mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,897
- 18,477
NI mtu wa ajabu tu ambaye anaweza kudhani kuwa mahakama itakuwa na muda wa kusoma makablasha hayo ndani ya siku 14!! Wataambiwa waoneshe matokeo yao ni kura ngapi wamepata maana wana nakala za matokeo nya kila kituo!! Jibu lao litamaliza kesi!!
Hivi si mshindi anatakiwa kupata 50% + 1 kwa hiyo hata kama hiyo 2 decimal points . 99 ikiwa rounded 50 bado siyo halali kutangaza ushindi. Kama nimekosea kuelewa nieleweshwe.Nimeiona hiyo petition ni ya kisiasa hakuna content ya maana.
Kwa mahesabu ya Raila anasema Ruto kapata 49.997% ya valid votes.
Kwanini kachagua three decimals na sio two decimals . Its Obvious anajua mwenyewe kuwa inampa faida yeye.
Kwa matokeo hayo ya Raila ukiweka kwenye two decimals Ruto anapata 50%.
Anadai matokeo ya counties 27 hayakujumuishwa kwenye matokeo ya jumla. Je matokeo haya yanaweza kuathiri matokeo ya jumla??
Anadai kuwa kuna raia wa kigeni walikamatwa na vifaa vyenye access ya network ya IEBC na vifaa hivyo vimekamatwa pia.
Sasa kama culprits wametiwa nguvuni na vifaa vyao, hii inaathiri vipi matokeo ya jumla??
Je kuna ushahidi wa mifumo ya IEBC kuingiliwa.
Anadai kura za Rais , gavana,wabunge na wawakilishi wa wanawake zinatofautiana.
Nani kasema ni lazima zote ziwe sawa. Mpiga kura halazimishwi kuchagua wagombea wa nafasi zote , anaweza chagua mtu anayemtaka. Akaondoka zake.
Variance nyingi ni human error tu hakuna makosa makubwa kiasi cha kusema kwamba hapa hawa watu wamedhamiria kupora uchaguzi.
Wala hakuna error kubwa za kuweza kuinvalidate the whole election.
Binafsi sioni Raila akishinda hii kesi kama jopo la majaji wakituliza akili.
Hawezi kukuelewa huyo, akili yake imekaa ki-CCMMkuu unaona kama kujumlisha kura na kuongeza kura ni kosa dogo kweli sheria yao ina hitaji mshindi apate 50%+1 kura sasa huyu alipata 49.999 kwa hiyo hiyo 0.01 ni insignificant kweli? hata angepata 50% net bira additional ya kura 1, lazima chaguzi irudiwe, tunacho subiria hapa ni jinsi watakavo kisheria ila tayari iyo dosari inatosha sana ku-nulfy uchaguzi huo
Upo sahihi kabisa MkuuHivi si mshindi anatakiwa kupata 50% + 1 kwa hiyo hata kama hiyo 2 decimal points . 99 ikiwa rounded 50 bado siyo halali kutangaza ushindi. Kama nimekosea kuelewa nieleweshwe.
Una ufahamu wowote kuhusu election petition? Mahakama haiangalii ukubwa wa kosa bali inahitaji tu kuthibitisha "beyond reasonable doubt" kwamba palikuwa na udanganyifu full stop.Huo mfano ni tofauti na aina ya kesi inayozungumziwa hapa.
Ishu hapa ni kama hiyo tofauti ni kubwa kiasi gani kuweza kunullify matokeo..
Hakuna uchaguzi ambao hauna makosa madogo madogo.
Ukichukua huo mfano wako mshindi hata patikana milele.
Kila uchaguzi utakua unarudiwa.
Kwamba wewe mpemba wa Wete sijui Chake Chake unajua masuala ya ndani ya chaguzi za Kenya kuliko waliokuwepo kwenye kinyang'anyiro hicho?Kuna mambo kadhaa yanahitajika kueleweka hapa.
1. Kwa katiba ya Kenya ni haki kwa mgombea aliyeshindwa kwenda kuyapinga mahakamani matokeo. Hivyo katika hilo Raila yuko sahihi kwa 100%.
2. Sio kila dosari ya uchaguzi inatosha kuufuta uchaguzi. Ukubwa wa dosari ndio unaoweza kuamua kuufuta uchaguzi ikiwa athari zake zinatosha kuathiri matokeo ya jumla ya kumpata mshindi.
3. Mahakama ina option kadhaa katika kuamua kesi hii, kwa mfano:
-Kuamuru kura zipigwe upya
-Kuamuru kura zihesabiwe upya (ama kura zote au eneo fulani tu)
-Kutupilia mbali kesi hii.
4. Baadhi ya hoja za Raila alizoziweka wazi mpaka sasa hazina mashiko kabisa, ikiwemo;
-Madai ya kusema Ruto hakufikia 50%+1 ya kura zote halali. (Wakati kiuhalisia taasisi tofauti tofauti zilizojumlisha matokeo ya kura zilizopo mtandaoni zinaonyesha kufanana na matokeo ya IEBC yaliyompa ushindi wa 50%+1 Ruto)
-Madai ya Kaunti 27 hayakutangazwa matokeo ya Urais. (Ukweli ni kuwa hesabu ya jumla ya kumtangaza mshindi ilijumuisha kaunti zote ikiwemo hizo kaunti 27 zilizokuwa za mwisho kutakiwa kutolewa matokeo yake).
Binafsi naona kesi hii huenda Raila atashindwa na ikiwa mahakama itampa ushindi Raila basi ushindo huo utakuwa wa kwenda kuhesabu upya kura (hususani kwenye maeneo machache yenye utata) au kupitia upya majumuisho ya kura ili kupata mshindi halali (kitu ambacho nadhani kitaishia kumpa tena ushindi Ruto). Kuurudia upya uchaguzi wa Kenya ni jambo gumu, zito, gharama na tata sana, sio rahisi kihivyo kwa mahakama kulifikia.
Huoni kwamba ana hoja za msingi juu ya malalamiko yake? Uchaguzi wa 2007 mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya alikiri wazi kushinikizwa kumtangaza Mwai Kibaki kama mshindi wa Urais tofauti na uhalisia.Huyu mzee uchaguzi kila sikua analalamika tu, akubali kuwa uraisi sio zali kwake
Matokeo ya uchaguzi mkuu kenya 2022 yatafutwa Uhuru Kenyatta yuko kazini.
Fomu zipi hazikuwa verified? Mi nazungunzia fomu 34A ambazo ndiyo fomu kutoka vituoni na ndio msingi wa matokeo yote kwenye fomu nyingineForm za online hazikua verified, ndio maana kuna zilizofika kufanyiwa verification zikaenguliwa. Kwenye hiyo process kuna fomu kutoka majimbo 27 hazikuwa verified or at least matokeo yake hayakutangazwa pale Bomas sasa haraka ya nini kutangazwa Urais kabla ya kujiridhisha na hayo majimbo tajwa??
Ndio maana Mahakama zipo, zitatoa majibu ya maswali haya tuwe na subira tu
Kasome petition kule zimewekwa fomu 34A ambazo Zina conflict kwenye tallying. Nyingi ni za Mount Kenya ambako Odinga hakua na mawakala wengi.Fomu zipi hazikuwa verified? Mi nazungunzia fomu 34A ambazo ndiyo fomu kutoka vituoni na ndio msingi wa matokeo yote kwenye fomu nyingine
Fomu 34A kuna copy zake zote online ambazo mtu yoyote unaweza kujumlisha na kupata matokeo na hardcopy za 34A zote zilipelekwa Bomas na pia mawakala wa Odinga walipewa, kama kuna uchakachuaji wowote wangesema ni wapi
Petition nimeisoma mkuu, kwenye petition hakuna ushahidi wowote kuwa kuna utofauti wa matokeo ya fomu 34A zilizopo kwenye server na zilw hardcopy, hakuna.!Kasome petition kule zimewekwa fomu 34A ambazo Zina conflict kwenye tallying. Nyingi ni za Mount Kenya ambako Odinga hakua na mawakala wengi.
Kingine form34A za kwenye portal ni provisional ila zinazotambulika ni zile verified pale BOMAS, na mpaka matokeo yanatangazwa hawakuwa wameverify 34 A za majimbo 27!! Kinyume na sheria.
Mahakama itatupa mbivu na mbichi
Kirahisi hivyo? Odinga ni taasisi mkuu sio individual. Kama wakimfanyia figisu nchi haitotawalikaUtasikia madai yametupwa mbali, kijana ingia Ikulu kwa raha zako.
Sent using Jamii Forums mobile app
Petition umeisoma kweli?Petition nimeisoma mkuu, kwenye petition hakuna ushahidi wowote kuwa kuna utofauti wa matokeo ya fomu 34A zilizopo kwenye server na zilw hardcopy, hakuna.!
Hiyo ya mount Kenya ulikosema, wanachodai wao ni kuna kaunti ya Kirinyaga ambapo matokeo ya kura za urais yalikuwa na total votes nyingi zaidi ya 22,000 kuliko total votes za ugavana, kitu ambacho nacho ni uwongo kura zimewekwa wazi, za urais na ugavana zinatofautiana kwa 900 pekee
Kutokuwa na mawakala hilo ni kosa lake mwenyewe na sio proof kuwa aliibiwa kura
Na hao wanaosema hawaku verify matoeo ya majimbo 27 ni wale makamishna 4 ambao ni famba wasiojua hata hesabu, kila kitu kilikuwa verified