Mzee Yusuph aamua kuachana na muziki na kumrudia Mungu wake

Mzee Yusuph aamua kuachana na muziki na kumrudia Mungu wake

Kishakusanya za kutosha kwa miaka mingi, sasa ndiyo anagundua kama ni dhambi. Arudishe basi na pesa zote alizopata alipokuwa akitenda dhambi ya kuimba nyimbo mbali mbali za taarab.
Hapo chacha, sijui na wake zake wataacha kuimba
 
Aliyekuwa Mfalme na gwiji wa muziki wa taarabu Afrika mashariki MZEE YUSUF ameamua kuachana na mziki na kumrudia Allah.

Mzee Yusuf ametangaza Nia yake hiyo leo ijumaa tarehe 12-08-2016 Muda mfupi baada ya kumaliza kuswali swala ya ijumaa ktk msikiti wa ilala bungoni (Masjid Taqwa)

Alizungumza huku akibubujikwa na machozi mengi Mzee Yusuf amemuomba Allah amsamehe madhambi yake yote pamoja na kuwaomba waumini wote wamuombee msamaha kwa Allah. Kadhalika amewaomba wanamuziki wengine ambao ni waislamu kuachana na muziki na kuzitumia fani zao walizonazo ktk kutangaza na kusifia Shamaail za bwana mtume muhammad (s.a.w).

Gwiji huyo wa zamani wa taarabu amewaomba watu wote waliokuwa na Cd zake majumbani mwao kuacha kupiga nyimbo zake na wakikaidi wafahamu madhambi yote yatakuwa juu yao kwani yeye hivi sasa anafanya toba kwa Allah.

Pia amevitaka vituo vyote vya televisheni na redio kuacha kupiga nyimbo zake kwani yeye Hana dhimma hiyo Tena. Ikumbukwe hali kama hii ilishawahi kutokea kwa aliyekuwa msanii wa bongo fleva SUMA LEE kuamua kuachana na mziki na sasa ni mpenzi mkubwa wa mtume muhammad (s.a.w)

Yaa rabbi awape tawfiiq wanamuziki wote wa kiislamu waachane na muziki pamoja kutupa mwisho mwema wao pamoja nasi in shaa Allah.

Hakuweza kuendelea kuongea zaidi ya maneno hayo na kuangua kilio kilichomsababishia maneno kutoweza kutoka mdomoni mwake.


NB: ukitaka kujua ibliis huwa hapendi kuona watu wakiwa kwenye njia sahihi subiri comments hapa chini za ibilisi waliobaki ambao jambo hili limewakera na litawakera sana
Hahahaaaaaa
Dah! Haya maisha bhana!
Eti Mtu akishapiga Maisha akafungua Miradi mbali mbali yakumuingizia Kipato ndipo anapomrudia Mola!

Hapa kitaani kwetu kuna jamaa alikuwa mfanyabiashara ya Madawa ya Kulevya miaka (9) mingi kinoma akajenga Majumba 4 yakupangisha plus Guest 3
Then hivi majuzi naye kasema Amemrudia Mola hivyo hafanyi tena Biashara haramu.

Allah anasema "TUBU INNALLAH TAUBAT NASUA"

Yani "fanya toba ya kweli na usirudiye makosa yako"

Hakusema piga kazi haram upate pesa za kutosha halafu ufunguwe Miradi mingi ikuingizie Pesa ndipo "UFANYE TOBA"
 
Mziki wa taarabu umeharibiwa sana siku hizi. Ulikua miongoni mwa aina za mziki zenye maadili ya hali ya juu.

Hawa wanaojiita waimba modern taarabu wakaharibu sifa ya taarabu. Taarabu sasa inatia aibu, huwezi kwenda kwenye show kama unaijua asili hasa ya taarabu ya enzi zile.

Kuna yule anajiita mashauzi, anakoipeleka taarabu ni hatari sana.

Kwa muimba taarabu halisi kama akina Patricia Hilal hawawezi kusimama na kulia kujutia kazi zao, walifanya mziki wenye maadili sana.

Haswaa umenena mkuu mashauzi ndie anayeendelea kuuharibu anaimba rhumba anasema ni taarab
halaf viguo anavyovaa kwenye taarab hadi hasira anavaa vinguo ambavyo ni.kinyume na maadili
 
Wiki 2 zilizopita nilienda magomeni alikuwa hayupo ila nyimbo zake kuna muimbaji mwengine aliimba sauti zao zimefanana.na alikuja late akaimba baadae akaondoka.kumbe mzee ameshajitoa.kwa hiyo jahazi itakuwa basi tena
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hujaambiwa muziki ni haramu ila kile ukitoacho kwa kupitia muziki ndicho haramu,Je una uhakika Mungu alitoa vipaji vya mziki,unasoma wapi au umepata wapi hili
Tunaposema Mungu ni muumba wa vyote ina maana vipaji vya mziki havihusiki?
 
Niulize mara ngapi?

Kasoma nyakati, kupiga shoo moja 2,000,000 sasa hivi atapata wapi wakati FM Academia wanapiga bonanza la bure Toroka uje?
Mkuu ilisemekana ile ajali ya five star miaka ile iliyoua wasanii wengi yeye ndio aliitengeneza kwa hofu ya kufunikwa na marehemu ISSA KIJOTI aliefariki kwenye ajali hiyo maana marehemu alikuwa anakuja juu sana kisanii. Na hili lilipelekea Mzee kukataa kushiriki wimbo uliotungwa na wasnii wa taarab wa kumuenzi marehemu Issa.
 
Hapa kwenye dini hii yetu ni shida tu, kila uapande una dhambi yao, wengine kuburuza nguo kwa mwanamke na mwanaume kuvaa kipensi nndio sawa, wengine kuvaa suruali ndefu na wanawake kuvaa nguo ndefu zisizo buruza chini ndio sawa, wengine kufunika nyuso ndio dini wengine kuacha uso wazi wanja(suna) uonekane ndio sawa. Tafrani tupu. Eti gitaa ni dhambi ila ngoma ni halali haaaa. tafrani.
 
Kama Imani yake ina Mungu wa kweli,Huyo Mungu huondoa magugu taratibu shambani asije haribu na ngano pamoja hivyo vyote vilivyochumwa katika anasa/haramu vitaisha na vya halali vitabaki,tusubiri tutashuhudia hapa,Mungu sio dikteta kwamba hakupi muda wa toba kamili na malipizi
Bwana weeeee, unapomkataa shetani yakatae na mambo yake. Huwezi kuendelea kulamba fedha za trade mark ya shetani huku unajifanya ni wa Mungu.

Labda tu Mzee Yusufu angetoa angalizo kwa wafuasi wake kwamba 'alikuwa akifanya dhambi kwa hiyo nao waache'
 
Bwana weeeee, unapomkataa shetani yakatae na mambo yake. Huwezi kuendelea kulamba fedha za trade mark ya shetani huku unajifanya ni wa Mungu.

Labda tu Mzee Yusufu angetoa angalizo kwa wafuasi wake kwamba 'alikuwa akifanya dhambi kwa hiyo nao waache'
Tunaacha taratiiiibu
 
Back
Top Bottom