Naibu Waziri wa Afya amuondolea madaraka Mkuu wa Idara Paul Koroso, aliyemjibu “Sijali lolote hata nikifukuzwa kazi”

Naibu Waziri wa Afya amuondolea madaraka Mkuu wa Idara Paul Koroso, aliyemjibu “Sijali lolote hata nikifukuzwa kazi”

wenzetu huko waziri mkuu yuko anajambishwa na kupikwa kitimoto sisi huku tunakalia kulazimisha heshima ya kiungu.

huu upumbavu ndio unatukamatilia kwenye hili tope la umasikini
Anajambishwa na wabunge sio watumishi wa umma.
 
Wote kwenye Utumishi wa Umma tukianza kuwajibu viongozi wetu hivyo itakuwaje?
Lazima kuwe na order ndani ya serikali katika utekelezaji wa majukumu yao.
Huyo ni wa kumuondoa kabisa. Unamjibuje mwajiri wako hivyo? Katibu Mkuu ndio mwajiri wizarani lakini na yeye yupo chini ya Waziri na Naibu wake. Ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa maadili wa hali ya juu.
Serikali sio familia ya Kambale kwamba kila mtu ana ndevu.
Mbona unajichanganya? Unasema Katibu Mkuu ndio mwajiri halafu unamlaumu Injinia kwa kumjibu vibaya mwajiri wake? KM hawajibiki kwa Waziri au Naibu Waziri. Kwa kifupi mtu mzima usipotaka kutukanwa usiwatukane walio chini yako. Hapa hatujaambiwa Naibu Waziri huyu alimwambia nini huyo Injinia mpaka akamjibu vile.
Aliyekosa maadili na nidhamu ni huyo unayemtetea. Kiongozi kazi yako sio kumdhalilisha kiongozi aliye chini yako hadharani. Angekuwa na nia njema angefanya kikao cha ndani ambamo angesikiliza pande zote husika halafu angemtaarifu KM wake ili achukue hatua stahili.

Serikali sio jeshini kwamba kila mmoja anatakiwa atekeleze lolote ambalo ambalo analoamriwa na kiongozi wake bila kuhoji. Na waziri ni kiongozi sio mnyapara. Tabia kama hizi ndio zinawafanya wenye taaluma zao kukataa kufanya kazi serikalini. Na hao viongozi wenu kuona kuwa wana haki ya kuwachapa bakora watu wanaodhani wako chini yao.

Wa kufukuzwa hapa ni huyo Daktari wa meno, sio mhandisi. Wakiachiwa hawa wataturudisha kule ambapo Mwenyekiti wa CCM wa Kata anatoa amri Daktari Bingwa afukuzwe kazi!

Amandla....
 
Huyo jamaa kashindwa kuelewa kuwa yeye ameolewa lazima awe na utii kwa waume zake.
Ngoja akanyeee ndoo akitoka aanze kuzungusha CV kitaa na akizubaa akewe ataliwa kwa kukosa good time za awali.
 
Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel ameagiza kuondolewa madarakani kwa Mkuu wa Idara ya Ujenzi wa wizara hiyo, Paul Koroso kutokana na mgogoro ulioibuka katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe unaotekelezwa kwa gharama ya zaidi ya Sh2.9 bilioni.

Dk Mollel pia ameagiza Koroso aswekwe mahabusu akidai amemtolea majibu na lugha ya kijeuri kuwa “hajali lolote hata akifukuzwa kazi”.

Dk Mollel ametoa maagizo hayo Julai 5 akiwa mjini Nansio Ukerewe alipofika kutatua mgogoro uliobuka kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi hospitali ya Rufaa ya mkoa katika kisiwa hicho ndani ya Ziwa Victoria.

"Kutokana na changamoto zilizojitokeza kwenye mradi huu, Koroso utakoma kuwa mkuu wa Idara ya Ujenzi Wizara ya Afya. Katibu mkuu atamteua mkuu mpya wa idara ambaye atakuja kusimamia mradi wa Ukerewe," alitangaza Dk Mollel.

Pamoja na viongozi na wataalamu wa Wizara, mkoa na wilaya, kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi wa CCM, halmashauri na mkandarasi Suma JKT.

Miongozi mwa malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa Wilaya ya Ukerewe dhidi ya Koroso ni kutowashirikisha viongozi wa wilaya na halmashauri katika utekelezaji wa mradi huo.

"Ofisi ya DC, halmashauri na CCM Wilaya ya Ukerewe hawakushikishwa katika utekelezaji wa mradi huu," Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Kanali Denis Mwila alimweleza Dk Mollel.

Muda mfupi kabla ya amri ya kuswekwa mahabusu, Koroso alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa Serikali ingeokoa kati ya Sh180 milioni hadi Sh260 milioni iwapo ungetekeleza mradi huo kwa mtindo wa Force account (kutumia nguvu za wananchi) badala ya ukandarasi.

Kiwango kilichotajwa na Koroso kilitofautiana na kiwango cha Sh600 milioni kilichotajwa na mhandisi wa mkoa wa Mwanza, Chagu Nghoma.

Kutokana na tofauti hiyo, Dk Mollel akamtaka Koroso kutoa ufafanuzi, ndipo akasisitiza kuwa hesabu zake ndizo sahihi kwa mujibu wa kanuni na msingi wa kitaaluma na kwamba yuko tayari kuchukullwa hatua yoyote.

"Mheshimiwa Naibu Waziri, kiwango nilichotaja kimezingatia kanuni, vigezo na hesabu za kitaaluma; nitaendelea kusisitiza hilo hata kama ukinifukuza kazi sitajali," alisema Koroso.

Kutokana na kauli hiyo, Koroso aliyeketi jirani na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi Wilaya ya Ukerewe akajikuta anawekwa chini ya ulinzi na kupelekwa mahabusu.

Chanzo: Mwananchi
Ubabe ubabe tu
 
Kuna kitu cha kujifunza:
Mjadala unaohusu eneo la kitaalam,inatakiwa kuwa na majadiliano ya hatua kwa hatua,na wala sio kusikiliza upande mmoja.
Kazi anafanya SUMA JKT,viongozi ndani ya wilaya wanasema hawajashirikishwa katika mradi.Inaonekana kuna mjadala uliokuwepo uliopelekea Mhandisi kuonyesha msimamo na kauli aliyoitoa.
1.SUMA JKT,kama amechelewesha kazi maelekezo yanakuwaje?kupitia kwa Amanda Mkuu?
2.Kama kazi ingefanywa kwa "force account",kiasi cha fedha kingeokolewa,na viongozi ndani ya Wilaya wangekuwa na uwezo wa kufahamu kinachoendelea kwenye mradi,kwa hiyo makosa yalianza katika maamuzi ya namna ya kutekeleza mradi.
3.Yaliyotokea ni kama anatafutwa mtu wa kubebeshwa lawama,bila kutafuta majawabu ya hoja zilizojitokeza katika kikao.
 
Anajambishwa na wabunge sio watumishi wa umma.
umeyafuatilia maoni ya watu wa chini yake?
Wengine mpaka wameamua kujiuzuru ili kutounga mkono kiongozi wake.

Ingekuwa huku kwetu tungeishia kusifu tuu
 
Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel ameagiza kuondolewa madarakani kwa Mkuu wa Idara ya Ujenzi wa wizara hiyo, Paul Koroso kutokana na mgogoro ulioibuka katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe unaotekelezwa kwa gharama ya zaidi ya Sh2.9 bilioni.

Dk Mollel pia ameagiza Koroso aswekwe mahabusu akidai amemtolea majibu na lugha ya kijeuri kuwa “hajali lolote hata akifukuzwa kazi”.

Dk Mollel ametoa maagizo hayo Julai 5 akiwa mjini Nansio Ukerewe alipofika kutatua mgogoro uliobuka kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi hospitali ya Rufaa ya mkoa katika kisiwa hicho ndani ya Ziwa Victoria.

"Kutokana na changamoto zilizojitokeza kwenye mradi huu, Koroso utakoma kuwa mkuu wa Idara ya Ujenzi Wizara ya Afya. Katibu mkuu atamteua mkuu mpya wa idara ambaye atakuja kusimamia mradi wa Ukerewe," alitangaza Dk Mollel.

Pamoja na viongozi na wataalamu wa Wizara, mkoa na wilaya, kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi wa CCM, halmashauri na mkandarasi Suma JKT.

Miongozi mwa malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa Wilaya ya Ukerewe dhidi ya Koroso ni kutowashirikisha viongozi wa wilaya na halmashauri katika utekelezaji wa mradi huo.

"Ofisi ya DC, halmashauri na CCM Wilaya ya Ukerewe hawakushikishwa katika utekelezaji wa mradi huu," Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Kanali Denis Mwila alimweleza Dk Mollel.

Muda mfupi kabla ya amri ya kuswekwa mahabusu, Koroso alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa Serikali ingeokoa kati ya Sh180 milioni hadi Sh260 milioni iwapo ungetekeleza mradi huo kwa mtindo wa Force account (kutumia nguvu za wananchi) badala ya ukandarasi.

Kiwango kilichotajwa na Koroso kilitofautiana na kiwango cha Sh600 milioni kilichotajwa na mhandisi wa mkoa wa Mwanza, Chagu Nghoma.

Kutokana na tofauti hiyo, Dk Mollel akamtaka Koroso kutoa ufafanuzi, ndipo akasisitiza kuwa hesabu zake ndizo sahihi kwa mujibu wa kanuni na msingi wa kitaaluma na kwamba yuko tayari kuchukullwa hatua yoyote.

"Mheshimiwa Naibu Waziri, kiwango nilichotaja kimezingatia kanuni, vigezo na hesabu za kitaaluma; nitaendelea kusisitiza hilo hata kama ukinifukuza kazi sitajali," alisema Koroso.

Kutokana na kauli hiyo, Koroso aliyeketi jirani na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi Wilaya ya Ukerewe akajikuta anawekwa chini ya ulinzi na kupelekwa mahabusu.

Chanzo: Mwananchi
mkuu naomba kujuwa umuhimu wa halmashauri ya ccm kuhusishwa ktk utekelezaji wa mradi huo kisheria.
 
Sasq hayo majizi ya CCK nayo yalikua yanafanya nini hapo kwenye kikao?

Nchi ya ajabu sana.
 
Hata Nyerere alikuwa anapingwa, ni zaidi ya miaka 25 toka afariki sema aina ya viongozi wenu vilaza wanapopingwa hata ndio matokeo yake
Nani alikua anampinga nyerere??

Si bora hata sasa kuna vyama pinzani kipindi kile yeye alikua kama mungu mtu. Si unaona mpaka leo anavoimbwa kila kona utadhani ni yeye peke yake alieikomboa nchi.
 
Ni cement ya wapi? Imenunuliwa wapi? Hivi unategemea mkandarasi anunue simenti bila kuweka faida yake, gharama ya kusafirisha n.k.? Na kwenye BoQ hamna kitu kama bei ya mfuko kwenye rates. Kinacholipiwa ni zege au tofali lililotumika kwenye mradi.
Wahindi wa Shoppers Plaza wakiuza embe 10,000 ni wezi, duniani wanaita price gouging: occurs when a seller increases the prices of goods, services, or commodities to a level much higher than is considered reasonable or fair.

Lakini nina maswali:

1 / Kwa nini BOQ ina gharama za tofali na zege lakini haina simenti, hizo tofali zinajengewa na nini ?

2/ Wewe kama ndio mteja ( ofisa wa serikali au hata tajiri mdogo unaejenga ghorofa la kuishi) ukiletewa BOQ inasema zege litagharimu milioni 50, haisemi kokoto ni kiasi gani na ni shiiing ngapi, mchanga lori ngapi na ni shiiingi ngapi, kumwaga hilo zege labor shiiing ngapi lina ukubwa gani litachukua vibarua wangapi, mafundi wangapi, utakubali, utalipa tu ???????
 
Wahindi wa Shoppers Plaza wakiuza embe 10,000 ni wezi, duniani wanaita price gouging: occurs when a seller increases the prices of goods, services, or commodities to a level much higher than is considered reasonable or fair.

Lakini nina maswali:

1 / Kwa nini BOQ ina gharama za tofali na zege lakini haina simenti, hizo tofali zinajengewa na nini ?

2/ Wewe kama ndio mteja ( ofisa wa serikali au hata tajiri mdogo unaejenga ghorofa la kuishi) ukiletewa BOQ inasema zege litagharimu milioni 50, haisemi kokoto ni kiasi gani na ni shiiing ngapi, mchanga lori ngapi na ni shiiingi ngapi, kumwaga hilo zege labor shiiing ngapi lina ukubwa gani litachukua vibarua wangapi, mafundi wangapi, utakubali, utalipa tu ???????
Itachukua muda mrefu kukufahamisha kwa nini katika Boq kinachozumziwa ni zege na sio mchanga, simenti, chuping na maji.
Kuhusu Shoppers bei zao hazihusiani na price gouging kwa sababu kuna wengine wanaouza bei ya chini yao. Aidha, gharama zao ni tofauti na anayeuza Tandale ambae amepanga maembe yake kwenye sakafu!

Price gouging inatokea mwezi mtukufu wa Ramadhan unapokuta wauza mihogo wote wamepandisha bei ili ku take advantage ya ulazima wa watu kula futari.

Ushauri wangu kwako ni tafuta Quantity Surveyor atakufahamisha kuhusu rates, Boq na specifications.

Amandla...
 
Kwani Korosso angesema tu kwa taaluma yangu au hesabu nilizo nazi ninhivi na hivi bila kuongeza "hata ukinifukuza kazi" angepungukiwa na nini?

Wakati mwingine ni hekima tu ndio tunakosa.

Waziri amekosea ila pia Korosso amekosea. Kutakiwa kujieleza haimaanishi ndio umeshahukumiwa. Ange handle tu professional
Umeshawahi kuona kale kasura ka Mollel kwa karibu?
 
Approach aliyotumia waziri haipo sawa. Ila kuhusu watumishi kudhalilishwa nayo haipo sawa japo nao ni mabingwa wa kudhalilisha wananchi wenye shida
Pili ukweli usiopingika ni kuwa kwenye miradi hiyo Kuna wizi wa kutisha, waziri au kiongozi yoyote asipokua macho basi hakutakua na thamani ya pesa inayoonekana.

N.b
Wafanyakazi wengi iwe wa serikali au binafsi tuna uwizi Sana(Mimi nikiwemo)
Hongera mkuu kwa kuwa mkweli.👊🏾👊🏾
 
JAMAA YUKO PERFECT... HESHIMA KWAKE.
Ni kibri tu hana lolote! kwa nn hakutekeleza mradi kwa force account kama maelekezo yalivyo ili kusudi fedha iokolewe? na badala yake akatumia utaratibu tofauti?
kwa nn hakushirikisha walaji wa mradi ambao ni halmashau na Dc? huyo amejitakia, ktk utumishi wa umma ili uwe na maisha marefu Acha kibri na dharau kwa watu.
 
Back
Top Bottom