TANZIA Mzee Said Mohamed (baba yake GSM) afariki dunia
Hiyo ndio moja ya tafauti kubwa kati ya watu wa ngozi nyeupi na watu wa ngozi ya kiza. Yani mzee alistaafu miaka 25 nyuma akaachia wanawe waendeleze biashara. Mzee wa kiafrika mtoto hua anapata tabu sana hata baba akiwa na mkwanja. Yeye bado hujiona ndio anaakili nyingi hata kama zama zake zimeshapita.
Ni ajabu sana unakuta kampuni kubwa inakufa mikononi mwa hicho kizee kikongwe cha kiswahili wakati kina mitoto kibao tena mingine misomi mikubwa imeajiriwa tu na huko inategemewa sana kwa uwezo wao

Lakini kizee kinakomaa tu kuendesha kinawaona watoto wajinga chenyewe ndio zimo
 
Mzee Said Mohamed ambaye ni Baba Mzazi wa Mfanyabiashara Ghalib Said Mohamed (GSM) amefariki dunia alfajiri ya leo Machi 1 2022 na anatarajiwa kuzikwa leo saa kumi jioni kwenye makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.

Marehemu Mzee Said ni Mfanyabiashara wa muda mrefu Tanzania ambapo alianzisha biashara ya kwanza mwaka 1955 kwa kuuza bidhaa ndogondogo Tanga lakini baadaye alihamia kuuza nguo na kuhama kutoka Tanga hadi Songea ambako alijitanua katika kilimo cha korosho ambacho Familia yake imekiendeleza hadi leo.

Marehemu Mzee Said alistaafu mwaka 1996 na kuruhusu kizazi kilichofuatia kuchukua usukani wa kila siku wa biashara na kuamua kuhamia Dar es Salaam na kuwa wasambazaji wakubwa wa mazulia ya PVC ndani ya Tanzania na nchi jirani.

Ghalib Said Mohamed (GSM) ni mdhamini wa Klabu ya Yanga ambapo amekuwa na msaada mkubwa miaka ya hivi karibuni tangu alipoanza uwekezaji klabuni hapo.

Poleni sana,muwe na subira,nafikiri huyu ndio alikuwa mume wa yule mama wa Pangani,mwenye asili ya makabila ya Pangani.
 
Lala mahali pema mzaa chema.
Nina miaka zaidi ya arobaini ya kuishi Dar. Sijawahi kuona muislamu asiye na pesa au wadhfa akizikwa hapo atakapozikiwa mpendwa wetu.

Je! Kisutu Kuna nini?
Mjomba yangu,tumemzika hapo,usafiri wake ni baiskeli,Dar,hata hela ya daladala,ilikuwa shida.
 
Lala mahali pema mzaa chema.
Nina miaka zaidi ya arobaini ya kuishi Dar. Sijawahi kuona muislamu asiye na pesa au wadhfa akizikwa hapo atakapozikiwa mpendwa wetu.

Je! Kisutu Kuna nini?
Aunt yangu tumemzika hapo na wala ss sio mabwanyenye
 
Lala mahali pema mzaa chema.
Nina miaka zaidi ya arobaini ya kuishi Dar. Sijawahi kuona muislamu asiye na pesa au wadhfa akizikwa hapo atakapozikiwa mpendwa wetu.

Je! Kisutu Kuna nini?
Yale ni makaburi ya watu maarufu.
 
Siku ya leo hii....yaani nimeamka nasikiliza wimbo wa GK tutakukumbuka daima milele mara unaisha tuu simu inaingia ya kuondokewa na binamu yangu hapo Muhimbili.
Mkuu Poleni kwa msiba. Huo wimbo, Crazy GK mwenyewe alisema kwenye interview moja kuwa kwa sasa anauogopa sana huo wimbo, maana akiusikia redioni anajua kuna mwamba ametangulia.
 
Usikate tamaa lakini usiwaibie wenzako Wala usiiibie serikali na mwisho kabisa achana na utajiri wa kumwaga damu za ndugu zako wa karibu a.k.a utajiri wa kikinga na kingoni.

Umeongea ukweli mtupu
% kubwa wanaamini utajiri ni ndagu tu
Ila hawajui wengine tumeendeleza biashara walioanzisha wazee wetu miaka 75 iliyopita na mpaka leo tunaziendeleza na sisi watoto wetu wanazisimamia baadhi na sisi tukiwa nao sambamba kwa hali,ushauri,msaada na hata jasho pia
 
Masikini wengi tu miaka na miaka wanazikwa Kisutu

Wale tuliozaliwa na kukulia katikati ya jiji bila ya kujalisha kipato chako utazikwa Kisutu au makaburi ya Tambaza
Thank you for this vital information.
LABDA ni kwasababu sijaona wakazi wa huku usweken Kimara wakizikwa pale ndio maana nilidhani pale ni ushuani
 
Back
Top Bottom