nguvu ili waweze kukusanya mtaji na waweze kukopeshana. lakini sura zilivyokuwa zimekata tamaa kidogo nishindwe pa kuanzia yaani choka mbaya!
lakini ghafla wazo likaja niwaulize matumizi ya sukari kwa watoto wao ni kiasi gani kwa kila wiki? kiukweli nilipata majibu ambayo sikuyategemea yakaonekana ni makubwa na kati yao wapo wanatumia zaidi ya tano ndani ya wiki mbili! nikagundua kuwa naongea na matajiri na sio kama ninavyofikiria.
hivyo tukaanzisha duka la dharura(bubu) ili kila mwanachama akihitaji sukari aje anunue kwenye kituo na jinsi unavyonunua kwa wingi ndivyo utarajie faida kubwa mwisho wa mwaka.
walifanya na wakagawana faida iliyowatosha na wengine ili waweze kuchukua sukari nyingi walianzisha biashara zinazoweza kuwasaidia kuongeza matumizi ya sukari kwa kupika vitafunwa na kuuza. siwakumbuki tena lakini wengi wao walishabadilika sana.
sasa nini nataka kusema kama hatuwezi kubadili mtazamo na kufanya tofauti hakuna jinsi ambavyo tutaweza kufanikiwa.
lazima tujitume na kwakweli ifike wakati tunaweza kugoma kuchukua bidhaa kwa hao matajiri na tukainuana wenyewe na wao wabaki kama wauzaji wa jumla.
 
Heshima yako mkuu Sean Paul

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Heshima kwetu sote mkuu.
Raia wanaona kuvaa tai ndio heshima na status. Halafu tukipita na magogo yetu toka porini tunakuja kuuza mbao mjini wanatuomba rushwa.
Anakagua vibali vyote vimetimia. Mzigo haujazidi hata nusu kilo, lakini anakuambia umpe hata ya maji........
Hiyo mil 20 ya kukopa unarudisha miaka 5. Sisi huku tunaitengeneza ndani ya miezi kadhaa.
Nakiri si kazi rahisi, businesses are full of chaos.
 
Inahuzunisha sana kuona kazi wafanyazo watoto waliosomeshwa kwa gharama wakiwa bodaboda na wachoma chips.

Mzazi kugharamia masomo ya mwanao ili aje kuwa mpambaniaji wa kazi hizo na za namna hiyo au kutokuja kuwa na future yoyote mtaani inaleta huzuni kwa mtoto mwenyewe hata kwa mzazi pia.

Wanasiasa hawafanyi ujinga huu kamwe wao na kizazi chao wanaandaliana future bora watoto wao. Hakuna mwanasiasa hata mmoja ataruhusu mwanae awe boda boda au mchoma chipsi wala kutanga tanga mtaani hovyo bila future yoyote ile.

Mzazi jukumu lako lisiishie kuzaa na kupeleka mtoto shule pekee bali muandalie na future bora mtoto wako.

[IMG alt="lukesam"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/275/275627.jpg?1500562796[/IMG]

lukesam

JF-Expert Member​

  • "Hatuwezi kuwa matajiri wote kama Bakhresa lakini ni vizuri sisi watu weusi tukajifunza kwao na jamii nyingine kama za wahindi.
Inawezekana wazee wetu walishakosea huko nyuma ila sasa ni muda wa kujisahihisha na kuwa bora kuliko wao.

Wazazi wa kiafrika wana tabia za kichoyo na kibinafsi, hata akiwa na duka lake hataki mtoto wake auze au ajue jinsi ya kuendesha biashara, anaogopa kuibiwa hata kijana wake hamuamini.

Watoto wetu wanahangaika sana kutafuta ajira kwasababu walienda shule kusomea taaluma za ndoto zao bila kujua baada ya kumaliza wataenda kufanyia kazi wapi. Tofauti na sisi, hawa wenye asili ya kihindi na matajiri wengine, watoto wao wanaenda shule kusomea taaluma ambazo wanajua wakitoka hapo wataenda kupata ajira kwenye miradi ya familia.

Tuweke nguvu katika kuanzisha miradi ya kifamilia, familia za kitanzania tuache ubinafsi. Ndio maana hata ukimshauri mtu aandike wosia au agawe mali zake akiwa hai anakushangaa, mzee kabisa anataka afe akiwa anamiliki mali zake zote.

Suluhisho la kusomea uhasibu au uchumi na kuishia kuwa muuza chipsi au bodaboda ni kuanzisha miradi ya kifamilia. Binafsi naona hii itapunguza sana tatizo la ajira na hali ya umaskini katika familia zetu.

Inaumiza sana kupoteza miaka mingi shuleni na kuishia kufanya kazi ambazo hata hazihitaji elimu".
Iwapo wauza chipsi na bodaboda wote wataamua leo hii kuacha hizo kazi, trust me tutatamani warejee. Kila mmoja ana umuhimu wake
 
Back
Top Bottom