TANZIA Mzee Said Mohamed (baba yake GSM) afariki dunia
Nadhani ni tabia tu na uamuzi wa mhusika, SIYO suala la utaifa - eti mhindi au mwarabu au mpemba! Waafrika wengi na Watanzania wengi tu, wamerithisha watoto wao biashara na wanaendesha vizuri tu. Sikutajii majina au familia, nakuachieni wewe na wana JF wengine mlifanyie hili utafiti.
Naona mzee machache kaacha mali familia ipo kwa pilato
 
Mzee Said Mohamed ambaye ni Baba Mzazi wa Mfanyabiashara Ghalib Said Mohamed (GSM) amefariki dunia alfajiri ya leo Machi 1 2022 na anatarajiwa kuzikwa leo saa kumi jioni kwenye makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.

Marehemu Mzee Said ni Mfanyabiashara wa muda mrefu Tanzania ambapo alianzisha biashara ya kwanza mwaka 1955 kwa kuuza bidhaa ndogondogo Tanga lakini baadaye alihamia kuuza nguo na kuhama kutoka Tanga hadi Songea ambako alijitanua katika kilimo cha korosho ambacho Familia yake imekiendeleza hadi leo.

Marehemu Mzee Said alistaafu mwaka 1996 na kuruhusu kizazi kilichofuatia kuchukua usukani wa kila siku wa biashara na kuamua kuhamia Dar es Salaam na kuwa wasambazaji wakubwa wa mazulia ya PVC ndani ya Tanzania na nchi jirani.

Ghalib Said Mohamed (GSM) ni mdhamini wa Klabu ya Yanga ambapo amekuwa na msaada mkubwa miaka ya hivi karibuni tangu alipoanza uwekezaji klabuni hapo.

Kwa hiyo Yanga wana msibamsibal
 
Wengine tukifa tusipowakumbusha ndugu zetu tunaweza kusahaulika mochwari.

RIP.
 
RIP. Wanawezaje kutunza na kukuza utajiri vizazi hadi vizazi?
Mkuu sisi waswahili tuna matatizo sana vichwani mwetu.

Mtu mmoja kwenye ukoo au wawiki wakiwa na pesa nyingi au mali nyingi ikitokea mmoja wa wana ukoo akawa anashirikiana nae bega kwa bega basi itaanza fitina na wivu usio na maana yeyote ile zaidi ya kufarakana na hatimae kujengeana uhasama wa kifamilia.

Roho mbaya na chuki ndio imetawala mioyoni mwetu kwa wengi wenye mawazo na fikra za kimasikini.

Kiuhalisia wenzetu wanarithishana mali kuanzia mababu mpaka vitukuu na watu hauwezi kusikia wakiwa na mgogoro kati ya watoto wa baba mkubwa na mdogo au mjomba na shangazi.

Hii ni kitu mimi imeshanikuta kwenye familia zetu hizi na kupelekea watu kukuwekea,

chuki na wengine kuwaacha na hatimae watu kufilisika na kisha kuanza kuona kwamba wametengwa lakini chanzo cha yote ni ubinafsi na kujiona kwamba,

wao kama wao wanaweza kusimama peke yao ila ukweli siku zote ikitokea kwenye familia mmeanzisha jambo na muanzilishi ni mwenye taaluma hiyo na yeye ndio anarun na kuwafundisha wenzake basi shikamaneni haswaa na si kuvurugana kama ilivyo kwa familia nyingi sana za kiswahili zilivyo.

Na ndio maana utaona mfano akifa mzee aliyekuwa akiendesha kampuni au biashara kubwa tuu utaona inaathirika moja kwa moja sababu ni waliomzunguka walikuwa ni watu wenye kujali unafaika wake pekee bila kujali maslahi mapana ya familia/ukoo wote na unakuta mzee huyo hao aliokuwa akiwaamini ndio hao hao wenye roho mbaya ambayo hapo awali hawakuionesha.
 
Lala mahali pema mzaa chema.
Nina miaka zaidi ya arobaini ya kuishi Dar. Sijawahi kuona muislamu asiye na pesa au wathifa akizikwa hapo atakapo zikiwa mpendwa wetu.
Je. Kisutu Kuna nini?

Mama yangu mdogo amezikwa hapo ila kwetu sisi ni Kapuku na hatuna wadhifa wowote
 
Masikini wengi tu miaka na miaka wanazikwa Kisutu

Wale tuliozaliwa na kukulia katikati ya jiji bila ya kujalisha kipato chako utazikwa Kisutu au makaburi ya Tambaza
Lala mahali pema mzaa chema.
Nina miaka zaidi ya arobaini ya kuishi Dar. Sijawahi kuona muislamu asiye na pesa au wathifa akizikwa hapo atakapo zikiwa mpendwa wetu.
Je. Kisutu Kuna nini?
 
Apumzike kwa Amani.
Grazzimile 🙏🏽

Screenshot_2022-03-01-15-02-48-69.jpg
 
Back
Top Bottom