Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Naona sasa mmeanza kuweweseka kama kawaida yenu. Hata kabla ya kuwa mkuu wa wilaya na baadaye mkuu wa mkoa kila mmoja hakufahamu majukumu ya nafasi hizo, pamoja na mamlaka yake katika kuchochea maendeleo.ni mpaka alipoteuliwa mwamba mwenyewe Mheshimiwa Makonda kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara.

Mheshimiwa Makonda ni kijana jasiri na anayetambua majukumu yake.afanyayo ni majukumu yake kabisa. Chama ndicho kilichounda serikali na siyo serikali iliyounda chama. Ni chama kinachokwenda kwa kuomba kura na siyo serikali.

Kwa akili yako hiyo hiyo unafirikiri chama kikianguka hao wakuu wa mikoa watabaki? Hao mawaziri watakuwepo ? Hao madc na watabakia? Sasa kwanini wasikiheshimu chama kilichowapa nafasi hizo kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM?
Umeelewa swali la mtoa mada au umekurupuka tu uonekane umekitetea chama!? Kila mtu anajua chama ndicho chenye serikali ila issue hapa ni nguvu hizo za katibu itikati na uenezi anazitoa wapi? Je hayo ndo majukumu yake? Wapi katibu mkuu, wapi makamu mwenyekiti?
 
Umeelewa swali la mtoa mada au umekurupuka tu uonekane umekitetea chama!? Kila mtu anajua chama ndicho chenye serikali ila issue hapa ni nguvu hizo za katibu itikati na uenezi anazitoa wapi? Je hayo ndo majukumu yake? Wapi katibu mkuu, wapi makamu mwenyekiti?
Nguvu za Mheshimiwa Makonda zinatoka kwa wananchi wanaoiunga mkono CCM na Serikali yake. Ndio hayo ni majukumu yake kabisa na hakuna alipokiuka .huyo ndiye msemaji mkuu wa chama kilichounda serikali iliyopo madarakani.

Kwa hiyo acha kukurupuka na kuropoka ropoka tu hapa ujinga wako.
 
Ufahamu huo baki nao wewe...!

Mimi sio Mwana siasa...!

Kilichofanya Maghufuri apendwe na Raia wa kawaida wa nchii hii, ni kwa sababu alikua anawasikiliza, alichofanya Maghufuri hata kingefanywa na PM, baada ya Maghufuri kufariki, angepata nafasi mioyoni mwa wananchi masikini.

Nkizulumiwa kiwanja nikaenda Mahakani nikashindwa kesi, baadaye nikaja kuambiwa ukiendelea mbele, tutaitoa roho yako, then kesho kuna kiongozi akaja akanisikiliza, Nikarudishiwa Kiwanja changu, hayo mambo ya Sheria na utawala Bora yatanisaidia nini....!?

Kama nilipewa Tenda na Minispaa na leo ni maka 10 nawadai hawataki kunilipa, hakuna office sijawahi kwenda mpaka mkoani, na hakuna msaada, then Mkurugenzi ananambia coz unapeleka malalamiko mpaka kwa mkuu wa mkoa, basi hutokaa ulipwe.... Then kesho anakuja Kiongozi kama Maghufuri ama Makonda, ananisikiliza, anatoa amri nilipwe, na kweli kesho yake nalipwa.....! Aaah...! Hayo mambo ya Sheria na Utawala bora baki nayo kwenye makaratasi....!

Wananchi masikini wanataka mtu wa kuwasikiliza na kutatua changamoto!

Ukitaka ku win mioyo ya Masikini, Wasikilize then tatua changamoto zao.... Simple!

Otherwise njoo na mambo yako uone kama sisi masikini tutakuelewa.

Mfumo mzima wa utawala nchii hii ulishaferi, na Viongozi hawana mawazo ya maana, ndo utakumbuka mawazo ya Mwanasheria mkuu mbele ya Rais, mawazo yasio na tija yoyote, Viongozi wa umma hawatimizi majukumu yao....!

Ni bora twende hivi tunaenda, ndo maana natamani Makonda angekua hata PM kwa faida ya Masikini.
🤣🤣🤣 shida ni ccm mkuu
 
Labda walikaa kikao wakaambiwa je nani atakeenda kuwakosoa wote wasiofanya kazi walizopewa na badala yake wamelala tu au hakuna la maana wanalofanya?
Wakaona asie na haya ni huyo
Au kaambiwa wewe unafaa kuwa na cheo kikubwa serikalini ambapo wengine kimewashinda hebu tuonyeshe kidogo sarakasi zako
Kama Samia alitaka mtu wa kusukuma utendaji wa kiserikali, angemteua katika cheo cha kiserikali kinachosimamia mawaziri, wakuu wa mikoa nk, kama Biteko. Hili la Makonda kujipa nguvu na kujiamini nakuhakikishia halikupangwa, huenda hata Samia anashangaa lakini hana la kusema
 
Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.
Hawa woote ni genge moja wamekuingiza Mkenge hii ni Movie yao na wao ndio Characters kila mtu anachez part yake.

Wasikuhadae na vsimu na vimaneno neno wanatoa mitandaoni.
Lao ni moja.

Failure yao ni moja hakuna wa kumkebehi mwenzake.
 
Makonda ziara zake kama amewakojolea Chadema🤣🤣

Mbumbumbu wa Chadema wanaweweseka
Kawakojolea Chadema? Umeona katika ziara hata moja Makonda kawapigia simu Chadema? Anawakojolea watu wake hao hao wa CCM, mawaziri, wakuu wa mikoa nk, anaowaamrisha kesho uwe hapa, bila kujua huyo mtu kesho anaweza kuwa na appointment na raisi. Ndio maana kuna mmoja alisema mimi huyu hawezi kabisa kuniamrisha, ambapo ni kama kusema huyu hawezi kabisa kunikojolea!

Makonda anachofanya katika ziara zake ni kuonyesha udhaifu wa serikali ya CCM katika kusimamia uongozi wa nchi na kutatua matatizo ya wananchi. Lakini ni watu wenye akili tu kama kina Ftama Karume wanaona hilo, sio watu kama wewe na wengine wanaoshabikia hizi ziara. Wao hawaoni tatizo bali wanaona Makonda anasuluhisha.

Yaani Makonda akipita Mwanza na kusikiliza watu wawili au wanne, anakuwa ametatua matatizo yote ya wananchi wa Mwanza ndio maana anaenda Shinyanga? Hivi watu mmesoma shule gani?
 
Ufahamu huo baki nao wewe...!

Mimi sio Mwana siasa...!

Kilichofanya Maghufuri apendwe na Raia wa kawaida wa nchii hii, ni kwa sababu alikua anawasikiliza, alichofanya Maghufuri hata kingefanywa na PM, baada ya Maghufuri kufariki, angepata nafasi mioyoni mwa wananchi masikini.

Nkizulumiwa kiwanja nikaenda Mahakani nikashindwa kesi, baadaye nikaja kuambiwa ukiendelea mbele, tutaitoa roho yako, then kesho kuna kiongozi akaja akanisikiliza, Nikarudishiwa Kiwanja changu, hayo mambo ya Sheria na utawala Bora yatanisaidia nini....!?

Kama nilipewa Tenda na Minispaa na leo ni maka 10 nawadai hawataki kunilipa, hakuna office sijawahi kwenda mpaka mkoani, na hakuna msaada, then Mkurugenzi ananambia coz unapeleka malalamiko mpaka kwa mkuu wa mkoa, basi hutokaa ulipwe.... Then kesho anakuja Kiongozi kama Maghufuri ama Makonda, ananisikiliza, anatoa amri nilipwe, na kweli kesho yake nalipwa.....! Aaah...! Hayo mambo ya Sheria na Utawala bora baki nayo kwenye makaratasi....!

Wananchi masikini wanataka mtu wa kuwasikiliza na kutatua changamoto!

Ukitaka ku win mioyo ya Masikini, Wasikilize then tatua changamoto zao.... Simple!

Otherwise njoo na mambo yako uone kama sisi masikini tutakuelewa.

Mfumo mzima wa utawala nchii hii ulishaferi, na Viongozi hawana mawazo ya maana, ndo utakumbuka mawazo ya Mwanasheria mkuu mbele ya Rais, mawazo yasio na tija yoyote, Viongozi wa umma hawatimizi majukumu yao....!

Ni bora twende hivi tunaenda, ndo maana natamani Makonda angekua hata PM kwa faida ya Masikini.

Kwamba mfumo wote huo ushindwe kufanya kazi, ila mtu mmoja anayepita siku 2 ndio amalize hayo matatizo uyasemayo?! Yaani ni sawa na kusema mtaani kwenu hakuna maji, na wanaopaswa kushughulikia upate hawawajibiki, kisha aje mmoja kati Yao akupe maji ya kunywa ww mwenyewe hapo mtaani, ndio uone huyo ni mtatua kero ya maji?

Kama kweli yeye ni mtatua kero, chama chake ndio Kiko madarakani aweke ni jinsi gani kero za wananchi wengine nchi nzima zitatuliwa, au Kila mwenye kero atamsubiri Hadi yeye amfikie?
 
Si Wapendi CCM, Simkubari Makonda kwa historia yake...!

Ila nakubaliana na anachokifanya, tena nilitamani angepata nafasi ya juu zaidi....!

Kama anaweza kuwafikia Wananchi na kuwasikiliza, hilo binafsi ni Muhimu sana, sisi hohehahe ndo tunataka, mtu atusikilize, pale tunapofukuzwa kwenye office za Umma, pale tunapoambiwa kama hujatoa kitu kidogo, kiwanja chako kinaenda kupotea, halafu anakuja mtu ananambia nieleze matatizo yako ntakusaidia, sisi tutampenda huyo....!

Kama nafasi yake haitambuliki kikatiba, hiyo sisi sio juu yetu, kama yeye sio kitu mbele ya Waziri ki cheo ama mbele ya Katibu Mkuu, hilo sisi hatujari, sisi tunajua kuna mtu ana nafasi huko CCM, anapita nchi nzima kujaribu kutatua changamoto zetu masikini...!

Hata kama kwa namna yoyote mkamwondoa, tutaendelea kuomba siku moja aje apatikane kiongozi kama yeye ambaye atatusikiliza...!

Kama anavunja Sheria hiyo sisi haituhusu, coz hata wanaofata sheria hawataki kutusikiliza...!

Makonda wewe ni Wapoti wangu, japo mimi sikukubari wewe kwa historia yako.... Ila piga kazi hivyo hivyo, mradi kuna Masikini wenzangu wanasaidika....!!!!
Hii comment Mods naomba waiprint alafu waifanyie lamination kabisa

Mhariri
 
Kawakojolea Chadema? Umeona katika ziara hata moja Makonda kawapigia simu Chadema? Anawakojolea watu wake hao hao wa CCM, mawaziri, wakuu wa mikoa nk, anaowaamrisha kesho uwe hapa, bila kujua huyo mtu kesho anaweza kuwa na appointment na raisi. Ndio maana kuna mmoja alisema mimi huyu hawezi kabisa kuniamrisha, ambapo ni kama kusema huyu hawezi kabisa kunikojolea!

Makonda anachofanya katika ziara zake ni kuonyesha udhaifu wa serikali ya CCM katika kusimamia uongozi wa nchi na kutatua matatizo ya wananchi. Lakini ni watu wenye akili tu kama kina Ftama Karume wanaona hilo, sio watu kama wewe na wengine wanaoshabikia hizi ziara. Wao hawaoni tatizo bali wanaona Makonda anasuluhisha.

Yaani Makonda akipita Mwanza na kusikiliza watu wawili au wanne, anakuwa ametatua matatizo yote ya wananchi wa Mwanza ndio maana anaenda Shinyanga? Hivi watu mmesoma shule gani?

Hii nchi imefika hapa kutokana na aina ya watu wauelewa finyu kama wa huyo unayemjibu. Yaani hayo maigizo anaita utatuzi wa kero, na kibaya zaidi hata hao wanaosemwa kutatuliwa kero zao wanaandaliwa kwanza!
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
Nguvu ya Makonda iko kwenye ujinga wake. Namaanisha kuwa ni wale watu wajinga ambao unaweza kumwambia ''nenda kamzabe mama yako yako makofi'', na akaenda kufanya kweli. Kwa kifupi nataka kusema kuwa mwenyekiti amemchagua yeye kwa sababu anajua ni mjinga na yuko tayari kujitoa ufahamu afanye lolote bila kujali madhara yake. Hivi mtu mwenye akili zako unaweza kufanya ujinga anaofanya wa kudhalilisha watu na wakati kuna kesho? Hajiulizi kama Samia kesho hayupo ni nini kitampata? Kuna watu walikuwa wanasema baada ya kufa Magufuli basi atakuwa amejifunza, lakini ukweli ni kwamba ndiyo amezidisha. Tuombe Mungu uzima uje uone mwisho wake utakavyokuwa mbaya.
 
Nguvu za Mheshimiwa Makonda zinatoka kwa wananchi wanaoiunga mkono CCM na Serikali yake. Ndio hayo ni majukumu yake kabisa na hakuna alipokiuka .huyo ndiye msemaji mkuu wa chama kilichounda serikali iliyopo madarakani.

Kwa hiyo acha kukurupuka na kuropoka ropoka tu hapa ujinga wako.
Unajua wewe ni mtu ninaemuona kibaraka mmoja wa kujipendekeza ambae anatafuta kila namna ya kujipendekeza kwa Samia na CCM yake angalau wakurushie ugali wa uteuzi wa namna fulani, lakini hata wao wamekudharau ndio maana hadi leo bado unahangaika na propagaganda zako na hakuna hata anaekujali.

Endelea, labda kuna siku kuna mjinga fulani atakukumbuka.

Sasa kama una akili kawaambie hao watu unaojikuwadi kwao kwamba wenye akili wanasema hivi, ziara na kujitutumua kwa Makonda hakusaidii bali kunabomoa CCM mbele ya watu wenye akili, na anasababisha migongano ndani ya chama na serikali. Kwa mfano, akimwamrisha waziri live mbele ya watu, aende mahali fulani, kumbe huyo mtu ana appointment na raisi, itakuwaje? Anamdhalilisha raisi mbele ya wateule wake, lakini hilo hamlioni nyie.

Kuna watu Makonda anawaumbua bila kuona kwamba anapofanya hivyo anamuumbua aliyewateua.

Makonda anachofanya katika ziara zake ni kuonyesha udhaifu wa serikali ya CCM katika kusimamia uongozi wa nchi na kutatua matatizo ya wananchi. NI watu semi-iliterate ambao wataona anatatua matatizo. Wewe kwa akili yako, Makonda akipita Mbeya na kusikiliza watu kumi siku hiyo, anakuwa ametatua matatizo ya wananchi wa Mbeya? Umesoma lakini wewe?

Mie ngoja nikuambie ukweli. Kinachowaangusha Chadema na kushindwa kuwaondoa CCM madarakani ni kwa sababu hadi leo Chadema hawajatambua wapiga kura wa Tanzania ni kama nilivyosema kwenye signature yangu hapa chini,

Usimdharau mjinga, mwelimishe. La sivyo atajikusanya na wajinga wenzake na watatumia nguvu yao ya wajinga wengi kukuchagulia mbunge au hata raisi mjinga kama wao .

na hii ni kutia ndani watu kama wewe Mwashambwa. Chadema wanapaswa kubadilika na kuongea na wajinga wa nchi hii katika lugha iliyo nyepesi mjinga kuelewa, kama wanavyofanya CCM, japo CCM hawafanyi kwa lengo la kuelimisha wajinga, bali kuwadumaza katika ujinga wao ili waendelee kuwa wajinga katika pindi za uchaguzi. Kuna watu tunajua hilo.
 
Si Wapendi CCM, Simkubari Makonda kwa historia yake...!

Ila nakubaliana na anachokifanya, tena nilitamani angepata nafasi ya juu zaidi....!

Kama anaweza kuwafikia Wananchi na kuwasikiliza, hilo binafsi ni Muhimu sana, sisi hohehahe ndo tunataka, mtu atusikilize, pale tunapofukuzwa kwenye office za Umma, pale tunapoambiwa kama hujatoa kitu kidogo, kiwanja chako kinaenda kupotea, halafu anakuja mtu ananambia nieleze matatizo yako ntakusaidia, sisi tutampenda huyo....!

Kama nafasi yake haitambuliki kikatiba, hiyo sisi sio juu yetu, kama yeye sio kitu mbele ya Waziri ki cheo ama mbele ya Katibu Mkuu, hilo sisi hatujari, sisi tunajua kuna mtu ana nafasi huko CCM, anapita nchi nzima kujaribu kutatua changamoto zetu masikini...!

Hata kama kwa namna yoyote mkamwondoa, tutaendelea kuomba siku moja aje apatikane kiongozi kama yeye ambaye atatusikiliza...!

Kama anavunja Sheria hiyo sisi haituhusu, coz hata wanaofata sheria hawataki kutusikiliza...!

Makonda wewe ni Wapoti wangu, japo mimi sikukubari wewe kwa historia yako.... Ila piga kazi hivyo hivyo, mradi kuna Masikini wenzangu wanasaidika....!!!!
Haya ni mawazo ya watu wasio na upeo kwenye mambo ya uongozi wa nchi, wanaodhani kuwa nchi inaongozwa kama kijiji. Hivi huoni kuwa tatizo la Tanzania ni rais na wateule wake wote akiwemo huyo Makonda? Makonda atawasikiliza wangapi? Kwa nini usililie mfumo ambao matatizo yatatuliwa kuanzia ngazi za chini na hayasubiri mtu mmoja anayezunguka? Kweli kukosa akili ni hatari sana.
 
Kama Samia alitaka mtu wa kusukuma utendaji wa kiserikali, angemteua katika cheo cha kiserikali kinachosimamia mawaziri, wakuu wa mikoa nk, kama Biteko. Hili la Makonda kujipa nguvu na kujiamini nakuhakikishia halikupangwa, huenda hata Samia anashangaa lakini hana la kusema
Ajabu sana kwa kweli, ila mkuu naona unajua au uelewa wako mpana kwa masuala haya
Pia linawezekana hilo
Tutaona mbio zake zitafika wapi maana ameanza kukimbia na jukwaa kama Luca alivyosema 😄
 
Back
Top Bottom