Naibu Waziri wa Afya amuondolea madaraka Mkuu wa Idara Paul Koroso, aliyemjibu “Sijali lolote hata nikifukuzwa kazi”

Sijui kama unaujua utaratibu wa upandishaji wa vyeo.
 
Hapo kosa liko wapi sasa!! Tuna viongozi wanaopenda kuabudiwa sana.
 
Hivi yule jamaa aliyempiga
kofi raisi wa ufaransa, mwisho wake ulikuwa upi?
 
Dk Mollel pia ameagiza Koroso aswekwe mahabusu akidai amemtolea majibu na lugha ya kijeuri kuwa “hajali lolote hata akifukuzwa kazi”.
Mollel kumbuka huo ubunge wako ni wa wizi wa kura pia uwaziri ulisadiwa tu na mwendazake kama kulipa fadhila baada ya kuwasaliti CDM..acha kutesa watu.
 
wenzetu waliostraabika waliyafanya mambo haya ya kuwekana ndani katika karne ya 16 na 17, tutawafikia tu tuwe na subra.
 
Itachukua muda mrefu kukufahamisha kwa nini katika Boq kinachozumziwa ni zege na sio mchanga, simenti, chuping na maji.


Ushauri wangu kwako ni tafuta Quantity Surveyor atakufahamisha kuhusu rates, Boq na specifications.

Amandla...
Nimtafute quantity surveyor anifahamishe?

Hatuendi hivyo hapa bana, you know this as well as anybody; ukitoa lecture ya BOQ then jibu maswali ya quantity surveying yanayofuatia.

Vinginevyo futa kakli zako ulizoongelea kuhusu mambo ambayo huyajui.

Unaambiwa zege lita cost milioni 50, kama ni hela yako utatoa bila kuhoji breakdown ya hiyo milioni 50? Huna jibu!

Ndio maana Magufuli alihangaika sana na makandarasi na mafundi kila mradi. Mnataka mfanye kazi ambayo haina oversight, haina accountability, kisa wataalam.. Mkiachwa bila usimamizi mnajenga bwawa la kuoshea mifugo kwa hela ya kujengea suspension bridge la kwenda Zanzibar. Engineers form the linchpin of the venal syndicate that is stiffling national development.
 
Wewe uliyejiunga juzi ndio leo unifundishe mimi jinsi hili jukwaa lilivyo?

Mtu unaedhani zege inapimwa kwa lita hauwezi kuelewa mambo ya Boq mpaka ukae na mwalimu ana kwa ana!

Usichokijua ni kuwa ukisha ingia mkataba na mkandarasi hauna namna ya kuhoji rate alizoziweka baada ya ku sign mkataba. Kama unaona hastahili, vunja mkataba halafu umlipe gharama za kuvunja mkataba.

Aidha, msimamizi wa mradi anaainishwa katika mkataba. Kama hajaainishwa, mkandarasi halazimiki kumpa taarifa yoyote kuhusu mradi. Ila kwa sababu mnawatisha na wengi hawajui haki zao ndio wanakubali muwaendeshe. Hivyo hivyo kwa msimamizi wa mradi. Huyo nae anawajibika kwa aliyemuajiri tu na si mwingine. Hao wanasiasa hawaajiri mtu.

Kumbe mliwanyang'anya usimamizi wa miradi ya ujenzi wahandisi na wataalamu wengine na mkawapa walimu wa shule za msingi, makatibu kata na kamati za shule za ujenzi kwa sababu mlitaka miradi iwe na oversight, accountability n.k. Ndio maana mkatumia mfumo ulioundwa kwa kazi ndogo za dharura ulioitwa "force account" kwenye ujenzi wa miradi yote!

Na mwisho, wenye lugha yao wanasema " are the linchpin sio form the linchpin". Ila kweli umethibitisha kuwa msomi kwa kutumia maneno magumu kama "venal" na "stifle".
Bahati mbaya sina muda wa kupoteza kujaribu kukuelimisha kijana ambae haujui usichojua.

Amandla...
 
Archetypical fundi wa kibongo, ukimhoji kidogo tu mmekwaruzana, umeshindwa kujibu hoja unaanza vioja vya kukosoa conjuction na viambishi vya Kiingereza. Utoto na ulimbukeni mtupu.

Wapi nimesema zege linapimwa kwa lita ?? Umebanwa kwa hoja umeanza vioja.

Tuliongelea content ya BOQ, ambayo ni adendum ya mkataba, kwa hiyo inajadiliwa wakati wa kufunga mkataba. Ili kujua detailed breakdown of project costs. Sijasema tubadili rate za gharama za zege baada ya mkataba kufungwa.

Kwanza unajuaje hizo rates anazozitetea Mhandisi zilikuwemo kwenye mkataba au kwenye BOQ?

NI KWA NINI KIASI CHA MATERIALS kinachotengeneza zege kisiwemo kwenye BOQ ???

BOQ inasema zege: milioni 500!
Hakuna kiasi cha zege wala vipimo vya content ya zege! Unataka serikali itoe tu hela. Wewe ungetoa ingekuwa nyumba yako ?????

Unajenga nyumba yako, unaambiwa kesho kutwa tunamwaga zege la jamvi, fundi anasema zege milioni 20 utatoa bila kuhoji kapataje mil 20 ????

Hayo ndio yaliyokushinda. Ulitaka kumtetea Mhandisi wa serikali kwa hoja nyepesi nyepesi ukakwama.
 
Unaweza kuishauri serikali Boq iwe ina quantify mchanga, simenti, kokoto badala ya zege. Au tutumie tu schedule of materials badala ya Boq.
Boq inasema quality ya zege (1:2:4 19 mm aggregates) inayotakiwa, kiasi cha zege na rate yake. Hamna Boq inayosema tu zege milioni 500 bila kuwa na rate na amount ya zege. Kisichokuweko ni mifuko mingapi ya simenti, mchanga tripu ngapi, kokote tripu ngapi, labour tripu ngapi, gharama za usafiri kiasi gani, faida ya mkandarasi kiasi gani zinajumuishwa katika hiyo rate ya zege. QS anaweza kujua kiasi cha simenti, mchanga, kokoto zinazoingia katika cubic metre moja ya zege. Ndio maana anapaswa kujua reasonable rate ya zege ili wakati wa evaluation ya bid imuongoze kufanya maamuzi. Lakini ijulikane kinachopimwa kwenye mradi ni kiasi kilichoingia kwenye mradi na sio kilichonunuliwa na mkandarasi. Mathlani Boq inaposema tiles sqm 20 haina maana kuwa mkandarasi alinunua sqm 20 za tiles. Mara nyingi ananunua zaidi akijua kuwa wakati wa kuziweka nyingine zitavunjika. Kwa sababu hiyo rate yake inajumlisha pia hesabu ya zile zinazovunjika. Hivyo hivyo kwenye zege. Mifuko mingine ya simenti inapasuka wakati wa usafirishaji, kokoto nyingine na mchanga zina baki kwenye udongo ( makandarasi wengi hawatunzi simenti na aggregates kwa namna inavyotakiwa). Kwa sababu hiyo cubic metre za zege zinazopimwa ni za ile ilitumika kwenye mradi na iliyokubaliwa.

Sasa mtu kusema tu tumemlipa mkandarasi milioni 500 kwa ajili ya zege hakutoi picha halisi bila ya kutaja kiasi cha zege na quality yake. Hiyo wanafanya mafundi wa ulaya peke yake.

Ni fundi wa ulaya huyo huyo ndio anatumia Boq kujenga nyumba yake. Mafundi wa kibongo wanaenda kwa schedule of materials na sio Boq.

Mimi kama fundi mchundo wa kibongo, uelewa wangu umeishia hapo. Na ninakiri kuwa fundi wa ulaya lazima anajua kuliko mimi. Kwa sababu hiyo, nakutakia jumapili njema na sitakujibu tena.

Amandla...
 
na sitakujibu tena.
Fine and dandy, I get the last word then.

Vema umekiri BOQ ni kichochoro cha kupitishia na chaka la kufichia wizi na uhujumu. Ndo maana umesema nikaishauri serikali BOQ iwe more detailed and specific kwenye suala kama la zege.

Hivi unapimaje au unahakikije kwamba zege limejengwa kwa kiwango cha 1:2:4 dash 14 mm aggregate ???? Tofali linapelekwa lab kupima compressive strength, zege linapimwaje ?

Tunataka kujua trip za kokoto na mchanga na cement na risiti za manunuzi.

Fundi akichepusha njia ya malori kwenda kwake anatengeneza smoking gun evidence za kumkamatisha.

Mkurugenzi wa Halmashauri Arusha kakutwa na malori kwenye saiti yake binafsi kwa sababu Mbunge wa Arusha alifatilia mpaka michanga na kokoto zinakuja site lori ngapi badala ya kusubiri kujengewa concrete specs za One Two Four dash 14mm aggregate.

Na mwisho, kama umeona kuna hoja ya kuishauri serikali iziangalie upya specs za BOQ basi hukupaswa kubeza na kunanga nilipokutaka utoe maelezo ya kina. Kunambia nikakae ana kwa ana na walimu na ma Surveyor wanieleweshe kwa sababu wewe huna muda ni dharau ya kutotaka kuhojiwa. Huna muda, umeandika ma page mangapi kwenye hii topic alone ? Hapa jamvini kila andiko linahojika, hatujali utaalam wako!

Na wahandisi wa Tanzania msiposimamiwa mnavuruga, na tutaendelea kuwakalia kooni. Mmechimba kishimo cha futi 2 mkakiita ni bwawa la milioni 200, Waziri Aweso kawakamata with your pants down. Crying shame on the profession.

Kongole naibu waziri wa afya Mollel, kongole mbunge wa Arusha Gambo, kongole waziri wa maji Aweso.

And above all else, rest in peace Pombe Magufuli, mlinzi wa mali ya umma aliyeasisi na kuendeleza mapambano dhidi ya shenanigans za mafundi wa nchi hii mpaka siku anakufa.
 
Huyo Katibu Mkuu amewiva kiutendaji.
Tabia za hovyo wanasiasa kuwatia ndani watendaji na makandarasi ili kujipatia promo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…