Nafasi za Ajira za muda za Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

Nani anakupa hizi taarifa?
 
sioo utani masta hiyo ni kweli kabisaa

Ndo muwe mnasema ni wapi?
Utaratibu gani umetumika au unatumika huko ili na wengine wajipange.

Hii ya kusema kimenuka, oyaa mambo tayari, majina tayari nk..
Ndo inafanya jobless wengi kukosa fursa kwa kubaniana info ili tu aonekane ana info nyingi na watu kumzonga awaambie na wakati mwingine info zenyewe zinakua za uongo na anakufa na mafamba yake.

Haya tiririkeni hapa ..
 
Ni kweli majina yametoka kwa baadhi ya kata.

Majina yanabandikwa kwenye kata husika na sio kwenye website ya nbs.

usahili ni 19-21 kwenye kata.
 
Mkuu wa Wilaya ya Magharibi B anawatangazia wale wote waliomba nafasi za kazi ya muda kwa ajili ya Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 kwa nafasi za karani , msimamizi maudhui na Tehama kuangalia majina yao yaliobandikwa katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Magharibi B zilizopo Mwanakwerekwe karibu na kituo cha kuuzia umeme .

Wale wote wataoyaona majina yao wanatakiwa kufika katika usajili { Interview } utaofanyika Siku ya Jumanne tarehe 19/07/2022 katika Skuli ya Sekondari Aboud Jumbe Fuoni kuanzia saa moja na nusu asubuhi.

Aidha muombaji anatakiwa kuja na vyeti halisi vya kumalizia masomo na Kitambulisho cha Mzanzibari mkaazi au Mtanzania.

Ahsante.

Imetolewa na :
Kitengo cha Habari na mawasiliano
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Magh B
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…